Breaking News TZ

Breaking News TZ

Share

Habari za haraka, sahihi na kwa wakati kutoka Tanzania na dunia nzima �. Tukikuletea taarifa za kisi

11/08/2025

KIMEUMANA! Yanga Watoa Taarifa Hii Nzito Kwa Umma Usiku Huu, Mashabiki Walipuka
SportsupdatesAug 10, 2025 8:54 PM
Mabingwa wa kihistoria wa ligi kuu Tanzania Bara klabu ya Yanga Sc wametoa taarifa ambayo imeacha maswali mengi kwa mashabiki na wadau wa soka nchini Tanzania.

Taarifa iliyotolewa na klabu ya Yanga Sc usiku huu wa leo Jumapili tarehe 10 Agosti, imeeleza wazi kwamba "Ofa imekataliwa!", ikiwa ni mwendelezo wa tetesi zinazoeleza kwamba klabu hiyo imekuwa ikigomea ofa mbalimbali ambazo zimekuwa zikitolewa na vilabu mbalimbali ambazo vinavihitaji saini ya mshambuliaji wao anayejulikana kwa majina ya Clement Mzize.

Siku ya leo vyanzo mbalimbali vya habari za michezo nchini Tanzania vimedokeza kwamba klabu ya Esparance Sportive De Tunis wametoa ofa nono inayokadiriwa kufika bilioni 2 za kitanzania ili kuhitaji saini ya Clement Mzize.

Taarifa za kuaminika kutoka katika kambi ya klabu ya Yanga Sc zinaeleza kwamba viongozi wa klabu hiyo hawako tayari kupokea ofa hiyo kwa sababu wao pia kuna ofa kutoka uarabuni ambayo ndiyo waliyovutiwa nayo zaidi kuliko hii ya Esparance Sportive De Tunis ya nchini Tunisia.

Taarifa hii iliyotolewa na klabu ya Yanga Sc usiku huu inaweza ikawa inatoa majibu kwamba wamegomaa kumuuza Mzize kwenda Esparance na sasa pengine watakuwa wanakaribisha ofa zingine kutoka katika vilabu vingine ambavyo vinavutiwa zaidi na huduma ya Clement Mzize.

Kuna mvutano mkubwa sana baina ya viongozi wa klabu ya Yanga Sc na meneja wa Jasmine Razack kwani meneja na Mzize mwenyewe wanalazimisha Yanga Sc wakubali ofa ya Esparance Sportive De Tunis lakini viongozi wa klabu ya Yanga Sc wanaonekana kutokuwa tayari kumuachia kinda huyo ambaye amekuwa kwenye ubora mkubwa sana tangu alipoanza kuitumikia klabu hiyo miaka kadhaa iliyopita.

Chanzo: ukurasa wa Instagram wa klabu ya Yanga Sc.

From Opera News

Maudhui yaliyoundwa na kutolewa na Sportsupdates . Opera News ni jukwaa huru hivyo maono na maoni yaliyotolewa humu ni ya mwandishi pekee na hayawakilishi, hayaakisi au hayatoi maoni ya Opera News. Maudhui yoyote/yote yaliyoandikwa na picha zinazoonyeshwa hutolewa na mwanablogu/mwandishi

11/08/2025

Ahmedy Ally Avunja Ukimya: Aivaa Yanga Baada ya Kumfanyia Jambo Hili Clement Mzize
Erick GrationAug 11, 2025 12:07 PM
Msemaji wa Simba SC, Ahmedy Ally, ameungana na mashabiki wa soka nchini katika kutoa maoni kuhusu mkataba wa kiungo wa Yanga SC, Clement Mzize, baada ya taarifa kuenea kuwa mchezaji huyo alikubali kuhamia nje ya nchi lakini hatimaye alikosa fursa hiyo.

Katika ujumbe aliouandika kwenye mitandao ya kijamii, Ahmedy Ally alisema kuwa ni wakati sahihi kwa yeye kuingilia kati sakata la Sheikh Walid na kuhakikisha kuwa kijana anatimiza ndoto yake ya kucheza nje ya nchi, huku akisisitiza kuwa ni muhimu mchezaji huyo kuuza thamani yake halisi kwa biashara makusudi na sio kwa bei iliyopangwa kwa manufaa ya wengine.

Pia, Ahmedy alisisitiza kuwa hawezi kuunga mkono juhudi za kumzuia mtu kutimiza malengo yake kwa kutumia lugha inayojificha. Alisema, "Haiwezekani kila mchezaji akitaka kuondoka kwenu ianze vita, kwa Mayele tulijua bahati mbaya kwa Feisal tukasema haitojirudia tena na sasa kwa Walid hii haikubaliki," akionyesha wazi kwamba kila mchezaji anapaswa kuwa na uhuru wa kuendeleza ndoto zake.

