AFYA Kwanza

AFYA Kwanza

Share

�PID, UTI, FANGASI SUGU
�VIMBE KWENYE KIZAZI
�MIFUPA NA MAUNGIO
�KISUKARI & PRESSURE
�BAWASIRI

31/01/2024

𝗙𝗔𝗛𝗔𝗠𝗨 𝗝𝗨𝗨 𝗬𝗔 𝗧𝗔𝗧𝗜𝗭𝗢 𝗟𝗔 𝗡𝗚𝗜𝗥𝗜 (𝗛𝗘𝗥𝗡𝗜𝗔) 👇

Tatizo hili la ngiri hutokea pale ogani au viungo vya tumboni K**a vile utumbo vinapoweza kuingia misuli au tishu zilizowazi katika kuta za tumbo au korodani.

𝗦𝗔𝗕𝗔𝗕𝗨 𝗭𝗜𝗡𝗔𝗭𝗢𝗪𝗘𝗭𝗔 𝗞𝗨𝗦𝗔𝗕𝗔𝗕𝗜𝗦𝗛𝗔 𝗧𝗔𝗧𝗜𝗭𝗢 𝗟𝗔 𝗡𝗚𝗜𝗥𝗜 (𝗛𝗘𝗥𝗡𝗜𝗔) 👇

Zipo sababu mbalimbali zinazoweza kupelekea mtu kupata tatizo la ngiri k**a zifuatazo.
👉 Umri.
👉 Uzito mkubwa.
👉 Kunyanyua vitu vizito.
👉 Kikohozi cha muda mrefu.
👉 Kukosa choo au kupata choo kigumu (Constipation)
👉 Kurithi yaani hutoka kizazi hadi kizazi ndani ya ukoo.

𝗗𝗔𝗟𝗜𝗟𝗜 𝗭𝗔 𝗧𝗔𝗧𝗜𝗭𝗢 𝗟𝗔 𝗡𝗚𝗜𝗥𝗜 (𝗛𝗘𝗥𝗡𝗜𝗔)👇

🍀 Tumbo kujaa gesi.
🍀 Tumbo kuungurumba mara kwa mara.
🍀 Kupata choo kigumu, au kutokupata choo
🍀 Maumivu ya mgongo na kiuno.
🍀 Maumbile ya kiume kuwa madogo
🍀 Kuvimba kwa korodani moja.
🍀 Kupotea kwa korodani.
🍀 Ngiri maji (korodani kujaa maji
🍀 Kupata Tatizo la Busha
🍀 Maumivu ya korodani zote mbili au moja wapo.


🥏WhatsApp♻️
🪀+255 767388246

15/09/2023

Ugonjwa Wa Kutetemeka (Parkinson’s Disease)





Parkinson’s disease ni ugonjwa wa neva unaoanza na kukua taratibu na kuathiri matumizi ya maungo ya mwili. Dalili huanza taratibu kwa mkono mmoja kuanza kutetemeka kwa mbali. Parkinson’s disease ni ugonjwa unaoweza kusababisha kukak**aa kwa misuli au kupunguza kasi ya mwendo.

Katika hatua zake za mwanzo, mgonjwa anaweza akaonyesha kwa mbali au akashindwa kabisa kuonyesha hisia zake usoni. Mikono inaweza ikashindwa kucheza wakati akitembea. Kuzungumza kukawa kwa shida na hali ya ugonjwa ikawa inazidi kuwa mbaya zaidi siku zikisogea.

Pamoja na kuwa ugonjwa huu hauna tiba, matumizi ya dawa yanaweza kupunguza baadhi ya dalili. Mara nyingine daktari anaweza kushauri upasuaji ili kurekebisha baadhi ya sehemu za ubongo.

Dalili Za Parkinson’s Disease

Dalili na viashiria vya ugonjwa huu huweza kuwa tofauti kwa watu tofauti. Dalili za mwanzo huweza kuchukua muda mrefu bila kutambulika. Kwa kawaida, matatizo huanzia upande mmoja na huendelea kuwa mabaya zaidi upande huo huo mmoja, hata baada ya kuwa upande wa pili umeanza kuathirika.

Dalili za parkinson’s ni pamoja na:dalili za parkinson's

Kutetemeka. Kutetemeka huanzia kwenye mkono au vidole. Unaweza kujikuta unavisugua dole gumba na kidole cha shahada (pill-rolling.) Mkono wako unaweza kutetemeka ukiwa umetulia.


