dr. Ndauka

dr. Ndauka

Share

tunawasaidia wahanga wa magonjwa mbalimbali kwa kuwapa ushauri na tiba asili kwa kutumia mimea tiba.

19/02/2023

Welcome to swiha herbal clinic

19/02/2023

*VIDONDA VYA TUMBO(PEPTIC ULCERS),SABABU, DALILI NA TIBA ZAKE*

*VIDONDA VYA TUMBO*
Hivi ni vidonda ambavyo vinapatikana kwenye kuta za tumbo (stomach) na utumbo mwembamba (duodenum).

*▪️FAIDA*
_Kwenye kuta za tumbo kunazalishwa utando mzito wa k**asi (protective mucous coating) kwaajili ya kulilinda tumbo na utumbo mwembamba. Pia huzalishwa asidi (Hydrochloric acid) kwaajili ya kusaidia kumeng'enywa chakula na kuua vijidudu (bacteria) wanaongia tumboni kupitia chakula, maji au kugusana midomo kati ya m/Maambukizi na mzima mfano kissing ._

*SABABU ZA VIDONDA VYA TUMBO*
Vidonda vya tumbo husababishwa na sababu kuu mbili.:

1.*▶️ Maambukizi ya bacteria (Helicobacter Pylori i.e H.Pylori infections)*
H.pylori mara baada ya kuingia tumboni hudhoofisha ute mzito wa k**asi ndani ya tumbo na utumbo mwembamba, hivyo huruhusu asidi kupenya na kuingia ndani zaidi ya kuta za tumbo. Asidi na bacteria husababisha maumivu na kidonda kwenye kuta za tumbo na utumbo mwembamba. Umbile la mnyongoroto la huyu bacteria pia huchangia kuchimba zaidi kuta za tumbo na utumbo mwembamba.
_*FAIDA*_
Nilisema ndani ya tumbo kunazalishwa asidi kwaajili ya kuua vijidudu (bacteria).
_*Swali*_: Kwanini bacteria huyu hauliwi(hadhuriki) na hiyo asidi?.
_*Jibu*_: H.pylori anaweza kuishi tumboni bila kuuliwa na hiyo asidi kwasababu anajizalishia kemikali (enzymes) iitwayo *UREASE ENZYMES*, ambayo inabadili urea kuwa ammonia (basic compound) ambayo inapambana na asidi (neutralization) na kufanya mazingira yawe ya kawaida kwake.

2.*▶️ Matumizi ya muda mrefu madawa ya kuondosha maumivu (Nonsteroidal anti-inflammatory drugs i.e NSAIDS)*
Ndani ya tumbo na utumbo mwembamba kunazalishwa kemikali iitwayo *Cyclo -oxygenase (COX-1)* isoenzymes inayobadili asidi iitwayo *arachidonic acid* kuwa kemikali iitwayo *prostaglandins*. Hii prostaglandin huupa ukuta wa tumbo na utumbo mwembamba ulinzi. Madawa haya ya kuondosha maumivu mfano Aspirin,Ibuprofen Diclofenac n.k yanapotumika kwa muda mrefu huleta madhara ya kuzuia kuzalishwa kwa COX-1 ambapo husababisha prostaglandin iwe finyu tumboni mwishowe kuta za tumbo hupata michubuko na vidonda vya tumbo hutokea.

*▪️ DALILI ZA VIDONDA VYA TUMBO*
Hizi ni baadhi ya dalili za mgonjwa wa vidonda vya tumbo:
1.👉🏽 Kuhisi maumivu katikati au juu ya tumbo na kupata nafuu mara baada ya kula chakula au kunywa dawa za kupunguza asidi tumboni (antiacid medications).
2.👉🏽 Kujihisi tumbo limejaa, kubeua muda wote.
3.👉🏽 Kujihisi kiungulia
4.👉🏽 Kujisikia kichefuchefu
5.👉🏽 Kutapika au kutapika damu yenye mchanganyiko wa damu
6.👉🏽 Kupata choo kikubwa kigumu cheusi au chenye damu yenye uweusi.
7.👉🏽 Kujisikia kizunguzungu
8.👉🏽 Kupungukiwa na uzito kusiko kawaida
9.👉🏽 Kubadilika kwa hamu ya kula
10.👉🏽 Kujihisi maumivu ya mgongo, kifua au mbavuni.

