Dalilah

Dalilah

Share

ربنا أفرغ علينا صبرا و ذاب’بيت أقدامنا وان’صورنا العال قوميلكفر
Rabbana afrigh alayna sabran wa thab’bit aqdaamanaa wan’surna alal qawmil-kafireen

25/09/2024

Allah Subhana Wa Ta'ala. na Mtume wake (Swala Allahu Aleyhi wa Salam) Wametufunulia ndani ya Qur-an na Hadithi majina ya Malaika 12 pamoja na shughuli zao, k**a ifuatavyo.

Alhamdulillah jana tulisoma kuhusu Jibril (Aleyhi Salam). Na Leo tutaendelea na hao Malaika wengine wakubwa.

2.MIKAIIL.
Mikaiil ni Malaika mwingine mwenye daraja ya juu mbele ya ALLAH. k**a Alivyomtaja katika Suratul Baqarah aya ya 98, “

 ﻣَﻦْ ﻛَﺎﻥَ ﻋَﺪُﻭًّﺍ ﻟِﻠَّﻪِ ﻭَﻣَﻼﺋِﻜَﺘِﻪِ ﻭَﺭُﺳُﻠِﻪِ ﻭَﺟِﺒْﺮِﻳﻞَ ﻭَﻣِﻴﻜَﺎﻝَ ﻓَﺈِﻥَّ ﺍﻟﻠَّﻪَ ﻋَﺪُﻭٌّ ﻟِﻠْﻜَﺎﻓِﺮِﻳﻦَ 
Maana yake, “Aliyekuwa adui wa ALLAH na Malaika Wake na Mitume Wake na Jibril na Mikaiil (basi mtu huyo anatafuta kuangamia) kwani ALLAH ni adui wa makafiri.”

Naye Amewakilishwa kwa ajili ya mvua na mimea kwa amri ya Mola wake. Allah Subhana Wa Ta'ala Kasema katika Suratul A`araaf aya ya 57, “

 ﻭَﻫُﻮَ ﺍﻟَّﺬِﻱ ﻳُﺮْﺳِﻞُ ﺍﻟﺮِّﻳَﺎﺡَ ﺑُﺸْﺮًﺍ ﺑَﻴْﻦَ ﻳَﺪَﻱْ ﺭَﺣْﻤَﺘِﻪِ ﺣَﺘَّﻰ ﺇِﺫَﺍ ﺃَﻗَﻠَّﺖْ ﺳَﺤَﺎﺑًﺎ ﺛِﻘَﺎﻻ ﺳُﻘْﻨَﺎﻩُ ﻟِﺒَﻠَﺪٍ ﻣَﻴِّﺖٍ ﻓَﺄَﻧﺰَﻟْﻨَﺎ ﺑِﻪِ ﺍﻟْﻤَﺎﺀَ ﻓَﺄَﺧْﺮَﺟْﻨَﺎ ﺑِﻪِ ﻣِﻦْ ﻛُﻞِّ ﺍﻟﺜَّﻤَﺮَﺍﺕِ ﻛَﺬَﻟِﻚَ ﻧُﺨْﺮِﺝُ ﺍﻟْﻤَﻮْﺗَﻰ ﻟَﻌَﻠَّﻜُﻢْ ﺗَﺬَﻛَّﺮُﻭﻥَ 
Maana yake, “Na Yeye Ndiye anayepeleka pepo (za kuvuma) kuwa ni bishara (khabari njema) kabla ya kufika Rehema Yake (mvua). Hata hizo pepo zinapobeba mawingu mazito tunayachunga mpaka kwenye nchi iliyo kufa. Kisha tunateremsha kwayo maji, ndio k**a hivyo tukatolesha kila aina ya matunda. Basi hali kadhalika tunavyo wafufua wafu, ili mpate kukumbuka.

