AFYA BORA
Umuhimu wa uzazi wa mpango
03/02/2022
Nini kinasababisha kuwahi kufika kileleni?
Kuna sababu nyingi ikiwemo za kisaiokolojia na za kihisia zinazokufanya uwahi kumwaga mbegu na kushindwa kumridhisha mpenzi wako.
Baadhi ya matatizo ya kisaikolojia ni ya muda mfupi. Mfano inawezekana ulishapata tatizo la kuwahi kufika kileleni, lakini kadiri umri unavoenda na kufanya zaidi tendo, unapata uzoefu na tatizo linaisha. Lakini pia kwa upande mwingine tatizo la kuwahi kufanya kileleni linaweza kuongezeka na umri, kutokakana na uzee.
Sababu za kisaikolojia
Kuwahi kufika kileleni kunaweza kuchangiwa na changamoto za kiafya ikiwemo matatizo ya kisaikolojia k**a
Kujiona huna thamani (low self esteem)
Msongo mawazo kupitiliza
Historia ya kunyanyaswa kingono mfano ulazimishwa tendo bila hiyari.
kujiisi mkosaji inaweza kukufanya uwahi kumaliza tendo
Hofu ya kushindwa kumridhisha mpenzi wako
Wasiwasi wa kutokuwa mzoefu wa kimapenzi kuliko mpenzi wako (pengine unahisi atakucheka na kukudharau)
Changamoto za kutoridhika kimapenzi wenye uhusiano wako uliopita
Sababu za kimwili zinazopelekea kuwahi kufika kileleni
Changamoto zingine za kimwili zinaweza kuchangia kuwahi kufika kileleni. Mfano k**a una tatizo la uume kutosimama vizuri inaweza kukufanya uwahi kumwaga kabla uume haujalegea.
Kuzidi kwa baadhi ya homoni k**a testosterone na baadhi ya kemikali(neurotransmitters) zinazozalishwa kwenye neva huchangia kuwahi kumwaga mbegu. Kuvimba kwa tezi dume au njia ya mkojo inaweza kupeleka dalili mbaya ikiwemo uume kulegea na kuwahi kumwaga mbegu.
Tiba ya kuwahi kufika kileleni
Kwa kiasi fulani unaweza kutibu tatizo kwa kurekebisha mtindo wa maisha na vyakula. Baadhi ya waaume wanasolve tatizo kwa kupiga punyeto goli la kwanza kabla ya kuanza tendo.
Pia unaweza kujaribu michezo mingine ya kimahaba kwa nusu saa kabla ya kumuingilia mwanamke. Hii itapunguza ule muhemko na presha ya tendo.kwa mawasiliano ☎️zaid +255768464704
02/02/2022
KUWAHI KUFIKAKILELENI KWA WAVULANA KWENYE TENDO
Pre mature ej*******on ni nini?
Hii ni hali ambayo mwanaume anatoa mbegu mapema sana kipindi cha tendo la ndoa na mara nyingi huambatana na kushindwa kumridhisha mpenzi wake.
Tatizo hili limekua likiwapata wanaume wengi na kujisikia aibu mbele za wenzi wao pale wanaposhindwa kuendelea kabisa baada ya hali hii kutokea.
Kimsingi mwanaume anatakiwa achukue dakika nne mpaka nane kabla ya kutoa mbegu za kwanza lakini watafiti wanasema tatizo hili hugundukiwa mtu anapotoa mbegu ndani ya dakika moja au kabla ya dakika moja. Tatizo hili huweza kutokea mara tu baada ya kubalehe,{primary pre mature ej*******on} mda mrefu baada ya kubalehe{secondary PE} au kutokana na aina ya mwanamke uliompata.{situational PE}
Chanzo ni nini?
