Afya Tips

Afya Tips

Share

Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Afya Tips, Health/Beauty, Dar es Salaam.

Ninasaidia kutatua changamoto za kiafya k**a sukari,pressure, pid,uti sugu,mgongo,magoti, fangasi,miwasho,harufu mbaya ukeni,matatizo ya mifupa,nguvu za kiume, ubora wa mbegu za kiume,goiter bila upasuaji,vimbe mbalimbali, tezi dume,uzazi,n.k

17/02/2022

Tiba na ushauri +255679972904

17/02/2022

Kwa tiba na ushauri +255679972904

13/11/2021

MADHARA YA KUNYONYA UUME KWA WANAWAKE

Kitendo hiki ni pale mwanamke anapoweka uume wa mwenza wake mdomoni mwake na kuanza kunyonya k**a p**i au mwanaume kuingiza ulimi ukeni pamoja na kunyonya via vya mwanamke pindi wapenzi hawa wawapo faragha.

Kumekua na ongezeko la kitendo hiki kwa vijana na imekua k**a ni sehemu ya mahaba kwa wapenzi hata inafikia hatua mwanaume ANAONA MKE/MPENZI WAKE HAJUI MAHABA K**A HAJAMNYONYA UUME AU MWANAMKE KUONA HIVO ASIPONYONYWA YEYE.VILIVILE KUNA WANAWAKE WANAONA KUFANYA MAPENZI BILA KUNYONYA NI USHAMBA

Vyumbani mambo mengi sana hutokea katika suala zima la mapenzi, nitaenda kusema kwa ufupi madhara ya kunyonya

KISONONO CHA KOO.
K**a unafanya hiki kitendo halafu ukute mwanamke/mwanaume ana magonjwa ya zinaa k**a kisonono inakua rahisi kwa mnyonyaji kuambukizwa.kumbukeni k**a mwanamke ana kisonono sio rahisi kumgundua k**a ilivyo kwa mwanaume.TUWENI MAKINI.

SARATANI YA KOO.
Hii hasa huwapata wanawake ambao hupenda kunyonya uume wanaume wengi na hivo kuwaweka katika hatari ya kuambukiwa vimelea wanaosababisha saratani hiyo mfano HPV

KUBADILISHANA BACTERIA.
K**a wote tunavofaham ya kwamba kwenye miili yetu kuna bacteria Rafiki(normal flora);sasa hao bacteria wakiingia sehem ambayo sio yake huleta madhara kwani wameingia eneo ambalo hawajazoea,wataingia sehemu mpya kwa kuwanyonya kutoka kwa mwanamke au mwanaume.Hii inaeza isilete madhara mapema lakini uendeleaji wa kunyonya nyonya wanaume au wanawake wengi mara kwa mara hupelekea kupata madhara mengi na mengine ni magumu kutibu.

Kupata maambukizi ya HIV

Kupata madonda mdomoni

Kujiweka katika hatari ya kupata saratani za mdomo, ulimi nk

SASA WADAU WANGU MPAKA HAPO NIMEFIKIA MWISHO WA MAKALA FUPI.TUJIHADHARI NA VITENDO HATARISHI AMBAVYO TUMEIGA KUTOKA KWA WAZUNGU.SOTE TUNAFAHAMU KAZI YA MDOMO NA ULIMI KWA HIYO TUSIVIFANYIE KAZI AMBAYO SIO YAKE

ACHENI KUSHABIKIA PAGE,MAKUNDI YA WATSAP,VIDEO AMBAZO ZINAHAMASISHA UFANYAJI WA HAYA MAMBO..ZIPUUENI KWAN HAO WANAOHAMASISHA WENGI WAO NI WAFANYABIASHARA WA NGONO NA HAWAWATAKII MEMA WATU WEMA
TAG VIJANA WENGI WA K**E NA KIUME ILI WAACHE HII TABIA

12/11/2021

MAUMIVU WAKATI WA KUKOJOA

Maumivu wakati wa kukojaoa ni hali inayotokea kwa watu wengi ikisababishwa na magonjwa mbalimbali. Maumivu wakati wa kukojoa hujulikana kwa kitaalamu k**a dysuria. Kati ya sababu kuu za maumivu wakati wa kukojoa ni maambukizi ya mfumo wa mkojo (Urinary tract Infection – UTI) hasa kwa wanawake na magonjwa ya zinaa.

