Helth products

Helth products

Share

Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Helth products, Health/Beauty, rogasiandoris03 @gmail. com, Dar es Salaam.

30/04/2024

*🤷‍♂️CHEMBE YA MOYO (ANGINA) NI TATIZO GANI?*


🌹Chembe ya moyo ni hali ya kusikia kubanwa, kwamba kuna uzito, au maumivu kwenye kifua. Watu wengine wenye chembe ya moyo husema kuwa wanasikia k**a vifua vyao vinaminywa au k**a kuna kitu kizito kimewekwa kwenye kifua.

🌹Tatizo hili kitaalamu huitwa angina au angina pectoris. Pamoja na kwamba ni tatizo linalowapata watu wengi, bado ni vigumu kutofautisha angina na maumivu ya aina nyingine, k**a kutojisikia vizuri kutokana na chakula kutoyeyushwa vizuri tumboni (indigestion.)

🌹Angina ni aina ya maumivu ya kifuani yanayotokana na kupungua kwa mtiririko wa damu kwenye eneo la misuli ya moyo.

🌹Chembe ya moyo si tatizo la kutishia sana maisha, lakini inaweza kuwa na dalili za heart attack , na ni kiashiria cha ugonjwa wa moyo (coronary heart disease -CHD.) Kwa kawaida, angina hutokea kutokana na moja au ateri zaidi ya moja za kupeleka damu kwenye moyo zikiwa nyembamba au zikiziba.

🌹Dalili za chembe ya moyo ni pamoja na maumivu ya kifuani, ambayo yanaweza kuelezewa k**a kubana, kuwaka au kujaa kwa kifua. Unaweza kuona maumivu kwenye mikono, shingo, taya, mabega au mgongoni. Dalili nyingine za chembe ya moyo ni:

🖍. Kizunguzungu
🖍. Uchovu
🖍. Kichefuchefu
🖍. Kukosa pumzi
🖍. Kutoka jasho

🌹Dalili hizi zinatakiwa zichunguzwe na daktari ili kuweza kubaini k**a una stable angina au unstable angina, ambayo inaweza kuwa ni kiashiria cha heart attack.

🌹Stable angina hutokea wakati moyo ukifanya kazi zaidi ya kawaida -k**a wakati wa mazoezi. Hali hii huchukua k**a dakika tano. Ni tatizo linalojirudiarudia, na linaweza kumpata mtu kwa miezi kadhaa au miaka. Kupumzika au kutumia dawa huondoa tatizo. Kwa mfano, maumivu wakati unapanda mlima au kwenye hali ya baridi.

🌹Unstable Angina (inahitaji uangalizi)
Unstable angina hutokea hata wakati wa kupumzika na huwa tofauti na maumivu yale uliyoyazoea. Unstable angina huja bila kutarajia, maumivu huwa makali zaidi na huchukua muda mrefu zaidi, dakika 30 au zaidi. Unstable angina inaweza isiondoke kwa kupumzika au kutumia dawa. Unstable angina inaweza kuwa ni kiashiria cha heart attack.

🌹Kuna aina nyingine ya angina, iitwayo variant angina au Prinzmental’s angina. Hii huonekana mara chache sana. Angina hii husababishwa na kukaza kwa ghafla kwa ateri za moyo ambako kwa muda mfupi hupunguza mtiririko wa damu kuelekea kwenye moyo.

🌹Variant angina mara nyingi hutokea ukiwa unapumzika na huja kwa nguvu sana. Angina hii huondoka kwa matumizi ya dawa.

🌹Angina Kwa Wanawake
Dalili za angina kwa wanawake zinaweza kuwa tofauti na zile zinazowatokea wanaume. Tofauti hizi huweza kusababisha wanawake kupata tiba. Kwa mfano, maumivu ya kifuani ni dalili ya kawaida kwa wanawake wenye angina, lakini inaweza isiwe dalili pekee au inayojionyesha zaidi. Wanawake wanaweza kuwa na dalili nyingine k**a:

🖍. Kichefuchefu
🖍. Kubanwa pumzi
🖍. Maumivu ya tumbo
🖍. Usumbufu shingoni, kwenye taya au mgongoni
🖍. Maumivu ya kuchoma badala ya kubanwa kifua.

🌹Chanzo Cha Chembe Ya Moyo
Chembe ya moyo hutokana na kupungua kwa mtiririko wa damu kwenye misuli ya moyo.

🌹Damu huisafirisha oksijeni, ambayo huhitajika na moyo ili uwe na afya. Misuli ya moyo ikikosa oksijeni kwa kiwango cha kutosha, hali iitwayo ischemia hutokea.