3.ISRAFIIL.
Israfiil ni jina la Malaika ambaye atakayepuliza baragumu siku ya Kiama. Naye ni mmoja wa Malaika ambaye aliyekuwa akitajwa sana na Mtume wetu (Swala Allahu Aleyhi wa Salam) katika dua yake kila anapoamka usiku kuabudu.

Alikuwa Mtume Mtukufu. anamtaja yeye pamoja na Jibril na Mikaiil, kasema katika Hadithi iliyopokelewa na Aisha (R.A) na iliyotolewa na Abu Daud, “
" ﺍﻟﻠَّﻬُﻢَّ ﺭَﺏَّ ﺟِﺒْﺮِﻳﻞَ ﻭَﻣِﻴﻜَﺎﺋِﻴﻞَ ﻭَﺇِﺳْﺮَﺍﻓِﻴﻞَ ﺃَﻧْﺖَ ﺗَﺤْﻜُﻢُ ﺑَﻴْﻦَ ﻋِﺒَﺎﺩِﻙَ ﻓِﻴﻤَﺎ ﻛَﺎﻧُﻮﺍ ﻓِﻴﻪِ ﻳَﺨْﺘَﻠِﻔُﻮﻥَ ، ﺍﻫْﺪِﻧِﻲ ﻟِﻤَﺎ ﺍﺧْﺘُﻠِﻒَ ﻓِﻴﻪِ ﻣِﻦَ ﺍﻟْﺤَﻖِّ ﺑِﺈِﺫْﻧِﻚَ ﺇِﻧَّﻚَ ﺗَﻬْﺪِﻱ ﻣَﻦْ ﺗَﺸَﺎﺀُ ﺇِﻟَﻰ ﺻِﺮَﺍﻁٍ ﻣُﺴْﺘَﻘِﻴﻢٍ ".
Maana yake, “Ewe ALLAH, Mola wa Jibril na Mikaiil na Israfiil Wewe Ndiye Unayehukumu baina ya waja Wako katika yale waliokuwa wakikhitilafiana, niongoze kwendea haki katika yale waliokhitilafiana kwa idhini Yako, Unamuongoza Umtakae kwendea njia iliyonyooka.”

4.MAALIK.
Maalik ni jina la Malaika mkubwa wa Malaika walio walinzi wa Motoni.

Allah Subhana Wa Ta'ala Kasema katika Suratul Zzukhruf aya ya 77, “
 ﻭَﻧَﺎﺩَﻭْﺍ ﻳَﺎ ﻣَﺎﻟِﻚُ ﻟِﻴَﻘْﺾِ ﻋَﻠَﻴْﻨَﺎ ﺭَﺑُّﻚَ ﻗَﺎﻝَ ﺇِﻧَّﻜُﻢْ ﻣَﺎﻛِﺜُﻮﻥَ 
Maana yake, “Nao watapiga kelele (kumwambia yule Malaika anayewaadhibu waseme) “Ee Maalik! Naatufishe Mola wako!” (Maalik) aseme “Bila shaka mtakaa humu humu (Motoni).”

5.RIDHWAAN.
Ridhwaan ni jina la Malaika ambae kazi yake ni mlinzi wa Peponi. Mwanachuoni Ibn Kathiir kasema, “
" ﻭﺧﺎﺯﻥ ﺍﻟﺠﻨﺔ ﻣﻠﻚ ﻳﻘﺎﻝ ﻟﻪ ﺭﺿﻮﺍﻥ ، ﺟﺎﺀ ﻣﺼﺮﺣﺎ ﺑﻪ ﻓﻲ ﺑﻌﺾ ﺍﻷﺣﺎﺩﻳﺚ ".
Maana yake, “Na mlinzi wa Peponi ni Malaika anaeitwa Ridhwaan. Malaika huyu hajawahi kucheka toka ameumbwa, ila aliwahi kutabasam pale mtume Muhammad (Swala Allahu Aleyhi wa Salam) alikwenda kutembelea motoni, na malaika huyu kwa kumuona kiumbe mtukufu Muhammad ndipo akatabasam.