Kupungua uwezo wa kuvimudu viungo (bradykinesia). Baada ya muda utajikuta umepungukiwa kasi ya vitendo vya mwili na kufanya shughuli ndogo tu ikachukua muda mwingi sana. Hatua zako zinaweza kuwa fupi ukitembea. Utapata shida kunyanyuka kwenye kiti. Unaweza kuburuza miguu wakati ukitembea.
Kukak**aa kwa misuli. Kukak**aa kwa misuli kunaweza kujitokeza kwenye sehemu yo yote ya mwili. Kukak**aa kunaweza kuambatana na maumivu na kukufanya ushindwe kukamilisha vitendo vya mbali.
Mkao na kuyumba. Unaweza kupinda mgongo kuanzia kiunoni ukainamia mbele, au ukawa na matatizo ya kuyumbayumba.
Kusimama vitendo vinavyojiendesha. Vitendo vinavyojiendesha k**a kukonyeza, kutabasamu, kutupa mikono utembeapo vitapungua.
Mabadiliko ya uzungumzaji. Unaweza kuanza kuzungumza taratibu, haraka haraka au kwa kusitasita. Zungumza yako inaweza kuwa ya sauti moja bila vionjo.
Mabadiliko ya uandishi. Unaweza kupata ugumu katika kuandika na maandishi yako yakawa madogo.

Chanzo Cha Parkinson’s

Kwenye hali ya ugonjwa wa Parkinson’s, seli fulani za neva (neurons) katika ubongo huvunjika au kufa. Dalili nyingi zinatokana na upungufu wa neurons ambazo hutengeneza kemikali ya utoaji taarifa iitwayo dopamine. Kiwango cha dopamine kikiwa chini, utendaji kazi wa ubongo huwa si wa kawaida, hali ambayo husababisha ugonjwa wa Parkinson’s.





Chanzo halisi cha ugonjwa huu hakieleweki, lakini kuna baadhi ya vipengele vinavyochangia, ambavyo ni pamoja na:
Sababu za kijenetiki Sababu za mazingira

Utafiti umeonyesha pia kuwa kuna mabadiliko mengi ndani ya ubongo wa mtu mwenye ugonjwa wa Parkinson’s, ingawa bado hawajaweza kujua sababu za mabadiliko hayo. Mabadiliko hayo ni pamoja na:

Vitu Vinavyochangia Parkinson’s
Umri. Watu wazima ndiyo wanaopata ugonjwa huu. Unaanzia kwa watu wa umri wa kati au baadaye kwenye maisha. Watu huupata ugonjwa huu wanapokuwa na umri wa miaka k**a 60 au zaidi.
Urithi. Kuwa na ndugu wa karibu mwenye ugonjwa huu kunaongeza uwezekano wa wewe pia kuupata. Lakini yamkini ni ndogo hadi uwe na ndugu wengi wenye tatizo hili kwenye familia yako.
Jinsia. Wanaume wanapata ugonjwa huu zaidi ya wanawake.
Sumu. Kuwa kwenye mazingira ya madawa ya kuulia majani na wadudu kwa muda mrefu kunaweza kukuongezea uwezekano wa kuugua.



Madhara Yatokanayo na Parkinson’s

Ugonjwa wa parkinson’s huambatana na matatizo mengine, ambayo hutibika:
Ugumu wa kufikiri. Unaweza kupata matatizo ya kutambua na kufikiri. Matatizo haya mara nyingi hujitokeza kwenye hatua za mwisho za ugonjwa. Matatizo haya ya utambuzi huwa hayasikii dawa.

parkinson's tiba Mfadhaiko na mabadiliko ya hisia. Unaweza kusikia mfadhaiko, wakati mwingine kwenye hatua za mwanzo za ugonjwa. Tiba ya mfadhaiko inaweza kurahisisha uondoaji wa changamoto nyingine za parkinson’s.

Unaweza kupata mabadiliko mengine ya hisia, k**a woga, wasiwasi, au kukosa motisha. Madaktari wanaweza kukusaidia kukupatia tiba ya matatizo haya.
Matatizo ya kumeza. Unaweza kupata matatizo ya kumeza kadiri ugonjwa unavyozidi. Mate yanaweza kujazana mdomoni kwa sababu ya kupungua kwa kasi ya kuyameza na kusababisha kuchuruzika.
Matatizo ya kutafuna na kula. Hatua za mwisho za parkinson’s huathiri misuli ya kwenye mdomo, na kufanya utafunaji kuwa mgumu. Hali hii huweza kusababisha lishe duni.
Matatizo ya kulala. Watu wenye parkinson’s mara nyingi hupata matatizo ya kulala, ikiwa ni pamoja na kuamka mara nyingi usiku, kuamka mapema sana asubuhi au kulala mchana.
Matatizo ya kibofu. Ugonjwa wa parkinson’s huweza kuleta matatizo ya kibofu, ikiwa ni pamoja na kushindwa kuudhibiti mkojo au shida kupata haja ndogo.
Tumbo kujaa. Watu wengi wenye parkinson’s hupata matatizo ya choo kigumu kwa sababu ya kupungua kwa uyeyushwaji wa chakula.

