m-afya

m-afya

Share

provide health advice service

03/11/2024

Jina langu Dr WASHA kutoka katika taasisi ya m-afya.
Leo nimeona ni vizuri tuzungumze kuhusu huduma ya kwanza (first aid).
Watu wengi wanajikuta kwenye matatizo ya kiafya ya kudumu au kuchukua muda mrefu kupona kwa sababu tu awakupata huduma ya kwanza. Hii ni kwa sababu watu wengi hatuna elimu ya umuhimu wa huduma ya kwanza.
Watoto wanapokuwa nyumbani, mara nyingi hujishughulisha na michezo mbalimbali ambayo husaidia kujiburudisha na kujenga mahusiano mazuri baina yao.

Kila hatua ya ukuaji wa watoto huleta matukio mengi ya furaha, lakini pia kuna nyakati ambazo matukio hayo yanaweza kuhatarisha usalama wao.

Swali muhimu la kujiuliza ni je, wazazi tunajua vya kutosha kuhusu elimu ya huduma ya kwanza kwa watoto pindi wanapokabiliwa na dharura nyumbani?

Ni wazi kwamba wazazi wengi hatuna uelewa wa kutosha kuhusu huduma ya kwanza kwa watoto wetu. Hivyo, wakati dharura inapotokea, mara nyingi tunajikuta tukishindwa kujua cha kufanya ili kuokoa hali ya hatari inayowakabili watoto.



Huduma ya kwanza
Ni msaada wowote anaopewa mhanga ilikupunguza maumivu baada ya janga alilolipata kabla yakupelekwa hospitalini kwenda kupata huduma zaidi.
Huduma ya kwanza inamaanisha huduma au msaada unatolewa kwa mtu anayekabiliwa na ugonjwa au madhara ya ghafla wakati daktari hayupo karibu na kabla hajapelekwa hospitalini kwa matibabu zaidi.

Zifuatazo ni faida za huduma ya kwanza.

• Kuokoa maisha.

• Kupunguza maumivu.

• Kumpa matumaini mhanga.

• Kumsaidia daktari kupata taarifa kamili ya mgonjwauliyempeleka.

Want your business to be the top-listed Beauty Salon in Dar es Salaam?
Click here to claim your Sponsored Listing.

Category

Website

Address

Uhasibu
Dar Es Salaam