6.MUNKAR NA NAKIIR.
Munkar na Nakiir ni Malaika wawili ambao amewataja Mtume Mtukufu katika Hadithi sahihi kuwa ni Malaika waliowakilishwa kuuliza watu maswali kaburini.

Nao wana umbo la kutisha na sauti kali sana. Allah Subhana Wa Ta'ala Atuepushe na adhabu ya kaburi.
Kila mmoja wetu baada ya kufa kwake anapozikwa kaburini mwake humjia Malaika hawa wawili na kumuuliza maswali k**a vile.

"Nani Mola wako?

Nani Mtume wako?

Na ipi dini yako?"

Ikiwa mtu huyo hapa duniani alikuwa mtiifu kwa Allah Subhana Wa Ta'ala na Mtume Wake Mtukufu ataweza kujibu maswali hayo kwa urahisi lakini ikiwa ni kinyume ya hivyo maswali hayo yatakuwa magumu kwake, hivyo inatupasa tujitayarishe kwa maswali hayo ya kaburini.

Na urahisi wa kujibu kwake inategemea na jinsi mtu alivyoishi katika maisha yake hapa duniani. Yaani mtu mwema au muovu?

7.HARUUT NA MARUUT.
Nayo haya ni majina ya Malaika wawili aliowatuma Allah Subhana Wa Ta'ala. kwa watu wa Baabil (Babylon hivi sasa ni nchi ya Iraq) ili wawafanyie mtihani wa kuwafundisha uchawi.

Na walikuwa hawamfundishi mtu yeyote yule ila baada ya kumuonya kwao kwamba ukitaka tukufunze basi utakufuru.

Allah Subhana Wa Ta'ala kasema katika Suratul Baqarah aya ya 102, “

 ﻭَﻣَﺎ ﻛَﻔَﺮَ ﺳُﻠَﻴْﻤَﺎﻥُ ﻭَﻟَﻜِﻦَّ ﺍﻟﺸَّﻴَﺎﻃِﻴﻦَ ﻛَﻔَﺮُﻭﺍ ﻳُﻌَﻠِّﻤُﻮﻥَ ﺍﻟﻨَّﺎﺱَ ﺍﻟﺴِّﺤْﺮَ ﻭَﻣَﺎ ﺃُﻧﺰِﻝَ ﻋَﻠَﻰ ﺍﻟْﻤَﻠَﻜَﻴْﻦِ ﺑِﺒَﺎﺑِﻞَ ﻫَﺎﺭُﻭﺕَ ﻭَﻣَﺎﺭُﻭﺕَ ﻭَﻣَﺎ ﻳُﻌَﻠِّﻤَﺎﻥِ ﻣِﻦْ ﺃَﺣَﺪٍ ﺣَﺘَّﻰ ﻳَﻘُﻮﻻ ﺇِﻧَّﻤَﺎ ﻧَﺤْﻦُ ﻓِﺘْﻨَﺔٌ ﻓَﻼ ﺗَﻜْﻔُﺮْ … 
Maana yake, “Na (Nabii) Suleiman hakukufuru, bali Mashetani ndio waliokufuru, wakiwafundisha watu uchawi (waliokuwa wakiujua wenyewe tangu zamani) na (uchawi) ulioteremshwa kwa Malaika wawili, Haruut na Maruut, katika mji wa Baabil. Na wala (Malaika hao) hawakumfundisha mtu yeyote mpaka wamwambie: “Hakika sisi ni mtihani, basi usikufuru…”

8.IZRAIL.
Na hili ndilo jina alilopewa Malaika wa Mauti, jina hili halikutajwa ndani ya Qur'an wala halikutajwa katika Hadithi sahihi, lakini hii ni kauli ya Wanavyuoni kwa jina hili.

