Nuru Better Health

Nuru Better Health

Share

Naitwa madam Nuru Nawasaidia wanaume na wanawake kutatua changamoto za kiafya . 0715946540

22/05/2024

Nimekutana Na Video hii, nikasema ngoja nikupe Elimu kidogo Itakusaidia

SABABU 8 AMBAZO HUCHANGIA MAZIWA YA KINAMAMA KULALA

01. Gene zako za urithi

Maziwa huweza kulala sio kwa sababu umenyonyesha mwanao bali kwa sababu ya chembe zako za urithi. Chembe za urithi huwa ndo zinaamua ukubwa wa maziwa ya mwanamke, pia ndo huamua uimara wa tishu zinazoshikiria maziwa.

Baadhi ya wanawake kiasili huwa na tishu imara ambazo hufanya maziwa yasimame, wengine huwa na tishu ambazo ni dhaifu hivyo maziwa huwahi kulala.

Kuna wanawake wana maradhi ya kurithi ambayo huathiri uimara ya tishu aina ya ligaments ambazo zinashikiria maziwa na kufanya yawe. Mfano wa ugonjwa ni ugonjwa unaitwa Ehler’s Danlos.

02. Ukubwa wa maziwa huchangia maziwa kulala.

Kutokana na ujazo na uzito maziwa makubwa huwa rahisi kulala. Hali hii sio tatizo la kiafya bali ni hali ya kawaida ya maziwa kukaa kulingana na uzito (normal variation)

-

03. Maziwa Hulala kwa sababu ya UMRI sio kwa sababu ya kunyonyesha…..

Maziwa yameshikiliwa kwenye kifua na kiwambo kinachoitwa cooper’s. Kadri umri unavyokwenda hiki kiwambo hulegea na kupoteza nguvu ya kushikiria maziwa. Sababu nyingine ni kwamba baada ya mwanamke kufikia ukomo wa hedhi (Menopause) tishu ndani ya maziwa husinyaa hii hutokana na kushuka kwa homoni k**a estrogen ambayo husaidia kufanya maziwa yajae.

04. Maziwa hulala mapema kwa kinamama wanaovuta SIGARA…

Sigara hutoa kemikali ambazo huingia kwenye damu na kwenda kuharibu kampaundi inayoitwa elastin ambayo ina kazi ya kufanya ngozi iwe mwororo na inayovutika. Sigara ikiharibu kampaundi hii kwenye ngozi; ngozi ya maziwa huwa dhaifu na kuzeeka hivyo hushindwa kushikiria ziwa vizuri, na ziwa hulala na kuwa tepetepe.

22/05/2024

VITU VITATU VINAVYOPUNGUZA KIUNGULIA KWA MAMA MJAMZITO.

1. Kula kiasi kidogo cha chakula na usile ukashiba sana. Kwa kuwa mama mjamzito huwa anasikia njaa mara kwa mara na anahitajia kula vyema ili aujenge vizuri mwili wake na watoto,
basi ni bora chakula chake ukigawe katika sehemu kadhaa ndogo, na ale mara kadhaa, badala ya kula sana wakati mmoja.

Suala hilo litafanya tumbo lake lisijae na kusaidia kuzuia asidi isipande juu ya tumbo na kusababisha kiungulia na gesi.

2. Jitahidi usinywe maji mengi sana baada ya chakula au wakati wa kula,

3. Jitahidi usilale tu mara baada ya kula, subiri k**a nusu saa hivi ipite ndio ulale.
Unapolala usilaze kichwa moja kwa moja bila mto, bali tumia mito kuegemeza kichwa ili kuzuia asidi isirejee juu ya tumbo na kusababisha kiungulia.
Unapohisi kiungulia kunywa glasi ya maziwa au kula mtindi.
Na k**a hali hiyo haijatoweka kunywa maji ya moto glasi moja yaliyowekwa kijiko kimoja cha asali.