Msemaji huyo aliongeza kuwa kwa upande wa Simba, wao wanaendelea kupigania mafanikio katika Ligi ya Tanzania, na kuwa wataendelea kutafuta ushindi kwa nguvu zote. Alihitimisha ujumbe wake kwa kusema, "Kwako Walid wewe endelea kuipigania Tanzania, sisi tutapambana nao na mwisho wa siku tutakukabidhi ushindi, Insha Allah."

Kauli hii inadhihirisha ari ya Ahmedy Ally ya kupigania maslahi ya wachezaji wa Tanzania na kuhakikisha kwamba wanapata nafasi za kuonyesha uwezo wao kimataifa, huku akisisitiza umuhimu wa kuacha wachezaji kutimiza malengo yao na kuwa na maono ya kimataifa.

SOURCE

https://www.instagram.com/p/DNNOw4lKueJ/?igsh=eGFnMXMwNWkwcXhz

From Opera News

Maudhui yaliyoundwa na kutolewa na Erick Gration . Opera News ni jukwaa huru hivyo maono na maoni yaliyotolewa humu ni ya mwandishi pekee na hayawakilishi, hayaakisi au hayatoi maoni ya Opera News. Maudhui yoyote/yote yaliyoandikwa na picha zinazoonyeshwa hutolewa na mwanablogu/mwandishi

11/08/2025

Hii hapa orodha kamili ya klabu zilizofuzu UEFA champions league 2025/2026
SokoninewsJul 25, 2025 11:43 PM
Hadi sasa, Klabu 29 kati ya 36 zimefuzu moja kwa moja kwa hatua ya Ligi (zamani Makundi) ya Ligi ya Mabingwa Ulaya (UEFA Champions League) msimu wa 2025/26. Klabu hizi zimefuzu kupitia nafasi zao katika Ligi Kuu za ndani, ushindi katika mashindano ya UEFA, au kwa vigezo maalum vya utendaji wa kitaifa. Zifuatazo ni klabu zilizofuzu:

Uingereza (6)

- Manchester City

- Arsenal

- Liverpool

- Chelsea

- Newcastle United

- Tottenham Hotspur (Mabingwa wa Europa League 2024/25)

Hispania (5)

- Real Madrid

- Barcelona

- Atlético Madrid

- Athletic Club

- Villarreal

Italia (4)

- Inter Milan

- Napoli

- Atalanta

- Juventus

Ujerumani (4)

- Bayern Munich

- Borussia Dortmund

- Bayer Leverkusen

- Eintracht Frankfurt

Ufaransa (3)

- Paris Saint-Germain (Mabingwa wa UEFA Champions League 2024/25)

- Olympique de Marseille

- AS Monaco

Uholanzi (2)

- PSV Eindhoven

- Ajax

Ureno (1)

- Sporting CP

Ubelgiji (1)

- Union Saint-Gilloise

Uturuki (1)

- Galatasaray

Jamhuri ya Czech (1)

- Slavia Prague

Ugiriki (1)

- Olympiacos (Alipewa nafasi kupitia mfumo wa “rebalancing” baada ya PSG kufuzu kupitia Ligi yao ya ndani)

Nafasi saba za mwisho zitajazwa kupitia raundi za mtoano (qualifying rounds) zinazoendelea hadi Agosti 2025. Baadhi ya klabu zinazoshiriki katika mtoano ni:

- Celtic (Scotland)

- Benfica (Portugal)

- Feyenoord (Uholanzi)

- Club Brugge (Ubelgiji)

- Fenerbahçe (Uturuki)

- Red Star Belgrade (Serbia)

- Dynamo Kyiv (Ukraine)

- Rangers (Scotland)

- Panathinaikos (Ugiriki)

- FC Copenhagen (Denmark)

Klabu hizi zinapambana katika njia ya mabingwa (Champions Path) na njia ya Ligi (League Path) kupata nafasi katika hatua ya Ligi ya msimu wa 2025/26.

- Agosti 28, 2025: Hii ndiyo tarehe ya droo rasmi ya upangaji wa makundi (hatua ya Ligi) ya UEFA Champions League 2025/26. Droo hiyo itafanyika ili kuamua klabu zipi zitakutana katika hatua ya Ligi.