9.RAQIIB NA ATIID.
Hayo ni majina ya Malaika wawili, ambao wamewakilishwa na Allah Subhana Wa Ta'ala kwa ajili ya kuandika kauli na vitendo vya watu.

Na maana ya majina haya Raqiib na Atiid ni kuwa wamehudhuria, mashahidi kwa vile daima hawaachani wako pamoja na watu ila kwa baadhi ya mambo fulani k**a vile mtu akiwa na janaba au akiwa uchi au akiingia msalani (chooni).

Allah Subhana Wa Ta'ala Kasema katika Suratul Qaaf aya ya 17 na ya 18, “

 ﺇِﺫْ ﻳَﺘَﻠَﻘَّﻰ ﺍﻟْﻤُﺘَﻠَﻘِّﻴَﺎﻥِ ﻋَﻦْ ﺍﻟْﻴَﻤِﻴﻦِ ﻭَﻋَﻦْ ﺍﻟﺸِّﻤَﺎﻝِ ﻗَﻌِﻴﺪٌ * ﻣَﺎ ﻳَﻠْﻔِﻆُ ﻣِﻦْ ﻗَﻮْﻝٍ ﺇِﻻ ﻟَﺪَﻳْﻪِ ﺭَﻗِﻴﺐٌ ﻋَﺘِﻴﺪٌ 
Maana yake, “Wanapopokea wapokeaji wawili, anaekaa kuliani na (anaekaa) kushotoni, (Malaika). Hatoi kauli yoyote isipokuwa karibu nae yuko mngojeaji (mwangalizi) tayari (kuandika).”

Ndugu zangu ktk Imaan malaika wa ALLAH hawana sifa ya kumuasi Allah wanafanya yale walio amrishwa na mola wao.

Binaadam tumeumbwa kwa Udongo

Majini wameumbwa kwa Moto

Na Malaika wa wameumbwa kwa Nuru, yaani mwanga mzuri.

Hivyo tufanye tutakayo malaika wapo kwaajili yetu.

Hao ndio Malaika wakubwa na kazi zao. K**a Kuna popote pale nlipokosea ktk Malaika hawa, numuomba Allah Subhana Wa Ta'ala Anisamehe.

21/09/2024

DARAJA LA MWANAMKE WA KIISLAMU
Fakhari ya wanawake ktk uislamu ni kuwa : Ndani ya qur an imeteremshwa sura yenye jina lenu Wanawake✰✰
Shahidi wa kwanza kabisa ktk uislamu alikuwa Mwanamke " Sumaiyyah r.a "
Mtu wa kwanza kumuamini Rasulullah s.a.w ni mwanamke " Khadija r.a "
Mmoja kati ya wapiganaji hodari ktk uislamu ni mwanamke " Khawlah r.a "
Mmoja kati ya walio jitolea kwa kila hali na Mali kwaajili ya uislamu ni mwanamke " Khansaar r.a " Usiya wa mwisho wa Rasulullah s.a.w kabla ya kufariki ni kuwatendea wema wanawake Mwanamme anapo muoa mwanamke hua anakamilisha nusu ya dini , na hivi ndivyo wanawake walivyo na hadhi kubwa ... ✰✰
Kwa sababu ya thamani yao kubwa uislamu umewapa heshima kwa kuwapa hijaab ili kuhifadhi utakaso wa nyoyo zao na heshima na usafi wa nafsi na miili yao . Japo wengi wao hawaoni kuwa ni kuthaminiwa na Allah wanataka wawe sawa na wasio kuwa waislamu
tijistiri enyi wanawake wenzangu pepo yetu kuipata ni rahisi saana uzito tunajipa wenyewe tusiombe mwisho mwema hali yakua
unazini
unasengenya
unafanya shirk
yarabby tusamehe waja wako hakuna aliechelewa mwenyezimungu mwingi wa huruma anasamehe tumrejeee Alla
mwenyezimungu Awajaze kheri Azidi kuwapa furaha Na Afya
As’salamu alaykum ah’lad diyaari minal mu’mineena wal Muslimeen;
Wa innaa in’shaa Allahu bikum la’hiqoon;
Nas’allul’laha lana wala’kumul a’afiyah.