Unaweza kuona pia :
Mabadiliko ya Pressure. Matatizo kusikia harufu. Uchovu. Maumivu. Shida ya tendo la ndoa.



Katika mada yetu nyingine tutauzungumzia ugonjwa wa kifafa. Uwe huru kuuliza maswali uliyo nayo au kutoa ushauri ulio nao kuhusu uandishi wa mada zetu.

15/09/2023

*URIC ACID NI NINI?*
*kwaufupi 👇* ..

Uric Acid ni kemikali ya asilia ambayo inapatikana katika mwili wa binadamu.
Kemikali hii hupatikana baada ya kuvunjwa vunjwa kwa vyakula ambavyo ndani yake kuna kundi la kemikali aina ya “Purine” ambayo baada ya kuvunjwa ndipo huzalisha kitu kinachojulikana k**a “Uric Acid”.

Katika mwili wa binadamu, kiwango ambacho ni cha kawaida mtu kuwa nacho ni 2.4-6.0 mg/dL (kwa mwanamke) na 3.4-7.0 mg/dL (kwa mwanamme).
Kiwango cha uric acid mwilini hupimwa kwa kutumia njia ya damu.

Kiwango hiki endapo kitazidi mwilini kitasababisha matatizo mwilini na hasa katika maeneo ya mwili ambayo ni maungio ya mifupa/jointi.

Katika maungio ya mifupa au jointi, mtu atapatwa na maumivu makali, kuvimba na kubadilika kwa umbile la maungio ya mifupa na kuwa k**a kumepinda.

Hali hii kitaalamu au ugonjwa hujulikana k**a “Gout”.

Pia kuzidi kwa kiwango cha uric acid mwilini kinaweza kuwa ni dalili ya magojwa k**a vile magonjwa ya ini, figo pamoja na saratani.

Tupigie Sasa

15/09/2023

DAWA YA KUTIBU GAUTI(URIC ACID)

GAUTI hutokea pale tindikali aina ya URIC ACID inapozidi kiwango mwili wa binaadamu hali ambayo kitaalaamu huitwa (hyperuricemia).
Tindikali hii ni matokeo ya kuvunjwavunjwa mwilini kwa aina fulani za chakula k**a nyama na chakula cha baharini. Tindikali hii kwa kawaida huchanganyika na damu na mwisho hutolewa nje ya mwili pamoja na mkojo kupitia figo. Tindikali hii ikitengenezwa kwa wingi mno au isipotolewa nje ya mwili kwa kiwango kinachostahili, ile inayobaki husababisha mrundikano wa tindikali hiyo katika majimaji yanayo zunguka maungio (joints) yanayoitwa (synovial fluid) na hatimaye hutengeneza vijiwe vidogovidogo vya tindikali ya UREA yaani URIC CRYSTALS ambavyo husababisha joint kuvimba na maumivu kwenye joint na maeneo yaliyo karibu.

GAUTI tofauti na ugonjwa mwingine wowote, Gout ni ugonjwa ambao hupoteza sana maisha ya watu Matajiri kuliko hata maskini,Wafalme wakuu, watawala, wakurugenzi na wengineo wote wamepoteza maisha kutokana na ugonjwa huu.Wanaume huwa na ugonjwa zaidi kuliko wanawake. Kiwango cha asidi ya URIC huongezeka kwa wanaume wa umri wa miaka 20 na kwa wanawake huongezeka baada ya kukoma kwa hedhi.
Kwa kawaida asidi ya Uric hutengana kwenye damu na hupita kwenye figo. Lakini wakati mwingine wakati mwili unazalisha sana Asidi ya URIC (kwa wanawake zaidi ya 6.0mg/ db na wanaume zaidi ya 7.0mg/dL) au figo haziwezi kuweka asidi ya Uric vizuri basi kiwango cha asidi huongezeka na kuna malezi ya sindano k**a fuwele za mkojo kwa pamoja ambayo iko maumivu,uvimbe na kuvimba.

VISABABISHI VYA GAUTI
Gauti husababishwa na kuwepo kwa kiwango kikubwa kuliko kawaida cha uric acid katika damu.Hali hutokea iwapo mwili wa mgonjwa unatengeneza uric acid nyingi kuliko kawaida au kushindwa kutoa uric acid mwilini k**a inavyotakiwa.
Ongezeko hili husababisha mrundikana wa uric acid katika majimaji yanayozunguka jointi yanayoitwa synovial fluid na hatimaye kutengeneza vijiwe vidogovidogo vya tindikali ya Urea yani Uric acid Crystals ambayo husababisha jointi kuvimba na hatimaye kuathirika.