🌹Chanzo kikubwa cha kupungua kwa mtiririko wa damu kwenye misuli ya moyo ni ugonjwa wa ateri ya coronary -coronary artery disease (CAD).

🌹Ateri za coronary za moyo zinaweza kupungua kipenyo kwa sababu ya matabaka ya mafuta yaitwayo plaques. Hali hii huitwa atherosclerosis.

🌹Wakati wa mahitaji madogo ya oksijeni -kwa mfano, wakati unapumzika -misuli ya moyo wako inaweza kuendelea kufanya kazi vizuri bila ya kukuletea dalili za tatizo la chambe ya moyo. Lakini ukiongeza mahitaji ya oksijeni, k**a unapofanya mazoezi ya mwili, angina itatokea.

🌹Stable angina kwa kawaida husababishwa na mwili kufanya kazi. Unapopanda ngazi, ukifanya mazoezi au kutembea, mwili wako unahitaji damu zaidi, lakini mishipa ya ateri iliyosinyaa hupunguza mtiririko wa damu. Zaidi ya mwili kufanya kazi, vitu vingine k**a msongo wa mawazo, hali ya hewa ya ubaridi, milo mizito na kuvuta sigara vinaweza kuzifanya ateri zisinyae na kusababisha angina.

🌹Unstable angina. K**a matabaka ya mafuta (plaques) yatavunjikia ndani ya mshipa wa damu au damu ikiganda na kutengeneza vijibonge ndani ya mishipa, vinaweza kwa haraka kuziba au kupunguza mtiririko wa damu kwenye mshipa ulio na kipenyo kidogo na kupunguza kwa kiasi kikubwa damu inayofika kwenye misuli ya moyo.

🌹Unstable angina inaweza vile vile kusababishwa na vibonge vya damu vinavyoziba kabisa au kuziba kwa kiasi fulani mishipa ya damu ya moyo.

🌹Unstable angina huendelea kuwa mbaya na haipungui kwa kujipumzisha au kutumia dawa. Mtiririko wa damu usipoongezeka, moyo wako utakosa oksijeni na heart attack inaweza kutokea. Unstable angina ni hatari na huhitaji tiba ya dharura.

🌹chembe ya moyo coronary artery
Prinzmetal’s angina. Aina hii ya angina inatokana na mkazo wa ghafla kwenye ateri ya coronary, ambao kwa kipindi kifupi huibana ateri. Kubana huku hupunguza mtiririko wa damu kwenye moyo, na kusababisha maumivu makali ya kifua. Aina hii ya angina kwa kawaida hutokea wakati umepumzika, na hasa usiku. Maumivu hutokea mfululizo kisha kuacha kwa muda. Msongo wa mawazo, uvutaji wa sigara, madawa yanayosababisha mishipa ya damu kubana (k**a dawa za kipandauso) na matumizi ya co***ne yanaweza kusababisha Prinzmetal’s angina.

Kwa tiba na ushauri wasiliana nasi kwa namba 0754600379

04/05/2021

Kampuni ya brigth feature Tanzania tunahitaji watu wakufanya nao kazi piga simu namba 0754600379

