Dr Kisuzuki
Health diet
07/02/2025
Vidonda vya tumbo.
Ni vidonda vinavyo patikana kwenye utando wa tumbo au duodenum (utumbo ndogo).
Vidonda vya tumbo vinaweza kusababisha dalili k**a vile maumivu na kichefuchefu.
Sababu za Vidonda vya Tumbo:
1. Maambukizi ya Helicobacter pylori:
Maambukizi ya bakteria ambayo hudhoofisha utando wa tumbo, na kulifanya liwe hatarini kuharibiwa na (Hydrochloric acid) asidi ya kusaga chakula.
2. Matumizi ya muda mrefu ya dawa za maumivu aina ya (NSAIDs):
Dawa hizi zinaweza kusababisha utando wa tumbo kupunguza ute wake wa kinga.
3. Unywaji wa pombe kupita kiasi:
Pombe inaweza kuharibu utando wa tumbo na kusababisha vidonda.
4. Uvutaji wa Sigara:
Uvutaji wa sigara unaweza kuongeza uzalishaji wa asidi ya tumbo na kupunguza uwezo wa tumbo kujikinga na asidi hiyo.
5. Mfadhaiko( msongo wa mawazo):
Ingawa mfadhaiko hausababishi vidonda moja kwa moja, unaweza kuchangia ukuaji au kuongezeka wa vidonda, ikishirikiana na sababu zingine.
6. Uzalishaji wa asidi kupita kiasi:
Hali k**a vile ugonjwa wa Zollinger-Ellison husababisha uzalishaji kupita kiasi wa asidi ya tumbo, ambayo inaweza kusababisha vidonda.
Dalili:
- Tumbo kuuma.
- Kichefuchefu au kutapika
- Kupoteza hamu ya kula
-Maumivu makali na ya ghafla ya tumbo yanayoambatana na:
- Kutapika damu
- Kupata choo cheusi
Kwa ushauri zaidi wasiliana nasi.
Karibuni.
Click here to claim your Sponsored Listing.
Category
Website
Address
Dar Es Salaam
11101