AMBAO WAKO KATIKA HATARI KUBWA YA GOUT:
+ mtu ambaye ni mnene kupitiliza.
+ watu ambao hunywa sana pombe.
+ mtu ambaye anaugonjwa wa moyo wa ischemic.
+ mtu ambaye ana shinikizo la damu.
+ Wenye magonjwa ya sukari.
+ wenye magonjwa ya figo.
+ugonjwa wa sickle cell anemia au wenye upungufu wa damu.
+ salatani ya damu (leukemia).

DALILI ZA GOUT:
+ Dalili za gout kwa kawaida huhusisha joint moja au joint chache. Joint zinazo athiriwa zaidi ni pamoja na kidole kikubwa mguuni, magoti au kiwiko cha mguu.
+kuna maumivu makali zaidi ambayo humfanya mtu kuamka mapema asubuhi.
+mtu hupata maumivu makali yasiyo weza kuhimilika.
+mtu hupata maumivu mpaka hushindwa kuvaa soksi na viatu.
+kuzidisha au kutokuwepo kwa jasho.
+ katika hali nyingine dalili hujiondoa katika Sikh 4 hadi 5 mtu huhisi kawaida baada ya hali hiyo.
+ Mgonjwa anaweza kujhisi homa.
+ baadhi ya wagonjwa hupata gauti sugu ambayo huwaletea madhara sugu katika joint (chronic arthritis) hali ambayo husababisha mgonjwa maumivu na muda mwingine kushindwa vizuri kutumia vizuri joint zake.
Wagonjwa wenye gauti kwa muda mrefu huwa pia na vinundu chini ya ngozi inayozunguka joint zilizoathirika. Vinundu hivi kitaalamu huitwa (trophy) na ni ishara ya muhimu kwa daktari.

VIPIMO
Vipimo vya gauti hujumuisha,
Kiwango cha Uric Acid katika damu. Hata hivyo si kila aliye na kiwango kikubwa cha uric acid katika damu huwa na gauti.
+ Kiwango cha uric acid katika mkojo.
+Uchunguzi wa majimaji yanayozunguka jointi (synovial fluid) kuchunguza vijiwe katika jointi.
+ XRAY ya jointi iliyoathirika.
Uchunguzi wa utando unaozunguka jointi (synovial biopsy).

MATIBABU
Utamaduni wa mitishamba ya asili ya kihindi maarufu k**a AYURVEDA, kwa muda mrefu sasa umekuwa na matokeo bora Ulimwenguni kwa Kupambana na ugonjwa wa Gauti. Dawa ya ARTHPLUS na MUFASIL ndio mkombozi kwa kupambana na uric acid na yenye matokeo bora katika kukupatia afya njema.

15/09/2023

*FAHAMU JUU YA TATIZO LA PRESHA YA KUPANDA NA YA KUSHUKA PAMOJA NA MATIBABU YAKE*

*Magonjwa ya moyo, presha ya kupanda/presha ya kushuka/presha.*

*Presha ni msukumo wa damu kwenye vishipa vya damu, msukumo huo huzalishwa baada ya moyo kusukuma damu kwenye sehemu mbalimbali za mwili.*

*Aina za presha.*

*Zipo aina kuu mbili za presha, yaani;*
*1️⃣PRESHA YA KUPANDA*
*2️⃣PRESHA YA KUSHUKA.*

*PRESHA YA KUPANDA.*
*Presha ya kupanda ni msukumo wa damu unaosukumwa na moyo kwenda kwenye vishipa vya damu (artery) kuwa mkubwa kuliko njia ya mishipa hiyo.*
*Presha itaitwa kuwa presha ya kupanda ikiwa iko juu zaidi ya presha ya kawaida ambayo ni 120/80mmHg.Presha yaweza kupanda mpaka kufikia 240/120mmHg.*

*SABABU KUU ZA KUPANDA KWA PRESHA*
*1️⃣Utumiaji wa chumvi nyingi kwenye chakula.*
*2️⃣Unywaji wa pombe/sigara uliokithiri.*
*3️⃣Msongo wa mawazo na kutokufanya mazoezi*
*4️⃣Familia zenye matatizo ya moyo pamoja na kurithi.*
*5️⃣uzito mkubwa,unene na kitambi.*

*DALILI ZA PRESHA KUPANDA*
*1️⃣Kushikwa na kizunguzungu*
*2️⃣Kichefuchefu, tumbo kujaa na kutapika kusiko kwa kawaida*
*3️⃣Kuvimba/kujaa maji kwa miguu,uso na mikono.*
*4️⃣Kutokuona vizuri (kuona ukungu).*

