Afya Timilifu

Afya Timilifu

Share

Tunajali afya yako kwa kutatua changamoto uliyo nayo .

20/11/2024

TEZI DUME NA KANSA YA TEZI DUME INATIBIKA by Dr NEEMA
( 0653 893 557)
Dalili za kupanuka kwa tezi dume
Dalili huonekana baada ya umri wa miaka ya hamsini . Karibu wanaume wote wenye umri wa sabini na themanini huwa na tatizo hili.Dalili huanza polepole na kuzidi jinsi miaka inavyoongezeka.Dalili hizi ni k**a zifuatazo:

Kukojoa mara nyingi hasa nyakati za usiku.Hii ni dalili ya mapema sana.
Kulazimika, mara nyingi hasa nyakati za usiku, kutumia nguvu kuanzisha mkojo kutoka. Hata pale mgonjwa anahisi kibofu kimejaa. Hii ni dalili ya mapema sana.
Mkojo kutiririka polepole, hukatikakatika na hutumia nguvu kutoka.
Mkojo kushidwa kutoka hata wakati mtu anapohisi kukojoa.
Mkojo kuendelea kutoka kidogokidogo baada ya kukojoa, matone ya mkojo huendelea kutoka hata baada ya kukojoa hivyo nguo za ndani hulowa.
Kibofu hakiishi mkojo.
Matatizo ya tezi dume iliyotanuka

Tezi dume ikitanuka sana huleta matatizo mengi kwa wagonjwa wengine hali hii isipotibiwa. Matatizo hayo ni k**a yafuatayo:

Mkojo kukosa kutoka kabisa
Wagonjwa wenye tatizo hili lazima wawekewe katheta ili kumimina mkojo.
Madhara kwenye kibofu na figo
Kwa sababu ya kibofu kuwa na mkojo wakati wote, ukuta na misuli yake hupanuka na mwishowe hudhoofika hivi kwamba haiwezi kuzuia mkojo.
Kwa sababu ya kibofu kujaa
mkojo hurudi kwenye figo na mwishowe huharibu figo.
Ugonjwa wa tezi dume husababisha mkojo kutiririka polepole na mtu kukojoa mara nyingi hasa usiku.
Maambukizi na mawe
Kwa sababu kibofu hakimimini mkojo wote kuna hatari kubwa ya maambukizi kwenye njia ya mkojo nakuwa na mawe kwenye kibofu.
Kumbuka
Kutanuka kwa tezi dumehakusababishi ugonjwa wa saratani.

Utambuzi wa kupanuka kwa tezi dume
Historia na dalili zikiashiria uwepo wa hali hii, basi uchunguzi ufuatao ufanywe.
Uchunguzi wa ukubwa wa tezi

Uchunguzi huu hufanywa kwa kuingiza kidole chenye glovu nyuma hadi kwenye tezi dume. Daktari huweza kujua ukubwa na hali yake. Iwapo mtu ana ugonjwa huu tezi dume ni kubwa kuliko kawaida, laini na gumu yote pamoja. Iwapo tezi lina vifundo basi inaweza kuwa na kansa (saratani)au inaweza kuwa imepanuka.

Dalili za tezi kilichopanuka na saratani hufanana.Lazima uchunguzi wa kina ufanywe ili kujua ni ugonjwa upi.

PIGA (0653 893 557)KWA USHAURI ZAIDI

05/09/2023
Photos from Afya Timilifu's post 05/09/2023
05/09/2023

Ugonjwa wa saratani ya tezi dume kwa mujibu wa kitengo cha Saratani Ocean Riad

04/07/2023

SARATANI YA TEZI DUME
Tezi dume ni nini?

Tezi dume ni tezi inayopatikana kwa jinsia ya kiume. Tezi hii ina kazi ya kutengezeza majimaji meupe mepesi yenye unato kidogo. Majimaji haya husaidia mbegu za kiume kutembea kwa urahisi.

Ipo wapi?

Tezi dume iko mwishoni mwa kibofu cha mkojo. Pia inauzunguks mrija unaounganisha kibofu cha mkojo na na mrija wa mkojo wa uume (urethra) na iko mbele kidogo ya utumbo mpana ndani ya fupa la nyonga.
Saratani ya tezi dume ni nini?
Saratani ya tezi dume maana yake ni tezi dume imepata ugonjwa wa saratani..Na hii hutokea pale ambapo chembechembe hai za tezi huasi na kuanza kujigawanya bila kufuata utaratibu wa mfumo wa mwili, chembechembe asi hizi mwishowe hutengeneza vivimbe hatari ndani ya tezi dume na hatimaye husambaa mwilini
Visababishi hatarishi kwa saratani ya Tezi dume
Umri Mkubwa kuanzia miaka 50
Nasaba (ukoo wenye historia a saratani hii
Lishe hatarishi-nyama nyekundu kwa wingi, mafuta/samli,maziwa ya krimu
Unene uliokithiri
Ukosefu wa mazoezi
Upungufu wa virutubisho,mfano vit D.
Maambukizi ya mara kwa mara kwenye tezi dume

Want your business to be the top-listed Beauty Salon in Dar es Salaam?
Click here to claim your Sponsored Listing.

Category

Website

Address

705
Dar Es Salaam

Opening Hours

Monday 09:00 - 17:00
Tuesday 09:00 - 17:00
Wednesday 09:00 - 17:00
Thursday 09:00 - 17:00
Friday 09:00 - 17:00
Sunday 09:00 - 17:00