- Septemba 2025: Huu ndio mwezi rasmi wa kuanza kwa mechi za hatua ya Ligi (zamani ilikuwa inaitwa hatua ya makundi). Klabu 36 zitacheza mechi 8 kila moja dhidi ya wapinzani tofauti kwa mfumo mpya wa Ligi.

10/08/2025

Hii Ndio Simba ya Msimu Ujao ni Hatari Sana Hapa Ubingwa Mgongoni
MgayaB_13Jul 26, 2025 1:55 PM

Klabu ya Simba SC imeonyesha mwanga wa matarajio makubwa kuelekea msimu ujao wa mashindano kwa kutangaza kikosi chao kipya chenye mfumo wa 4-2-3-1, kinachoashiria mabadiliko ya kimkakati na kiu ya mafanikio. Katika mfumo huu, Kocha mkuu ameonesha dhamira ya kushambulia zaidi huku akiimarisha ulinzi wa kati na pembeni.

Mlinzi wa lango ni Camara, ambaye anatarajiwa kuwa ngome madhubuti msimu mzima. Safu ya ulinzi imejengwa na wachezaji wenye uzoefu na nguvu: Diaw na Kapombe pembeni, huku De Reuck na Hamza wakisimama katikati kuhakikisha lango haliguswi kirahisi.

Katikati ya uwanja, Kagoma na Maema wanapewa jukumu la kudhibiti kasi ya mchezo na kusambaza mipira kwa ubunifu, huku Ahoua akiwa kiungo mkabaji wa kusaidia safu ya ulinzi. Mbele yao, Mpanzu, Sowah na Maseko wanaunda safu ya mashambulizi ya kati na pembeni – wakiwa na jukumu la kumlisha mshambuliaji wa kati au kufunga wenyewe.

Kwa muundo huu, Simba SC imeonyesha kwamba inalenga kurudi kwenye ubora wa juu barani Afrika na kutawala Ligi Kuu Tanzania Bara. Usajili mpya na matumizi ya wachezaji wenye vipaji vikubwa vinaashiria msimu wa ushindani mkubwa, huku mashabiki wakingoja kwa hamu kuona mafanikio ya mabadiliko haya ya kimkakati.

From Opera News

Maudhui yaliyoundwa na kutolewa na MgayaB_13 . Opera News ni jukwaa huru hivyo maono na maoni yaliyotolewa humu ni ya mwandishi pekee na hayawakilishi, hayaakisi au hayatoi maoni ya Opera News. Maudhui yoyote/yote yaliyoandikwa na picha zinazoonyeshwa hutolewa na mwanablogu/

Photos from Breaking News TZ's post 10/08/2025

Siri Imefichuka:Kumbe Hii Ndiyo Sababu Ya Viongozi Wa Yanga Na Wakala Wa Mzize Kutoelewana
AZUMANEWSAug 10, 2025 10:50 PM
Taarifa zinazosambaa zinaonyesha kuwa mahusiano kati ya msimamizi wa mchezaji Clement Mzize, Jasmine Razack, na viongozi wa klabu ya Yanga SC yameingia kwenye mgogoro mkubwa. Inadaiwa kuwa hali hiyo imefikia hatua mbaya kiasi cha kusemwa kuwa “mahusiano hayo yapo ICU”, ikimaanisha hali ni mbaya sana na mawasiliano yamevunjika au yamejaa mvutano.

Kitu kinachoonekana hapa ni mvutano wa nguvu na mamlaka kati ya Jasmine na viongozi wa Yanga. Kila upande unatamani kuonekana ndiye mwenye ushawishi mkubwa juu ya mustakabali wa Mzize. Jasmine, ambaye anaonekana k**a mlezi na mtu wa karibu wa Mzize, anataka kuhakikisha mchezaji anaenda kwenye mazingira anayoyaona yatakuwa bora kwake kitaaluma na kimaisha. Kwa upande mwingine, Yanga wanataka kuhakikisha wanapata faida kubwa kifedha na kimipango kabla ya kumuachia mchezaji huyo ambaye wamewekeza kwake kwa muda mrefu.

Katika mvutano huu, mchezaji mwenyewe – Clement Mzize – ndiye anayekumbwa na presha kubwa zaidi. Yupo katikati ya watu wawili muhimu katika maisha yake ya soka. Kwa upande mmoja yupo Jasmine, ambaye amekuwa k**a mlezi au hata mama kwake, na kwa upande mwingine kuna Yanga – klabu iliyomkuza, kumpa jukwaa la kuonesha uwezo wake na kumtoa hadi kufikia kiwango cha kimataifa. Hali hii inamweka njia panda kubwa.