Tatizo hili halina sababu za kitaalamu zilizofanyiwa utafiti zikakakubalika ila wanasayansi wanaamini sababu zifuatazo zinaweza kua chanzo kikuu cha tatizo hilo
Kupiga punyeto au kujichua;
Mara nyingi watu wanaopiga punyeto hua wanafanya haraka kwa kujificha ili wasikutwe na mtu. tabia ile ya kulazimisha mbegu zitoke haraka huweza kuleta tatizo
Kukaa muda mrefu bila kushiriki tendo la ndoa;
Kukaa muda mrefu sana bila kushiriki tendo la ndoa husababisha mkusanyiko mkubwa wa mbegu za kiume ambazo zinaleta msisimko mkubwa na ukichelewa sana kushiriki tendo la ndoa zitatoka kwenye ndoto nyevu. Kawaida mwanaume anatakiwa ashiriki tendo angalau mara nne kwa wiki.
Kuwa na wasiwasi wakati wa tendo la ndoa;
Mtu akiwa na historia ya kupata hali hii kabla, huwa hajiamini na kuwa na wasiwasi kwamba litatokea tena na matokeo yake hulipata kweli.
Madhara ya dawa zinazofanya kazi kwenye mishipa ya fahamu;
Baadhi ya dawa za usingizi, mawazo na zingine zinazofanya kazi kwenye mishipa ya fahamu huleta tatizo hili mfano amitriptyline.
Diagnosis{ kuutambua ugonjwa]
Mwanaume yeyote ambaye anatoa mbegu chini ya dakika moja au mbili ni muhanga wa hili tatizo na anatakiwa apewe matibabu.
Kurithi;
Baadhi ya koo au familia fulani hurithi vimelea vya kuwa na ugonjwa huu kwa vizazi mbalimbali vya familia husika.
Magonjwa ya mfumo wa uzazi wa mwanaume mfano prostatitis.
Matibabu
Matibabu ya ugonjwa huu yamegawanyika sehemu kuu mbili kulingana na ukali wa tatizo husika.
Non pharmacological treatment{matibabu yasiyo hitaji dawa}: Matibabu haya hupewa watu ambao wanahimili mpaka dakika tatu bila kutoa mbegu.
Pharmacological treatment{matibabu yanayohusu dawa}: Matibabu haya hupewa watu ambao hutoa mbegu ndani ya dakika moja baada ya kuanza kushiriki tendo la ndoa, watu hawa hushauriwa kutumia na mbinu zote mbili za matibabu.
Kwa maelezo zaid wasiliana nasi ☎️+255768464704 WhatsApp &☎️
31/01/2022
MATATIZO YANAYOHUSIANA NA HEDHI YA KILA MWEZI
Iwapo unapata matatizo kuhusiana na hedhi, jaribu kuongea na mama yako, dada zako au marafiki zako. Unaweza kugundua kwamba hata wao wanayo matatizo yanayofanana na wanaweza kukusaidia.
Mabadiliko ya hedhi
Wakati mwingine ovari hazitoi yai. Hili likitokea, mwili hutengeneza homoni ya projesteroni kidogo, ambayo inaweza kusababisha mabadiliko ya lini hedhi itatokea na kiasi cha damu. Wasichana ambao ndiyo wameanza kupata hedhi, au wanawake ambao wameacha kunyonyesha siku za karibuni – wanaweza kupata hedhi kwa miezi michache au kupata damu ya hedhi kidogo au kupata damu nyingi kupita kiasi. Mizunguko yao hutulia taratibu na hatimaye kurudia hali ya kawaida baada ya muda.
Wanawake wanaotumia njia za uzazi wa mpango za homoni wakati mwingine hujikuta wanapata hedhi katikati ya mwezi.
Wanawake wenye umri mkubwa ambao bado hawajafikia hatua ya hedhi kukomaa wakati mwingine hutokwa na damu nyingi zaidi, na wakati mwingine mara nyingi zaidi kuliko walivyokuwa wakati wa ujana. Wanavyokaribia umri wa hedhi kukomaa, wanaweza kutopata hedhi kwa miezi kadhaa, na baadaye kurudia kupata hedhi tena k**a kawaida. Maumivu wakati wa hedhi ya kila mwezi
Wakati wa hedhi, tumbo hujikamua kusukuma utando ili uweze kutoka nje. Kujikamua kwa tumbo kunaweza kusababisha maumivu eneo la chini ya tumbo au mgongo. Maumivu yanaweza kuanza kabla ya hedhi au punde mara baada ya hedhi kuanza.
