bf suma
Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from bf suma, Health/Beauty, p. o. box 123, Dar es Salaam.
14/11/2025
✨ MAMBO AMBAYO HUTAKIWI KUYAFANYA WAKATI WA KUJIFUNGUA ✨
Wakati wa kujifungua ni hatua ya kipekee ambayo mama mjamzito huingoja kwa hamu kubwa baada ya kuvumilia miezi 9 au zaidi.
Huu ni muda wa kutulia, kutia moyo na kuzingatia hatua ya mwisho ya safari ya ujauzito.
Lakini kumbuka, kuna mambo ambayo hupaswi kuyafanya unapokaribia kujifungua 👇
---
1️⃣ KUTOKULA VYAKULA VYA MAFUTA
Katika kipindi hiki mfumo wa umeng’enyaji huwa dhaifu. Kula vyakula vya mafuta au vizito kunaweza kusababisha usumbufu na kutapika.
👉 Badala yake, pendelea matunda, yogurt na kunywa maji mengi.
---
2️⃣ KUTOKULAZIMISHA KUSUKUMA (PUSH)
Kujifungua ni mchakato wa asili uliopangwa na mwili. Usijilazimishe kusukuma kabla ya wakati wake.
👉 Fuata maelekezo ya daktari au mkunga, badilisha staili za kulala, lakini epuka kulala chali au tumbo. Inashauriwa ulale kiubavu.
---
3️⃣ KUPIGA MAKELELE
Wakati mwingine mama anaweza kujikuta akipiga kelele kwa maumivu. Lakini kupiga kelele hupunguza nguvu ambazo zingetumika kusukuma.
👉 Jaribu kutuliza akili na kuelekeza nguvu zako kwenye mchakato wa kujifungua.
---
👩🏽⚕️ Ushauri wa Daktari:
Wakati wa kujifungua, usalama na utulivu wako ni kipaumbele. Sikiliza mwili wako, zingatia ushauri wa wataalamu na utulie — safari ya kuwa mama ipo karibu kufika mwisho kwa ushindi. ❤️
Kwa msaada wa haraka na ushauri
Karibu WhatsApp & piga
Madam jesca 0614051991
14/11/2025
✅ VIDONDA VYA TUMBO (PEPTIC ULCER DISEASE)– JINSI YA KUTIBU VIDONDA VYA TUMBO
Vidonda vya tumbo ni jeraha au mmomonyoko kwenye ukuta wa tumbo au utumbo mdogo unaosababishwa na acid nyingi au bakteria wa H. pylori. Hali hii husababisha maumivu, kiungulia, gesi, kukosa hamu ya kula, kichefuchefu na uchovu wa mara kwa mara. Mara nyingi maumivu huzidi ukichelewa kula, au unapokula vyakula vyenye viungo, chai kali, kahawa, soda, pombe au sigara.
Kila mtu anayeendelea kupuuza huongeza hatari ya:
Kupasuka kwa ukuta wa tumbo (perforation)
Kutokwa damu ndani kwa ndani
Upungufu wa damu na kupungua uzito
Maambukizi makubwa tumboni
Saratani ya tumbo kwa vidonda sugu
Hii siyo hali ya kufumbia macho.
Mtu akianza kuona dalili za maumivu ya mara kwa mara, kiungulia kingi, gesi isiyoisha, au anatapika damu / choo chenye damu, anahitaji kuanza hatua za matibabu mapema kabla haijawa mbaya zaidi.
✅ Badilisha ulaji na epuka viungo vikali, pombe, soda, chai kali, kahawa na tumbaku
✅ Kula kwa wakati na kunywa maji ya kutosha
✅ Epuka kutumia dawa za maumivu hovyo
✅ Fanya vipimo na upate ushauri sahihi wa kitabibu
Kumbuka: Vidonda vya tumbo vinapona kabisa endapo chanzo kinadhibitiwa na matibabu sahihi yanaanza kwa wakati.
K**a wewe au mtu unayemjua unateseka na changamoto hizi, usisubiri hali iwe mbaya – jichukue hatua mapema kwa ushauri na tiba sahihi.
