Health Talk

Health Talk

Share

Ni mshauri wa afya. Nawasaidia wenye changamoto ya Ngozi pamoja na changamoto ya kitambi, uzito mkubwa na nyama uzembe kwa kutoa ushauri na suluhisho sahihi.

14/03/2023

Kwanini ngozi yako haivutii na kwanini ngozi yako haina Afya na Mvuto wa Asili.
👉Hautumii mlo wenye kuleta Afya.
Vitu unavyokula vinamchango mkubwa sana katika Afya yako na ngozi pia. Ila kupata ngozi nzuri na laini, nyororo na inayong'aa inabidi Vyakula na vinywaji vinavyotengenezwa viwandani, wanga, mafuta na sukari na badala yake kula protini, matunda, mboga za majani na kunywa maji kwa wingi.
Hakikisha unakunywa maji si chini ya glasi 8 kwa siku na matunda pamoja na mboga za majani kila unapopata mlo.
Matunda na mboga za majani vinasaidia oksijeni kuzunguka vizuri mwilini mwako na kwenye ngozi kuliko mafuta au kipodozi chochote unachoweza kupaka.
Protini inakusaidia kujenga ulinzi zaidi katika seli za ngozi ambayo ngozi yako inahitaji kukabiliana na ukavu wa ngozi. Maji nayo yanakusaidia kufanya mzunguko wako wa damu kuwa vizuri na vinakusaidia vinyweleo vyako kupumua vizuri hivyo kuzuia bakteria chini ya ngozi.
👉Haupati mda wa kutosha kupumzika. Hakikisha unapata mda wa kutosha kulala usiopungua masaa 8. Kwanini nasema hivyo ni kwasababu mda mwingi wakati wa Mchana Ngozi inafanya kazi kubwa kukabiliana na mionzi ya jua, kukabiliana na vijidudu mbalimbali k**a bakteria na virusi na kutizamia joto la mwili. Kwahiyo ngozi yako hujijenga wakati umepumzika ili kuweza kuendelea kuchunga mwili wako ipasavyo.
👉Haufanyi Usafi vizuri wa ngozi yako.
Ndio maana unapata hata ukurutu au kutoa harufu mbaya.
Fanyia usafi mwili wako kwanzia juu hadi chini kwa siku oga au safisha mwili wako hata mara mbili kwa siku na uhakikishe umefanya usafi vizuri na baada ya hapo tumia mafuta ili kuiacha ngozi yako iwe vizuri. Na kwa ushauri wangu nakushauri wakati umeoga usiku tumia mafuta ya n**i au Vaseline ni mazuri sana kwa afya yako ya ngozi hasa pale mwili wako unapokua umetulia na sio kujipaka vipodozi vikali kwani uharibu ngozi.
👉Haufanyi mazoezi. mwili unahitaji kufanyishwa mazoezi either ukimbie nk. Wasiliana nasi kupitia 0743324708 ili upate msaada zaidi

12/02/2023

Ni sababu zipi basi zinafanya ngozi ya mwili wako kuwa na makunyanzi. Kuna baadhi ya sababu zinaweza kuzuilika na kuna ambazo haziwezi kuzuilika na sababu hizo ni:

👉Umri: Unapozidi kuwa Mkubwa ngozi yako hupunguza uwezo wa kunyumbuka na kuwa ngumu. Utendaji kazi wa seli mpya hupungua na kufanya tabaka la chini ya ngozi yako kupungua unene wake.
Pia kupungua kwa utengenezaji wa mafuta hufanya ngozi yako ikauke kwahiyo mafuta yakipungua kwenye ngozi (maana ngozi inaasili ya kujitengenezea mafuta yake) Inafanya ngozi yako kulegea na kutengeneza vijibonde na kufanya mistari ionekane juu ya ngozi yako.

