TIBA BORA

TIBA BORA

Share

suluhisho la uzazi kwa wanaume na wanawake

11/01/2024

Njia tano za asili za kuondokana na miguu kuwaka moto

Huu ni ugonjwa unaowasumbua watu wengi sana na mara nyingi humfamnya mtu mwenye tatizo hilo kushindwa kusinzia japo anahisi kusinzia.

Miguu kuwaka moto ni ugonjwa unaotokea ambapo katika mwili wa binadamu kutakuwa na matatizo k**a kudhoofika kwa neva za pembezoni mwa mwili yani za miguuni hivyo kupoteza uwezo wa utendaji kazi wa neva miguuni, sababu zingine ni k**a kutokuwa na mzunguko mzuri wa damu, kuwa na sumu nyingi mwilini,kurithi au mwili kushindwa kufanya kazi zake vizuri.

Dalili za ugonjwa wa miguu kuwaka moto
Ugonjwa huu una dalili nyingi zikiwemo:
- Kuhisi ganzi,
- kuhisi kuchomwa na kitu chenye ncha Kali miguuni,
- kuhisi miguu kuwa na majimaji kwa ndani,
- joto Kali miguuni,
- kuhisi k**a unaungua miguuni,kushindwa kushika au kubeba vitu na maumivu makali.

Vitu/ mambo yanayoweza kupelekea mtu miguu yake kuwaka moto
Kuna mambo mengi sana yakiwemo:
- Uzito mkubwa wa mwili (hii husababisha uti wa mgongo kukaa tofauti na unavyostahili hivyo baadhi ya neva kukandamizwa na uzito wa mwili au misuli hivyo kusababisha miguu kupata maumivu na kufa ganzi.
- Matumizi ya baadhi za dawa zenye kemikali kwa muda mrefu au mara kwa mara mfano dawa za TB, HIV nk.
- Upungufu wa virutubusho mwilini hasa mkusanyiko wa Vitamini B
- Magonjwa ya sukari na Shinikizo la damu , magoti , mzio na fangasi
- Matatizo ya moyo
- Matatizo katika mishipa ya damu
- Ulevi wa kupindukia kwa muda mrefu

Jinsi ya kuepuka ugonjwa wa miguu kuwaka moto
- Kuwa na uzito unaoenda na na kimoja chako
- Fanya mazoezi ya mwili
- Kula chakula kinachokupatia virutubisho mwili hasa VITAMINI B
- Usafi wa viatu, sox na miguu
- Ondoa sumu au kemikali mara kwa mara mwilini

Matibabu:
- Kula vyakula vyenye mkusanyiko wa vitamini B za kutosha
- Fanya mazoezi ya mwili k**a kukimbia, Kutembea n.k pia kufanya massaging
- Punguza uzito uliopitiliza
- Tumbukiza miguu katika maji ya vuguvugu yenye chumvi
- Tibu maradhi ya sukari hakikisha sukari ipo sawa
- Ondoa sumu kali mwilini mara kwa mara
- Chua miguu yaki kwa vitu vinavyopunguza maumivu ,vinavyosaidia mzunguko wa damu kuwa Vizuri (paka Asali mbichi, shubiri na limao).

06/01/2024

Tiba Bora na Afya ya mifupa na maungio bila upasuaji.
📞 +255 652924081
Maumivu ya joint ni tatizo linalosumbua watu wengi kwa sasa kutokana na mabadiliko ya mitindo ya Maisha. Umri mkubwa ni moja ya sababu inayopelekea kutokea kwa tatizo, ambapo tishu za mwili zinakuwa kavu na kupoteza uwezo wa kuvutika.

Tatizo hili limewafanya watu wengi kushindwa kukaa na kutembea umbali mrefu sababu ya maumivu makali wanayoyapata..

Pia limewaondolea watu uwezo wa kushiriki kwenye michezo na shughuli zingine za kujenga uchumi na wengine wengi kupata ulemavu wa maisha sababu ya kuwa na tatizo kwa muda mrefu sana na kulichukulia kawaida kwa kutumia dawa za maumivu (ant pains)

Na changamoto hii endapo isipotatuliwa mapema inaweza kukuondolea uwezo wa kutembea milele.

Kubwa Zaidi Wengi wamekuwa wakihangaika kupata Suluhu ya kudumu bila mafanikio.

Wengine wamekuwa wakipata tiba za kutuliza maumivu na baada ya muda mfupi tatizo linarudi tena.

K**a wewe umekuwa ukihangaika kupata suluhu la hili tatizo,usiwaze tena. Nina habari njema kwako.

