Mwaga Natural Solution

Mwaga Natural Solution

Share

Tunasaidia wanawake waliojifungua na kunenepa kurudisha umbo (shape) lao la awali wakiwa nyumbani kw

30/08/2021

FAHAMU MAMBO 2 YANAYOONDOA KITAMBI CHAKO UKIWA NYUMBANI KWAKO BILA KUTUMIA GHARAMA YOYOTE.
Achana na elimu ya kuhesabu kalori na kufanya mazoezi magumu kwani haijawahi kufanya kazi kwa watu kabla yako na wala haitakuja kukutendea miujiza kwako badala yake badili mtazamo wako kidogo tu ili uweze kuondoa kitambi chako na upone magonjwa nyemelezi.

Leo nitakufahamisha mambo 2 ambayo yana uwezo wa kutenda miujiza ukiwa nyumbani kwako bila kutumia gharama yoyote au kutumia nguvu nyingi.

Mambo 2 haya yameshawasaidia watu kabla yako na yanaendelea kuwasaidia wanaokuwa serious nayo kwa kuyachukuwa na kuyafanyia kazi.

Kitambi ni kero inayotokana sababu nyingi sana hivyo k**a unahitaji kuiondoa unatakiwa kuzuia vyonzo vyote vya tatizo hili.
Leo nitakufahamisha kwa ufupi mambo 2 makubwa yanayoweza kutokomeza kitambi chako ikiwa utayafatilia kwa moyo mmoja.

1.Chakula gani ule.
Ili uweze kuondoa kero ya kitambi chako unapaswa kuwa na uelewa wa chakula gani sahihi ule na kipi usile.
Huwezi kuondoa kitambi kwa kula chochote kipitacho mbele yako.Jambo hili huwafanya watu wengi kushindwa kudhibiti vitambi vyao kwa kukosa maarifa ya chakula sahihi kwaajili ya kuondoa kitambi.Siku utakayojua vyakula sahihi wakati wa kuondoa kitambi ndiyo siku utakayoanza kuona matokeo chanya kinyume na hapo utaendelea kuteseka.

2.Muda gani ule
Tumekuwa tukifundishwa kuwa kuna milo mikuu 3 na milo midogo midogo kwa siku na tumekuwa tukifanya hivyo kwenye maisha yetu ya kila siku.
Kwakuwa umeshapata changamoto ya kitambi unahitaji kupata maarifa zaidi ya muda sahihi wa kula,madhara na faida ya kula milo mingi na kula muda wowote.
Usipofahamu muda sahihi wa kula hutoweza kudhibiti kero ya kitambi maisha yako yote kwani si kila muda ni sahihi wa kula hasa unapohitaji kuondoa kitambi.
Kwa msaada/ushauri,
Piga/whatsapp 0745327327
ni mtaji

24/08/2021

AINA HII YA MATUNDA NI HATARI UNAPOTAKA KUONDOA KITAMBI.

Vyakula na vinywaji mbalimbali ndiyo sababu kubwa ya wewe kupata kitambi na kushindwa kukiondoa kirahisi.
Hivyo unapohitaji kuondoa kitambi hicho unalazimika kuacha matumizi ya vyakula na vinywaji vilivyopelekea kitambi chako.

Huwezi kudhibiti kitambi huku ukindelea kula vile vile vilivyopelekea upate kitambi hicho.Yaani ni sawa na kutumia dawa za malaria huku ukiendelea kulala bila chandalua(net).

Leo nitakufahamisha kwa ufupi sana matunda usiyotakiwa kula unapotaka kuondoa kitambi ili upate matokeo ya haraka bila kutumia nguvu nyingi.

Acha kutumia matunda yote yanayopelekea uzalishwaji mkubwa wa maji maji yanayotengeneza na kushikilia mafuta mwilini mwako yaani homon ya INSULIN.

Homon ya INSULIN ni homoni inayozalishwa kwa lengo la kuondoa sukari iliyozidi kwenye damu na kuihifadhi k**a mafuta na kuyazuia yasiunguzwe.Kwahiyo matunda yanayopelekea kuzalishwa kwa homon inayonenepesha ni yale yote yenye sukari nyingi mfano nanasi,chungwa,embe,tikiti,fenesi na mengineyo.

Anayehitaji kuondoa kitambi analazimika kuacha matumizi ya matunda ya aina hii mpaka atakapofikia malengo yake ndipo ataendelea kula ila kwa mpangilio mzuri ili kuzuia uzalishwaji wa homon inayonenepesha na kuzuia mafuta.