NAMNA MAUMIVU WAKATI WA KUKOJOA YANAYOTOKEA ⁶

Maumivu haya hutokana na kuchubuka kwa njia ya mkojo. Maumivu huwa yanakuwa ya kuungua wakati mkojo unatoka. Yanaweza kuwa wakati wote unakojoa, mwanzoni au mwishoni mwa kukojoa.

Pia yanaweza kuambatana na dalili k**a homa, kuokwa na usaha au uchafu sehemu za siri, kutokwa mkojo wenye damu damu na maumivu chini ya kitovu.

Maumivu haya hutegemea na chanzo cha ugonjwa unaoleta dalili hii. Baadhi ya sababu za maumivu wakati wa kukojoa ni:

Maambukizi ya Njia ya Mkojo (Urinary Tract Infection – UTI)

Ugonjwa huu huleta maumivu k**a ya kuungua kwenye njia ya mokojo. Pia maumivu yanaweza kufika mpaka chini ya kitovu wakati wa kukojoa. Dalili nyingine zinazoweza kuambatana na hali hii ni homa, kukojoa mara kwa mara, kuhisi mkojo hauishi kwenye kibofu na maumivu ya mgongo.

Magonjwa ya Zinaa

Huleta maumivu wakati wa kukojoa hasa kwa wanaume, maumivu k**a ya kuungua wakati mkojo unatoka. Dalili nyingine zinazoweza kuambatana na magonjwa haya ni kutoa uchafu k**a usaha sehemu za siri, maumivu chini ya kitovu na homa.

Kichocho

Kichocho husababisha maumivu wakati wa kukojoa ikiambatana na kutoa mkojo wenye damu.

Magonjwa mengine yanayoweza kusababisha maumivu wakati wa kukojoa ni:

Saratani ya kibofu cha mkojo

Mawe ya figo

Kuumia wakati kufanya mapenzi

mawasiliano +255679972904

12/11/2021

KUPATA HEDHI MARA MBILI KATIKA MWEZI MMOJA (INTERMENSTRUAL BLEEDING,METRORHAGIA)

Hii ni ile hali ambayo mwanamke hupata hedhi au kutokwa na damu ukeni muda wowote katika mzunguko wake tofauti na tarehe au muda aliiouzoea.. na damu hii hutokea pasipokua ama kuhusiana na tendo la ndoa.. mfano kwa mwezi huu wa 6 mwanamke anaweza kupata hedhi tarehe 10/6 halafu akapata tena tarehe 25/6

Kuna wanawake wenye mzunguko ambao uko vizuri yaani haubadiliki badiliki na wanapata damu kidogo au matone kidogo tu katikati ya mzungukoCyclic midcycle intermenstrual bleeding) wake yaani wakati wa yai kutoka(ovulation);na kuna wengine hutokwa na damu nyepesi siku chache kabla ya kupata hedhi au baada ya kumaliza hedhi kwa siku kadhaa(Cyclic premenstrual or postmenstrual intermenstrual bleeding). hii ni hali ya kawaida ya kimwili tu kwani kunakua na mabadiliko kidogo ya vichocheo ama vichocheo vinabadilishana majukumu nyakati hizi.

VISABABISHI VYA KUPATA HEDHI MARA MBILI

Matumizi ya vidonge vya majira(Oral contraceptives)

Maambukizi ya shingo ya kizazi(Cervicitis)

Maambukizi ya ndani ya kizazi(Endometritis)

Saratani ya kizazi(Uterine cancer)

Saratani ya shingo ya kizazi(cervical cancer)

Saratani ya uke(vaginal cancer)

Saratani ya sura ya uke na mdomo wa uke(Vulva cancer)

Maambukizi ya Uke(Vaginitis)

Madonda ya magonjwa ya zinaa kwenye mfumo wa uzazi(Sexually transmitted ulcerations)

Uvimbe ndani ya kizazi,shingo ya kizazi,uke nk(Benign growths)

PATA SULUHISHO LA TATIZO LA KUPATA HEDHI MARA MBILI KWA MWEZI,WASILIANA NASI +255679972904

12/11/2021

HIKI NDIOO CHANZO CHA HARUFU MBAYA MDOMONI

Katika maisha ya kila siku yawezekana umewahi kukutana na mtu ambaye ukiwa karibu naye akiongea au kutoa pumzi kinywani au puani utasikia harufu mbaya.