21/03/2024

Mafundisho ni muhimu kwa kila mmoja wetu.
Lengo letu ni kujifunza mengi zaidi.
MIMBA KUHARIBIKA (Miscarriage)

MIMBA CHANGA KUHARIBIKIWA/KUTOKA, CHANZO NA SABABU, DALILI NA NINI UFANYE ILI KUZUIA ISITOKEE TENA

Somo hili ni refu na kwa hiyo limegawanyika sehemu kuu tatu
1- Dalili za mimba kuelekea kuharibikiwa
2- Chanzo na sababu za mimba kuharibika
3- Nini cha kufanya ikiwa huwa unapatwa na hali hiyo mara kwa mara.

SEHEMU YA KWANZA

Ni kawaida sana mimba kutoka au kuharibika bila kukusudia au bila wewe kujua k**a imetoka au inakaribia kutoka. Wakati mwingine hutoka tu bila sababu yeyote na hata k**a utapimwa na vifaa vya kisasa kabisa bado sababu za mimba kuharibika hazitajulikana. Ikiwa utajua ya kwamba mimba imetoka

CHAKWANZA ni vizuri kujua sababu ya mimba hiyo kutoka, hasa k**a imeharibika kwa mara ya pili na zaidi. Sababu zinaweza kuwa nyingi k**a vile utakavyo ona katika aya zifuatazo

CHA PILI kupambana na icho kisababishi, baada ya kupima na kupata ushauri basi itakufaa sasa upate dawa au kufuata ushauri uliopewa, ukimaliza dozi rudi hospitalini ili uweze kujua k**a umepona kabisa au la.

Kunayo tabia ya watu wengi tu askisha maliza dozi ndio inakuwa basi anaendelea na Maisha yake, hapo unakuwa unakosea. Jitahidi kurudi hospital na kupima tena upate uhakika wa tatizo k**a limeisha au la. K**a halijaisha inakuwa rahisi kwa daktari kuchukua vipimo vingine au kukupa dawa ingine.

CHA MWISHO ni kujaribu tena kubeba mimba, baada ya kuona mambo yote yako sawa, au sasa unaamini uko vizuri basi unajaribu tena kupata mimba. Zingatia siku zako za uzazi, na zingatia kupika vyakula vizuri ili mume wako apate nguvu ya kutoa mbegu nyingi na zenye afya njema.

Usafi pia wa mwili na kitanda ni muhimu. Usinuke na kutoa harufu mbaya.
Mara nyingi swala la kwanza na pili watu huruka na kuendelea nakutafuta mimba.

Zamani wakati vifaa na wataalamu walikuwa hakuna hiyo ilikuwa sawa lakini Siku hizi kuna vifaa ujitahidi kutafuta sababu.

Hii ni Kwa sababu pia uwezo wa wanawake kuzaa umepungua sana. Wanawake wachache wanazaa watoto zaid ya 6 hata wakitaka kuzaa wanajikuta hawawezi. Wengine wanachelewa kuolewa, kwa mana hiyo wanaanza kutafuta watoto wakati Mayai bora mengi yameishaisha.

DALILI ZA MIMBA CHANGA KUWA IMEHARIBIKA AU KWAMBA INAELEKEA KUHARIBIKA

Kwahiyo ukiona dalili zifuatazo basi jua mimba yako changa imetoka au inataka kutoka kimyakimya.
1- maumivu makali ya tumbo la uzazi (yanachoma)
2- kutoka uchafu k**a ugoro au damu ya bleed au mabonge ya damu.
3- kutoka na kitu k**a kinyama lakini chenye damu.

Note: unaweza tokwa na damu k**a matone hiyo inaweza isiwe mimba imetoka. Jaribu kupima tena na tena. Usipime Siku iyoiyo Kwa kuwa Homoni za mimba zinakuwa Bado zipo.

