Dokta Mifupa

Dokta Mifupa

Share

Ninawasaidia Watu k**a Wewe Kuondokana na Changamoto za Mifupa na Viungo bila kufanyiwa Upasuaji

07/08/2024

Kukaa Kwa Muda Mrefu kinaweza kukusababishia Maumivu ya Mgongo hapo baadaye.

Jenga Utaratibu wa Kupata Muda wa Kufanya hata mazoezi mepesi ya kunyoosha mgongo baada ya Kazi .

Afya Yako ni MTAJI Muhimu sana.

20/07/2024

𝙑𝙄𝙅𝙐𝙀 π™‘π™”π˜Όπ™†π™π™‡π˜Ό π™ˆπ™π™ƒπ™„π™ˆπ™ π™†π™’π˜Ό π˜Όπ™π™”π˜Ό π™”π˜Ό π™ˆπ™„π™π™π™‹π˜Ό π™‰π˜Ό π™ˆπ˜Όπ™π™‰π™‚π™„π™Š

Mifupa imeundwa kwa Madini mbalimbali ikiwemo madini ya calcium na phosphorus kwa kiasi kikubwa hivyo ili uweze kuwa na mifupa imara unahitaji kula vyakula vyenye calcium na phosphorus kwa wingi.

Vyakula hivyo ni k**a ifuatavyo:-

βœ“Samaki.
Samaki wana madini k**a calcium ambayo ni muhimu katika mifupa pia mafuta ya samaki (omega 3 fatty acids) yana umuhimu sana katika afya ya mifupa pamoja na mfumo wa damu.

βœ“Mboga za majani.
Tunapata calcium na vitamin mbalimbali ambavyo vinaweza kuimarisha mifupa na viunga pia zina uwezo wa kuzuia vimeng'enya hatari vinavyoweza kusababisha kuvimba na maumivu katika viunga.

βœ“Matunda.
Baadhi ya matunda yana lycopene na anthocyanins na vitamin C ambazo huepusha udhaifu wa mifupa. Matunda hayo ni k**a machungwa, nyanya,limao, strawberries, ndizi mbivu nk

βœ“Mafuta.
Vyakula vyenye kiasi kikubwa cha omega 3 mfano mafuta ya parachichi na mafuta ya mzeituni

βœ“Maharage.
Maadhi ya maharage ni mazuri katika afya mifupa mfano maharage ya
soya,maharage meusi nk haya yana virutubisho ambavyo vinaweza kuimarisha mifupa.

βœ“Maziwa.
Maziwa yana calcium na vitamin mbalimbali ikiwemo vitamin D ambayo husaidia ufyonzaji mzuri wa calcium.

βœ“ Mayai.
Haya yana madini mbalimbali ikiwemo calcium na vitamins kwa wingi hivyo husaidia kuwa na mifupa imara.

βœ“ Vyakula vyenye Phosphorus ni k**a ndizi mbivu,apples, broccoli,maharage nk

Afya Bora ya mifupa Yako ni Matokeo ya Machaguo Bora ya vyakula unavyoulisha Mwili wako .

Linda Afya Yako , Linda mifupa Yako .

Kwa Ushauri zaidi wasiliana nasi

wa.me/25576388352

20/07/2024

Ugonjwa Wa Arthritis Ni Nini?

Arthritis ni ugonjwa unaotokana na namna yo yote ya hitilafu katika maungio ya mifupa ya binadamu ambao husababisha maumivu na pengine kuvimba katika sehemu moja au zaidi ya maungio hayo. Neno arthritis halilengi ugonjwa mmoja bali jamii ya magonjwa ambayo kwa ujumla yapo zaidi ya 100. Tabia kuu ya magonjwa haya ni maumivu kwenye maungio ya mifupa (joints) ambayo ni endelevu na ambayo hutokea eneo hilo moja.

Chanzo Cha Arthritis ni nini?

Kusudi kuelewa chanzo cha ugonjwa huu, hebu kwanza tutazame muundo wa joint au sehemu mifupa miwili inapokutana. Fikiria goti ambapo mifupa miwili mmoja wa paja na mwingine wa mguu vinapokutana:

Maungio ya mifupa

Ligaments: Ndicho kitu kinachoshikilia mifupa hii miwili pamoja. Hii ni k**a utepe wa plastiki au mpira unaonyumbuka uliozunguka eneo hilo kwa nje, ukikunja goti inanyumbuka na ukinyoosha mguu inarudi.

Cartilage: Huu ni utando unaofunika eneo ambalo mifupa hugusana ili kuzuia mifupa hii isisuguane moja kwa moja. Utando huu ambao kwa kiswahili tunauita gegedu huyawezesha maungio hayo kufanya kazi kiulaini pasipo kusababisha maumivu.

Capsule: Hiki ni kitu kinachofunika maungio haya kikizunguka pande zote. Ndani ya mfuko huu wa capsule kuna ukano (synovial fluid) ambao huzalishwa na synovial membrane. Ukano ni ute wa kulainisha sehemu hiyo ya maungio na synovial membrane ni utando ulio kwenye kuta za ndani za capsule.

Ugonjwa wa arthritis unasababishwa na hitilafu yo yote katika sehemu hizo za maungio ya mifupa. Inaweza kuwa gegedu inalika, upungufu wa ukano (synovial fluid), maambukizi ya vijidudu katika moja ya maeneo hayo au mchanganyiko wa matatizo.

