Wambinguni

Wambinguni

Share

Wambinguni

11/04/2025
11/04/2025

Somo: *'FAIDA YA KUDUMU KATIKA MAFUNDISHO"*

MATENDO YA MITUME 2:42 *“Wakawa wakidumu katika fundisho la mitume, na katika ushirika, na katika kusali.”*

Watu waliookoka katika kanisa la kwanza la mitume walikuwa wanapenda sana kudumu katika mafundisho ya neno la Mungu. Ndio maana walikuwa na kanisa lenye nguvu za Mungu.

Hali hiyo sivyo ilivyo kwa wakristo wengi leo. Nyakati tulizonazo wakristo wengi hawapendi mafundisho. Na kwa msingi huo, wamekuwa hata wavivu wa kuhudhuria ibada na makusanyiko kwa sababu hawaoni faida za mafundisho. Ziko faida nyingi sana za kuhudhuria makusanyiko na kudumu katika mafundisho. Hapa tutaangalia faida chache kati ya hizo nyingi;

1.*KUKUA KIROHO.* Mkristo anayedumu katika mafundisho ya Neno la Mungu, hukua haraka kiroho. Mkristo ambaye hadumu katika mafundisho ya Neno la Mungu hudumaa kiroho, 1PETRO 2:2, WAEBRANIA 5:11-14.

2.*IMANI YETU KUKUA.* Maisha ya wokovu ni maisha ya imani. Kuishi kwetu ni imani, WARUMI 1:17. Sasa hatuwezi kuwa na imani k**a hatudumu katika mafundisho. Maana chanzo cha imani ni kulisikia Neno la Mungu, WARUMI 10:17.

3.*HUONGEZA NGUVU YA MAOMBI YETU.* Mtu aliyejaa Neno la Mungu, maombi yake huwa na nguvu sana. Kwa sababu huomba sawasawa na mapenzi ya Mungu, YOHANA 15:7.

4.*HUTUDHIHIRISHA KWAMBA SISI NI WANAFUNZI WA YESU.* Yesu alishasema, “mkikaa katika neno langu, mmekuwa wanafunzi wangu kweli kweli,” YOHANA 8:31-32.

5.*HUTUSAIDIA KUJITENGA NA DHAMBI.* Mafundisho hutusaidia tujae Neno la Mungu. Na mioyo yetu ikijaa Neno la Mungu ni vigumu kumtenda Mungu dhambi, ZABURI 119:11.

*JINSI YA KUDUMU KATIKA MAFUNDISHO*

1.*Kuokolewa na kufanyika wanafunzi wa Yesu.* Tunapaswa kutubu dhambi zetu kwa kumaanisha kuziacha, ili Yesu atawale maisha yetu, MATHAYO 28:19-20.

2.*Kuwa tayari kuhudhuria vipindi vya wiki. Ili kuendelea kujifunza na kujazwa hekima na maarifa ya Neno la Mungu,* WAEBRANIA 10:25.

3.*Kuwa watendaji wa neno. Tunapaswa kuwa watendaji wa Neno,* YAKOBO 1:22.

4.*Kuishi maisha ya maombi. Kupenda kujiombea na kuwaombea wengine.* Huku tukiwaombea na washirika wenzetu, 1WATHESALONIKE 5:17.

5.*Kuitumainia neema ya Mungu.* Kumuomba Roho Mtakatifu atuwezeshe kudumu katika neema ya wokovu, YOHANA 1:16-17.

09/04/2025

Somo: *"TUTANYAKULIWA PAMOJA NAO, ILI TUMLAKI BWANA MAWINGUNI”*
Sehemu Ya 1

Mtu akishazaliwa hatakoma kuishi. Ataendelea kuishi milele na milele. Kifo ni mlango tu wa huyo mtu kwenda kuanza kuishi maisha mapya. Baada ya mtu kufa, kuna maisha ya aina mbili tu.

Aina ya kwanza ni maisha ya mateso na adhabu kwenye moto wa milele kwa wale wote ambao walimkataa Mungu hapa duniani.