Kwa kawaida mdomo na pua huweza kutoa pumzi nje ambayo huwa na harufu asilia ambayo haiwezi kumkera mtu mwingine, lakini mara zingine hali hiyo inaweza kujitokeza kutoa pumzi yenye harufu mbaya.

Watu wa karibu au wanaokutana na mwathirika wa hali hii wanaweza wakadhani kuwa ni mchafu mwenye tabia ya kutopiga mswaki au kutosafisha kinywa chake vizuri.

Pasipo kujua kuwa upo uwezekano mtu huyo akawa na tatizo linalojulikana kitabibu k**a Halitosis,maana yake ni kutoa pumzi aidha kwa mdomoni au puani yenye harufu mbaya isiyo vumilika.

Mtu mwenye tatizo hili anaweza kukumbana na kunyanyapaliwa na wanajamii wanaomzunguka kiasi cha kuweza kumsababishia matatizo ya kisaikolojia.

Muathirika anaweza kupatwa na tatizo la woga/hofu iliyopitiliza anapokuwa kwenye kundi la watu, anaweza akajiondoa kutoka katika kundi hilo na kujitenga na vilevile, baadaye huweza kupata sonona (depression).

Tatizo hili linalowakumba asilimia 20 ya wajamii duniani, ni moja ya tatizo linalowafanya kufika katika huduma za afya kuwaona madaktari wa kinywa na meno.

Hufika kwa wataalam hawa wakidhani wana magonjwa ya kinywa ikiwamo mashimo katika meno, kulika kwa meno, kuoza kwa meno na magonjwa ya fizi.

Si wagonjwa wote wenye kutoa pumzi yenye harufu mbaya wana tatizo halisi la halitosis, kati ya asilimia 5 hadi 72 wanaofika katika huduma za afya hugundulika kuwa hawana tatizo hilo moja kwa moja.

Tatizo la kutoa pumzi yenye harudu mbaya ambalo ndiyo halitosis halisi huwa linasababishwa na uwapo wa mrundikano wa bakteria katika uvungu wa mafizi na nyuma ya ulimi jirani karibu na koo.

Kinywa kwa ujumla, ikiwamo meno, fizi, ulimi na vifuko vya mate yanaweza kuwa ni maficho mazuri kwa mamia ya bakteria.

Ndio maana inaaminika tatizo la harufu mbaya mdomoni ni kinywa chenyewe.

Kinywani pekee kuna karibu jamii 600 za bakteria ambao huambatana na mabaki ya vyakula tunavyokula kila siku. Uwapo na protini ya kwenye mate na protini ya vyakula tunavyokula, uvunjwaji wa mabaki yake na bakteria waliopo mdomoni ni chanzo cha kuwapo kwa harufu mbaya.

Mabaki ya protini mdomoni ambayo huvunjwavunjwa na bakteria na kuwa tindikali ya amino na hapo baadaye inapovunjwa, hutoa gesi yenye harufu mbaya.

Mfano mzuri ni pale protini ijulikanayo k**a methionine na cysteine inapovunjwa vunjwa kinywani huweza kutoa gesi yenye harufu mbaya ijulikanayo k**a hydrogen sulphide.

Mara nyingi harufu ya kinywa inaweza kuwa nzito Zaidi baada ya kuamka ni kwa sababu wakati wa kulala mdomoni kunakuwa na kiasi kidogo cha hewa ya oksijeni.

Bakteria waliopo mdomoni ni wale wasiohitaji hewa ya oksijeni, hivyo kipindi cha usiku tuiwa tumelala ndipo huvunjavunja mabaki ya chakula ambayo huambatana na kutolewa gesi zenye harufu mbaya.

Vilevile, harufu ya kinywa inaweza kubadilika kutokana na vyakula tunavyokula vikiwamo vitunguu maji, vitunguu swaumu, iliki, tangawizi na pia uvutaji sigara na unywaji wa pombe.

Hivyo si mara zote kupumua harufu isiyo ya kawaida, bali mara nyingine inakuwa tatizo la muda tu lililochangiwa na vyakula na matumizi mengine ya vitu.