Habari njema nikwamba unauwezo wa kutumia dawa asili zitokanazo na virutubisho lishe (food suppliments) ambazo zimewasaidia wengi kutibu matatizo yao yaliyo wasumbua kwa muda mrefu sana
karibu tukuhudumie sasa ASANTE.
📞 +255 652924081

28/12/2023

*Kuna hatua kadhaa unazoweza kuchukua kwa lengo la kupunguza hatari ya kuzidi kiasi kwa tezi dume (BPH).*

Hapa kuna miongozo kadhaa ya kufuata:

1. *Fanya Mazoezi:* Kufanya mazoezi mara kwa mara kunaweza kusaidia kudumisha uzito na afya ya mwili, ambayo inaweza kupunguza hatari ya kuzidi kiasi kwa tezi dume.

2. *Kula Lishe Bora:* Kula chakula kilichojaa matunda, mboga, nafaka nzima, protini zenye afya (k**a vile samaki na kuku), na kupunguza matumizi ya vyakula vyenye mafuta mengi.

3. *Punguza Matumizi ya Chumvi:* Kupunguza ulaji wa chumvi kunaweza kusaidia kudumisha afya ya mfumo wa mkojo.

4. *Epuka Uvutaji wa Tumbaku na Matumizi ya Pombe:* Tabia hizi mbili zinaweza kuongeza hatari ya kuzidi kiasi kwa tezi dume.

5. *Kunywa Maji Mengi:* Kudumisha mwili wako mwenye afya kunaweza kusaidia katika kuzuia matatizo ya tezi dume.

6. *Punguza Msongo:* Kupunguza msongo wa mawazo kunaweza kuwa na athari nzuri kwa afya ya mwili na inaweza kusaidia kuzuia matatizo ya tezi dume.

7. *Pata Uchunguzi wa Mara Kwa Mara:* Ikiwa una dalili zozote au wasiwasi kuhusu afya ya tezi dume, ni muhimu kushauriana na daktari wako.

8. *Kuwa na Maisha Yenye Afya:* Kudumisha maisha yenye afya kwa jumla kwa kula vizuri, kufanya mazoezi, kupumzika vya kutosha, na kuacha tabia mbaya kunaweza kusaidia kuzuia matatizo mengi ya kiafya, pamoja na kuzidi kiasi kwa tezi dume.

*Ni muhimu kufahamu kuwa wakati hatua hizi zinaweza kupunguza hatari, haziwezi kutoa dhamana ya kuzuia kabisa kuzidi kiasi kwa tezi dume. Ikiwa una wasiwasi wowote au dalili, ni vyema kushauriana na daktari wako kwa ushauri zaidi na uchunguzi.*
Piga +255 652924081

23/12/2023

Jinsi Ya Kutibu Ugonjwa Wa Tezi Dume Bila Upasuaji: Safari Ya Afya Bora Kupitia Tiba Asili.0652924081

23/12/2023

Dalili ya tezi dume iliyovimba ni:
Shida katika kuanza kukojoa au kuubana mkojo Mtiririko dahifu wa mkojo Kukojoa kwa shida Kujisikia kuwa hujamaliza mkojo Mkojo kuendelea kudondoka kwa muda mrefu baada ya kumaliza Hali ya kujisikia kukojoa mara kwa mara au ghafla Kuamka mara nyingi zaidi usiku kwa ajili ya kwenda haja ndogo

Kwa baadhi ya wanaume, dalili zinaweza kuwa ndogo ambazo hazihitaji tiba. Kwa wengine, zinaweza kuwa kubwa na kuathiri maisha yao. Wanaume hupatwa hofu kuwa kuvimba kwa tezi dume kunasabihiana na upataji wa kansa ya tezi dume. Hii siyo kweli kwani uwezekano wa kupata kansa wa mtu mwenye tez i iliyovimba hauzidi ule wa mtu asiye na tatizo hili la tezi.
Usisite kunipigia au Tuma sms kawaida kwa MSAADA zaidi +255 652924081

20/12/2023

UFAHAMU UGONJWA WA VIDONDA VYA TUMBO
Vidonda vya tumbo ni tatizo linalotokea baada ya kuta za tumbo au utumbo mdogo kuwa na vidonda, hii hutokea ni baada ya kuharibika kwa ukuta wenye ute unaozuia kemikali za kuyeyusha chakula unaoitwa mucus. Kemikali ambayo ni acidi inayozalishwa mwilini kiasili husaidia kuyeyusha chakula na kuua wadudu tumboni, k**a ukuta wenye ute ukiharibiwa na kushindwa kufanya kazi basi kemikali (acid) itaathiri tumbo au utumbo na kuruhusu bakteria kuendelea kusababisha vidonda vya tumbo.

Vidonda vya tumbo vinatibika kirahisi ila vikicheleweshwa bila kutibiwa huweza kusababisha tatizo kubwa. Ni tatizo linalotesa sana na kuwanyima raha watu wengi, linahitaji umakini na pia husababisha magonjwa mengine k**a kansa, amoeba (amiba), homa, kupungua uzito.

