ahmashmatasi

ahmashmatasi

Share

Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from ahmashmatasi, Health/Beauty, Dar es Salaam.

09/06/2022

Asalamu alaykum

Ndugu zangu tusipeane mtihani

Sio kila anaeota anafanya tendo la ndoa anajini mahaba

Kuna wanaoota kwasababu ya kukua (baleghe)
Kuna wanaoota kwakuwa hawajashirikibtendo la ndoa kwa muda mrefu
Kuna wanaoota km ndoto ya kawaida tuu (aghalabu huwa na maana ya mafanikio au furaha kwa kadri ya vile atakavyofurahi ktk ndoto)

Sio umeota tuu tendo la ndoa basi nna jini mahaba naomba dawa mambo hayawi hivyo jamani

Usije kutibiwa ukajifanya nawewe tabibu

Photos from ahmashmatasi's post 27/12/2020

Life is full of tests, each and every day you are tested, sometimes you pass, sometimes you fail, all that matters is that you learn.
💪🏿💪🏿💪🏿

Photos from ahmashmatasi's post 02/09/2020

Asalamu alaykum warahmatullahi wabarakaatuh

Usiyasahau mauti maana hata ukiyasahau yenyewe yanakukumbuka

Vyovyote iwavyo iposiku utakua maiti

Cheo nguvu elimu ukubwa mamlaka pesa vyote haviwezi kuzuia umauti

Jiandae muda wowote unaweza kuwa maiti

Tekeleza wajibu wako kwa muumba wako maana ndio njia pekee ya kusalimika kabla na baada ya mauti

Photos 20/08/2020

Asalamu alaykum warahmatullahi wabarakaatuh

Mola ajaalie mwaka 1442 hijria uwe mwaka wa kheri na izzah kwa umma wa kiislamu

Mola atupe nguvu ya kubaki ktk haki hadi mwisho wa uhai wetu bila kukhofu mitihani na lawama za wenye kulaumu

Photos 02/08/2020

ASALAMU ALAYKUM WARAHMATULLAHI WABARAKAATUH

NI BORA UKASAMEHE KULIKO KUHUKUMU KWA MAKOSA

Wengi leo wanajuta kwa maneno ama matendo walioyafanya kwa dhana mbaya

Kila mtu hutazama mambo kwa kipimo chake huenda jambo uliloona ni kosa kwa mtazamo wa mtu mwingine hakuona kua ni kosa aidha kwa kutofahamu ama kwa mazingira aliyopo

Pamoja na kua kutokujua kosa hakukufanyi kutokua mkosefu Jitahidi kujua uhalisia wa jambo kabla ya kulitolea maamuzi maana majuto hua mjukuu na mwenye kuonewa hasahau hujitahidi kuvumilia tuu

Mhukumu mtu kwa kiwango cha kosa lake na k**a huna hakika juu ya kosa lake ni bora ukasamehe

Jitahidi kupunguza mizigo ya matatizo kwa kusamehe na kuwa na hakika na maamuzi yako ili usiwaumize wengine kwa makosa yasiokua yao








#0653732303

12/07/2020

Asalamu alaykum

Ikiwa uwepo wako na kutokuwepo kwako hakuna tofauti jua wewe ni maiti unaetembea

Badilika kuwa mtu mwenye faida kwa umma

.abdallah



#0653732303

10/07/2020

ABU HESHIMA HAILAZIMISHWI

Ni miongoni mwa maneno nilioyapata toka kwa mzee wangu mlezi wangu baba yangu ambae alipenda sana kuniita ABU

Naam heshima hailazimishwi huja kikawaida kulingana na namna ya maisha yako

Mwanao atakuheshimu kulingana na vile unavyoishi nae
Kadhalika ndugu jamaa na marafiki majirani na hata wafanyakazi wenzako ama washirika watakuheshimu kulingana na vile unavyoishi

Ukiwa mlevi utapewa heshima anayostahiki mlevi
Ukiwa mwizi kadhalika utapewa heshima kwa misingi ya wizi
Ukiwa mchamungu utapewa heshima kwa misingi hio n.k

Kamwe usilazimishe kuheshimiwa watu watakupa heshima kulingana na vile wanavyokuchukulia