Walikataa kuokoka au waliokoka lakini wakawa vugu-vugu, kwa Mungu wapo na kwa Shetani (dhambi) wapo, LUKA 16:19-24, UFUNUO 3:15-16, MATHAYO 25:41.

Kwa msingi huo mtu anapokufa akiwa ni mwenye dhambi haendi mbinguni, sehemu yake ni jehanamu ya moto; kwenye mateso ya moto wa milele na milele.

Aina ya pili ni maisha ya raha, kufurahi na kushangilia kwa wale wote ambao waliishi maisha ya haki na utakatifu katika ulimwengu huu.

Hao ni wale waliokuwa tayari kuishi sawasawa na Neno la Mungu, bila kujali kuchekwa, kudharauliwa, kutukanwa au kuonekana washamba mbele ya jamii. Watu ambao hawakuipenda dunia wala mambo yaliyomo katika dunia, walijitenga na maisha ya dhambi.

Mtu wa jinsi hiyo anapokufa anakwenda mbinguni kukaa na Mungu milele na milele, MATHAYO 25:34, WAEBRANIA 12:14. Yesu Kristo anafafanua vizuri jambo hili katika Injili ya MATHAYO 25:46 soma.

Matarajio yetu makubwa watu wote tuliookoka ni kwamba Yesu Kristo, mwokozi wetu atakuja mara ya pili. Safari hii hatakuja tena kuifia dhambi, bali atakuja katika utukufu kwa kuwachukua watu waliookoka na tutanyakuliwa na kumlaki Bwana hewani.

Biblia inasema hivi katika WAEBRANIA 9:28 *“Kadhalika Kristo naye, akiisha kutolewa sadaka mara moja azichukue dhambi za watu wengi; atatokea mara ya pili, pasipo dhambi, kwa hao wamtazamiao kwa wokovu.”*

Mara tu baada ya parapanda na kumlaki Bwana mawinguni basi tutakuwa pamoja na Bwana wetu YESU Kristo mbinguni, milele na milele, Amina!

Biblia inasema hivi katika 1WATHESALONIKE 4:13-17 “……... *Kwa sababu Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni pamoja na mwaliko, na sauti ya malaika mkuu, na parapanda ya Mungu; nao waliokufa katika Kristo watafufuliwa kwanza. Kisha sisi tulio hai, tuliosalia, tutanyakuliwa pamoja nao katika mawingu, ili tumlaki Bwana hewani; na hivyo tutakuwa pamoja na Bwana milele.”*

Na ndio maana Bwana wetu Yesu Kristo alisema anaenda kutuandalia makao, ili pale alipo sisi nasi tupate kuwepo. Wakati wowote atarudi tena ili atukaribishe kwenye hayo makao mapya, mbinguni.

Biblia inasema hivi katika 14:1-3 *“Msifadhaike mioyoni mwenu; mnamwamini Mungu, niaminini na mimi. Nyumbani mwa Baba yangu mna makao mengi; k**a sivyo, ningaliwaambia; maana naenda kuwaandalia mahali. Basi mimi nikienda na kuwaandalia mahali, nitakuja tena niwakaribishe kwangu; ili nilipo mimi, nanyi mwepo.”*

Mungu akupe neema na nguvu za kudumu katika neema hii ya wokovu ulioupokea, ili uwe miongoni mwa wale ambao wataenda kukaa na Mungu mbinguni milele na milele. Yakupasa uishi maisha ya maombi siku zote huku ukimtegemea Roho Mtakatifu katika neema yake.

ENDELEA KUFUATILIA MFULULIZO WA SOMO HILI, *“WAITWAO NI WENGI, BALI WATEULE NI WACHACHE”* - BILA SHAKA MOYO WAKO UTAKUWA NA KIU NA SHAUKU YA KUMTAFUTA MUNGU ZAIDI;-

08/04/2025

Welcome all of you in my group "Wambinguni" to hide our treasor in heaven

Want your business to be the top-listed Beauty Salon in Bujumbura?
Click here to claim your Sponsored Listing.

Category

Website

Address

Bujumbura