*MADHARA YATOKANAYO NA PRESHA KUPANDA*.
*1️⃣ Uvimbe kwenye kuta za vishipa vya damu/kuziba kwa mishipa ya damu(artery) inayopelekea shambulio la moyo (Heart attack).*
*2️⃣Moyo kushindwa kusukuma damu (Heart failure)*
*3️⃣Kiharusi(stroke)*
*4️⃣ Kuharibika kwa ubongo.*

*Kwa upande mwingine;*

*PRESHA YA KUSHUKA.*
*Presha ya kushuka ni ile hali msukumo wa damu unakuwa mdogo kuliko upana (unene) wa vishipa vya damu hali inayopelekea damu chache kufika kwenye ubongo na viungo vingine vya mwili.*
*Presha ikishuka mpaka kufikia 90/60mmHg kutokea 120/80mmHg inatafsiriwa k**a presha iliyoshuka.*
*Presha ya kushuka huchangiwa hasaa na moja ya sababu zifuatazo;*
*🔘Matatizo ya homoni.*
*🔘Maradhi ya moyo pamoja na maambukizo ya vishipa vya damu.*
*🔘Kisukari.*
*🔘Kubeba Ujauzito.*
*🔘Ukosefu wa virutubisho mwilini k**a vile protini,madini ya chuma,Vitamin B-12 n.k*
*🔘Kushikwa na hasira pamoja na msongo wa mawazo.*
*Na moja ya dalili za presha hii ni k**a vile;*
*🔘Mchoko(udhaifu), mwili kukosa nguvu na kuhisi kizunguzungu*
*🔘Maumivu ya kifua pamoja na homa kali*
*🔘Kupumua kwa shida na moyo kwenda mbio (mapigo ya moyo yasiyo ya kawaida).*
*🔘Maumivu kwenye kifua, bega la kushoto pamoja na kiwiko cha mkono.*
*Moja ya madhara yanayotajwa* *yatokanayo na presha hii ni mshtuko/kifo cha ghafla kunakotokana na* *viungo vya mwili kutokupata oxygen ya kutosha.*
*Epuka,dhibiti moja ya mambo yafuatayo ikiwa unasumbuliwa na tatizo la presha (aina zote) pamoja na athari zitokanazo na magonjwa ya moyo.*
*✔️Kupata wasaa wa kufanya mazoezi ya viungo, kukimbilia au kuendesha baiskeli (wastani wa dk 45 kwa siku)*
*✔️Epuka matumizi ya sigara, pombe na matumizi mengine ya madawa k**a Heroine*
*✔️Tumia kiasi sahihi cha chumvi, sukari au mafuta kwenye chakula chako(Sikiliza miongozo ya wataalamu).*
*✔️Pata wasaa wa kupumzika (Zaidi ya saa 8 kwa siku)*
*✔️Punguza unene au uzito uriokithiri kwa kutumia veggie veggie & Detoxilive *

*MATIBABU YA PRESHA_TUMIA MICRO2 CYCLE NA PURE & BROKEN KUTIBU NA KUPONA KABSA TATIZO LA PRESHA*

*FAIDA ZA MICRO2 CYCLE TABLETS & PURE*
*● Huzuia Damu kuwa nzito isivyo kawaida*
*● Husaidia damu kuzunguka kwenye mishipa (capillary) kwa urahisi*
*● Ni nzuri kwa kukinga na kuondoa stroki,Pumu,Presha na kupona kabsa*
*● Inasaidia oxygen na virutubisho kusambazwa kwa urahisi /Huzuia KUSINYAA KWA MISHIPA YA DAMU*
*● Huongeza ufanisi wa mwili kuweza kujiponya wenyewe*
*● Huondoa mafuta ya Lehemu( Cholestral)kwenye kuta za mishipa ya damu*
*● Huongeza ufanisi wa macho kuona vizuri*
*● Huzuia kuganda kwa damu*
*● Huondoa maumivu ya miguu yanayotokana na kuziba kwa mishipa midogo.*
*● Huimarisha mfumo wa Neva ...*
*● NZURI KWA WASIOPATA USINGIZI *
*● Nzuri kwa wenye MAUMIVU YA KICHWA MARA KWA MARA*
*TUNAPATIKANA*
*Arusha*
*Dar es salaam,*
*Mwanza ,*
*Dodoma,*
*Mbeya *
*Morogoro na nk*
*Tunafanya delivery maali ulipo inakufikia bila shaka

09/09/2023

MADHARA YA UPIGAJI PUNYETO. DR. DORCAS

1.PUNYETO INAUA NGUVU ZA KIUME.
Ukipiga punyeto unaweza kusababisha upungufu wa nguvu za kiume,kwani kipindi unapiga punyeto jua ili mishipa inayo fanya uume usimame unakuwa unaichua na uume unakuwa umesimama kwa mda mrefu sasa sasa ikitokea ukawa unafanya hivi kila siku ile mishipa inalegea na uume unakuwa unakosa nguvu hata ukisimama haui strong unakuwa k**a umelegea.