AINA ZA VIDONDA VYA TUMBO

Kuna aina zipatazo mbili za Vidonda vya Tumbo (Peptic Ulcers)

Vidonda vya tumbo kubwa (Gastric ulcers) – Hivi ni vidonda vya tumbo vinavyotokea ndani kwenye tumbo kubwa
Gastric_Ulcer-1200x720

2. Vidonda vya utumbo mdogo (Duodenal ulcers) – Hivi ni vidonda ambavyo hutokea kwenye utumbo mdogo (hasa juu)
duodenal-ulcer

CHANZO CHA VIDONDA VYA TUMBO

Vidonda vya tumbo vina vyanzo tofauti ili vyote ni vile vinavyohusiana na mmeng’enyo, vyanzo hivyo ni;

Bakteria waitwao Helicobacter pylori (H. pylori)
Matumizi ya dawa za kupunguza maumivu k**a asprin, (NSAIDs), (Advil, Aleve, na zingine)
Kuwa na mawazo mengi
Kula vyakula vinavyozalisha acid kwa wingi
Kunywa pombe na vinywaji vikali
Uvutaji wa sigara
Kuto kula mlo kwa mpangilio

DALILI ZA VIDONDA VYA TUMBO

Dalili za vidonda vya tumbo hujitokeza baada ya kula au kabla ya kula, ila mara nyingi wengi huwa wanazipuuzia na endelea kukuza tatizo, vidonda vya tumbo vinadalili k**a;

gastrita

Kupata maumivu ya tumbo yanayokuwa k**a ya moto (kuunguza) baada na kabla ya kula
Kupatwa na kiungulia karibu na chembe ya moyo
Tumbo kujaa gesi na kuvimbiwa
Kichefuchefu na kutapika tena yawezekana kutapika damu
Kupata haja kubwa ya rangi kahawia au nyeusi yenye harufu mbaya sana, pia haja yaweza kuchanganyikana na damu
Kupoteza hamu ya kula na kupungua uzito
Kushindwa kupumua vizuri.

WASILIANA NASI SASA TUKUSAIDIE KUONDOKANA NA TATIZO LAKO
PIGA +255 652924081

20/12/2023

TEZI DUME SIO BUSHA, ZIJUWE DALILI ZA TEZI DUME

Watu wengi wamekuwa wakidhania kuwa tezi dume ni busha ama ngiri maji kwa jina jinngine. Hapana hii sio sahihi kabisa. Mpenzi msomaji tambuwa kuwa tezi dume sio busha na haifananni kabisa na busha. Tezi dume isipotibiwa kwa haraka inaweza kuwa hatari sana kwani ina maumivu makali sana. Sasa nini hasa hii tezi dume?. katika makala hii nitakwenda kukupa mwangaza kuhusu tezi dume., dalili za tezi dume na athari za tezi dume kwa afya ako.

Nini maana ya tezi dume
Tezi hii kitaalamu hufahamika k**a prostate gland. Hii ni tezi inayopatikana katika mfumo wa uzazi wa kiume. Tezi hii inapatikana jirani na kibofu cha mkojo na mirija ya mkojo. Tezi hii ina kazi ya kuzalisha majimaji ambayo hubeba mbegu za kiume. Majimaji haya ndio yale anayotoa mwanaume anapofikia kilele. Hivyo tezi hii ni muhimu sana katika mfumo wa kizazi wa mwanaume. Tezi hii si kubwa saana inapata sentimita zisizozidi 5. lakini tezi hii hukuwa kadiri umri unavyoenda.

Kwa ufupi wa maneno ni kuwa tezi dume ipo zini ya kibofu karibu na shingo ya kibofu. Na imezunguka mrija unaotoa mkojo kutoka kwenye kibofu kuja nje (urethra). hivyo mkojo unapotoka kwenye kipofu hipitia katikati kwenye tezi dume ukiwa kwenye mrija wa urethra. Urethra ndio mrija unaotoa mkojo kutoka kwenye kibofu.

Vipi ugonjwa wa tezi dume hutokea?
K**a ulivyojifunza hapo juu mkojo ukiwa kwenye mrija hupita katikati ya tezi tume. Sasa tezi hii ina kawaida ya kukuwa kadiri mtu anavyopata umri zaidi. Hivyo basi kadiri tezi hii inapoongezeka ukubwa ndivyo inavyoanza kuminya mirija ya kupitisha mkojo na hatimaye huanza tatizo la ugonjwa wa tezi dume. Tatizo hili kitaalamu hufahamika k**a Benign Prostatic Hyperplasia (BPH).