KWA WAGONJWA
Adh’hibil bah’sa rabban naas;
Washfi antash shafee;
La shifaa’a illah shifa’uk;
Shifaa’ul laa yu’gaa-diru saqa’maa.
AMiiN

20/09/2024

"UNATAKA NDOA"

Sheikh Ibn ‘Uthaymiyn (Rahimahu Allaah) amesema:

"Mwanaume anaweza kusikia kuna mwanamke ana tabia nzuri, mwema, mchamungu, na ana elimu hivyo anaweza kutaka kumuoa.

Au mwanamke anaweza kusikia kuwa kuna mwanaume Ambae ni mwenye tabia njema na mwema na mjuzi na mwenye imani na dini, hivyo anaweza kutaka kuolewa nae.

Lakini mawasiliano kati ya wawili hao wanaopendana kwa njia zisizokubalika Kiislam ndio tatizo, ambalo husababisha matokeo mabaya na kuwapeleka kwenye zinaa.

Katika hali hii haijuzu kwa mwanaume kuwasiliana na mwanamke au kwa mwanamke kuwasiliana na mwanaume, na kusema kuwa anataka kumuoa/kuolewa.

Bali mwanaume anapaswa amwambie walii wake (Ndugu) kuwa anataka kumuoa binti fulani na mwanamke amwambie walii (ndugu) wake kuwa anataka kuolewa na bwana fulani.

Hii ndio njia sahihi ya wao kuwasiliana k**a ‘Umar (Radhiya Allaahu ‘anhu) alipomwozesha binti yake Hafsah kwa Abu Bakr na ‘Uthmaan (Radhiya Allaahu ´anh).

Lakini ikiwa mwanamke atawasiliana na mwanaume moja kwa moja, hii ndiyo njia ambayo sheytwani huitumia na kuwapeleka kwenye fitnah.
Dalilah Said

20/09/2024

ADABU ZA MWANAMKE KUTOKA NYUMBANI.

1. Kufunika kichwa (Hijaab).

2. Kujiepusha kupaka manukato.

3. Kiasi cha mwendo wake ni wakawaida kiasi kwamba sauti za viatu vyake hazisikiki.

Anasema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

“Wala wasipige miguu yao ili kudhihirisha wanayoyaficha katika mapambo yao…”

[an-Nuur (24):31]

Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa mkweli kiasi gani aliposema:

“Mwanamke yuko faragha (‘Awrah), basi anapotoka kwenye nyumba yake basi shetani humpamba).”

4. Ikiwa anatembea na mwenzake wa k**e mbele ya wanaume, basi asizungumze na mwenzake.
Hii haimaanishi kuwa sauti ya mwanamke ni kutoka sehemu zake za siri (‘Awrah) ambayo haiwezi kudhihirika; lakini kusikia kwa wanaume sauti ya mwanamke kunaweza kusababisha majaribu.

5. Na aombe ruhusa kwa mumewe (kabla ya kuondoka) ikiwa ameolewa.

6. Iwapo umbali anaotaka kuuendea unazingatiwa kuwa ni umbali wa kusafiri, basi asiondoke peke yake bila mtu ambaye ni jamaa yake (Mahaaram) halali.