Kwa msaada/ushauri
Piga/whatsapp 0745327327 BURE
ni mtaji

20/08/2021

Usipomfahamu vizuri adui yako hutopata njia/silaha sahihi ya kumuangamiza badala yake utaishia kujaribu jaribu kila njia bila mafanikio yoyote.

Baada ya kuangalia video hii utagundua jinsi mafuta yanavyotengenezwa na utafahamu njia sahihi ya kuondoa mafuta hayo bila kutumia nguvu nyingi au kutumia gharama kubwa.
Kwa msaada/ushauri,
piga/whatsapp 0745327327
ni mtaji

09/08/2021

MAMBO 5 MUHIMU KUYAFANYA ILI URUDISHE UMBO LAKO BAADA YA KUJIFUNGUA..
Kuna mambo 5 unayopaswa kuyafahamu na kuyatekeleza kwa moyo mmoja ili kuondoa kitambi chako baada ya kujifungua..

1.Jipe muda wa kutosha.
Unachopaswa kukijua kuwa kero au changamoto yako haijaingia siku moja hivyo haiwezi kuondoka siku moja,jipe muda wa kutosha kabla haijatoweka na kurudi kwenye umbile lako la awali.

2.Nyonyesha sana.
K**a kuna jambo ambalo lina msaada mkubwa sana kwenye kuondoa kitambi na nyama zilizotokea mara baada ya kujifungua basi ni kujitahidi kunyonyesha kadri iwezekanavyo.
Kwa kufanya hivyo kuna faida 2 au 3 kubwa,kwanza itakusaidia kuondoa kitambi,pili itamsaidia mtoto kupata maziwa ya kutosha kwani uzalishwaji unaongezeka kulingana na matumizi na tatu mtoto atapata afya njema.

3.Kunywa maji ya kutosha.
Hakikisha unakunywa maji ya kutosha kwani itakusaidia kuondoa sumu na kusaidia uzalishwaji wa kiwango cha juu cha maziwa kwaajili ya mtoto lakini kubwa zaidi itakusaidia kuongeza kasi ya kuondoa kitambi.

4.Kula kiafya.
Kuwa mjamzito au Kunyonyesha siyo kigezo au tiketi ya kula kila kitu.K**a ulifanya kosa hilo wakati wa ujauzito hakikisha hurudii wakati wa unyonyeshaji.Unahitaji kula vyakula vitakavyokusaidia kupungua na kuweka kando vyakula vitakavyopelekea ukwame.
Kula vyakula vya mafuta salama,protini na mboga mboga na ujiepushe na sukari na wanga.

5.Fanya mazoezi.
Kujifungua au kunyonyesha si sababu ya kutoushughulisha mwili wako kwa namna yoyote.Ili uondoe kitambi na manyama ya tumboni unahitaji kuutumikisha mwili wako kwa shughuli ndogo ndogo na mazoezi maalum angalau dakika 30 kwa siku .

Kwa msaada zaidi,
Piga/whatsapp 0745327327
Karibu
ni mtaji

04/08/2021

Hili ni swali ambalo wanawake wengi huuliza na wengine wamekuwa wakitumia njia hii ya kupunguza kiasi cha chakula na kuongeza mazoezi ili warudishe shape zao za awali baada ya kujifungua..
Sikiliza ukweli juu ya dhana hiyo..👆🏼👆🏼
Kwa msaada zaidi
Piga/whatsapp 0745327327
BURE

02/08/2021

Huenda njia uliyotumia ni sahihi ila ulishindwa kuondoa kitambi kwa njia hiyo kwasababu njia hiyo si kwaajili ya kuondoa kitambi.

Usijitese tena.!
Sikiliza video hii ujue kosa lako lipo wapi.

Kwa ushauri zaidi,
Piga/whatsapp 0745327327
BURE
ni mtaji

30/07/2021

K**a wewe ni mama bila shaka neno hili si geni kwako.
Naamini ulishalisikia zaidi na zaidi,lakini kuna ukweli wowote kuhusu neno hili "TUMBO/KITAMBI CHA UZAZI"..?
Tazama video hii kujua ukweli wa neno hili..
Kwa msaada zaidi.
Piga/whatsapp 0745327327
ni mtaji.

24/07/2021

🌴Kushindwa kwa juhudi za kuondoa kitambi kunasababishwa na kutofahamu elimu ya kitambi hasa sababu yake na muundo wake kiujumla..

🌴Kwenye video utajifunza njia 1 pekee na ya uhakika ya kudhibiti kitambi bila kuhatarisha afya yako au kutumia gharama yoyote..