Usilazimishe watu wakuheshimu utajiingiza ktk msongo wa mawazo bali ishi maisha ambayo unatakiwa kuishi utapata watakao kuheshimu na kukuthamini sana kwa vile ulivyo

Na ni hatari kubwa sana kuigiza maisha ili upate kuheshimika itakupa tabu ktk maisha yako maana utaishi kwa hofu na mashaka kila unapotaka kuwa ktk maisha yako halisi

Usihofie baadhi ya watu kukucheka na kukudharau maana vyovyote iwavyo watu wataendelea kukusema vibaya tuu
lakini punguza hofu maana MRUSHA TOPE HUMRUDIA

Mola akughufirie zambi zako mzee wangu na aifanye kaburi yako kuwa bustani ktk bustani za peponi SHEKH KAMBI RAMADHANI MATASI haupo nasi lakini maneno yako bado yanaishi ktk nafsi zetu



*oudkipanya




#0653732303

08/07/2020

MFANO WAKO NI WENGI

Moja ya walimu zangu alinihadithia wakati anaelekea ma*omoni nchini misri aliona bango limeandikwa مثلك كثير MFANO WAKO NI WENGI

Ni maneno mafupi lakini yana maana kubwa

Yaani ukiwa msomi basi wapo wa*omi wengi mfano wako
Ukiwa muhuni wapo wengi mfano wako
Ukiwa mlevi pia wapo wengi mfano wako
Ukiwa fundi wapo wengi mfano wako

Alayhaal vyovyote utakavyokua wapo wengi km wewe

Nilipotazama maneno ya Allah NAJUU YA KILA MJUZI KUNA MJUZI ZAID

Nikafahamu kua vyovyote utakavyokua kuna watu mbali ya kuwa km wewe bali wamekuzidi ktk hilo ambalo wewe wajivunia kwalo

Km ni elimu mali cheo uzur ujuzi n.k wapo waliokuzidi kiasi huwezi hata kuwakaribia

Maisha ya duniani tunategemeana a*o hili ana lile

Kila mmoja ana umuhimu wake asiekufaa kulima atakufaa kuvuna

Majivuno dharau kujiona n.k havita kusaidia utakapofikwa na mtihani

Thamani ya gari lako la kifahari haitaonekana ukinasa ktk matope na yule anaetembea kwa miguu ndie atakaekuwa msaada kwako

Sote ni sawa tunatakiwa kula tukashiba kuvaa tukasitirika kutibiwa tukiumwa

Hata iwe tutatofautiana ktk namna ya kumaliza shida zetu lakini bado sote ni sawa mbele ya alietuumba kwa muktdha wa kuwa ni binadamu tumetokana na maji tutakwenda kuwa vumbi

Amini usiamini ila
SIKU WATOTO WAMEJAZA MAKOPO UWANJANI KWAKO NAWE UMECHOKA NDIPO UTAKAPOONA UMUHIMU WA CHIZI🚶🚶🚶🚶🚶🚶

07/07/2020

Usilazimishe mwendo ikiwa wewe ni kinyonga wahi kuanza safari mapema usisubiri kuanza safari na farasi atakuacha njiani

Kusota na kukimbia zote ni njia za kujongea muhimu ufike kwa wakati wako sahihi

Ukiona mwenzako amewahi kufika usiwe na pupa nawe muda wako wa kufika utafika tuu

Huenda aliyekutangulia amepitia magumu ambayo lau nawe ungeyapitia yangeondoa uhai wako

KILA UKIONACHO KINA UTAMU NA UCHUNGU CHAGUA KITU AMBACHO UCHUNGU WAKE UNAFAIDA

06/07/2020

MFATILIA MAKOSA YA WATU HUTUMBUKIA KTK MAKOSA MENGI NA HUZUNI NYINGI

Want your business to be the top-listed Beauty Salon in Dar es Salaam?
Click here to claim your Sponsored Listing.

Category

Telephone

Website

Address


Dar Es Salaam

Opening Hours

Monday 08:00 - 18:00
Tuesday 08:00 - 18:00
Wednesday 08:00 - 18:00
Thursday 08:00 - 18:00
Saturday 08:00 - 18:00
Sunday 08:00 - 19:00