Kwa msaada wa haraka na ushauri
Karibu WhatsApp & piga
0614051991
C9 & F15 Package Kusaidia Kusafisha Mwili Na Kupunguza Uzito
Collagen Kusaidia Kwenye Ngozi, Kucha, Joints Na Nywele
Berry Nectar Husaidia Kwenye Ngozi, Kutoa Taka Pia Kwa Njia ya Mkojo Nzuri Sana Kwa Wanawake Na Wanaume
kwa Maelezo Zaid Wasialiana Nasi 0614051991
28/10/2025
🧬 Collagen ni nini kwa ufupi
Collagen ni protini inayopatikana kwa wingi mwilini — inaunda sehemu kubwa ya ngozi, mifupa, misuli, mishipa, na tishu unganishi. Kadri mtu anavyozeeka, mwili huzalisha collagen kidogo, na hivyo kuleta dalili za uzee k**a ngozi kulegea, mikunjo, na maumivu ya viungo.
🌊 Marine collagen ni nini hasa
Marine collagen hutengenezwa kwa kutumia peptides kutoka kwa collagen ya samaki. Peptides hizi ni molekuli ndogo zinazoyeyuka vizuri na kufyonzwa kwa urahisi zaidi na mwili kuliko collagen kutoka kwa wanyama wa nchi kavu (k**a ng’ombe au nguruwe).
💪 Faida kuu za marine collagen
Huimarisha ngozi
Husaidia kupunguza mikunjo na kuongeza unyevu wa ngozi.
Inasaidia ngozi kuwa laini na yenye mwonekano mchanga.
Huimarisha nywele na kucha
Hupunguza kukatika kwa nywele na kucha dhaifu.
Huchochea ukuaji wa nywele zenye afya.
Husaidia viungo na mifupa
Hupunguza maumivu ya viungo na kuboresha uhamaji, hasa kwa watu wazee au wanaofanya mazoezi mengi.
Huongeza uimara wa misuli
Inaweza kusaidia kujenga misuli na kurejesha tishu baada ya mazoezi.
Huweza kusaidia mmeng’enyo wa chakula
Baadhi ya tafiti zinaonyesha collagen inaweza kusaidia utando wa njia ya mmeng’enyo (gut lining).
⚖️ Jinsi ya kutumia
Marine collagen hupatikana k**a poda, vidonge, au vinywaji.
Inashauriwa kuchukua gramu 5–10 kwa siku, kutegemea bidhaa na maelekezo ya mtengenezaji.
Unaweza kuchanganya kwenye maji, juisi, chai, au smoothie.
⚠️ Tahadhari
Watu wenye allergy ya samaki au dagaa hawapaswi kutumia.
Ni vyema kushauriana na daktari kabla ya kuanza virutubisho
Kwa maelezo zaidi 0614051991
C9 CHALLENGE IMERUDI !!!
Na safari hii, imerudi kwa kishindo kikubwa zaidi!
afya yako Ni siku pekee - lakini zenye nguvu ya kubadilisha na kuboresha mwili wako ndani na nje!
Just
■ Kwa wewe unayetaka:
■Kusafisha mwili (detox)
■Kupunguza uzito au kitambi
Keep Kujiamini zaidi na kuwa na mwonekano bora
Huu ndio mwanzo mpya wa safari yako ya afya!
Ungana na mamia ya watu waliothubutu na sasa wanafurahia matokeo bora kupitia
24 Tunaanza rasmi tarehe 8 November!
Usikose nafasi hii ya kubadilika kabla ya mwaka kuisha!
Kupitia C9 CHALLENGE, utapata:
Mwongozo kamili wa kutumia C9 hatua kwa hatua
Mwongozo wa lishe sahihi kwa matokeo bora
Mazoezi mepesi unayoweza kufanya ukiwa nyumbani
Inawezekana ulishawahi kujaribu kupunguza uzito ukashindwa...
Lakini safari hii usiache nafasi hii ikupite!
Chukua hatua leo!