Jambo la kufanya:
dole gumba likibonyeza sehemu laini kwenye kiganja
Kubonyeza kwa nguvu sehemu laini kati ya dole gumba lako na kidole cha pili kunaweza kusaidia kutuliza aina nyingi za maumivu
Pangusa sehemu ya chini ya tumbo. Hii itasaidia kulegeza misuli.
Jaza chupa ya plastiki au chombo kingine maji ya moto na kukiweka juu ya sehemu ya chini ya tumbo lako au sehemu ya chini ya mgongo. Au tumia kitambaa kizito ambacho kimelowekwa kwenye maji ya moto. Jaribu kufanya mazoezi na kutembea
Dalili za awali za hedhi
mwanamke akionekana kutojisikia vizuri, akiwa ameshikilia paji la uso na tumboni
Baadhi ya wanawake na wasichana hujisikia vibaya siku chache kabla ya kuingia kwenye mzunguko wao wa hedhi ya kila mwezi. Huweza kupata kundi moja au zaidi ya dalili zifuatazo, ambazo hujulikana k**a dalili za awali:
Maumivu ya matiti.
Kujisikia tumbo la chini kujaa.
Shida katika kupata choo.
Kusikia uchovu usiyo wa kawaida
Wanawake wengi hupata angalau dalili mojawapo kila mwezi na baadhi ya wanawake hupatwa na dalili zote. Mwanamke anaweza kupata dalili tofauti kutoka mwezi mmoja kwenda mwingine. Kwa wanawake wengi, siku zinazotangulia hedhi huwa ni siku zisizo na utulivu. Lakini wanawake wengine husema kwamba hujisikia vizuri zaidi kwa maana ya ubunifu na utendaji wao kwa ujumla. Jambo la kufanya:
Kinachomsaidia mwanamke kukabiliana na dalilia za awali za hedhi hutofautiana kati ya mwanamke mmoja na mwingine. Ili kuweza kujua ni njia ipi itakusaidia, mwanamke anapaswa kujaribu njia tofauti kuona ni ipi inampa unafuu zaidi
Yafuatayo ni mawazo mengine ambayo yanaweza kukusaidia:
Punguza matumizi ya chumvi. Chumvi hufanya mwili ulimbikize maji mengi ndani, hali inayokufanya kuhisi tumbo lako sehemu ya chini kujaa.
Epuka vinywaji vyenye kemikali ya kafeini vikiwemo kahawa, chai, na soda za aina ya kola.
Jaribu kula nafaka ambazo hazijachakatwa, karanga, samaki wabichi, nyama, maziwa au vyakula vingine vyenye protini.
30/01/2022
Jinsi mwili wa mwanamke unavyobadilika
Mwili wa mwanamke hupitia mabadiliko mengi muhimu katika kipindi cha uhai wake – wakati wa kupevuka,wakati wa balehe, wakati wa ujauzito na unyonyeshaji, na wakati hedhi inapokomaa-umri wa kutoweza kuzaa tena. Zaidi ya hayo, wakati wa umri wa kuzaa, mwili wake hubadilika kila mwezi – kabla, wakati na baada ya hedhi ya kila mwezi. Sehemu za mwili ambapo mabadiliko haya hutokea ni ukeni, mji wa mimba(kizazi), ovari, mirija ya mayai ya uzazi, kwenye matiti-sehemu zote hizo huitwa mfumo wa uzazi. Mabadiliko haya mengi husababishwa na kemikali za asili maalum ziitwazo homoni.