Kwa asilimia 10 zilizobaki mara nyingi husababishwa na matatizo mengine ikiwamo magonjwa ya kooni, puani, shambulizi za nyufa za mifupa iliyopo usoni, magonjwa ya mfumo wa chakula, magonjwa katika mapafu, magonjwa ya masikioni na madhara ya ugonjwa sugu wa mafindofindo (tonsillitis).

Pia, uwapo wa majipu ya fizi/meno, vidonda mdomoni au michubuko, vidonda vya kooni, huambukiza virusi vya herpes simplex na HPV. Mara chache pia tatizo hili linaweza kuchangiwa na magonjwa ya ini ikiwamo kuharibika kwa ini na majipu katika ini.

Mara nyingine wanaolalamika tatizo hili hubainika kuwa ni tatizo la usafi wa kinywa. Na wanaposhauriwa kuboresha usafi wa kinywa kwa kutumia dawa za meno, au kusukutua na dawa maalum za kusafisha kinywa nyuma ya ulimi, tatizo huweza kuisha haraka.

Inapotokea tatizo hilo chanzo chake sio mdomoni, ni vigumu kuweka bainisho sahihi na vilevile hata kutibika kwake inakuwa vigumu.

Uchunguzi wa tatizo hili huanzia kwa mhusika mwenye we kwa kueleza historia ya tatizo kisha wataalam wa kinywa au daktari wa kawaida humchunguza kwa kumfanyia majaribio na vipimo kadhaa.

Baada ya wataalam wa afya kujua bainisho la ugonjwa ndipo ushauri na matibabu huanza. K**a chanzo cha harufu mbaya ni maradhi ambayo si ya kinywani, wataalam wa afya watakupa matibabu ya kutibu chanzo hicho.

K**a chanzo cha kutoa pumzi yenye harufu mabya ni kinywa, wahudumu wa afya watamuelekeza mgonjwa mambo mbalimbali k**a ifuatavyo;

Kuhakikisha kupiga mswaki katika ulimi mara mbili kwa siku kwa kutumia mswaki laini, kifaa k**a kijiko kwa ajili ya kukwangua uso wa ulimi, vilevile kutumia dawa yenye kiambata cha kuua bakteria.

Ulaji wa kifungua kinywa chenye afya ikiwamo kula matunda na mboga za majani yenye nyuzi nyuzi husaidia kusafisha kinywa eneo la nyuma ya ulimi wakati wa kumezwa.

Utafunaji wa bazooka unasaidia kuufanya mdomo usiwe mkavu na hewa ya oksijeni kuingia kinywani kwa wingi, vilevile utafunaji wa bazooka huweza kusaidia kutiririka kwa mate kwa wingi yanayosaidia kusafisha kinywa na kuua vimelea vya maradhi.

Mdomo ukiwa mkavu na hautafuni chochote huchangia kujiimarisha kwa bakteria wasihitaji hewa ya oksijeni.

Sukutua kwa maji mengi ikiwezekana ya uvuguvugu kila mara baada ya kula chakula, na kabla ya kwenda kulala. Unaweza pia kutumia dawa maalum za kusukutulia kinywa zenye dawa ya kuulia vimelea.

Jaribu kuboresha usafi wa kinywa kwa kuusafisha ulimi, safisha meno kwa mswaki kila unapomaliza kula chakula, ondoa mabaki ya chakula yaliyojibana katika meno na fizi na safisha na sukutua kinywa chako kwa dawa maalum kabla ya kulala.

Unaweza kutumia vitu asilia vikiwamo majani ya miti na karafuu k**a njia ya kupunguza kupumua hewa yenye harufu mbaya.

Vizuri kufanya uchunguzi wa afya ya kinywa mara kwa mara angalau kwa miezi sita mara moja ili kuweza kubaini magonjwa mbalimbali ya kinywa mapema.

NINA SULUHISHO LA HARUFU MBAYA YA KINYWA WASILIANA NASI +255679972904

11/11/2021

JE, NI BAADA YA MUDA GANI INAFAA KUBEBA MIMBA BAADA YA MIMBA ULIYOBEBA KUHARIBIKA?

