afyatips.1
Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from afyatips.1, Health/Beauty, Dar es Salaam.
10/02/2022
Kuziba mirija ya uzazi (fallopian tube obstruction)
Kuziba mirija ya uzazi mara nyingi haina dalili nyingi zaidi ya kushindwa kupata mimba. Wengine huhisi kuuma tumbo mara kwa mara.
Ni madhara ambayo yanatokea baada ya kuwa na maambukizi yasiyotibika kkwa mda mrefu. Pia inaweza kusababisha mimba kutunga nje ya mji wa uzazi (ectopic pregnancy)
Baadhi ya sababu za mirija kuziba Maambukizi ya mda mrefu kwenye mfumo wa uzazi (PID) Magonjwa ya ngono ie gonorrhoea Historia ya kufanya upasuaji kwenye mfumo wa uzazi Kujaa maji kwenye mirija
Unawezaje kujua kuwa mirija imeziba?
Vipimo ambavyo unaweza fanya kujua k**a mirija imeziba HSG Ultrasound Laparascopy
Una shida yeyote kwenye mfumo wa uzazi? tupo kwa ajili yako, bonyeza link ya whatsap kwenye bio itakupeleka mojakwamoja whatsap tukusikilize tukusaidie
10/02/2022
P 2 ni dawa ya kudhibiti uzazi ambayo hutumika kwa dharura endapo umefanya mapenzi katika siku za hatari na au umebakwa na haupo tayari kubeba mimba
Baadhi ya wanawake wamekua wakutumia hii dawa kiholela jambo ambalo linasababisha Athari mbaya katika uzazi wa mwanamke
Sitakiwi kutumia P2!! Kwani inamadhara gani?
1. Hupelekea maumivu makali chini ya kitovu, mgongo na kiuno wakati wa hedhi.
2. Kuvurugika kwa hedhi hasa kuwahi Sana kupata au kuchelewa kupata hedhi.
3. Hedhi kutoka ikiwa nzito, kidogo au nyingi.
4. Mimba kutunga nje ya mfuko wa uzazi na kupata shida baadae kwenye kupata mtoto.
5. Homa, Kichefuchefu, kizunguzungu,kuchoka na tumbo kuvurugika.
6. Damu huweza kutoka kidogo siku 1 au mbili baada ya kutumia P2.
K**a wewe ni muhanga wa kutumia p2 mara Kwa Mara na umepata mabadiliko ya homoni au shida yoyote Ile Kwenye kizazi Nipigie NIKUPE USHAURI NA SULUHISHO
Nipigie au Whatsap +255 629 888 746
09/02/2022
TATIZO LA UTOKWAJI WA UCHAFU KATIKA VIA VYA UZAZI VYA WANAWAKE
Kwa kawaida wanawake hutokwa na ute katika via vya uzazi na hasa wale waliopevuka na kuwa na uwezo wa kuzaa. Hii ni njia moja wapo ya kutoa uchafu au sumu mwilini. Hali hii ya ute kutoka huwa si ngeni na ni kawaida kabisa kwa wanawake wenye uwezo wa kuzaa.
Ute huu mara nyingi huwa hauna rangi ili kuutambua ni mpaka ukauke katika nguo za ndani. Ikumbukwe kuwa ute huu huwa ni kwa kiasi kidogo tu na hautoki mfululizo.
Majimaji ninayoyazungumzia yanaambatana na dalili mbalimbali k**a vile:-
1. Kuna wakati mwanamke hutokwa na majimaji yenye harufu mbaya na harufu hii haitoki hata k**a mwanamke huyo akioga na kubadili mavazi. Pia harufu hiyo huwa kali zaidi pale mwanamke huyo anaposhiriki tendo la ndoa na mwenzi wake kitu kinachofanya asifurahie raha ya tendo la ndoa.
2. Maumivu wakati wa kushiriki tendo la ndoa. Ni wanawake wengi sana wanatokwa na majimaji machafu katika njia ya via vyao vya uzazi, na wanaposhiriki tendo la ndoa na wenzi wao hupata maumivu makali sana kiasi ambacho wanashindwa kufurahia tendo la ndoa.
3. Majimaji hayo huwa na rangi k**a maziwa mtindi. Kwa urahisi majimaji hayo huwa na rangi ya usaha, kumbuka ute wakawaida unatambulika rangi yake mpaka ukauke kwenye nguo za ndani lakini ute huu unajibainisha waziwazi kwa kuwa na rangi hiyo ya usaha.