Homoni
Homoni ni vichocheo vya kemikali ambavyo mwili hutengeneza kudhibiti namna mwili unavyokua na lini. Muda kidogo kabla ya msichana kuanza hedhi ya kwanza ya kila mwezi, mwili wake huanza kutoa kwa wingi homoni ya estrojeni na projesteroni, ambazo ndiyo homoni kubwa za k**e. Homoni hizi husababisha mabadiliko makubwa kwenye mwili wake yaitwayo balehe. Wakati wa umri ambao msichana anaweza kubeba mimba, homoni hizi huwezesha kila mwezi mwili wa mwanamke kujiandaa kuwa tayari kwa uwezekano wa kubeba mimba. Pia huziambia ovari zake lini kuachia yai (yai moja kila mwezi). Hivyo homoni huamua lini mwanamke anaweza kubeba mimba. Njia nyingi za uzazi wa mpango hufanya kazi ya kuzuia mimba kwa kudhibiti, Homoni pia husababisha mabadiliko wakati wa ujauzito na wakati wa unyonyeshaji. homoni huzuia mwanamke anayenyonyesha asipate hedhi, na wakati wa ujauzito na mara baada ya kujifungua husababisha matiti kuanza kutengeneza maziwa. Ovari zake husitisha utoaji mayai, mwili wake huacha kujiandaa kwa ajili ya kubeba mimba, na hedhi yake ya kila mwezi husitishwa kabisa. Kipindi hiki huitwa ukomo wa hedhi (menopause).
Kiasi na aina ya homoni zinazozalishwa na mwili wa mwanamke zinaweza pia kuathiri namna anavyojisikia kwa ujumla, hisia zake kuhusiana na ngono, uzito wake, joto lake la mwili, njaa, na hata uimara wa mifupa yake. Kwa maelezo zaid +255768464704☎️whatsapp&kawaida
28/01/2022
Ni kweli kuna madhara ya njia za kisasa za uzazi wa mpango kwa wanawake?
Masuala ya uzazi na malezi kwa wanawake ni jambo lililo wazi kabisa lakini kutokana na maadili baadhi wamekuwa na woga wa kujadili wazi wazi. Hata vivyo baadhi ya wanawake hawa hupenda kuzungumzia maswala haya hasa wanapo kutana ili kubadilisha mawazo na hata kujifunza zaidi.
Katika swala la uzazi majadiliano mara kwa mara yamekuwa ni kuhusu malezi, kunyonyesha kipindi cha mimba na hasa njia gani itumike katika uzazi wa mpango ambayo ni salama na haina madhara.
Kuna ambao hutumia njia za asili za uzazi wa mpango, mfano mbinu ya kutegemea kalenda ambayo hufuata mzunguko wa hedhi au kumwaga mbegu za kiume nje ya njia ya uzazi.
Baadhi ya wanawake huchagua kutumia njia za uzazi wa mpango za kisasa, mfano: kuweka kitanzi au sindano.
NJIA MBALI MBALI ZA KISASA ZA UZAZI WA MPANGO
Njia ya Vidonge
•Njia ya sindano
•Kutumia kizuizi yaani kondom ya k**e au ya kiume
•Kuweka Kitanzi
•Kuweka kipandikizi/ Kijiti
Hata hivyo kumekuwa na majadiliano ama jumbe mbali mbali katika mitandao ja kijamii zinazo zungumzia madhara ya njia za kisasa za uzazi wa mpango.
Baadhi ya madhara yanayo tajwa ni hatari kwa kutumia uzazi wa kisasa .
kupata ugumu wa kushika mimba baada ya kutumia njia hizo, kutokwa na damu mara kwa mara, kupungua au kuongezeka mwili, kuongezeka kwa hamu ya kula, kupotea kwa hamu ya tendo la ndoa, mabadiliko ya siku za hedhi, maumivu ya kichwa, nk.
Kwa Ushauri ushauri kwa wanawake na wanaume kuwa ni vyema wakazielewa njia zote za uzazi wampango kabla ya kutumia.
Kwa Maelezo Zaid wasiliana nasi ☎️+255768464704Whatsapp &phone call
27/01/2022
Je! Unajuwa Shindano za Uzazi Kwa Mwanamke huchelewa kupata mimba endapo utatumia?
Moja ya madhara ya njia hii ya uzazi wampango ni pamoja na:kusababisha Mwanammke Kuchelewa Sana Kubeba mimba pale anapohitaji yaani kwa kitaalamu Prolonged fertility ability.
