Acid Reflux
Health/Medical (Acid reflux)
21/08/2023
SULUHISHO LA KUZIDI KWA KIWANGO CHA ACID TUMBONI (ACID REFLUX).
____________________________________________
PANDEX HERBAL CLINIC
PHONE: +255749526546
Gastroesophageal reflux disease (GERD-ACID REFLUX).
⚫ Ni hali inayotokana na kuzidi kwa kiwango cha Acid tumboni (Hydrochloric Acid) ambapo hupelekea kupanda kwa acid kutoka tumboni kuelekea katika koo la Chakula (Oesophagus) na kupelekea kudhurika/Kuharibika kwa mfumo wa chakula upande wa juu ambao unahusisha koo la chakula na mdomo pia.
⚫ Watu wengi sana wanasumbuliwa na tatzo hili bila wao kujua wanasumbuliwa na tatzo hili na hufikia hatua wengine kudhani wamerogwa kutokana na dalili za tatzo hili. Tutaangalia dalili ambazo mtu anaweza kugundua kuwa anasumbuliwa na tatzo hili katika kila hatua.⤵️
________________________________________
HATUA ZA GERD (GASTROESOPHAGEAL REFLUX DISEASE) NA DALILI ZAKE.
________________________________________
Zipo hatua 4 ambazo GERD (kuzid kwa acid tumbon) hupitia,hatua hizo ni k**a ifuatavyo:⤵️
_____________________________________
1️⃣.HATUA YA KWANZA (MILD GERD).
_____________________________________
Wengi katika watu wanaosumbuliwa na GERD huangukia katika hatua hii ya kwanza ya GERD ambapo tatizo huwa katika hatua za mwanzo sana.
___________________________________________
DALILI ZA GERD HATUA YA KWANZA (MILD GERD)
___________________________________________
1.🖇️ Kiungulia
2.🖇️ Maumivu ya kifua
3.🖇️ Kuhisi k**a kuna vitu vya kunata katika kooni
4.🖇️ Kucheua chakula au vinywaji
⚫ Katika Hatua hii,mtu anaweza kujitibia kwa kubadili mfumo wake wa maisha kwa kuepuka vyakula na mifumo isiyofaa kutokana na hali yake mfano ajiepushe na Caffeine, pombe,vyakula vyenye mafuta mengi nk. Lakini pia ni rahisi mgonjwa kupona akitumia dawa katika hatua hii ya awali.
________________________________________
2️⃣ HATUA YA PILI YA GERD (MODERATE GERD)
________________________________________
Katika hatua hii,watu wenye GERD hupatwa na dalili za GERD mara kadhaa ndani ya wiki na dalili zake hutokea mara kwa mara ukilinganisha na Hatua ya kwanza na dalili huanza kuwa kali kiasi.
____________________________________________
DALILI ZA GERD HATUA YA PILI (MODERATE GERD)
____________________________________________
1.🖇️ Kiungulia kikali kiasi
2.🖇️ Maumivu ya kifua
3.🖇️ Kuhisi uteute wenye kunata kooni
4.🖇️ Kucheua chakula au vinywaji
5.🖇️ Moyo kupaparika(Heart palpation)
⚫ Katika hatua hii,mtu anahitajia matibabu ya dawa pia kumshirikisha daktar kwaajili ya ushauri wa kimatibabu na dawa.
_____________________________________________
3️⃣.HATUA YA TATU YA GERD (SEVERE GERD)
_____________________________________________
Katika hatua hii,asilimia 15% ya wagonjwa waliopo katika hatua hii hupata dalili za GERD kali mara nyingi zaid kwa wiki au kila siku.
__________________________________________
DALILI ZA GERD HATUA YA TATU (SEVERE GERD)
__________________________________________
1.🖇️ Kiungulia kikali
2.🖇️ Kucheua sana chakula na vinywaji na wakati mwingine kucheua Acid (uchachu)
3.🖇️ Kuvimba kwa koo(sore throat)
4.🖇️ Kikohozi kisichoisha
5.🖇️ Sauti ya kukwaruza
6.🖇️ Mapigo ya moyo kwenda kasi
7.🖇️ Wasiwasi uliopita kiasi bila sababu
8.🖇️ Kuota ndoto za kutisha
9.🖇️ Kichwa Kuvurugika na kuhisi kuchanganyikiwa
10.🖇️ Kizunguzungu
11.🖇️ Maumivu ya kichwa
12.🖇️ Macho kupungua nguvu ya kuona
13.🖇️ Maumivu makali ya mgongo
14.🖇️ Mwili kudhoofika
15.🖇️ Kuhisi dunia imekutenga
16.🖇️ Kujisaidia choo kigumu zaidi.