Pata C9 yako, na tuanze pamoja safari ya:
Kupunguza uzito
Kwa maelezo zaidi wasilaina nasi 0614051991
11/10/2024
*HIVI UNAFAHAMU YA KWAMBA UNENE ULIOPITILIZA UNAATHIRI PIA MFUMO WA AFYA YA UZAZI?*
Na Hivi Ndivyo Inavyokuwa
*Kwa Wanawake Unene Uliopitiliza Unaathiri Afya Ya Uzazi Kwa Namna Hii*
* 1) Ni Hormonal Imbalance;* Wingi Wa Mafuta Yaliyopo Mwilini Unasababisha Mfurugiko Wa Hormones Mbali Mbali Ikiwemo Na Hormone Ya K**e (Estrogen) Na Hii Husababisha Mvurugiko Wa Siku Za Hedhi, Kutokupata Hedhi Kabisa Na Hivyo Kufanya Mchakato Mzima Wa Kubeba Ujauzito Kuwa Mgumu
*. 2), Unapunguza Uwezo Wa Uchavushwaji Wa Mayai;* Tafiti Zinaonyesha Kwamba Asilimia Kubwa Ya Wanawake Wenye Unene Uliopitiliza Wana Uwezekano Mdogo Sana Wa Kubeba Ujauzito Ukilinganisha Na Wale Wasio Na Unene Uliopitiliza Na Pia Uzito Na Unene Uliopitiliza Unaongeza Uwezekano Wa Kupata Changamoto Zinazotokea Kipindi Cha Ujauzito K**a Vile Kuharibika Kwa Mimba (Miscariage), Hypertension N.K
*Kwa Wanaume Unaathiri Kwa Namna Hii*
*1) Ni Mabadiliko Ya Hormones;* Unene Uliopitiliza Unaathiri Uzalishwaji Na Utendaji Kazi Wa Hormones Ya Kiume (Testosterone) Ambayo Huathiri Ubora Wa Mbegu Pamoja Na Mchakato Mzima Wa Tendo
* 2)Unene Uliopitiliza Unachochea Tatizo La Erectile Dysfunction (ED);* Hii Inatokana Na Matatizo K**a Magonjwa Ya Mfumo Wa Mzunguko Wa Mzunguko Wa Damu, Sukari, Pressure N.K Yote Haya Yanachochea ED
Hivyo Basi Kwa Pande Zote Mbili (Wanawake & Wanaume) Uzito/Unene Uliopitiliza Una Madhara Makubwa Sana Na Kupunguza Na Kudhibiti Uzito Wako Ni Njia Sahihi Ya Kujiepusha Na Madhara Haya Yote
11/10/2024
Unywaji Wa Maji Ni Muhimu Sana Kila Siku Sio Tu Kwenye Safari Yako Ya Kupungua Bali Kwa Afya Yako Kwa Ujumla
Kumbuka Zaidi Ya 70% Ya Mwili Wako Ni Maji
Pia Unywaji Wa Maji Ni Tabia K**a Ilivyo Tabia Zingine Na Tabia Huwa Inajengwa Haiji Tu Yenyewe Ndio Sababu Kuna Watu Wanapitisha Siku Bila Hata Kunywa Lita 1 Ya Maji Kwa Sababu Hawajajijengea Hiyo Tabia
Siku Zote Ili Tabia Ijengeke Ni Lazima Mazingira Yawe Supportive Sasa Usitegemee Utakunywa Maji Kiasi Cha Kutosha K**a Mahali Unapokaa (Nyumbani Au Ofisini) Hakuna Hata Maji Karibu
K**a Unataka Iwe Rahisi Basi Hakikisha Hukai Mbali Na Maji Yako
Muda Mwingine Inakuwa Rahisi Kujikuta Umeshakunywa Chupa Ya Soda Au Kinywaji Chochote Kisicho Na Faida Kwako Kwa Sababu Ndicho Unaweza Kukipata Kirahisi (Upo Karibu Nacho)
K**a Mimi Ninatumia Hii Chupa Inanisaidia Kutrack Na Kujua Leo Nimekunywa Maji Kiasi Gani, Unaweza Kutafuta Ya Kwako Pia Ili Iwe Rahisi Kujua Unakunywa Maji Kiasi Gani Kwa Siku Na K**a Yanatosha Au La
Ni Ngumu Sana Kujua K**a Umekunywa Kiasi Cha Kutosha Au La Iwapo Huna Kipimo Kinachokuonyesha Umekunywa Kiasi Gani
Zipo Chupa Nyingi Sana Na Ni Rahisi Sana Kubeba Hata K**a Unaenda Kazini Au Popote Pale Hata Ukiwa Nyumbani Itumie Usifanye Tu Kimazoea Zoea
Fanya Hivyo Kisha Utaona Namna Ambavyo Lifestyle Yako Itabadilika
12/05/2023
Click here to claim your Sponsored Listing.
Category
Contact the business
Telephone
Website
Address
P. O. Box 123
Dar Es Salaam
