Mahaba
Karibu Mahaba! ❤️Hapa tunakuletea elimu ya mahusiano, ndoa, mapenzi, na afya.Follow, Like, Share & Comment! Kwa matangazo: 0625850656
ILOVE
SIKIA HII JIFUNZE KITU
😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂🤣
27/12/2025
KIMAMBI PLESHA ZIMEPANDA AKAUNTI ZAKE KUFUNGWA NA KESI JUU.
27/12/2025
NENO MOJA KWA HAYATI MAGUFULI
SAMIA ANATAKA MAHUSIANO YA POLISI NA WANANCHI KULEJEA
26/12/2025
ELEKEZI YA SERIKALI KWA MBOLEA
MHE: MBUNGE CANONI ATOA MKONO WA POLE HOSPITAL YA WILAYA KALAMBO
: MBUNGE CANONI AKABIDHI MSAADA HOSPITAL YA WILAYA KALAMBO
25/12/2025
: CANONI ATOA MKONO WA POLE KWA WAGONJWA HOSPITALI YA WILAYA KALAMBO
Mhe: Edephons Joachim Canoni Mbunge wa jimbo la Kalambo leo tarehe 25/12/2025 siku ya Krismasi
Ametembelea hospitali ya wilaya ya Kalambo ili kutoa mkono wa pole kwa wagonjwa na madaktari walio kuwepo zamu,
Katika ziara hiyo Mhe: Mbunge ameweza kusikiliza kero na changamoto kutoka kwa wagonjwa na madaktari nae ameahidi kuzitafutia ufumbuzi.
Amewaomba wagonjwa na madaktari kuwa huru kumpigia au kufika ofisini kuwasilisha changamoto zao ili ziweze kutatuliwa.
Aidha katika mkono wa pole ameweza kutoa biskuti Miche ya sabuni mafuta ya kupakaa, juisi na jumla ya fedha laki mbili na na elfu ishilini TSh: 220,000/=
pamoja na kumlipia bili mgonjwa mmoja alie sema hajiwezi kifedha amefanyiwa opalesheni na kupatiwa matibabu hali ya afya inaendelea vizuri lakini hana fedha za kulipia huduma ya matibabu.
Wakati wa kuongea na madaktari wameweza kuomba Elimu itolewe kwa wananchi ili waweze kuwahi wakati wa kwenda kujifungua ili kuokoa maisha ya mama na mtoto,
Wamesema hali iliyopo kwa sasa ni hatari wakina mama wanacheweshwa kufika hospital wengine hujifungulia nje ya hospital
kabla ya kuingizwa leba jambo ambalo linawapa madaktari wakati mgumu wa kiutendaji na kuokoa maisha, jambo linalo weza kusababisha kifo cha mtoto au mama.
Mhe Mbunge Canoni amesema anatambua mchango wa madaktari kujitoa kuokoa wananchi ndio maana watu wengine wana sherekea sikukuu lakini wao wana endelea na matibabu.
Amewasihi kuendelea kuwa na moyo wa kujituma ili wananchi waendelee kupata huduma bora.
Hata jitahidi kuendelea kutoa Elimu kwenye mikutano ya hadhara ili wananchi wajue umuhimu wa kuwahi wakati wa kujifungua.
Imetolewa na
Musa Frackison Mzopola
Katibu wa Mbunge
25/12/2025
YA KRISMASI NA MWAKA MPYA
Mhe: Edephons Joachim Canoni Mbunge Jimbo la Kalambo anawatakia Krismasi na mwaka mpya mwema Msherekee kwa amani.
22/12/2025
WA MBUNGE KALAMBO ASHIRIKI MAAZIMISHO YA NYOTA NJEMA FOOTBALL CLUB
Ndugu Musa Frackison Mzopola Katibu wa Mbunge Jimbo la Kalambo Mhe: Edephons Joachim Canoni ameshiriki k**a mgeni Rasmi kwa niaba ya mhe Mbunge kwenye maazimisho ya siku ya Club ya Nyota Njema Queens na FC
Maadhimisho hayo yame fanyika tarehe 21/12/2025 kijiji cha Kateka kata ya Matai wilaya ya Kalambo.