Hivo Sindano za Uzazi wa Mpango huweza kuchelewesha uwezo wa mwanammke kubeba mimba pamoja na madhara mengine K**a Vile kulainisha mifupa,Kublid damu nying kwa muda mrefu zaid n.k
Kwa Ushauri Zaidi Elimu Au Tiba Juu ya Tatz Lolote tuwasiliane Kwa Namba ☎️+255768464704 WhatsApp & cell phone
27/01/2022
Kwa elimu Tiba Ushauri unapatikana apa kwa mawasiliano zaid +255768464704☎️WhatsApp &normal cell kwa pamoja tunaweza 💪🏿🇹🇿
27/01/2022
Mfumo wa uzazi wa mwanaume
Katika sura hii:
Sura ya 4: Kuielewa miili yetu
Mfumo wa uzazi wa mwanamke
Mfumo wa uzazi wa mwanaume
Jinsi mwili wa mwanamke unavyobadilika
Mzunguko wa hedhi wa kila mwezi
Viungo vya uzazi vya mwanaume ni rahisi kuonekana kuliko vya mwanamke kwa sababu kwa sehemu kubwa vipo nje ya mwili. Mapumbu, korodani au makende ndio hutengeneza homoni kubwa ya kiume kwenye mwili iitwayo testosteroni. Mvulana anapopita katika kipindi cha balehe, huanza kutengeneza homoni ya testosteroni kwa wingi. Homoni hii ndiyo huleta mabadiliko yanayomfanya mvulana azidi kuonekana k**a
mwanaume. Mfumo wa uzazi wa mwanaume
Katika sura hii:
Sura ya 4: Kuielewa miili yetu
Mfumo wa uzazi wa mwanamke
Mfumo wa uzazi wa mwanaume
Jinsi mwili wa mwanamke unavyobadilika
Mzunguko wa hedhi wa kila mwezi
Vitu go vya uzazi vya mwanaume ni rahisi kuonekana kuliko vya mwanamke kwa sababu kwa sehemu kubwa vipo nje ya mwili. Mapumbu, korodani au makende ndio hutengeneza homoni kubwa ya kiume kwenye mwili iitwayo testosteroni. Mvulana anapopita katika kipindi cha balehe, huanza kutengeneza homoni ya testosteroni kwa wingi. Homoni hii ndiyo huleta mabadiliko yanayomfanya mvulana azidi kuonekana k**a mwanaume.
mwanaume.
mwanaume akiwa uchi, anavyoonekana kutoka mbeleillustration of the parts described belowKibofu cha mkojoUumeMrija wa mbegu za kiumePumbu, korodani au kendeMfuko wa mapumbu au korodaniMrija wa kupitisha shahawa na mkojo
Mapumbu au korodani ndiyo begu za kiume husafiri kutoka kwenye pumbu kupitia mrija ndani ya uume mahali ambapo huchanganyika na majimaji yanayotengenezwa na tezi maalum.
Mchanganyiko wa mbegu na majimaji hayo huitwa shahawa au manii. Shahawa huachiwa na mwanaume anapofikia kilele wakati wa tendo la ngono. Kila tone la shahawa lina maelfu ya mbegu za kiume ambazo haziwezi kuonekana kwa macho.
26/01/2022
Kansa ni ugonjwa unaotokea baada ya kuharibika pia kubadilika kwa seli na kuanza kuzaliana katika mili nazo huitwa seli za kansa, Kansa hutokea kwa binadamu, wanyama na viumbe hai wengine. Seli huharibika,hurekebishika au kufa, ila seli zisipokufa au zisipo rekebishika huwa seli zisizo za kikawaida (hazihitajiki mwilini) ndipo huanza kuzaliana na kuwa seli za kansa. Seli za kansa hutumia seli za kawaida kuzaliana, kusafiri kwa kutumia damu na lymph. Seli za kansa huzaliana na kuhama tokea upande mmoja wa mwili kwenda mwingine hii hali huitwa metastasis
Kansa ni ugonjwa unaouwa kwa kiasi kikubwa duniani, idadi ya watu millioni 8.2 walikufa (Ikiwa ni asilimia 22% ya vifo vyote; Hizi ni taarifa kutoka Shirika la Afya duniani (World Health Organization,2016)). Na ikikadiriwa kufika mwaka 2030 idadi ya vifo kuwa million 13.1. Aina ya kansa zinazoongoza kuua kila mwaka ni pamoja na kansa ya mapafu, kansa ya tumbo, kansa ya ini, kansa ya utumbo, kansa ya matiti kwa mawasiliano zaid +255768464704 WhatsApp &normal call ☎️
21/01/2022
Huduma ya afya ya kimsingi ni nini?