17/04/2020
Photos from Helth products's post 14/04/2020
14/04/2020

U.T.I na fangasi ni tatizo kubwa ambalo huwapata wanawake wengi duniani mara kwa mara. Husababishwa na bakteria anaitwa E. coli ambaye huwa wanaishi kwenye utumbo mnene sehemu za tundu la haja kubwa, mwanamke anaambukizwa kirahisi sababu anapokuwa anachuchumaa kwenye haja kubwa au ndogo.
Madhara yake kwenye kibofu cha mkojo baada ya kuwa wengi wanahamia mwenye figo, ndio maana leo hii wanawake wengi wanaumwa figo. Figo zao zimeharibika sababu ya U.T.I. na kufa kifo cha ghafla.
Tafiti zinaonyeshwa kuwa nchini marekani watu milioni nane (8.1m) hupata U.T.I kila mwaka.
MIWASHO.
Kawaida mwanamke ana ulinzi ukeni kwake, yaani bakteria wazuri wanaishi kule kwa ajili ya kulinda uke, japo pia bakteria wabaya wanaishi kule lakini kwa uwiano, ya kwamba wale wazuri wanakuwa wengi ,kuliko wabaya (85:15). Sasa ikitokea kwamba wale bacteria wabaya wakawa wengi, hapo ndio utaona miwasho kwa mwanawake haishi kujikuna mara kwa mara.
FANGASI.
Inasababishwa na jamii ya fungi anaitwa CANDIDA. Seli za fangasi na bacteria wazuri huishi ukeni bila tatizo lolote.Tatizo linakuja endapo ukuaji wa fangasi hawa ukeni watakuwa wengi kushinda wazuri. Basi hapo ndio inapotokea ugonjwa wa fangas na miwasho mingi.
DALILI ZA U.T.I
1. Kukojoa mara kwa mara.
2. Mkojo kuwa na harufu kali.
3. Kusikia kichefu chefu na kupatika.
4. Maumivu ya misuli na tumbo hasa chini ya kitovu.
5. Kusikia maumivu wakati wa kukojoa.
6. Maumivu ya kiuno.
7. Kuwashwa sehemu za siri.
8. Kuhisi maumivu wakati wa kujamiiana.
9. Kupata vidonda vya ukeni.
10. Kuvimba na kuwa mwekundu kwa mdomo wa inje wa uke.
11. Kuhisi kuwaka moto sehemu za siri baada ya tendo la ndoa.
12. Kutokwa na uchafu wa rangi nyeupe au kijivu unaoweza kuwa mwepesi au mzito au majimaji.
VISABABISHI VYA FANGASI.
1. Mabadiliko ya homoni katika kipindi cha upevushwaji wa mayai kwa mwanamke kipindi cha ujauzito, utumiwaji wa uzazi, wa mpango na kukoma kwa hedhi.
2. Upungifu wa kinga mwilini: Mtu mwenye upungufu wa kinga mwilini k**a vile mwenye kuugua kansa,

31/03/2020

MAAMBUKIZI katika via vya uzazi kwa kawaida hujulikana k**a PID, kitaalamu kirefu chake ni Pelvic Inflammatory Disease, kwa Kiswahili maana yake ni maambukizi ya magonjwa katika via vya uzazi.
PID, ni maambuki yanayoathiri viungo vya uzazi vya mwanamke na hutokana na mchanganyiko mbalimbali wa magonjwa ya zinaa, hasa yaliyosababishwa na bakteria wa Pangusa (Chlamydia-ugonjwa huu tutaujadili siku zijazo) au kisonono.
Ugonjwa wa PID unapokaa muda mrefu bila kutibiwa, unaweza kusababisha uharibifu mkubwa usiobadilika katika mfumo wa uzazi wa mwanamke, hasa katika mfuko wa kizazi (uterus), vifuko vya mayai (Ovaries) na mirija ya mayai (fallopian tubes).
Ugonjwa huu unapokaa muda mrefu mwilini bila kutibiwa humfanya mwanamke kupatwa na ugumba. Wanawake wengi wamekuwa wakisumbuka na ugonjwa huu.
Ugonjwa wa kisonono pamoja na pangusa (Chlamydia) ndio vyanzo vikuu vya maambukizi katika via vya uzazi wa mwanamke.
Mwili wa mawanamke unapokuwa na afya kamili, mlango wa kizazi huwa na nguvu ya kuzuia bakteria wasiweze kuingia katika viungo vya ndani vya uzazi kutoka ukeni.
Hata hivyo, wakati mlango wa kizazi unapokuwa wazi na kuruhusu magonjwa ya zinaa kuingia, hasa kisonono na pangusa, mlango wa kizazi hupata maambukizi na kisha hupoteza uwezo wake, hivyo kuruhusu maambukizi na bakteria kuingia na kufika juu kwenye viungo vya uzazi.
Hapa kuna mambo ambayo huwafanya wanawake kupatwa na tatizo hili kwa urahisi, mambo hayo ni: Moja, kuwa na wapenzi wengi ama kutoka nje ya ndoa, pili; kuanza mambo ya mapenzi mapema hasa chini ya miaka 20, tatu; kupiga bomba ukeni kwaweza kusaidia vimelea kuingia ndani na kusababisha maambukizi katika viungo vya uzazi.
DALILI ZA MAAMBUKIZI
PID ikianza kuonyesha dalili zaweza kuwa k**a ifuatavyo; maumivu ya tumbo chini ya kitovu, kutokwa na uchafu ukeni, hasa wenye rangi ya njano unaoelekea kuwa kijani kwa mbali ukiwa na harufu mbaya, kuhisi maumivu ama hali ya kuungua wakati wa kukojoa.
Dalili nyingine ni kuwa na homa, kuhisi kichefuchefu ama kutap

19/03/2020

Afya njema kwa wote

Want your business to be the top-listed Beauty Salon in Dar es Salaam?
Click here to claim your Sponsored Listing.

Category

Telephone

Website

Address

Rogasiandoris03 @gmail. Com
Dar Es Salaam
0754600379