Reen Healthtalk

Reen Healthtalk

Share

Tunasaidia watu wenye changamoto mbali mbali za kiafya

30/07/2025

Historia na uchunguzi wa mwili ni muhimu sana ili kubaini na kutatua magonjwa ya ngozi.

Ugonjwa wa ngozi unaweza kuwa na historia katika familia au mtu binafsi, aina ya shughuli anazo fanya mtu, kupigwa na mwanga wa jua kwa muda mrefu au aina nyinginezo za mionzi, uwepo wa magonjwa sugu k**a kisukari, fangasi, homa ya ini (hepatitis C), historia ya kaswende na kisonono, matumizi ya dawa zenye sumu na kusafiri, yote hayo huleta magonjwa ya ngozi.

Magonjwa mengi ya ngozi yanatambuliwa na kutibiwa kwa muonekano wake.
+255792953948

30/07/2025

Pumu ya ngozi ni ugonjwa wa ngozi unaombatana na kuvimba,kuwasha na kukak**aa kwa ngozi. Ni ugonjwa usio wa kuambukizwa.

Chanzo kamili cha Pumu ya ngozi hakijulikani, lakini kutokea kwake huchangizwa na sababu k**a za urithi (vinasaba) endapo baba au mama alishawahi kuwa na ugojwa huu basi kunakuwa na nafasi kubwa ya mtoto kuupata pia, au mazingira anayoishi mtu, k**a uwepo vumbi, poleni, manyonya ya wanyama au vitakasa.

Dalili za Pumu ya Ngozi;
🔴 Ngozi kuwasha na kuwa kavu
🔴 Ngozi kuvimba na kuwa nyekundu.
🔴 Ngozi kuk**aa na kuwa na michirizi.
🔴 Kuwa na vipele vinavyotoa maji.

Upatapo dalili k**a hizo ni vyema kuwasiliana na daktari kwa ushauri wa karibu na ufatiliaji wa muda mrefu kwa afya ya ngozi yako.


Wa.me/255792953948

Want your business to be the top-listed Beauty Salon in Dar es Salaam?
Click here to claim your Sponsored Listing.

Category

Website

Address

Dar Es Salaam
Dar Es Salaam