🌴Kwa msaada zaidi,
Whatsapp 0745327327

01/05/2021

FAHAMU SIRI 1 KUBWA YA WANAWAKE WENGI KUSHINDWA KURUDISHA MAUMBILE YAO YA AWALI BAADA YA KUJIFUNGUA LICHA YA KUTUMIA NJIA NYINGI..
Wanawake waliojifungua hutumia njia au programme nyingi sana ili kuhakikisha waumbile yao yanarudi k**a yalivyokuwa kabla ya kujifungua lakini kwa bahati mbaya wanashindwa kabisa licha ya kutumia njia tofauti tofauti ikiwemo kufanya mazoezi mazito.
Wasichokijua wanawake wengi ni kwamba kuna jambo linapaswa kufanywa mwanzo kabla y programme za kuunguza mafuta,jambo hilo ni👇👇👇

KUONDOA SUMU MWILINI.
Hili ni jambo la mwanzo ambalo wanawake wengi wanaofikiria kurudisha maumbile yao ya awali baada ya kujifungua huwa hawalifahamu au husahau kulifanya kabla ya kuanza programme yoyote ya kuunguza mafuta na kurudisha maumbile yao ya awali.
Kwa kawaida mwili hupokea sumu ambazo huingia mwilini kwa njia tofauti tofauti mfano,kupitia hewa tunayovuta,chakula na vinywaji,madawa na bidhaa za urembo zenye kemikali n.k. Pia mwili wenyewe hutengeneza sumu kutokana na shughuli zake za kila siku.
Sumu hizo zinapokosa nafasi ya kutoka hukimbilia sehemu tofauti tofauti hivyo viungo hutengeneza mafuta kuzuia athari zitokanazo na sumu hizo.
Kwahiyo k**a utatumia njia yoyote ya kuondoa mafuta hayo kabla hujaondoa sumu hizo,mafuta hayataondoka na k**a yakiondoka baada ya muda yatarudi tena kwa lengo la kuzuia viungo visidhurike kwa sumu zilizobaki mwilini.
Kwahiyo wewe mwanamke unayetamani kurudisha umbo lako la awali baada ya kujifungua hakikisha unatafuta njia sahihi ya kukusaidia kuunguza mafuta hayo ila kabla ya kutumia njia hiyo ondoa sumu kwanza(detoxification).
Kwa elimu na utatuzi wa shida hii hakikisha unafatilia mfululizo wa mafunzo haya kwenye ukurasa huu ili uweze kufaidika.
Kwa msaada zaidi.
Wasiliana nasi,
0745327327 whatsapp

30/04/2021

HAKUNA TUMBO LA UZAZI,FAHAMU SIRI YA TUMBO/UZITO MKUBWA BAADA YA KUJIFUNGUA..
Wanawake wengi wamekuwa wakikutana na changamoto ya kuwa na tumbo kubwa(tumbo la uzazi k**a ilivyozoeleka) na uzito mkubwa mara baada ya kujifungua na kipindi anaponyenyesha.Mara nyingi wanawake wengi hushindwa kabisa kurudi kwenye maumbile yao ya awali hata baada ya kuacha kunyonyesha.Hili huwaumiza wanawake wengi sana na kujikuta wanatumia njia nyingi ili kurudisha maumbile yao ya awali lakini kwa bahati mbaya wanashindwa kabisa.

Ukweli ni kwamba uzazi si sababu sahihi ya wanawake waliojifungua kuwa na matumbo na uzito mkubwa na kushindwa kurudi kwenye maumbile yao ya awali,bali ipo sababu kubwa sana ambayo wengi huifumbia macho,sababu hiyo ni CHAKULA na mtindo wa maisha kwa ujumla kipindi cha ujauzito na baada ya ujauzito.

Chakula cha mwanamke mwenye ujauzito na anayenyonyesha kina athar kubwa sana kwenye muonekano wake baada ya kujifungua na baada ya kumaliza kunyonyesha.
K**a mtindo wa chakula na maisha kipindi cha ujauzito na kujifungua utakuwa mzuri, hakuna kitambi/tumbo la uzazi(k**a ilivyozoeleka) linaloweza kumuandama mwanamama huyo hata baada ya kuacha kunyonyesha ila ikiwa kinyume na hapo hatoweza kurudi kwenye umbile lake kwa kipindi kirefu au maisha yake yote.
Ni kweli mwanamke anapokuwa mjamzito kuna uzito huwa anaongezeka mbali na uzito wa mtoto na hata baada ya kujifungua lakini uzito huo hautakiwi kuzidi wala kuchukua muda mrefu bila kurudi k**a awali.
Kwa maarifa na ufumbuzi juu ya changamoto hii kwa wakina mama,endelea kufuatilia mfululizo wa nakala zetu hapa hapa na kuuliza maswali k**a utakuwa hujelewa.
Kwa msaada zaidi,
Wasiliana nasi kupitia
0745327327
Ahsante..