👉Mionzi ya jua (Ultraviolet light UV).
Mionzi ya jua inaongeza kasi ya kuzeeka na hiki ndicho chanzo kikubwa cha kufanya makunyanzi katika ngozi yako. Kwanini nasema hivyo ni kwasababu mionzi hiyo inapoingia kwenye ngozi yako huenda kuvunja collagen na elastin (Hii huleta uimara wa ngozi yako). Ngozi huanza kulegea na makunyanzi hutokea katika ngozi yako. Kwahiyo unapovaa kofia kubwa na kuvaa nguo zinazofunika sehem za mwili husaidia kutokupata makunyanzi haraka.

👉Uvutaji wa Tumbaku. Unapovuta tumbaku unapunguza kiwango cha damu kinachotakiwa kuifikia ngozi yako kwa kupunguza kipenyo cha mishipa ya damu inayoelekea kwenye matabaka ya juu ya ngozi. Pia tumbaku imetengenezwa na kemikali na hizo kemikali zinaharibu collagen na Elastin.

👉Unapojikunjakunja mara kwa mara wakati wa kuonyesha hisia zako.
Mistari ya juu ya kope za macho na inayoanzia kwenye kona za macho huwazinajenga mistari (Mikunjo) kutokana na kuonesha hisia kwa vitendo. K**a vile kukunja sura kuonyesha umekasirika pia kukonyeza yanachangia katika kuleta makunyanzi ya ngozi yako.

Kwa ushauri zaidi wasiliana nasi kupitia 0743324708 au tuma neno AFYA nawe utasaidiwa kwa haraka sana.

10/02/2023

*Mambo matatu muhimu ya kupungua uzito*

Hellow habarini za wakatu huu natumai wote mmeamka salama na mnaendelea vizuri na majukumu yenu Mungu awabariki katika kila kitu mnachokifanya.

Siku ya leo unatakiwa kujua mambo matatu nitakayo zungumza nawe yatakusaidia sana katika safari yako ya kupungua uzito.

Najua unatamani sana kupungua uzito na umetumia njia nyingi sana na umekata tamaa kwahiyo umeamua kuendelea kustahimili mwili wako k**a ulivyo.

Sasa basi leo nitakuelekeza vitu muhimu ambavyo unatakiwa uvijue kabla ya kuanza kupunguza uzito.

👉Jambo la kwanza na muhimu ni *Nidhamu*.
Kwanini nasema ivyo ni kwasababu watu wengi ambao wanatamani kupungua huwa hawana nidhamu katika malengo yao ya kupungua uzito.

Fatilia malengo yako kila siku ukiamka jua unataka kufanya nini napia panga ratiba zako vizuri kwamba nikiamka au nikitoka kazini nitafanya mazoezi au nitakwenda gym na ukiendelea kuweka nidhamu katika hili utaona mafanikio makubwa sana. Nafahamu kwa mtu ambae anatamani kupungua akianza mazoezi ndani ya week moja akiona hamna dalili yoyote ya kupungua anaacha anasahau Nidhamu ni kila kitu inahitaji muda ili uweze kupungua.

👉 Kuwa Committed au focus kwenye malengo yako. Tafuta Hamasa tafuta kitu ambacho kitakua kinaku inspire wewe kupungua uzito tamani kupungua nitakua nashare nanyi shuhuda mbalimbali za walio pungua ni wengi sana walio pungua na hiyo itakua inakupa hamasa ya wewe kutamani na kujua kua utapungua.

👉 Kua na Kiu au passion. Ukiwa na kiu ya kupungua yani unafata maelekezo unafanya mazoezi na kuacha baadhi ya tabia ambazo zinakupelekea kua mnene hakika utapungua. Kiu yako wewe ndio utakupelekea kupungua ila usipokua na Kiu usipo tamani kupungua hakika utaishia kuwaona wenzio wanatoa shuhuda za kupunguza kilo 5 mpaka 10 na kitu uko wewe upo pale pale..

Kwa ushauri zaidi na ukaribu ili kuweza kuondokana na changamoto yako wasiliana nasi kupitia 0743324708 au Tuma ujumbe wenye neno UZITO nawe utasaidiwa

Want your business to be the top-listed Beauty Salon in Dar es Salaam?
Click here to claim your Sponsored Listing.

Address


Makumbusho, Tanzanite Tower
Dar Es Salaam