2.KUWAI KUMARIZA MAPEMA KTK TENDO.

Mara nyingi mtu aliyezoea kupiga punyeto huwahi kumaliza mapema pindi akiwa anafanya tendo la ndoa na wakati mwingine uume hushindwa kusimama kwa mara ya pili na kujikuta anashindwa kurudia tendo ikiwa mwezake bado hajaridhika na anahitaji kuendelea kufanya tendo hilo.
athari nyingine ni k**a zifuatazo.

3.uchovu wakati wote, fatigte,feeling tired al the time.
4.maumivu ya nyonga, lower back pain.
5.kusinyaa kwa nywele,nywele kunyonyoka.

30/07/2023

*FAHAMU KUHUSU UGONJWA WA KISUKARI*.

*MSHAURI WA AFYA DR.
☎️📞. 0767388246


⚜️KISUKARI NI NINI....?

*Kisukari* Kwa jina la kitaalamu hujulikana k**a *Diabetes mellitus* huu ni ugonjwa unaoonyesha ongezeko ama kupungua kwa kiwango kikubwa cha sukari kwenye mfumo mzima wa damu.

👉 Mtu yoyote anaweza kupata ugonjwa huu wa sukari pale tu Tenzi iitwayo KONGOSHO itashindwa kuzalisha INSULIN ya kutosha kuweza kuzibiti ongezeko ama kupungua kwa kiwango cha sukari(Glucose) kwenye damu.

👉 Watu wengi tunapata ugonjwa wa kisukari kutokana na mfumo wetu wa Maisha hasa kwenye upande wa ulaji wa vyakula tunavyokula kila siku ambavyo hutumika kwa kuupa mwilini nguvu.

👉 Kwa kawaida kila mwanadamu ana sukari ambayo kwa jina la kitaalamu inafahamika k**a**GLUCOSE** na ndio nishati ya mwili(sukari hii hutumika kuupa mwili nguvu)

***AINA ZA UGONJWA WA KISUKARI**

👉 Kuna aina tatu za kisukari: kisukari cha aina ya 1, kisukari cha aina ya 2 na kisukari cha ujauzito.

1=.✍️ Aina ya 1 ya kisukari (kwa kifupi k**a DM1 au T1DM)

Aina ya 1 ya kisukari (au inayotegemea insulini) ni ugonjwa sugu unaotokana na tenzi ya KONGOSHO kushindwa kuzalisha insulin ya kutosha kuzibiti kiwango cha GLUCOSE kupanda na kushuka kwenye damu.

✍️ Hii ni aina ya ugonjwa wa kisukari ambayo huanza katika utoto na ujana (kati ya umri wa miaka 2 na 25, ndiyo sababu iliitwa ugonjwa wa kisukari wa utoto), ingawa kesi za watu wazima kabla ya umri wa miaka 40 sio kawaida.

2= ✍️ Aina ya 2 ya kisukari (kwa kifupi k**a DM2 au T2DM)

Aina ya 2 ya kisukari (isiyotegemea insulini) ni ugonjwa sugu unaosababishwa na mabadiliko katika kiwango na utendakazi wa insulini inayozalishwa na kongosho kupungukiwa na kinga za eneo ilo kuzidiwa na kiwango cha juu cha sukari kwenye damu.

Ni aina ya mara kwa mara ya ugonjwa wa kisukari (96%), kwa kawaida hutokea katika watu wazima, hasa kwa watu wazito au wanene ambao wana historia ya ugonjwa wa kisukari katika familia.

3=.✍️ Kisukari cha ujauzito (kifupi GDM)

Kisukari cha Gestational (GDM) au kisukari gravidarum ni aina ya kisukari ambacho hutokea kwa takriban 10% ya mimba na mara nyingi hupotea pale tu mama uyu anapojifungua lakini inakuwa ni (hali ya hatari) pia ni kiashiria kibaya cha kupata sukari siku za mbeleni.

Sababu za hatari kwa GDM ni: umri> miaka 35, historia ya familia ya ugonjwa wa kisukari.
NOTE;-
=):Kwa ujumla sukari endapo ikizidi ama kupungua sana ndipo madhara na dalili mbaya huanza kuonekana.

👉 Na sukari inayoingia mwilini inapokuwa nyingi ile ya ziada inahifadhiwa katika ini k**a mafuta. Mafuta hayo hubadilishwa kuwa sukari na kutumika wakati tukiwa na njaa kwa mda mrefu.

**DALILI ZA MGONJWA WA KISUKARI*

1.✍️ Kunywa maji mengi kuliko kawaida na kusikia kiu kila wakati.