Tatizo hapa si kwamba Mzize anaondoka Yanga – hilo limeshaeleweka na kukubaliwa na wengi – bali ni wapi anaenda? Je, anaelekea kule ambako Jasmine anaamini ni bora kwake au kule ambako Yanga wanaona ni dili bora zaidi kwa klabu? Hili ndilo fumbo linalozua mvutano. Jasmine anaweza kuwa na mawasiliano na klabu fulani nje ya Tanzania na kuona hiyo ndiyo fursa bora kwa mchezaji, wakati Yanga wao wanazungumza na timu nyingine – mfano Espérance – wanaotoa ofa kubwa zaidi kifedha lakini huenda si chaguo la Jasmine.

Hii ni hali ambayo hujitokeza mara nyingi katika soka la kisasa ambapo maslahi ya klabu na ya wasimamizi wa wachezaji hugongana. Ni muhimu kwa pande zote kuweka mbele maslahi ya mchezaji, kwani lengo kuu linapaswa kuwa kumpa mchezaji mazingira bora ya kukuza kipaji chake, kupata mafanikio na pia klabu kufaidika.

Iwapo busara haitatumika, kuna hatari Mzize akaathirika kisaikolojia, motisha yake ikashuka au hata akapotea katika maamuzi yasiyo na mshik**ano. Ni wakati sasa kwa Jasmine na Yanga kuweka pembeni ubinafsi na mvutano wa madaraka, wakae meza moja kwa heshima na kufanya uamuzi unaoendana na malengo ya mchezaji, klabu na mpira wa Tanzania kwa ujumla.

From Opera News

Maudhui yaliyoundwa na kutolewa na AZUMANEWS . Opera News ni jukwaa huru hivyo maono na maoni yaliyotolewa humu ni ya mwandishi pekee na hayawakilishi, hayaakisi au hayatoi maoni ya Opera News. Maudhui yoyote/yote yaliyoandikwa na picha zinazoonyeshwa hutolewa na mwanablogu/mwandish

10/08/2025

Hizi hapa mechi za awali za Ligi ya Mabingwa Afrika
HajoNewsAug 10, 2025 7:44 AM
“Vita ya Mabingwa Afrika Yaanza! Haya Ndio Mapambano ya Raundi ya Awali CAF Champions League 2025/26 Vigogo Wapewa Kibarua Kigumu!”

Mashabiki wa soka barani Afrika wajiandae kwa burudani ya kipekee baada ya Shirikisho la Soka Afrika (CAF) kutangaza droo ya raundi ya awali ya Ligi ya Mabingwa Afrika 2025/26. Mashindano haya yanayodhaminiwa na TotalEnergies yanatarajiwa kuanza kwa moto, huku timu kutoka kila kona ya bara zikisaka heshima na nafasi ya kufuzu hatua ya makundi.

Droo hii imepangwa kwa namna ya kuvutia mashabiki, kwani tayari kuna michezo mikubwa inayoweza kutoa mshindi wa kushtua. Miongoni mwa michezo ya kuvutia, APR FC ya Rwanda itapambana na Pyramids FC ya Misri, wakati Real de Banjul ya Gambia ikipambana na mabingwa mara nyingi AS FAR ya Morocco.

Timu maarufu k**a Esperance ya Tunisia itaanza safari yake dhidi ya AS FAN kutoka Niger, huku Simba SC ya Tanzania ikikutana na Gaborone United kutoka Botswana. Mpinzani wao wa jadi, Yanga SC, atakuwa na mtihani wa kucheza na Wiliete Benguela ya Angola.

Kutoka Zambia, Power Dynamos watakabiliana na ASEC Mimosas ya Ivory Coast – mchezo ambao wengi wanasema ni k**a fainali kabla ya fainali. Orlando Pirates wa Afrika Kusini nao watakuwa na safari ya Lesotho kumenyana na Lioli FC, mechi inayotarajiwa kuvuta hisia nyingi.

Kuna pia michezo mingine ya kusisimua ikiwemo:

Mogadishu City vs Kenya Police

Simba Bhora (Zimbabwe) vs Nsingizini Hotspurs (Eswatini)

Goldstars (Ghana) vs JS Kabylie (Algeria)

Rivers United (Nigeria) vs DR Congo 1

10/08/2025

Your welcome

Want your business to be the top-listed Beauty Salon in Dar es Salaam?
Click here to claim your Sponsored Listing.

Category

Address

Saidisalumumikidadi@gmail. Com
Dar Es Salaam
11101