Cha msingi pia ni kupata ushauri ukikutwa na hali hiyo. K**a ulikuwa unajua una mimba basi dalili

ZIFUATAZO NI HATARI NA LAZIMA ZIKUPATAPO UWAHI HOSPITALINI .
1- maumivu makali ya tumbo kichwa na mgongo wachini kwa pamoja au mara moja moja.
2- Mafua makali, kutapika sana, kuishiwa maji mwilini na kikohozi.
3- kupata damu ya bleed lakin yenye rangi tofauti na ya bleed.
4- kutokwa na uchafu unaomiminika kidogokidogo kutoka ukeni.
5- kupungua Kwa dalili za mimba, kujisikia kawaida na k**a imeharibika dalili zinakoma kabisa
Dr Nuru 0715946540..🥰🙏🥼

21/02/2024

NJIA RAHISI YA KUFAHAMU MZUNGUKO WAKO.

Hesabu siku tangu siku ile ya kwanza uliyoanza kupata damu za hedhi mpaka siku moja kabla ya kuona siku zako za hedhi zinazofuata.

Unashauriwa uchukue miezi mitatu mpaka sita ukihesabu ili ujue na uhakika kwamba mzunguko wa tarehe zako haubadiliki, k**a umeshahesabu siku za nyuma kabla ya kusoma makala hii ni vizuri pia.

Mfano umeanza kuona siku zako tarehe moja mwezi wa 11 alafu siku zako zingine ukaziona tarehe 29 mwezi 11, chukua 29 toa 1 utapata 28.. maana yake wewe unamzunguko wa siku 28.

👉Je siku za hatari ni zipi?
siku ya hatari ni siku ya 14 kabla ya kuona hedhi inayofuata na sio siku ya 14 baada ya kuona hedhi iliyopita na hapa ndio watu wengi wanachanganya na kupata mimba.

👉Mfano k**a mzunguko wako ni siku wa kawaida siku 28, chukua 28 toa 14 utapata 14. Hivyo siku yako ya hatari ni siku ya 14, lakini kwa kua mbegu ya kiume inaweza kuishi mpaka siku tano na yai la k**e linaweza kuishi mpaka masaa 24 ndani ya mfuko wa uzazi basi siku nne kabla na siku moja baada ya siku ya 14 ni hatari hivyo siku za hatari ni ni siku ya 10,11,12,13,14 na 15.

👉K**a mzunguko wako ni mrefu labda siku 36 basi chukua 36 toa 14 utapata 22. Hivyo siku ya 22 ni hatari na zingine ni 18,19,20,21,22 na 23.

👉K**a mzunguko wako ni mfupi, mfano mzunguko wa siku 21, sasa ukichukua 21 ukatoa 14 unapata 7 yaani siku ya saba ni hatari kwa huyu mtu.hivyo siku zingine za hatari ni 3,4,5,6,7(mtoto wa kiume) na 8.

Naamini umepata kujifunza, ukiona hauna mzunguko mzuri, hilo nitatizo, mwanamke anahitaji awe na mzunguko usioyumba kabisa.

Nb: K**a unasumbuliwa na tatizo lolote la uzazi, umehangaika Kwa muda mrefu bila mafanikio, nakuomba usikate tamaa, nafasi bado unayo.

Leo nitawapa watu wachache kipaumbele hapa nitumie ujumbe whatsp
0715946540 Dr Nuru.

21/02/2024

MADHARA YA VIZUIA MIMBA|sindano| vidonge| vipandikizi|
Leo tuangalie madhara yawapatayo Baadhi ya Akina Mama watumiapo vizuia Mimba.

A.MADHARA YA SINDANO YA KUZUIA MIMBA.

1.Usumbufu wa Hedhi.
2.Kichwa kuuma Mara kwa Mara.
3.Kupata kizunguzungu.
4.Kupata kichefu chefu?
5.Kuongezeka uzito usiokuwa na Faida.
6.Kupata hedhi yenye mabonge mabonge ya damu.
7.kutokwa damu nyingi zaidi ya siku 4 wakati wa hedhi.

B.MADHARA YA VIDONGE VYA KUZUIA MIMBA.