⚫ Katika hatua hii,GERD isipochukuliwa hatua basi kuna hatari ya mtu kupata matatzo makubwa zaid ya kiafya k**a vile KANSA YA KOO (EUSOPHAGEAL CANCER).
___________________________________
4️⃣.HATUA YA NNE YA GERD (REFLUX-INDUCED PRECANCEROUS LESIONS/ESOPHAGEAL CANCER)
____________________________________
Hatua hii inawakilisha matatzo makubwa zaidi kwa GERD ya muda mrefu na inakadiriwa ya kwamba,asilimia 10% ya wagonjwa wa GERD hufikia hatua hii ikiwa GERD haijadhibitiwa kwa muda mrefu. Hatua hii mgonjwa anaweza kupata Kansa ya koo nk.
________________________________
DALILI ZA GERD HATUA YA NNE
________________________________
1.🖇️ Kiungulia kikali
2.🖇️ Kucheua vyakula na vinywaji
3.🖇️ Sauti kukwaruza
4.🖇️ Kikohozi kikali
5.🖇️ Chakula kukwama kooni/kunasa koona wakati wa kula.
6.🖇️ Pamoja na dalili zote zilizopo katika hatua ya 3 ya GERD.
⚫Katika hatua hii mgonjwa anaweza kupata changamoto k**a vile esophageal strictures,Barrett’s esophagus* na hata KANSA YA KOO (esophageal cancers)
___________________________________________
MATIBABU YA TATIZO LA KUZIDI KWA ACID TUMBONI-GERD
___________________________________________
⚫Matibabu ya KUZIDI kwa Acid tumbon yamegawanyika katika aina mbili k**a ifuatavyo:⤵️⤵️
_____________________________
1️⃣ MATIBABU YA KISASA
_____________________________
-Matibabu haya yanahusisha utumiaji ya njia za hospital katika matibabu ikiwemo utumiaji wa PPIs(Proton pump inhibitors),Antacids,Histamine, H-2 Blockers k**a vile Cimetidine (tagament HB),famotidine (Pepcid AC),Nizatidine (Axid AR)
-esomeprazole (Nexium), lansoprazole (Prevacid), omeprazole (Prilosec), pantoprazole (Protonix), rabeprazole (Aciphex) and dexlansoprazole (Dexilant) .Magnesium nk.
Dawa hizi zimekuwa zikitumiwa sana na watu wenye changamoto za Acid nying tumboni na miongoni mwa changamoto ni kwamba dawa hizi zimekuwa zikionesha msaada mdogo sana kwa asilimia kubwa ya wagonjwa na hutoa naafuu ya muda tu.
____________________________________
2️⃣ MATIBABU KWA TIBA ASILI/TIBA MBADALA.
____________________________________
-Njia hii inahusisha matibabu kwa kutumia mimea tiba na imeonekana kuwa na ufanisi mkubwa kutokana na uwezo mkubwa wa mimea mingi katika kupambana na magonjwa mbalimbali kwasababu mimea hutibu kiini cha tatzo kwa kuzifanya kuwa mpya seli za mwili hivyo kuufanya mwili kuwa na uwezo mpya katika kufanyakazi zake.
-Ziko dawa nyingi asilia zenye uwezo mkubwa wa kupambana na matatzo ya ACID nying tumboni,mfano wa dawa hizo ni PEPTICOL POWDER,PEPTIC ULCERS+ NK
Wasiliana nami kwa msaada zaidi wa kitaalamu katika kupambana na tatizo hili na mengine kwa uwezo wa Mwenyezi Mungu
_____________________________
PANDEX HERBAL CLINIC
ILALA-DAR ES SALAAM
PANGANI-STREET
Phone: +255749526546
_____________________________
Click here to claim your Sponsored Listing.
Category
Telephone
Address
Dar Es Salaam
Dar Es Salaam