Swala hili limekuwa likiwatatiza wamama wengi wanaopatwa na tatizo la mimba kuharibika.

Ni vizuri kwanza kujua vitu vinavyoweza kusababisha mimba kuharibika.

Mimba nyingi huharibika kutokana na makosa ya ukuaji wa mtoto. Sehemu kubwa ya makosa haya huwa ni kwenye vinasaba vyake. Yanaweza kuwa ya kurithi au yasiyo ya kurithi yaliyotokea kwa bahati mbaya kwa mtoto.

Zipo pia sababu nyingine k**a vile maumbile ya viuongo vya uzazi, magonjwa ya mama k**a vile kisukari, magonjwa ya damu, magonjwa ya vijidudu (infection).
Pamoja na sababu za mimba kuharibika kuwa nyingi, mara nyingi linapotokea tatizo hili huwa sababu iliyosababisha haifahamiki. Hali hii husababisha akinamama wengi na wenza wao kubaki na maswali mengi kwanini imewatokea hivyo na hujiuliza k**a inaweza kutokea tena kwenye ujauzito mwingine.

Mara nyingi hali hii hutokea mara kwa mara na kujirudia Hii ni kwa sababu makosa ya ukuaji yanayotokea bahati mbaya huwa ni jambo lenye uwezekano mdogo sana kujirudia. Hata hivyo iwapo ujauzito umeharibika kwa sababu nyingine k**a vile za kimaumbile au magonjwa ya damu, uwezekano wa kujirudia huwa mkubwa iwapo hali hiyo haijagundulika na hatua stahiki kuchukuliwa.

Kujibu swali la msingi ni baada ya muda gani inafaa kubeba mimba nyingine, inategemea k**a ni mara ya kwanza ujauzito kubadilika au ni hali iliyojorudia.

K**a ni mara ya kwanza, unaweza kubeba ujauzito mwingine mara tuu unapopata siku zako (vizuri zaidi angalau baada ya wiki 6 baada ya ujauzito kuharibika). Kwa kipindi hiki mwili unakuwa tayari kupokea ujauzito mwingine.
Hata hivyo kwa vile swala la ujauzito kuharibika linapokelewa kwa hisia tofauti na linaowakuta, ni vizuri ukabeba ujauzito baada ya kuwa umeshakuwa katika hali ya kawaida kihisia.

Iwapo ujauzito kuharibika sio mara ya kwanza, kuna umuhimu wa kufanyiwa vipimo na daktari ili upewe ushauri juu ya kujiandaa na ujauzito mwingine. Aina ya ushauri inategemea na matokeo ya vipimo atakavyoshauri daktari. Vilevile inategemea k**a ujauzito (mtoto) ulioharibika ulikutwa na tatizo lolote linalohitaji muda kulichunguza. Vipimo hivi vinaweza kuwa pamoja na vipimo vya damu, kipimo cha ultrasound na vingine.

Daktari anaweza kushauri utumie dawa za folic acid au vitamin wakati ukijiandaa na ujauzito mwingine.

Wanawake wengi (asilimia 70) waliopata tatizo la ujauzito kuharibika walifanikiwa kupata ujauzito tena na kujifungua watoto wenye afya njema.

Kwahiyo usikate tamaa iwapo umekutwa na hali hii.

Kwa tiba na ushauri wasiliana nasi +255679972904

28/10/2021

MATATIZO YA NGOZI YANAYOTOKANA NA KUNYOA

Wakati unaponyoa ndevu na nywele Wakati wa kuota baadhi ya sehemu nywele hushindwa kutoka nje ya ngozi na kuota ndani ya ngozi hali inayopelekea kusababisha uvimbe na kovu.zipo aina mbili za mapele yanayotokana na Kunyoa nywele na ndevu.