1.Huathiri mfumo wa uzazi kwa ndani.
2.Huongeza uzito wa ute utokao utokao katika njia ya uke ili kuzuia mimba kutunga.
3.Kuumwa kichwa mara kwa mara.
4.kupata kichefu chefu.
5.Kutopata hedhi kwa Baadhi ya Wanawake.
6.Kubadilika kwa Mwenendo wa Damu(Hedhi)
7.Huathiri ini kidogo kidogo.
8.Kupata kisukari.
9.Kupata ugonjwa wa Moyo.
10.Kupooza upande mmoja.
11.Kupata hedhi yenye mabonge mabonge.
12.Kutokwa Damu nyingi wakati wa hedhi kwa zaidi ya siku 3.

C.MADHARA YA KITANZI CHA KUZUIA MIMBA.
1.Utokaji ovyo wa Damu.
2.Kutoboka mfuko wa uzazi.
3.Kuongezeka upana wa uke na kufungua lupa na kufunga kwa uzazi.
4.Kutoka hedhi yenye mabonge mabonge ya damu.
5.Kutokwa Damu nyingi wakati wa hedhi kwa zaidi ya siku 3.

D.MADHARA YA KIJITI.
1.Husababisha kansa.
2.Kuchanganyikiwa kwa akili.
3.kupata shinikizo la Damu (Presha)
4.Kupata maumivu makali wakati wa kujaamiana.
5.Kutoka hedhi yenye mabonge mabonge ya Damu.
6.Kutokwa Damu nyingi wakati wa hedhi kwa zaidi ya siku 3.

N.B
Kwanini Hutokwa na damu nyingi au damu yenye mabonge mabonge?kwa sababu mimba inapotungwa uharibiwa na vizuia mimba.
Kwa matibabu bora na uwakika
Asante sana. 0715946540

02/02/2024

PID NI NINI, DALILI, MADHARA NA TIBA YAKE.

PID (Pelvic informatory Disease) Ni maambukizi katika via vya uzazi.

Maambukizi hayo yanaweza kusababishwa na

1️⃣magonjwa: kisonono, kaswende, UTI au Fangasi rudizi
2️⃣Utoaji mimba
3️⃣Matumizi ya madawa kiholela
4️⃣Vizuizi mimba
5️⃣Kuwa na wapenzi Wengi
6️⃣Mtindo wa maisha (Ulaji mbovu na kutokuzingatia usafi) n.k

PID Ni ugonjwa hatari Sana kwa wanawake unaoshambulia via vya uzazi na Madhara yake Ni makubwa isipotibika kwa haraka.

HIZI NI BAADHI YA DALILI ZA PID

1️⃣Kutokwa na uchafu mzito sehemu za Siri, yawezekana ukawa Ni mweupe, njano, au maziwa na unaharufu mbaya
2️⃣Kuwashwa sehemu za Siri
3️⃣Uke Kuwa mkavu na kutoa Harufu mbaya
4️⃣ Maumivu ya tumbo chini ya kitovu
5️⃣Uke Kuwa na ulaini Sana kulegea
6️⃣ Maumivu wakati wa tendo la ndoa
7️⃣Kuvurugika kwa hedhi
8️⃣Kutokwa majimaji ukeni kupita kiasi
9️⃣ Maumivu wakati wa kukojoa na Wakati wa choo Kubwa
🔟Homa, uchovu, kuzunguzungu na kukosa hamu ya kula
1️⃣1️⃣ Maumivu ya chini ya kitovu upande wa kulia au kushoto

MADHARA YA PID
🔸Ugumba
🔸Kansa ya shingo ya kizazi
🔸Mirija ya uzazi kuziba
🔸Majeraha kwenye Mirija ya uzazi

ANGALIZO: Uonapo dalili moja au zaidi wahi katika kituo cha Afya ili kuepuka Madhara makubwa baadae.

TIBA YA PID
PID Inatibika na kupona kabisa. Kwa ushauri, swali juu ya tatizo hili waweza kuwasiliana nami Ni Bure kabisa. Karibu

Mawasilian 0715946540.

31/01/2024

Ushawahi kujiuliza kwanini unatumia dawa nyingi kupambana na utokwaji wa uchafu wenye harufu mbaya ukeni lakini huponi..?