*VICHOCHEZI VYA TATIZO*
Unaweza kuongeza ukubwa wa tatizo la vidonda vya tumbo au kuchelewa kupona hata K**a unatumia dawa ikiwa utafanya yafuatayo:
1. Uvutaji sigara (smoking)
2. Unywaji wa pombe (alcohol drinking)
3. Kuwa na msongo wa mawazo kupitiliza (untreated stress)
4.Kula vyakula vyenye viungo vingi
5. Kunywa kahawa
6. Kula vyakula vyenye kuleta gesi.
7. Kula vyakula vyenye asidi mfano jamii ya ndimu au nyanya.
8. Kula kupita kiasi
9. Kutokua na ratiba maalum ya kula mfano kukaa na njaa kwa muda mrefu n.k
_Itambulike hizi sio visababishi vya vidonda bali huchochea vidonda kutopona na kuchimbika zaidi._

*DALILI HATARISHI ZA VIDONDA VYA TUMBO (COMPLICATIONS)*
Vidonda vya tumbo vikiiachwa bila kutibiwa kwa muda mrefu au mgonjwa akijiweka kwenye vichochezi, hujiweka kwenye dalili hatarishi k**a zifuatazo:
1.👉🏽 Damu kuvujia ndani ya tumbo (internal bleeding)
2.👉🏽 Kupatikana tundu ndani ya tumbo au utumbo mwembamba(percolation)
3.👉🏽 Kuziba kwa njia ya chakula kitokacho tumboni kwenda kwenye utumbo mwembamba(obstruction).
4.👉🏽 Kupata saratani ya tumbo(gastric cancer)
5.👉🏽 Kupoteza maisha(death)

*TIBA ZA VIDONDA VYA TUMBO*
Tiba za vidonda vya tumbo ziko za aina mbili:
1.✍🏾 Tiba za kisasa (Hospital).
2.✍🏾 Tiba ya asili (Herbal medicines)
*1.Tiba za kisasa(Hospital)*
Hospitalini hutoa tiba za aina mbili
*▪️ ANTIBIOTICS*
Hizi ni dawa zinazofanya kazi ya kuua vijidudu (bacteria) mfano; metronidazole, tetracycline,clarithromycin, amoxicillin,cimetidine,ranitidine, famotidine,nizatidine n.k
_Dawa hizi huuwa bacteria tu, hivyo k**a mgonjwa ana dalili za mwanzo kabisa za kushambuliwa na bacteria H.pylori baada vipimo atapona kabla ya bacteria huyo kuleta madhara zaidi ya kuleta kidonda kwenye kuta za tumbo au utumbo mwembamba. K**a utachelewa na kujitibu mpaka bacteria akaleta kidonda,wakati huo dawa hizi zitaua bacteria lakini hazitoponesha vidonda.Mgonjwa ataendelea kujisikia dalili za vidonda vya tumbo licha ya kwamba akipimwa hospital (blood test au stool test) huambiwa hana vidonda_

*▪️PROTON PUMP INHIBITORS*
Hizi dawa ambazo husaidia kupunguza uzalishaji wa asidi tumboni kwa kuzuia *histamine* ambayo huchochea kuzalishwa kwa asidi iingie tumboni. Dawa hizi husaidia kupunguza maumivu ya kidonda kwa muda wa wiki chache, mfano; Omeprazole, esomeprazole, pantoprazole n.k

*2.Tiba ya asili(Herbal medicines)*
Hapa anashauriwa atumie dawa ya asili inayoitwa *PEPTIC SOLUTION* kwani hii dawa bora imetenezwa kwa mchanganyiko wa miti ambayo inauwezo wa kutibu ulcers kwa haraka sana hata vidonda vikiwa sugu.
Dawa hii inapatikana madukani kwetu tupo Ilala, Dar es salaam

Kwa mawasiliano zaidi tupigie
0745 217510
Dr.Ndauka
WhatsApp: 0674414276
Nyote mnakaribishwa.

Want your business to be the top-listed Beauty Salon in Dar es Salaam?
Click here to claim your Sponsored Listing.

Category

Telephone

Website

Address


Pangani Street
Dar Es Salaam
2015