Magonjwa haya ni k**a ifatavyo

1. Acne Keloidalis Nuchae

Acne keloidalis nuchae (AKN) Ni tatizo linalotakana na maambukizi ya bacteria P.Acnes kwenye ngozi baada ya kunyoa,hali inayopeleka vijitundu vya vinyweleo kuziba na kufanya nyele kushindwa kutoka nje ya ngozi na kukulia ndani ya ngozi hivo kusababisha mapele makubwa na makovu. Acne keloidalis nuchae (AKN) mara nyingi hutokea sehemu ya kisogo.
Mbali na kunyoa tatizo hili pia huweza kusababishwa na uvaaji wa kofia.
Image result for Acne Keloidalis Nuchae

2.Pseudofolliculitis barbae (PFB)

Tatizo hili huwapata watu wengi,hili hutokea sehemu za kidevu na mashavu.Hii pia husababishwa na kuziba kwa vinyweleo vyua ngozi baada ya kunyoa hivo kupelekea ndevu kukulia ndani ya ngozi na kusababisha uvimve kwa juu ya ngozi na baadae makovu meusi.

Pseudofolliculitis barbae (PFB)
MATIBABU YA PSEUDOFOLLICULITIS BARBAE (PFB) NA ACNE KELOIDALIS NUCHAE

Wasiliana nasi kwa number +255679972904

28/10/2021

JE, NINI SABABU YA UKE KUWA MKAVU?

Hali ya ukavu ukeni inaweza kuwa tatizo kwa wanawake katika umri wowote, ingawa hujitokeza zaidi mara kwa mara kwa wanawake wenye umri mkubwa, hasa pale wanapofikia ukomo wa hedhi.

Kupungua kwa viwango vya vichcocheo(hormone) huwa ndio sababu kuu ya kukauka kwa uke. Homoni za mwanamke husaidia sana kuutunza uke na kuzifanya tishu za uke kuwa zenye afya kwa kutengeneza unyevunyevu wa kawaida ukeni, tishu za uke kuvutika pamoja na hali ya uasidi yaani uchachuchachu. Visababishi vingine vya hali ya ukavu ukeni vinaweza kutokana na utumiaji wa madawa pasipo kufuata ushauri wa daktari au kutokufanya usafi maeneo ya uke.



Viwango vya homoni ya estrogen vinaweza kushuka kutokana na sababu zifuatazo, napenda leo uzijue. Sababu hizi huwa k**a ifuatavyo:



Kunyonyesha


Kujifungua mtoto


Uvutaji sigara


Athari kwenye vifuko vya mayai


Kushuka kwa kinga za mwili


Kukoma hedhi


Utumiaji wa madawa ya kuongeza homoni za uzazi


Kuondolewa kwa kifuko cha yai(ovary)


Kuosha maeneo ya uke kwa kutumia madawa yenye harufu kali na yenye kemikali.




Je, Dalili Zake Zinakuwaje?

Dalili za kukauka kwa uke huwa k**a ifuatavyo:

Kuhisi muwasho au moto maeneo ya mashavu ya uke


Kuhisi moto wakati wa kukojoa


Kukojoa mara kwa mara


Kuhisi maumivu wakati wa tendo la ndoa yakiambatana na damu kidogo


Kukosa hamu ya tendo la ndoa


Mashavu ya uke kuwa membamba


Kuwa na maambukizi ya UTI yasioisha au yenye kujirudiarudia.


TIBA ZAKE

Wasiliana nasi upate tiba ya kudumu,epuka kununua dawa zilizo na kemikali +255679972904

28/10/2021

🙏🙏🙏🙏dar to iringa

28/10/2021

MATATIZO KATIKA UZALISHAJI WA MBEGU ZA KIUME

Matatizo katika uzalishaji
wa mbegu za kiume huwatokea wanaume na ni chanzo kikuu cha kutopata watoto kwa wanandoa au watu walio katika mahusiano na wanatafuta mtoto.

Hili pia ni tatizo la ugumba kwa wanaume
Mbegu za kiume hupatikana katika manii au majimaji yanayotoka kwa mwanaume unapomaliza tendo la ndoa. Si kila mwanaume anayefanya tendo la ndoa vizuri au anatoa manii kwamba hana tatizo. Unaweza kuwa vizuri kumbe huna mbegu za kiume au mbegu zako hazina ubora wa kurutubisha yai la mwanamke.

MBEGU ZA KIUME
ni ndogo sana na hazionekani kwa macho hadi kwa vifaa maalum vya maabara.
Maumbile ya mbegu za kiume zina kichwa, mwili na mkia na huogelea kwenye manii na huwa na mwendo wa kasi sana.

