AFYA BORA
Ninawasaidia wanawake kutatua Shida mbalimbali za Uzazi kwa njia Rahisi na salama
*FAHAMU SABABU ZA MWANAMKE KUTOA UCHAFU NA HARUFU MBAYA UKENI*
Ni matumaini nyote mnaendelea vyema, Leo naona ni bora tukazungumzia tatizo la kutokwa na Uchafu wenye harufu mbaya ukeni,
✍🏻Kutokwa na harufu mbaya ukeni ni moja ya topic zinazokera na ngumu kuongeleka kutokana na kwamba wanawake huona aibu na kuhisi ni hali mbaya na nikujidhalilisha kwa mtu mwingine kuifahamu hali hii. Kutunza uke na kulinda afya ya uke ni jambo la muhimu sana kwa mwanamke, kutokwa na harufu mbaya ukeni inaweza kuwa kiashiria kwamba unaumwa na hauko sawa. Hali hii inaweza kuathiri heshima yako k**a mwanamke na pia mahusiano na mwenza wako. Pia watu wengi hudhani kuwa na harufu mbaya itokayo ukeni ni matokeo ya uchafu tu na ndio maana wanaume huwachamba wake zao kuwa hawajuhi kujisafisha na kufanya wanawake kuongeza jitihada katika kujisafisha ukeni, Ra hasha leo napenda kuzungumzia tatizo hili linalowasumbua wanawake wengi na kuwaumiza kichwa kutokana na kwamba lina athari kubwa sana kwani hufanya ndoa zao kudumaa NK,
✍🏻Kitaalamu Hali ya mwanamke kutokwa na maji yenye rangi nyeupe au njano ni Hali ya kawaida na sio tatizo Lakini endapo maji yanatoka yapo katika Hali ya ute mzito wenye rangi nyeupe au kahawia na yanatoa harufu kali au kuwasha hapo una tatizo
•majimaji au ute unaoteleza kutoka sehemu za siri ni njia inayowezesha viungo vya uzazi vya mwanamke kujisafisha au kutoa uchafu wa seli zilizokufa na mabaki ya damu ya hedhi nnje ya mwili pia huvikinga viungo vya uzazi dhidi ya maaambukizi ya bacteria kwa kawaida majimaji haya huwa hayatoi harufu na huwa hayawashi na huwa na rangi nyeupe au njano pia huwa na asidi ya LACTIN ambayo huzuia bacteria kuzaliana
•mwanamke hutoa kiasi cha grams 2 za seli zilizokufa kutoka kwenye mji wa kizazi na grams 3 za ute mwepesi kila siku, kiwango hicho kinaweza kuongezeka au kupungua kutegemeana na mzunguko wa hedhi pia Kuna wakati ute huwa mwepesi na unaovutika na Kuna wakati pia huwa mzito wa rangi ya njano hautoi harufu
Harufu mbaya ukeni kwa kiasi kikubwa husababishwa na fangasi wa candida, japo siyo kila mara ndio maana kuna umuhimu wa kutafuta chanzo cha tatizo la kunuka uke. K**a wewe muhanga wa tatizo hili basi tambua kwamba kuna njia za asili unaweza kuzitumia ikiwemo lishe na virutubisho na ukarudi katika hali ya kawaida. Kesi chache sana k**a tatizo litazidi kuendelea basi itatakiwa uende hospitali ili upate uchunguzi.
Ni kawaida kwa mwanamke kupata harufu ukeni kutokana na hali ya uke kujisafisha kutoa vimelea wabaya. Lakini pale harufu inapokuwa kali sana mfano wa harufu ya samaki basi ujue kuna tatizo kubwa. Kutokwa na harufu mbaya ukeni huwa inaambatana na dalili zingine k**a kuwasha na kuchomachoma na kutokwa na majimaji.