Nini sababu za kutokea kwa tezi duma?
K**a ilivyokwisha kutajwa hapo juu, tezi hii hukuwa kadiri mtu anavyokuwa. Kwa baadhi ya watu inapokuwa huwa kubwa kiasi cha kuanza kuminya mirija ya mkojo na kuleta shida kwenye mfumo wa mkojo. Tafiti mbalimbali zinaonyesha kuwa miongoni mwa mambo yanayohatarisha uwezekano wa kupata ugonjwa huu ni haya yafuatayo:-

1.Umri, kikawaida tezi dume huwapata watu wenye umri kuanzia miaka 40. ni mara chache sana kuwapata walio chini ya umri huo. Pia tezi dume kwa kiasi kikubwa huwapata walio kati ya miaka sitini na kuendelea. Hususan robo tatu ni wale walio na miaka kuanzia 60,na nusu yao ni wale walio na miaka kuanzia 80.

2.Tatizo la tezi dume pia huweza kurithiwa. Yaani k**a baba yako ana tezi dume ama yeyote katika damu yako hapo mwanzo alikuwa na tezi dume, hivyo upo uwezekana na wewe kurithi tatizo hili.

3.Pia inaonakana kuwa baadhi ya rangi huathiriwa sana na tatizo la tezi dume. Tafiti zinaonesha kuwa watu walio katika bara la Asia si sana kupatwa na tezi dume kuliko watu weusi na wazungu. Hata hivyo kwa watu weusi upo uwezekano wa kupatwa na tatizo hili katika umri mdogo kuliko wengine.

4.Maradhi, tafiti zinaonyesha kuwa kuna baadhi ya maradhi huweza kupelekea kupatwa na tatizo la tezi dume. Kwa mfano watu wenye maradhi ya sukari, na maradhi ya moyo wapo hatarini kupatwa na tezi dume ukilinganisha na watu wengine.
5.Staili za maisha. Tafiti pia zinaonyesha kuwa watu wenye kiribatumbo na wasiofanya mazoei wapo hatarini kupatwa na tatizo la tezi dume.

Ni zipi dalili za ugonjwa wa tezi dume?
Dalili za tezi dume zinaweza kuwa kali ama hafifu kutoka mtu hadi mtu. Ukali wa dalili hizi hautegemei ukubwa wa tezi. Inaweza kuwa tezi ni kubwa lakini dalili zisiwe kali. Miongoni mwa dalili za tezi dume ni:-

1.Kukojoa mara kwa mara, ama kuhisi kukojoa mara kwa mara
2.Kukojoa mara kwa mara wakati wa usiku
3.Kupatwa na uzgumu kutoa mkojo
4.Mchirizi wa mkojo kuwa dhaifu
5.Mkojo kukatakata unapofika karibu a mwisho
6.Kujichafua wakati wa kukojoa
7.Kushindwa kumaliza mkojo kabisa.
8.Damu kwenye mkojo
9.Kushindwa kukojoa kabisa.
10.Kupata mkojo mchache sana

Kuwa na dalili tajwa hapo juu pekee hakuwezi kukupa uhakika kuwa una tatizo la tezi dume. Kwani dalili tajwa hapo juu zinaweza kuambatananna shida nyingine za kiafya kwa mfano:-
1.Maambukizi ya UTI
2.Kuvimba kwa tezi
3.Kupunguwa ukubwa wa mrija wa mkojo
4.Kuwepo na vijiwe kwenye kibofu
5.Kuwa na shida kwenye mfumo wa neva ambazo hudhibiti ufanyaji kazi wa kibofu
6.Kuwa na saratani
7.K**a upasuaji katika kibofu haukufanyika sawa.

Ni zipi athari za tezi dume k**a haitawahi kutibiwa?
Tezi dume ni k**a maradhi mengine, inatibika bila wasi. Hata hivyo endapo matibabu yatachelewa athari zifuatazo zinaweza kupatikana:-
1.Kushindwa kabisa kukojoa
2.Kupatwa na maambukizi ya UTI
3.Kupatwa na vijiwe kwenye kibofu
4.Uharibifu wa kibofu unaweza kutokea
5.Figo inaweza kuharibika

Mwisho:
Mwisho napenda kumaliza kwa kusema kuwa tatizo la tezi dume linatibika bila wasi. Zipo dawa za Asili aina tofauti tofauti zilizofanyiwa utafiti wa kina ambazo mgonjwa anaweza kupewa na akapona kabisa.
K**atatizo lake ni kubwa zaidi anaweza kufanyiwa cupping therapy.

By; Dr ISAYA HURUMAEL✍🏾
wa.me/0652924081

Want your business to be the top-listed Beauty Salon in Dar es Salaam?
Click here to claim your Sponsored Listing.

Category

Telephone

Website

Address


Dar Es Salaam

Opening Hours

Monday 07:00 - 20:00
Tuesday 07:00 - 20:00
Wednesday 07:00 - 20:00
Thursday 08:00 - 20:00
Friday 07:00 - 20:00
Saturday 07:00 - 20:00
Sunday 12:00 - 20:00