Huduma ya afya ya kimsingi ni utaratibu unaoangazia afya na uzima wa jamii, huduma hizo zikijikita kwenye mahitaji na matakwa ya watu binafsi, familia na jamii. Hushughulikia masuala mapana yanayoelekeza afya na huangazia hali kamili na yenye mfanano kuhusu afya na uzima wa kimwili, akili na kijamii.
Hutoa huduma zote za afya kwa mtu katika maisha yake yote, sio tu kwa maradhi fulani. Huduma ya afya ya kimsingi huhakikisha watu wanapokea huduma kamili -kuanzia mahimizo na kuzuia hadi matibabu, urekebishaji na utunzaji –zikikaribia sana mazingira ya watu ya kila siku.
Huduma ya afya ya kimsingi imejikita katika kujitolea kudumisha haki na usawa wa kijamii na kutambuliwa k**a haki muhimu ya kufikia kiwango cha juu zaidi cha vigezo vya afya, k**a inayoelezwa katika Kifungu cha 25 cha Azimio la Kimataifa la Haki za Binadamu: “Kila mtu ana haki ya kufikia kiwango cha maisha yenye afya na uzima wake na wa familia yake, ambayo ni pamoja na chakula, mavazi, nyumba na matibabu na huduma zinazohitajika za kijamii[…]”.
Wazo la huduma ya afya ya kimsingi limeangaliwa upya mara kadhaa na kufafanuliwa upya. Katika baadhi ya miktadha, limerejelewa k**a utoaji wa huduma za ambulansi ama ngazi ya kwanza ya huduma za afya anazopokea mtu. Katika miktadha mingine, huduma ya afya ya kimsingi, imeeleweka k**a kundi la hatua muhimu za usaidizi wa kiafya kwa watu wa mapato ya chini (inatambuliwa pia k**a huduma banifu za afya). Wengine wameielewa huduma ya afya ya kimsingi k**a sehemu muhimu ya ukuaji wa binadamu, ikiangazia masuala ya kiuchumi, kijamii na kisiasa.
WHO imebuni fasili linganifu inayoegemea masuala matatu:
kutimiza mahitaji ya watu ya kiafya kupitia njia pana ya kuhimiza, kulinda, kuzuia, kutibu, kurekebisha na kutunza katika kipindi chote cha maisha, kwa kuzipa umuhimu huduma kuu za afya zinazolenga watu binafsi na familia kupitia kwa matibabu ya kimsingi, na watu kupitia kwa hafla za afya ya umma k**a masuala makuu ya huduma jumuishi za afya;
Kushughulikia kwa mpangilio masuala mapana yanayoelekeza afya (yakijumuisha ya kijamii, kiuchumi, mazingira, pamoja na desturi na tabia za watu ) kupitia sera thibitifu na fafanuzi ya umma, pamoja na hatua zilizochukuliwa katika sekta zote; na
Kuhamasisha watu binafsi, familia na jamii kuimarisha afya yao, k**a watetezi wa sera zinazohimiza na kulinda afya na uzima, k**a washirika wenza wa kuendeleza afya na huduma za afya za kijamii, na ili waweze kujitunza kibinafsi na kuwatunza wengine.
Click here to claim your Sponsored Listing.
Category
Contact the business
Telephone
Website
Address
Tanzania Street
Dar Es Salaam