4. Maumivu wakati wakujisaidia haja ndogo. Kuna wanawake kila anapohisi kwenda haja ndogo anajuta kwani anapata maumivu makali sana huku akiona kuna majimaji huwa yanamtoka katika via vya uzazi lakini bado hiyo hali haimbabaishi anaendele kuvumilia na kuona ni kawaida.
Mwanamke akiona dalili hizi atambue hali hiyo si ya kawaida na ni kuna uwezekano akawa na maambukizi ya fangasi katika via vyake vya uzazi. Ni vema awahi kuwaona wataalamu wa afya ili afanyiwe vipimo na kupata matibabu.
09/02/2022
MAAMBUKIZI YA FANGASI SUGU NA INAYOJIRUDIA RUDIA - VYANZO NA KINGA.
Fangasi Inasababishwa na jamii ya fungi anaitwa CANDIDA. Seli za fangasi na bacteria wazuri huishi ukeni bila tatizo lolote. Tatizo linakuja endapo ukuaji wa fangasi hawa ukeni watakuwa wengi kushinda wazuri. Basi hapo ndio inapotokea ugonjwa wa fangas na miwasho mingi.
K**a unapata maambukizi ya fangasi zaidi ya mara nne kwa mwaka basi kitaalamu hali hii hiyo hujulikana k**a vulvovaginal candidiasis (fangasi sugu au inayojirudia rudia). Na ni hatari sana K**a ukichelewa kuipatia matibabu sahihi mapema kwani upelekea tatizo la PID ambalo nalo upelekea tatizo la UGUMBA Kwa wanawake wengi asa kwa sasa.
VYANZO VYA FANGASI SUGU/INAYOJIRUDIARUDIA;
Zipo sababu kadhaa zinazoweza kupelekea fangasi kuwa sugu/kujirudia rudia. Sababu hizo ni:-
1. Vitu vinavyoweza kusababisha mvurugiko wa homoni k**a ujauzito, dawa za uzazi wa mpango, na matibabu ya estrogen.
2. Matumizi ya mara kwa mara ya antibiotic ambazo huondoa bakteria ambao husaidia kupunguza idadi ya candida.
3. Magonjwa yanayoshambulia kinga ya mwili k**a VVU (HIV)
4. Unene, unaoweza kusababisha joto na unyevu mazingira yanayofanya candida kuongezeka kwa wingi.
-
DALILI ZA FANGASI SUGU.
— Kuwa na miwasho sehemu za siri mara kwa mara.
— Vipele vidogo vidogo ukeni.
— Vidonda au kuwa na michubuko ukeni.
— Kutokwa na harufu mbaya ukeni.
— Kupatwa na maumivu makali wakati wa tendo la ndoa.
— Kuvimba au kuwa mwekundu katika mdomo wa nje ya uke.
— Kuwaka moto ndani na nje ya uke.
— Maumivu ya misuli na tumbo hasa chini ya kitovu.
— Maumivu ya kiuno.
— Kuhisi kuwaka moto sehemu za siri baada ya tendo la ndoa.
— Kutokwa na uchafu wa rangi nyeupe au kijivu unaoweza kuwa mwepesi au mzito au majimaji.
-
JINSI YA KUJIKINGA DHIDI YA MAAMBUKIZI YA FANGASI YANAYOJIRUDIARUDIA.
▶️ Vaa nguo za ndani zilizotengenezwa na pamba.
▶️ Epuka nguo za kubana.
▶️ Jisafishe kutoka mbele kwenda nyuma baada ya kujisaidia haja kubwa.
▶️ Tumia antibiotics pale tu unaposhauriwa na daktari.
▶️ Epuka kujisafisha kwa kuingiza vidole kwenye via vya uzazi.
▶️ Epuka kufanya mapenzi hadi utakapopona maambukizi ya FANGASI.
Kwa msaada zaidi tutafute whatsap link kwenye bio
07/02/2022
06/02/2022
Polycystic ovarian syndrome (Pcos)
Hivi ni vimbe vidogo vidogo kwenye mfuko wa mayai (vivimbe maji) havijawa uvimbe kamili vikipimwa huonekana k**a malengelenge vinaweza kuwa vingi vingi vomekusanyana bado lakin havijawa Ovarian cyst tayri ambavyo ni uvimbe kwenye mfuko wa mayai ovaries.
Mwanamke mwenye tatizo hili ni anapitia ugumu wa kubeba ujauzito kwa wakati au unaweza kubeba ukaishia kupata miscarriage
Na hivyo vyote source kubwa ya matatizo haya ni mvurugiko wa hormones (Hormonal imbalance )
Tiba ya tatizo hili inabidi iendane sambamba na kupangilia mlo vizuri ili tatizo lisijirudie.