📌Leo nakupa wazo dogo tu utaelewa ukifuatilia mpaka mwisho...

Iko hivi.👇👇

♻️Kinachofanya uchafu wenye harufu utokee ni uwepo wa MAJERAHA pamoja na WADUDU kwenye mfumo wa uzazi wako then Nini hutokea..??

🤔...JERAHA pamoja na WADUDU haya ni mazingira yanayozalisha uchafu wenye harufu kutokana na Maisha ya viumbe katika jamii hiyo kwenye kizazi chako.

🤷‍♀️...Huwa unafanya hivi unanunua dose (antibiotics) ambazo kazi yake ni kuua WADUDU na kinachobaki ni JERAHA.

🤦JERAHA .... Ama kidonda kikibakia huruhusu WADUDU tena kuja kuishi ndio maana wakati unatumia antibiotics kutatua changamoto ya kutokwa na uchafu wenye harufu mbaya ukeni utajiona unaendelea vizuri ...

👉Hutokea hivyo kwa sababu kazi ya antibiotics imetimia imeua WADUDU kwenye MAJERAHA huoni utundu wao kuzalisha uchafu...

😭Baada ya siku chache kumaliza dawa shida hii hapa tena kwanini irudie ???

😭Unaamini umelogwa umeshindikana hapana..

Ebu twende👇

😭Nguvu ya antibiotics ikiiisha JERAHA huruhusu WADUDU wapya kuja kuendeleza kazi yao....

🤷‍♀️ Sasa ufanye Nini ndugu yangu?????

🥰Hakikisha unapata dose yenye sifa hizi utakuwa umekomesha 👇

Dose yenye uwezo wa ....

1️⃣ Kuua WADUDU ( bacteria fangus ,n.k)

2️⃣kuponesha MAJERAHA (kwenye kizazi Kuna smooth muscle uponyaji ni taratibu)

3️⃣ Kubalance pH ya uke na mfumo wa kizazi

4️⃣ Kukaza kizazi

5️⃣ Kusafishaa kizazi

6️⃣ Kubalance hormones zako

🌹 Ninacho kijua chenye uwezo huu ni tumia uzazi package.

🌴 Kwa tatizo la uvimbe, PID, Fangasi, UTI SUGU N.K Nitumie ujumbe Whatsapp

No:0715946540 Dr Nuru

25/01/2024

UTI (Urinary tract infection) ni ugonjwa wa maabukizi katika mfumo wa mkojo na maambukizi haya yanasababishwa na bakteria aitwaye Escherichia coli.

Kwa kawaida bakteria hawa hupatikana katika utumbo mpana na kwenye njia ya haja kubwa,

Na inapotokea wakahamia katika njia ya mkojo husababisha mtu kupata tatizo hili la maambukizi katika mfumo wa mkojo.

Ugonjwa wa U.T.I unaweza athiri urethra, kibofu cha mkojo na figo.
-

DALILI ZA UTI .

➢ Kwenda haja ndogo mara kwa mara na maumivu wakati wa kukojoa.

➢ Kuhisi kuunguzwa na mkojo kwenye kibofu au mrija wa mkojo.

➢ Maumivu chini ya kitovu.

➢ Mkojo kuwa na harufu mbaya.➢ Kuhisi homa kali na uchovu na kichefuchefu.

➢ Mkojo kubadilika rangi kuwa nyeusi au rangi ya mawingu.

➢ Kushikwa na hamu ya kukojoa ila mkojo unatoka kidogo.

➢ Maumivu ya mgongo na kiuno.

➢ Uchovu kupita kiasi wa mwili mzima. .➢ Kupata hamu kubwa ya kwenda haja ndogo lakini inatoka kiduchu.
➢ Haja ndogo kutoka legevu au legelege.
-

JINSI YA KUJIKINGA:

📌 Unywaji wa maji mengi husaidia kuondoa sumu mwilini kwani huwezesha viungo k**a vile figo kufanya kazi yake vyema.

~ Mtu akinywa mengi inamsaidia kwenda haja ndogo mara kwa mara na itasaidia kuwaondosha wale bakteria wa UTI kabla hawajafika kwenye kibofu na kuleta madhara.