*Nini Kinasababisha Harufu Mbaya Ukeni*👇🏻👇🏻
Sababu namba moja ya kupata harufu mbaya ukeni ni ukuaji wa bacteria. Bacteria Vaginosis ni ukuaji wa bacteria usio wa kawaida kwenye uke. Rejea maelezo ya pale juu kuhusu sababu ya kukua kwa bacteria wabaya kwenye uke ikiwa ni pamoja na kubadilika kwa mazingira ya ukeni na kushuka kwa kinga. Bacteria vaginosis inaweza kupelekea mimba kutoka, kujifungua kabla ya wakati na kuongezeka kwa hatari ya kupata magonjwa mengine ya ngono. dalili mojawapo ya kwamba tayari una maambukizi ya bacteria ni kutokwana uchafu unaoambatana na harufu kali mfano wa harufu ya samaki wabichi.
*BACTERIA VAGINOSIS*
✍🏻Chanzo halisi cha ugonjwa huu hakijafanikiwa kuwa wazi,kinachotokea ni kuongezeka kwa ghafla kwa idadi ya ya bacteria hawa na kubadilisha uwiano wa kawaida katika mazingira ya uke, wanawake wenye wapenzi wengi na wanaofanya mapenzi kwa njia ya mdomo Wana hatari ya kupata tatizo hili
*TRICHOMONAS*
✍🏻maambukizi haya hutokana na Aina ya protozoa wa seli moja, trichomonas mara nyingi huambukizwa kwa njia ya ngono, protozoa huyo huweza kukaa kwenye unyevu unyevu kwa Muda wa saa 24 Bila kufa hivyo kufanya taulo na chupi zisizokauka kuwa chanzo kingine cha tatizo hili
*YEAST INFECTION*
✍🏻kwa kawaida Kuna kiwango kidogo cha yeast (candida albicans) katika uke, huwa tunasema Kuna maambukizi pale kiwango kinapozidi Hali ambayo inatokana na kubadilika kwa Hali ya hewa ukeni (Change in the PH balance of va**na)
®maambukizi ya *YEAST INFECTION* hayatokani na tendo la ndoa, mambo ambayo huchangia tatizo hili ni MATUMIZI YA DAWA ZA KUZUIA MIMBA, MAWAZO, UJAUZITO, KISUKARI NA MATUMIZI YA ANTIBIOTICS
*VAGINAL OR CERVICAL CANCER*
✍🏻mtu anapokua na kansa ya uke, hutokwa na maji ya harufu mbaya, hivyo ni heri uwe unafanya check up ili kujua Afya yako na kwakuwa cancer ya kizazi inapona hivyo ni vema ukatambua mapema uanze tiba
*SEXUAL TRANSMITTED DESEAS (STDs)*
✍🏻Kuna baadhi ya magonjwa k**a vile KASWENDE NA KISONONO yanasababishwa na ngono na kuwa chanzo cha tatizo hili
*POOR HYGIENE*
✍🏻tatizo la kutokwa na maji wakati mwingine husababishwa na muhusika kua mchafu yan mtu unaoga kwa siku mara moja, chupi moja ndio hiyo hiyo mwaka mzima, pads unakaa nayo saa 24, ukienda kukojoa ujitawadhi na maji masafi hivyo unategemea utakua salama kweli???
*Kutozingatia Usafi na Kutokwa sana na Jasho*
✍🏻Ni wazi kwamba uchafu na kuwepo kwa unyevunyevu sehemu za siri huzalisha harufu mbaya. Kisayansi ni kwamba tezi zilizopo ndani ya mwili (apocrine sweat glands )hutengeneza mafuta kuelekea kwenye maeneo k**a kwapa, pua, ndani ya sikio, uke, na kwenye chuchu, bacteria waliopo maeneo hayo huchakata mafuta haya na hivo kuzalisha harufu kali. Uvaaji wa nguo zilizobana na uzito kupita kiasi huchangia kuhifadhiwa kwa jasho kwenye mikunjo ya ngozi na hivo kuletekeza harufu.
*Kuvaa Pedi kwa Masaa Mengi*
✍🏻Pedi inapovaliwa kwa muda mrefu husababisha ngozi kucharuka,kututumka n kuwasha na pia kuchangiwa kukua kwa bacteria na fangasi wabaya ambao ni chanzo cha harufu.
