Mapishi na afya

Mapishi na afya

Share

Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Mapishi na afya, Health/Beauty, 0624251582, Dar es Salaam.

12/05/2022

Half cake

Mahitaji
Unga wa ngano kikombe 1na1/2 (k**a robo hivi)
Sukari 1/4 kikombe
Baking powder 1/2 kijiko cha chai
Magadi soda (bicarbonate soda/baking soda) 1 kijiko cha chai
Mafuta 2 vijiko vya chai
Mafuta ya kukaangia
Maji ya uvuguvugu kiasi

Matayarisho
Changanya unga na vitu vyote (kasoro mafuta ya kuchomea) kisha ukande (hakikisha unakuwa mgumu) Baada ya hapo sukuma na ukate shape uipendayo (hakikisha unakata vipande vinene kiasi na sio k**a mandazi) Baada ya hapo ziweke sehemu yenye joto na uache ziumuke. Zikisha umuka zikaange katika moto mdogo ili ziive mpaka ndani. Zikisha iva zitoe na uziweke katika kitchen towel ili zichuje mafuta. Ziache zipoe na hapo zitakuwa tayari kwa kuliwa.

dondoo muhimu:-👇👇👇👇👇
Jinsi ya kupika half keki zilizo pasuka na kuiva vizuri.
1.Hakikisha unatumia vipimo sahihi bila kusahau bicarbonate of soda(baking soda) hiki ndicho kiungo muhimu ktk half cake na baking powder...(hamira SI lazima kuweka kwa half cake za kula tu...labda ziwe za biashara)
2.Unga wako unapokanda uwe mgumu hata kidole kishindwe kupenya kwenye unga
Hauhitaji kuikanda sana k**a maandazi ukishashikana tu inatosha.
3.Weka half keki zako kwenye mafuta kabla hayajapata moto.
4.Poza mafuta yako kila baada ya mpiko mmoja.(unaeza kuepua ili yapoe chini...au ukaongeza mafuta ya baridi jikoni )

Chef nancy

16/10/2020

Njoo ujifunze kutengengeneza pilipili za biashara 1000
Utafunza pilipili aina sita za biashara zinazoweza kukaa mda mrefu bila kuharibika
Pia utaelekezwa na malighafi
Karibuni sana hutojuta kutakuwa na ofa yavkitabu cha mapishi pamoja na salads

03/10/2020

Hello habar zenu
Karibuni darasani kujifunza pilipili za biashara aina sita
Kwa buku yako tu

29/08/2020

vilainike
Tia chumvi kiasi, ndimu, rai, bizari zote na pilipili na vichanganye pamoja vizuri.
Kata madonge madonge na yazungushe zungushe katika mikono ili yawe duara
Chukua unga na tia bizari ya majano, chumvi kiasi na maji kiasi
Changanya mchanganyiko huo hadi uchanganyike vizuri uwe mzito mzito
Weka kikaango jikoni na subiri mafuta yapate moto
Kisha chukua donge moja moja na lichovyee lote katika unga ulio tengeneza hakikisha donge hilo limeenea unga huo sehemu yote
Kisha tumbukiza katika kikaango na fanya hivyo kwa madonge mengine yaliyo bakia
Baada ya kumaliza yote tia katika sahani na tayari kwa kuliwa

23/08/2020

My choice

Want your business to be the top-listed Beauty Salon in Dar es Salaam?
Click here to claim your Sponsored Listing.

Category

Telephone

Website

Address


0624251582
Dar Es Salaam
PASSWORD