2.✍️ Kwenda haja ndogo mara kwa mara na dalili kubwa kwa watoto kukojoa kitandani.

3.✍️ Kuwa dhaifu, kukosa nguvu na kujisikia mchovu kila wakati.

4.✍️ Kupungua uzito au kukonda licha ya kula vizuri.

5.✍️ Kusikia njaa kila wakati na kula sana.

6.✍️ Wanawake kuwashwa sehemu za siri na kupoteza hamu ya kushiriki tendo.
7.✍️ Kupungukiwa uwezo mzuri wa kushiriki tendo la ndoa(upungufu wa nguvu za kiume)

8.✍️ Kutoona vizuri(huoni hafifu)

9.✍️ Kupatwa na ganzi ya miguu na mikono kuwaka moto, kuchomwachomwa au kutohisi unapoguswa sehemu za miguu na hata kupata gangrini.

10.✍️ Kukaukwa na ngozi na ngozi kukosa nuru.

11.✍️ Vidonda au majeraha sehemu yoyote ya mwili kutopona haraka na Majipu mwilini.

12.✍️ Kukojoa mkojo ambao mara baada ya dakika chache hujaliwa na sisimizi.

✍️ Endapo ugonjwa wa kisukari utapuuza au kutotibiwa inavyostahili, yako madhara mengi makubwa yanaweza kujitokeza.

***MADHARA MAKUBWA YA UGONJWA WA KISUKARI***

1. Magonjwa ya moyo.

2. Kiharusi.

3.kupungua kwa nguvu za kiume(uume kutokusimama).

4. Figo kushindwa kufanya kazi

5.Kupata upofu.

6=Viungo vya Mwili kukatwa(ulemavu)

7=Kifo

NOTE;-
Epuka ugonjwa huu kwa kupunguza

1.✍️ Unene uliozidi.(obesity)
2.✍️ Fuata taratibu za kitabibu katika kula na kunywa pia epuka matumizi ya pombe.
3.✍️ Punguza msongo wa mawazo na uvutaji wa sigara.

4.✍️ Kunywa maji ya kutosha, fanya mazoezi na kula kiasi kingi cha mboga mboga na matunda.
****utaratibu huu utakusaidia kuimarisha afya yako na kupunguza hatari ya uongezekaji wa kiwango kingi cha sukari mwilini.

Mara uonapo dalili hizi wahi mapema hospitali kupima ugonjwa wa Kisukari kwani ni miongoni mwa magonjwa hatari yanayochukua muda mrefu kutibika endapo mgonjwa atachelewa kupata matibabu mapema, pia ni miongoni mwa magonjwa ambayo huua kwa kasi zaidi na imechukua nafasi ya tatu sasa kwakusababisha vifo duniani kote.
KWA USHAURI BORA NA NAMNA NZURI YA KUPATA MATIBABU TUWASILIANE KWA SIMU NO. +255(0)767388246

MSHAURI WA AFYA DR.

30/07/2023

*HABARI ZA ASUBUH NDUGU ZANGU NATUMAI KUMEKUCHA SALAMA KABISA, KWA WAGONJWA WA KISUKARI NA PRESSURE NA KWA AJILI YA WOTE PIA...NAPENDA KUWAKUMBUSHA ASUBUHI K**A HII NI MUHIMU KUFANYA MAZOEZI KWANI NO JAMBO LA MUHIMU SANA*

Hii husaidia metabolism ya
mwili kufanya vizuri

Jitahidi kufanya mazoez asubuhi na jioni angalau nusu saa au saa 1 ili kufanya mwili kuwa imara

NB, Kumbuka mbogamboga,matunda na protein ni vitu muhimu Sana kwa kila mlo wako

Mungu awabariki wote.

30/07/2023

Ukimaliza mazoezi jitahidi kunywa maji mengi angalau Lita moja mpaka tatu kwa siku u,maji ni muhimu kunywa alafu ndiyo unakula kitaalamu hushauri ivyo na maji tunayopendekeza ni Moto kwa asubh ni vyema ata kupata glass moja ya maji ya uvuguvugu ndugu zangu🤝🤝

28/07/2023

*MVURUGIKO WA HOMONI (HORMONES IMBALANCE)*

*BY MSHAURI WA AFYA

🛑➡️Mvurugiko wa homoni kwa mwanamke huweza kuchangiwa kutokuwepo na usawa katika homoni zifuatazo Estrogen, Progesterone na Testosterone.

🛑➡️ Kupungua au kuzidi kwa homoni hizi kupelekea mvurugiko wa homoni kwa mwanamke.