23/01/2022
Usisubir kupata madhara zaidi nipigie tuongee +255629888746
23/01/2022
Kuna wengine Wanapiga ultrasound Tu wakijua ndo kipimo Pekee( na akiambiwa Kizazi kipo vizuri ana relax kabisa), na wanajua wamechunguzwa ndo mwisho.
Hapana vipimo vipo vingi kuna kipimo cha mirija,kuna antibodies,kuna Homon mbali mbal
Vyanzo vya kutopata Mimba Ni Vingi,unaweza kuta chanzo ni kutoivisha mayai bora au kutopevusha mayai kabisa,yaan siku za hatari panakuwa hakuna YAI, haya yote huwa hospitali za kawaida Hawacheck haya...,
Lakin pia unakuta kachunguzwa mwanamke TU, mwanaume Hajachunguzwa, just kwa sababu amewah zaa na mwanamke mwingine, au Anasimamisha vizuri na kupiga goli 3 na kukojoa basi anaonekana hana matatizo, SI KWELI.anaweza kuwa anakojoa Vizuri lakin MBEGU kwenye yale maji maji, manii HAZINA UBORA....
Wewe hali ikoje?,mmefanya vipimo wote? wote HAMNA SHIDA kwa vipimo lakini bado hamjafanikiwa Kupata MTOTO? Mwanaume anasperm count ndogo?
halimayat ana jibu la shida yako, atakusaidia.
DM me.
22/01/2022
Tatizo la wanawake kupata maumivu makali wakati wa kushiriki tendo la ndoa limekua likiwasumbua wanawake wengi na wengine huona ni hali ya kawaida. Wanaume wengine huamini mwanamke anapopata maumivu makali wa tendo la ndoa basi inaonesha mwanaume huyo ana uwezo mzuri katika kushiriki tendo la ndoa.
UKWELI NI KWAMBA mwanamke anapopata maumivu makali kabla wakati au baada ya tendo la ndoa ni dalili ya matatizo katika afya yake ya uzazi ni vema akachukua hatua mapema ya kupata matibabu.
Zifuatazo ni baadhi ya sababu zipelekeazo mwanamke kupata maumivu makali wakati wa tendo la ndoa.
• Kukak**aa kwa misuli ya uke (Vaginismus), hali hii inasababishwa na mkazo katika misuli ya uke inayotakana na hofu ya maumivu au majeraha.
• Matatizo ya shingo ya kizazi, Wakati mwingine uume unaweza kuingia ndani zaidi hivyo kugusa shingo ya kizazi. Iwapo mwanamke ana maambukizi huisi maumivu mara shingo ya kizazi inapogusana na uume.
• Matatizo katika mfuko wa uzazi, Matatizo k**a fibroids yanaweza pia kuwa sababu ya maumivu wakati wa ngono.
• Maambukizi ya uke, aina yoyote ya maambukizi ya uke k**a vile maambukizi ya fangasi inaweza kusababisha maumivu wakati wa kujamiiana.
• Kuumia uke, majeraha kutokana na sababu kadhaa mfano kuchanika wakati wa kujifungua au kuongeza njia katika msamba wakati wa kujifungua.
• Endometriosis, Hii ni hali ambayo inasababisha tishu za mji wa mimba kukua nje ya mfuko wa uzazi, na hivyo kuchochea maumivu wakati wa kukutana kimwili.
• Maambukizi kwenye funga nyonga(PID), Viungo kwenye nyonga vinaweza kupata maambukizi hivyo kusababisha maumivu wakati wa ngono.
• Matatizo ya o***y, Matatizo haya ni pamoja na uvimbe kwenye mfuko wa mayai (ovarian cyst)
• Ukavu wa uke, wanawake wenye matatizo ya homoni hukumbwa na tatizo la kuwa na uke mkavu hali hii hupelekea maumbile yao yanasinyaa na kuwa kavu, hivyo kuchochea maumivu wakati wa tendo la ndoa.
• Magonjwa ya zinaa, magonjwa ya zinaa k**a malengelenge (herpes), masundosundo n.k, yanaweza kusababisha maumivu wakati wa ngono.
Tatizo hili linatibika vizuri tuna Virutubisho tiba nzuri sana ya kukusaidia na kuondoa tatizo hili. Ni dawa zinazotokana na mimea tiba na matunda.+255 629 888 746
Click here to claim your Sponsored Listing.
Category
Website
Address
Dar Es Salaam