7. Na asichanganyike na wanaume.

8. Na awe ni mwenye unyenyekevu na heshima.

9. Na ainamishe macho yake kwa kuepusha fitina.

10. Na asivue nguo zake katika nyumba isiyokuwa yake ikiwa anakusudia kujifunua uso wake.

Kwani hakika imetujia kwa njia ya Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:

“Mwanamke yeyote anayevua nguo zake katika nyumba isiyokuwa ya mume wake, basi hakika ameivua kifuniko kilichokuwa baina yake na Mola wake Mlezi.”
Dalilah Said

20/09/2024
20/09/2024

MAANA YA TALAKA
Talaka ni utaratibu wa kuvunja mkataba wa ndoa waliofunga mume na mke wakati wa kufunga ndoa mbele ya mashahidi wawili. Baada ya kuvunja mkataba huu kwa kufuata sharia ya Kiislamu, mwanamke aliyetalakiwa huwa huru kuolewa na mume mwingine.

TALAKA KATIKA UISLAMU
Talaka katika Uislamu si jambo Ia kupendeza. Kwa hiyo mume na mke wanatakiwa wajitahidi kusuluhishana na kuvumiliana iii hatua ya kupeana talaka isifikiwe.
Talaka ni jambo Ia halali lililo ruhusiwa inapokuwa hapana budi na wala Si jambo Ia kuhifanyia mas-khara k**a tunavyojifunza katika Hadith zifuatazo:

Ibn Umar amesimulia kuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu amesema: "Katika halali inayochukiza mbele ya Mwenyezi Mungu (s.w) ni talaka ". (Abu Daud).

Kwa upande mwingine, k**a Mwenyezi Mungu (s.w) angahiharamisha talaka, hali ya maisha ingahikuwaje katika famihia zile ambazo mume na mke wamekosana kiasi cha kila mmoja kutotaka kumuona mwenziwe! Kwa hiyo, mume au mke atakapofanya kosa au makosa makubwa yasiyovumihika kwa mwenziwe, Mwenyezi Mungu (s.w) ametoa ruhusa wapeane talaka na kuachana kwa wema na mapenzi k**a inavyosisitizwa katika Qur-an:

Talaka (za kuweza kurejeana) ni mara mbili. Kisha ni kumuweka kwa wema au kumwacha kwa ihsani ... ". (2:229). Na mtakapowapa wanawake talaka nao wakafikia kumaliza eda yao, basi warejeeni kwa wema au tokaneni nao kwa wema... (2:231). Basi wanapofikia muda wao, ima warejeeni kwa wema, au farikianeni nao kwa wema... (65:2).

Kwakuwa ndoa ni mkataba waliowekeana mume na mke wa kuishi kwa wema na kuachana kwa wema ikibidi kuachana, hapana sababu kabisa ya kujenga chuki na uhasama kati ya wawili hawa kwa sababu tu eti wanashindwa kuuendeleza mkataba wao. Katika aya hizi tunaamrishwa kuvunja mkataba huu kwa wema kwa kufuata utaratibu aliouweka Mwenyezi Mungu (s.w) na baada ya hapo kila mmoja kuwa huru.

20/09/2024

: Imepokewa kutoka kwa Abu Hurayrah radhi za Allah ziwe juu yake kuwa Mtume muhamma(ﷺ) amesema kwamba , " Ambaye amemdhulumu ndugu yake iwe kutokana heshima na utu au kwa kitu chochote kile , basi ajikomboe kutoka kwake ( amuombe msamaha au amrejeshee alivyomdhulumu ) , leo kabla ya siku ya hisabu ( ya Kiyama ) wakati ambao utakuwa hamna Dinari wala Dirhamu ( pesa na mali za kujikomboa ) , hapo akiwa anazo thawabu za amali njema zitachukuliwa kupewa yule aliyemdhulumu kwa kadiri ya alivyomdhulumu na ikiwa hana thawabu za wema ( au zimemalizika hizo thawabu za mema ) huchukuliwa madhambi ya maovu ya yule mwenzake aliyemdhulumiwa na kubebeshwa yeye aliyedhulumu ( atapunguziwa dhambi na kupewa aliedhulumu ) [ Al - Bukhari ] .

Want your business to be the top-listed Beauty Salon in Dar es Salaam?
Click here to claim your Sponsored Listing.

Telephone

Website

Address

Dar Es Salaam