Katika maadhimisho hayo yameweza kutolewa mafanikio ya Club ikiwa ni kusajili Club kwa namba *NSC 12340* kuwa na Timu ya kiume na k**e,kupata jezi na baadhi ya vifaa vya michezo
Kucheza mpira ngazi ya mkoa ligi daraja la pili, kushinda katika mashindano ya wilaya mwaka 2024, Kuongeza wigo wa Timu ya k**e katika wilaya ya Nkansi,
Kutoa baadhi ya wachezaji walio shiriki kuunda timu ya UMISSETA mkoa wa Rukwa kwenda kwenye mashindano ya Kitaifa.
Changamoto ni ukosefu wa mdhamini, Upungufu wa vifaa vya michezo, Wazazi kuto kuwaruhusu watoto wao wa k**e kushiriki michezo.
Kwaniaba ya Mbunge Mhe: Edephons Joachim Canoni, Katibu ameweza kutoa salamu za Mbunge na kumpongeza Meneja wa Club hiyo
Mwl Audiface Mwanakulya kwa jitihada zake za kuwaunganisha Vijana toka Mwaka 2018 Club ilipo anza mpaka sasa maana hakuna kundi gumu kuliongoza k**a kundi la vijana pia ameipongeza Club kwa mafanikio makubwa waliyo yapata
Amewakanya vijana kuto kujihusisha na makundi mabaya ya kuvuluga amani ya nchi yetu wanapaswa kutumia smartphone zao kupitia bando wanazo weka wazitumie kuingiza kipato
Wanapaswa kujikita kwenye utafutaji wa fedha na amewahakikishia kuwa Ofisi ya Mbunge ipo tayari kuwatafutia fursa za kujikwamua kiuchumi.
Ameishauri Club waweze kutanua wigo kiuchezaji badara ya kujenga afya pia wanapaswa watazame michezo k**a ajira
Amewashauri wasajili kikundi cha vijana ili kuweza kunufaika na mikopo ya 10% ya Halmashauri inayo tolewa bila riba
Mikopo hiyo itawasaidia kuendesha miradi ya ujasiriamali itakayo wasaidia kujikwamua kiuchumi na kutatua changamoto zinazo wakabili,
Amesema endapo watakuwa tayari kusajiri kikundi, wao watakaa na kujadiliana mambo muhimu yatakayo kuwepo kwenye katiba yao na kuyaleta kwenye Ofisi ya Mbunge
Ofisi ya Mbunge itawasaidia kuchapa katiba na kugharamia gharama za usajili na cheti baada ya usajili kukamilika
Kikundi kitaweza kuomba mkopo Halmshauri, Ofisi ya Mbunge itasimamia kuhakikisha mkopo huo unapatikana.
Aidha amesema changamoto ya mdhamini anaichukua ata iwasilisha Ofisini, Ofisi ya Mbunge ita shirikiana na wao kumtafuta mdhamini
kuhusiana na changamoto ya vifaa vya michezo ameelekeza wafanye tathimini ya gharama za kukamilisha vifaa hivyo waweze kuandika barua ya kuomba kwenye Ofisi ya Mbunge kupitia chama cha mpira wa miguu wilaya ya Kalambo Ofisi ya Mbunge ita saidia upatikanaji wa vifaa hivyo maana miongoni mwa majukumu ya Mbunge ni kutatua kero na changamoto za wananchi wake.
Changamoto ya wazazi kuto kuwaruhusu watoto wao wa k**e kushiriki kwenye michezo Ofisi ya Mbunge kushirikiana na chama cha mpira wa miguu wilaya
Wata endelea kutoa Elimu kwenye mikutano ya hadhara itakayo endelea kufanyika Ili kuwaondoa Wazazi wasiwasi waweze kutambua kuwa michezo ni afya pia ni ajira.
kwa kutambua umuhimu wa chama cha mpira wa miguu wilaya ya Kalambo akasema ame enda na Mwenyekiti wa chama cha mpira wa miguu wilaya Ndg: Caros Mbalazi ili nae abebe changamoto zinazo husu chama chake na kuzitafutia ufumbuzi.
Mwisho amewaomba wadau wa michezo na maendeleo wa wilaya ya Kalambo na Tanzania kwa ujumla waweze kujitokeza kusaidia na kudhamini Club hii ya vijana wa k**e na wa kiume wapatao 100 waweze kufikia ndoto zao.
Click here to claim your Sponsored Listing.
Category
Contact the business
Website
Address
Kaliakoo
Dar Es Salaam