*DALILI ZA MVURUGIKO WA HOMONI*

➡️🩸Mfumo wa homoni ni muhimu sana kwa afya ya ubongo na mili yetu. Husaidia kuzuia magonjwa yasiyo ambukizi kadri umri unavyo songa mbele. Baadhi ya dalili zinazoweza kuonekana kwa mtu mwenye changamoto ya mvurugiko wa homoni ni k**a vile:

• ➡️Ukavu ukeni

• ➡️Maumivu wakati wa tendo la ndoa

• ➡️Kutoa jasho usiku

• ➡️Maumivu chini ya kitovu wakati wa hedhi

•➡️ Upungufu wa hamu ya tendo la ndoa

• ➡️Mabadiliko ya siku za hedhi na kupata hedhi kwa muda mrefu unaozidi siku 7. (heavy bleeding, au kujaza pedi moja kwa saa moja)

• ➡️Kukosa hedhi kwa muda mrefu, na kutoa damu yenye mabonge mabonge wakati wa hedhi

• ➡️Uchovu wa mara kwa mara

• ➡️Hasira za mara kwa mara

• ➡️Kukosa usingizi

• ➡️Homa za usiku na Kizunguzungu cha mara kwa mara

• ➡️Mzio wa vyakula (Allergie), kuchagua chagua vyakula

• ➡️Ongezeko ya tumbo na nyama uzembe

• ➡️Kuharibika kwa ngozi (chunusi, vipele)

• ➡️Maumivu ya viungo

• ➡️Upungufu wa nywele kichwani.

• ➡️Kusahau sana (kukosa kumbukumbu)

• ➡️Kuwa na hamu ya kula vyakula au vinywaji vya wa ndani.

• ➡️Kupata hedhi wakati wa ujauzito (progesterone ikiwa imezidi)

•➡️ Kutokupata hedhi (balehe) adi umri wa miaka 20 na kuendelea

• ➡️Mwili kutokukua, kuonekana k**a binti mdogo, na kutokukua kwa via vya uzazi

•➡️ Msongo wa mawazo na kukosa kujiamini

• ➡️Kusinyaa na kupauka kwa
ngozi wakati wa siku za hedhi na wakati wa utumiaji wa njia za uzazi wa mpango

• ➡️Maumivu ya kichwa mara kwa mara

• ➡️Kuwa na tabia ya hamaki (kukosa utulivu)

• ➡️Kutokupata choo kwa wakati

• ➡️Misuli hudondoka

*MADHARA*


🌸 Mimba kuharibika mara kwa mara au Kukosa mtoto au Ugumba

🌸 Maumivu wakati wa tendo la ndoa

🌸 UTI (Urinary Tract Infection)

🌸 Kuziba kwa mirija ya uzazi

🌸 Uvimbe (Fibroids and Cysts)

28/07/2023

DALILI 16 ZA VIDONDA VYA TUMBO

1 kukosa hamu ya kula au kuskia kichefu chefu

2. Maumivu ya tumbo chini au juu upande wa kushoto zaidi

3. Vichomi tumboni au kifuani

4. Mwili kukosa nguvu gafla unapo chelewa kula

5. Kuumwa kichwa mara kwa mara na kuskia kizungu zungu

6. Kiungulia

7. Kukosa choo au kupata choo kigumu na kusababisha tumbo kuwa kuvwa

8. Maumivu ya mgongo hasa upande juu kushoto

9 kukosa hamu ya tendo la ndoa

10. Kuwa na hasira hasira

11. Kuharisha au kutapika

12. Kupata hofu ya gafla bila sababu ya msingi

13. Moyo kulipuka lipuka na kuhisi presha inapanda

14. Presha hushuka au mapigo ya moyo yanapungua

15. Uziplto kupungua

16. Pumzi kupana hasa nyakati za usiku

Chukua tahadhari

Wataalamu wa tiba lishe tunatoa ushauri na tiba ya virutubisho ya kuponesha kabisa vidonda vya tumbo kikubwa ufate ushauri na kutumia dozi kwa usahihi tuu.✍️

Na ili uweze pona kabisa tatizo la vidonda vya tumbo pig ☎️📞+255(0)767 388 246

26/07/2023

*KUTOPATA CHOO KWA MUDA MREFU AU KUPATA CHOO KIGUMU - (CONSTIPATION) - SULUHISHO*

*"CONSTPATION NI NINI ?*

Hili ni Tatizo la kutopata choo Kwa Muda Mrefu au Kupata Mara Chache
Lakini Kwa Shida Sana na Nguvu Kubwa huwa inatumika Katika Kuhakikisha Walau hicho Kidogo Kinatoka K**a Cha Mbuzi .

Want your business to be the top-listed Beauty Salon in Dar es Salaam?
Click here to claim your Sponsored Listing.

Category

Telephone

Website

Address


Dar Es Salaam