📌 Kwa wanawake wanatakiwa kujisafisha baada ya kujisaidia kutoka mbele kwenda nyuma na hutakuwi kurudi tena mbele.

Kwani kujisafisha kutoka nyuma kuja mbele huwahamisha bakteria na kuwaleta kwenye njia ya mkojo na kukusababishia maambukizi ya ugonjwa wa UTI.

📌 Ulaji wa matango na mboga mboga kwa wingi husaidia kuwaondosha bakteria. Juisi ya zabibu za aina zote zabibu nyekundu na nyeusi.

Unywaji wa juisi hii mara kwa mara husaidia kupunguza maambukizi ya bakteria wa UTI.

📌 Ni vema kuzingatia usafi wa mwili na mavazi unywaji wa maji mengi na kufuata ushauri wa kitaalamu ili kuboresha afya zetu.

Kwa msaada wa haraka wa changamoto zote za Afya ya Uzazi nichek watsap 0715946540 Dr Nuru.

20/01/2024

*Dalili za Chlamida kwa wanawake na wanaume*
👉maumivu ya sehemu ya chini ya tumbo
👉maumivu wakati wa kukojoa
👉maumivu wakati wa tendo la ndoa.
👉kutoka damu baada ya tendo kwa mwanamke.
👉maumivu ya nyonga.
👉usaha na uchafu kutoka kwenye uume au uke.
👉kutokwa damu njia ya haja kubwa.
👉kupata maumivu makali njia ya haja kubwa wakati wa kujisaidia.
👉kupata maumivu makali wakati wa kukojoa.
👉 kukojoa mara kwa mara.
*Hizo ni dalili za ugonjwa huu na ugonjwa huu unatibika kabisa kwa dozi iliyo sahihi na kamili, k**a una dalili hizo wasiliana/au tuma ujumbe mfupi watsap 0715946540.*

Nuru Better Health Naitwa madam Nuru Nawasaidia wanaume na wanawake kutatua changamoto za kiafya . 0715946540

19/01/2024

P.I.D ..!!
Wa.me+255715946540

P.I.D - Pelvic Inflammatory Disease ni maambukizi ya bakteria wabaya katika via vya uzazi wa mwanamke.
Ugonjwa umekuwa tatizo sugu kwa wanawake wengi hali ya kutumia dawa nyingi sana bila kupata matokeo mazuri.

.I.D :
●Kutokwa na uchafu mzito k**a maziwa mtindi wenye harufu mbaya.

●Maumivu makali wakati wa tendo la ndoa.

●Maumivu ya tumbo chini ya kitovu kabla au wakati wa hedhi.

●Kukosa ute wa uzazi na hamu ya tendo la ndoa.

●Mpangilio hafifu wa siku za hedhi/hedhi isiyo salama.

●Kutokwa na majimaji machafu yenye harufu mbaya.

●Miwasho, upele na maumivu sehemu za siri.

.I.D huwa na madhara makubwa na baadhi ya madhara hayo ni pamoja na:

●Mirija ya uzazi kuziba au kujaa maji.

●Mvurugiko wa homoni za uzazi.

●Kuchelewa au kutokupata ujauzito.

●Uvimbe kwenye kizazi au uvimbe maji.

●Saratani/kansa ya shingo ya kizazi.

wanawake wengi sana kuondokana na changamoto za uzazi bila kutumia kemikali dawa.
Hivyo tuwasiliane ikiwa k**a unapitia dalili, madhara ya P.I.D au tatizo lolote la uzazi.
Nipigie/tuma ujumbe/ Wa.me+255715946540

14/01/2024

Je ni wew au ndugu yako anachangamoto yoyote ya Afya. Wasiliana nami ili tuweze kutatuwa changamoto hiyo mapema.

Want your business to be the top-listed Beauty Salon in Dar es Salaam?
Click here to claim your Sponsored Listing.

Category

Website

Address


Dar Es Salaam
Dar Es Salaam
123