Aina Za Ugonjwa Wa Joints-Arthritis

K**a nilivyoeleza hapo juu, kuna aina zaidi ya 100 za ugonjwa huu wa joints au arthritis. Katika mada yetu ya leo tutatazama aina k**a nne hivi za ugonjwa huu, tukielezea chanzo cha kila aina.

Osteoarthritis: Hii ni aina ya arthritis inayosumbua watu wengi zaidi kuliko aina nyingine zote. Ugonjwa huu huwapata zaidi watu wenye umri mkubwa. Osteoarthritis hutokea pale cartilage inapopoteza uwezo wake wa kubonyea na kuwa ngumu hivyo kuharibika haraka. Cartilage ni kiungo cha kuhimili migandamizo ya ghafla (shock absorber). Cartilage hii inapopoteza ubora wake, tendons na ligaments huvutika na kusababisha maumivu. Hali ya uharibifu huu wa cartilage ikiendelea, mwishowe mifupa huanza kusuguana moja kwa moja na ndipo mgonjwa atakapoanza kupata maumivu makali sana.

Athari za ugonjwa huanza taratibu na kuongezeka na muda. Kutaanza kutokea maumivu kwenye joint baada ya kufanya shuguli fulani au baada ya mapumziko ya muda mrefu. Joints zitakaza, hasa mapema asubuhi unapotaka kuanza shughuli zako za kawaida. Siku zinavyosogea ndivyo utakavyoona ni vigumu zaidi kukitumia kiungo chako. Mara nyingine utaona uvimbe kwenye joint. Osteoarthritis hushambulia zaidi nyonga, mikono, magoti na uti wa mgongo.

Rheumatoid arthritis: Ugonjwa huu hutokea pale mfumo wa kinga ya mwili kwa bahati mbaya kuanza kushambulia viungo vya mwili ikiwa ni pamoja na synovial membrane (synovium) na kusababisha uvimbe na maumivu. Hali hii isipodhibitiwa, huweza kusababisha ulemavu. Ugonjwa huu unaweza pia kushambulia macho, ngozi, mapafu, midomo, damu na mishipa ya damu. Huu ni ugonjwa ambao zaidi

Endelea kufuatilia Ukurasa huu Kwa elimu na Msaada zaidi.




+255763881352

17/07/2024

πŸ’‰πŸ’Šπ‰π„ π”ππ€π’π”πŒππ”π‹πˆπ–π€ 𝐍𝐀 πŒπ€π“π€π“πˆπ™πŽ π˜π€ πŒπˆπ…π”ππ€ πˆπŠπˆπ–π„ππŽ πŒπ€π”πŒπˆπ•π” πŒπ€πŠπ€π‹πˆ π˜π€ πŒπ€π†πŽπ“πˆ 𝐍𝐀 πŒπ†πŽππ†πŽ 𝐍.𝐊 (πŽπ’π“π„πŽππŽπ‘πŽπ’πˆπ’) 🩺.

Ni ugonjwa ambao husababishwa na maambukizo ya bacteria katika mfupa na misuli inayozunguka mfupa bacteria hao ni (staphylococci).

Mara nyingi tatizo hili la mifupa hutokea ktk uti wa mgongo(mgongo kupinda na kuuma Mara kwa Mara), MAGOTI kuuma,nyonga na kifuani.

*SABABU ZINAZOSABABISHA MATATIZO YA MIFUPA (OETEOPOROSIS)

*1⃣Magonjwa ya figo.
*2⃣Upungufu wa hormone za estrogen hii ni kwa wanawake hasa wale wenye`` ( *MENOPAUSE) kikomo cha hedhi
*3⃣Upasuaji na kuondolewa (ovaries) mayai ya uzazi kwa wanawake
*4⃣ANOREXIA uzito mdogo kupita kias APA ni kwa wale wanaopenda sana kujinyima kula kupita kiasi wakikwepa kunenepa sana na kufanya mazoez`` kupita kiasi.
*5️⃣Ujito mkubwa.
*6️⃣Umri mkubwa.
*7️⃣Kurithi & Kutumikisha sana viungo.

*KINGA ZA MATATIZO YA MIFUPA.(OSTEOPOROSIS)

*1⃣Epuka matibabu yeye kutumia kemikali
*2⃣ Zingatia rishe bora haaa utotoni pia pendelea kula vyakula vya asili vyenye madini yakutosha yanayoimarisha MIFUPA
*3⃣ Acha au punguza matumizi ya pombe
*4⃣ Fanya mazoez ya kutosha na kunywa maji ya kutosha

ATHARI
*ZINAZOSABABISHWA NA TATIZO HILI
1⃣Mifupa kuvunjika kwa urahisi.
*2⃣kupinda mgongo wakati wa uzeeni
*3⃣Maumivu makali ya Mifupa hasa ktk uti wa mgongo,mabegani,kifuani na ktk nyonga.

MATIBABU YA OSTEOPOROSIS
kula kwa wingi vyakula vya vitamini D na vyenye madini ya calcium k**a` maziwa ubuyu,n.k`

Want your business to be the top-listed Beauty Salon in Dar es Salaam?
Click here to claim your Sponsored Listing.

Category

Website

Address


Dar Es Salaam
255