29/11/2020

JINSI MAZOEZI KWA MWANAMKE ALIYEJIFUNGUA YANAVYOWEZA KURUDISHA UMBO LAKE LA AWALI.
Wazazi wengi huwa hawafahamu umuhimu wa mazoezi katika kurudisha mvuto wa awali mara baada ya kujifungua ila wengine hupuuzia tu.
Hizi ni faida 5 za mazoezi kwa mwanamke anayehitaji kurudisha umbo lake la awali baada ya kujifungua

1.Huimarisha misuli
Kwa kawaida misuli hulegea baada ya mwanamke kujifungua na kupelekea mafuta kujirundika na kupoteza mvuto wa awali ila mazoezi hupelekea misuli hiyo kurudi katika hali yake ya kawaida na kuifanya iwe imara zaidi na kutoruhusu mafuta kuendelea kujikusanya baada ya kuunguzwa

2.Huongeza nguvu mwilini
Kwa mzazi anayefanya mazoezi huwa tofauti na asiyefanya kwani mwili wake huwa na nguvu(energy) za kutosha kumuwezesha kufanya shughuli mbalimbali bila kuhisi uchovu wa mara kwa mara.Hali hii hupelekea mafuta kuunguzwa na kutumika na kutoruhusu kujikusanya tena kutokana na kuushughulisha mwili mara kwa mara

3.Inazuia unyogovu/unyonge wa uzazi
Mazoezi kwa aliyejifungua ni njia nyepesi na rahisi ya kuondosha unyonge wa uzazi na kujikuta anarejea kwenye hali yake ya kawaida haraka zaidi kwani hali hii hupelekea kukaa bila kujishughulisha na shughuli yoyote jambo ambalo huongeza hatari ya kuongezeka kwa uzito wa mwili na kupoteza umbo la awali.

4.Hupelekea usingizi mnono
Moja ya mambo muhimu kwa wanawake waliojifungua na kuhitaji kurudisha miili yao k**a ilivyokuwa kabla ya kujifungua ni kupumzika kwa muda unaohitajika(kulala na kuamka mapema) hivyo mazoezi husaidia wanawake waliojifungua kupata usingizi mnono na kuamka mapema kwa ajili ya shughuli ndogo ndogo ambazo husaidia kurudisha miili yao ya awali kirahisi

5.Huondoa msongo wa mawazo(stress)
K**a tunavyofahamu msongo wa mawazo ni moja ya sababu nyingi zinazopelekea uzito kuongezeka kwani muhusika hutumia muda mwingi kufikiri kuliko kujishughulisha kwwnye shughuli mbalimbali hivyo mazoezi huwaweka mbali (wanawake waliojifungua) na msongo wa mawazo na hofu hivyo kurahisisha safari ya kurudisha shape zao zilizotoweka baada ya kujifungua.
Kwa msaada zaidi
Wasiliana nasi
Whatsapp 0745327327

28/11/2020

AINA 2 ZA VYAKULA VINAVYOPELEKEA USHINDWE KURUDISHA UMBO(SHAPE) LAKO LA AWALI BAADA YA KUJIFUNGUA.
K**a umejifungua na unahitaji kurudisha umbo lako la mwanzo lazima uzingatie chakula unachokula kwanza.
Wanawake wengi waliojifungua wamekosa elimu hii hivyo wamejikuta wakishindwa kurudisha maumbo yao ya awali pale wanapohitaji.

Kuna aina 2 ya vyakula hupaswi kutumia/kutumia kwa kiasi kikubwa k**a unahitaji matokeo mazuri,ambavyo ni sukari(sweet) na wanga(carbohydrates) ambavyo k**a vikitumika/kuliwa kwa wingi hupelekea kuzalishwa na kuhifadhiwa kwa mafuta mwilini na kukwamisha juhudi zote za wanawake waliojifungua kurudisha shape zao za awali.
Hivyo k**a wewe ni mwanamke unayehitaji kuanza safari ya kurudisha umbo lako la awali PUNGUZA ulaji wa vyakula vya sukari na wanga au ACHA kabisa na uanze kutumia vyakula vya mafuta asilia,protein asilia,matunda na mbogamboga kwa wingi hivyo vitakusaidia kurudisha umbo lako kwa urahisi baada ya kujifungua bila kuathiri afya ya mtoto na kwako pia.

Kwa msaada zaidi
Wasiliana nasi
Whatsapp 0745327327

Want your business to be the top-listed Beauty Salon in Dar es Salaam?
Click here to claim your Sponsored Listing.

Category

Address


Dar Es Salaam