MWANAUME
hutoa kiasi cha mbegu kati ya milioni ishirini hadi milioni mia tatu na hamsini kila anapotoa manii zenye ujazo wa milimita mbili na nusu hadi tatu na nusu.
Manii yenye ubora huwa nzito kiasi na huvutika k**a k**asi na zikikaa kwa muda kidogo huyeyuka.

MATATIZO YANAYOTOKEA
Matatizo ya mbegu za kiume kushindwa kurutubisha yai yapo mengi, mbegu zinaweza kukosa mwendo kasi zikawa goigoi, badala ya kwenda mbele zikaenda kinyumenyume au upandeupande, nyingine hazina mikia au vichwa vimekatika na nyingine zina mikia miwili badala ya mmoja.

MWANAUME
anayetoa mbegu za kiume chini ya milioni ishirini haweza kumpa mwanamke mimba. Kiwango cha manii kinachotakiwa kutoka na kubeba mbegu kisiwe chini ya milimita mbili na nusu na kisizidi tatu na nusu, kinyume cha hapo mbegu haziwezi kuwa na ubora.

CHANZO CHA TATIZO
Maambukizi ya mara kwa mara katika viungo vya uzazi vya mwanaume huchangia kwa kiasi kikubwa.

MFANO,
1️⃣UTI za mara kwa mara kwa mwanaume

2️⃣Maumivu ya mara kwa mara ya korodani

3️⃣kufanya kazi katika mazingira ya joto kali

4️⃣kuumia korodani ni miongoni mwa matizo yanayoathiri uzazi kwa mwanaume kwa kiasi kikubwa.

5️⃣Ukosefu wa nguvu za kiume
ni tatizo kubwa, kwani utashindwa kutoa manii.

6️⃣Matumizi ya dawa za kulevya mfano uvutaji bangi, mirungi, He**in, Coacaine na nyingine huathiri uzazi au huuwa kabisa uzazi kwa mwanaume.

7️⃣Uvutaji sigara
na ulevi wa kupindukia pia huathiri uzazi hasa unywaji wa pombe kali.

8️⃣Maambukizi ya virusi vinavyosababisha ugonjwa wa ‘Mumps’ pia huharibu korodani na kuua uzazi hasa unapopata ugonjwa huu katika umri wa kuoa na unatafuta mtoto utakuwa unafanya tendo la ndoa vizuri, unatoa manii lakini mimba hakuna. Hii ni kutokana na kutokuwa na mbegu za uzazi.

DALILI ZA TATIZO
1️⃣Hakuna dalili za wazi kwamba mwanaume mwenye tatizo la uzazi yupo hivi, bali dalili za moja kwa moja kwamba una tatizo la uzazi ni kutokuwa na nguvu kabisa za kufanya tendo la ndoa

2️⃣Kushindwa kabisa kutoa manii wakati wa tendo
kutoa manii mepesi sana k**a maji,
kutokuwa na korodani, unatakiwa uwe na korodani mbili, k**a unayo moja basi ni vema ukapima mbegu zako ili kuthibitisha k**a una uwezo wa kuzaa.

UCHUNGUZI
Hufanyika kwenye kliniki za matatizo ya uzazi, katika hospitali za wilaya na mikoa.

Vipimo vya manii ili kuangalia k**a unazo mbegu za kiume, je mbegu hizo zina ubora?

Zina kasi ya kutosha? Zina kiwango kizuri? Pia zitaangaliwa k**a hakuna maambukizi wala kasoro. Pia korodani itachunguzwa k**a kuna tatizo kwa ndani.

USHAURI
K**A WEWE NI MWANAUME NA UNA TATIZO AMBALO NIMEELEZEA HAPO JUU WASILIANA NASI KWA TIBA NA USHAURI
+255679972904

28/10/2021

P.I.D hupelekea PH ya uke kuwa unbalanced na kupelekea mwanamke kushindwa kubeba mimba (ugumba) sababu hupelekea mbegu za mwanaume kuwahi kufa lakini pia hupeleke mvurugiko w homoni kwa wanawake wengi.....

PACKAGE YA VIRGINAL DETOX NDIO MKOMBOZI.

piga au whatsapp 📞+255679972904

Want your business to be the top-listed Beauty Salon in Dar es Salaam?
Click here to claim your Sponsored Listing.

Category

Telephone

Website

Address


Dar Es Salaam