*DALILI ZA TATIZO HILI*
✍🏻kutokwa na uchafu ukeni unaoambatana na kuwashwa au kutokewa na vipele, hii hutokana na kuharibika kwa uwiano wa bacteria hivyo kuwa na madhara na uchafu hutoka wa aina tofauti hapa chini nitaelezea kila Aina ya uchafu na dalili zake👇🏻👇🏻👇🏻
*UCHAFU WENYE RANGI YA KAHAWIA AU DAMU*
★huu uchafu huonyesha dalili ya kuwa mzunguko wako wa hedhi umevulugika na wakati mwingine ni dalili ya kansa ya kizazi, mwanamke anayepata tatizo hili hutoa damu nyingi na kuumwa sana nyonga
*UCHAFU WENYE RANGI YA NJANO /KIJANI WENYE HARUFU MBAYA*
★Endapo uchafu huo utatoka k**a povu na wenye rangi ya kijani au njano na ukiambatana na harufu mbaya huwa ni dalili ya ugonjwa wa trichomonas, maambukizi ya parasite yanatokana na ngono zembe, dalili Yake nyingine ni maumivu na kuwashwa wakati wa kutoa haja ndogo
*UCHAFU MWEUPE MZITO K**A JIBINI*
★mara nyingi hii huwa ni dalili ya maambukizi ya fangasi(YEAST INFECTION) na dalili nyingine huwa ni kuvimba sehemu ya nje ya uke, kuwashwa na kupata maumivu makali wakati wa tendo la ndoa
*UCHAFU MWEUPE/KIJIVU WENYE HARUFU YA SAMAKI*
★uchafu wa Aina hii ni dalili ya maambukizi ya bacteria vaginosis, mara nyingi mwenye tatizo hili husikia muwasho na maumivu sehemu ya nje ya uke
*MAMBO MUHIMU YA KUZINGATIA KUEPUKA TATIZO HILI NA TIBA YAKE*
✓EPUKA KUJIINGIZA VIDOLE MARA KWA MARA UKENI
✓EPUKA MATUMIZI YA DAWA ZA ANTIBIOTICS MARA KWA MARA
✓PUNGUZA KULA VYAKULA VYENYE SUKARI NYINGI
✓TUMIA PADS ZENYE ANIONS NI SALAMA KWA AFYA YAKO
✓SAFISHA VIZURI NGUO ZAKO ZA NDANI NA UZIANIKE JUANI NA HATA KUZIPIGA PASI
✓KUNYWA JUICE YA APPLE,STRAWBERRY, NANASI KWA WINGI
✓EPUKA KUFANYA NGONO ZEMBE
✓HAKIKISHA UNAJISAFISHA KILA UNAPOMALIZA KUJISAIDIA
✓EPUKA KUTUMIA DAWA ZA KUZUIA MIMBA
✓EPUKA KUTUMIA SABUNI AU VITU VYA MANUKATO UKENI,
NB: Wanawake wengi mnapenda kutumia baadhi ya dawa kwa lengo la kuongeza vionjo kwenye mapenzi pia kufanya uke kunukia vizuri, au kukaza uke. Ngoja nikwambie kitu rafiki yangu uke una harufu nzuri sana ambayo haipatkan kokote hivyo haihitaji kuwekwa pafyumu Wala kusafishwa kwa sabuni za kemikali kwani huwa panajisafisha hivyo ni heri ukaacha kutumia kwani madhara Yake hayaonekani sasa ila baada ya Muda huonekana.
Mwisho Kabisa tatizo hili linapona kwa kutumia products za uhakika na haraka ambazo ninazo kwani hadi kufikia sasa zimesaidia wengi.
Kwa Ushauri/ Matibabu piga/sms katika 0744496372
Jali Afya yako kwa kutumia virutubisho vyenye madini na vitamini muhimu.
Click here to claim your Sponsored Listing.
Category
Contact the business
Telephone
Address
Ilala
Dar Es Salaam
