afya na tiba

afya na tiba

Share

Ushauri wa afya Kwa watu wote. Elimu ya mfumo wa maisha (chakula, mazoezi na virutubisho) k**a Tiba.

02/09/2023

BWANA AWABARIKI nyote

25/05/2023

Tunza KINYWA chako Kwa kukisafisha kila baada ya chakula na k**a unamatizo ya meno wasiliana nasi Kwa Whatsapp number 0753107557 Kwa ushauri natiba

24/05/2023

TATIZO LA KINYWA NA MENO
Tatizo hili kawaida hujulikana k**a meno kuoza/magego.
Hili tatizo hutokea endapo bakteria wataharibu sehemu ya juu ya jino. mara zote Kuna bakteria wanaopatikana katika KINYWA/ mdomo. Bakteria Hawa huungana na asidi , mate na mabaki ya chakula kutengeneza kitu kinachoitwa Kwa kitaalam plaque. Plaque ni dutu inayonata na mara nyingi hupatikana katikati ya meno na huanza kutengenezwa ndani ya dakika 20 baada ya kula. Bakteria walio ndani ya plaque hubadili mabaki ya chakula hasa VYA sukari na wanga kuwa asidi. Asidi hii husaga/ kuvunja enamel katika jino kutengeneza kijishimo ambapo hiki kijishimo kikibaki bila kutibiwa kitafikia fizi na Neva na kusababisha jino kuuma au KUPATA infection.
SABABU ZA KUOZA KWA MENO AU MENO KUUMA.
1. Ukosefu wa vyakula vigumu
2. Ulaji wa vyakula vyenye sukari nyingi au vyakula vitamu kupita kiasi ambavyo huchochea ukuaji wa bakteria.
3. Ukosefu wa madini ya kalsium katika mlo
4. Ukosefu wa vitamin D
5. Tatizo la kiafya .
K**a unatatizo Hilo unaweza kuwasiliana nasi Kwa tiba na ushauri Kwa Whatsapp number+255 753 107 557
Tambua afya Yako ndiyo mtaji wako ijali afya Yako na uitunze.na MUNGU ALIYE HAI ATUBARIKI SOTE

24/05/2023

MATATIZO YA MFUMO WA MMENG'ENYO WA CHAKULA NA TIBA YAKE
Mfumo wa MMENG'ENYO WA CHAKULA ni jumla ya viungo mwilini vinavyofanya kazi ya kuingiza chakula mwilini, kukisaga,, kukisafirisha ndani ya mwili, na kukimeng'enya .tunaposema MMENG'ENYO/umeng'enyaji ni Ile Hali au mchakato wa kukivunjavunja chakula Ili kiwe katika Hali ambayo kitaweza kusharabiwa/ kufyonzwa na kutumiwa na mwili.viungo VYA mwili vinavyo husika na mfumo huu wa MMENG'ENYO WA CHAKULA ni kinywa,umio, mfumo wa tumbo,ini,mfuko wa nyongo,utumbo mwembamba ,kongosho na utumbo mpana.
Huu ni mfumo muhimu sana ktk mwili wa mwanadamu maana ndio kitovu(center) Cha utendaji kazi wa mwili. Kila kitu kinachoingia mwilini kinapelekwa katika mfumo huu wa MMENG'ENYO WA CHAKULA ndipo baada ya kuchakatwa kila kitu kinapelekwa ktk seli(cell) husika ya mwili wa mwanadamu. Hiki ndicho kiini Cha afya ya mwanadamu.
MATATIZO YANAYOATHIRI MFUMO HUU WA MMENG'ENYO WA CHAKULA NI PAMOJA NA;
>BAWASIRI(MANG'ONDI)
>VIDONDA VYA TUMBO(ULCERS)
>KUPATA CHOO KIGUMU/KUTOKUPATA CHOO KABISA(CONSTIPATION)
>GESI KUJAA TUMBONI
>KUHARISHA
>KUTAPIKA
>MAUMIVU YA TUMBO
>KINYWA KUNUKA N.K
1.TATIZO LA BAWASIRI.
Huu ni ugonjwa unaotokana na kuathirika Kwa mishipa ya damu ya ndani na nje ya sehemu ya haja kubwa na wakati mwingine kusababisha kutoka kinyama au uvimbe kwenye sehemu hiyo. Tatizo hili huathiri watu wazima kuliko watoto na inakadiriwa kuwa karibu50% ya watu wote wako na hatari ya KUPATA tatizo hili katika umri wa miaka 30-40.
AINA ZA BAWASIRI
Kuna aina mbili za BAWASIRI.
YA NDANI
YA NJE
CHANZO CHA TATIZO HILI
CHANZO halisi Cha ugonjwa huu hakijapatikana ila Kuna vitu ambavyo huwa Chanzo Cha ugonjwa huu wa BAWASIRI ambavyo ni;
1. KUPATA CHOO KIGUMU
2. Kukaa kitako mda mrefu
3. GESI KUJAA TUMBONI
4. Magonjwa ya moyo na Figo
5. Uzito kupita kiasi
6. Kufanya mapenzi kinyume na maumbile
7. Matumizi ya vyoo VYA kukaa Kwa mda mrefu
DALILI ZAKE
1. Mwasho katika eneo la tundu la haja kubwa
2. MAUMIVU makali wakati wa kujisaidia
3. Kutoka uvimbe ktk eneo la tundu la haja kubwa
4. Kujitokeza kinyama katika eneo la tundu la haja kubwa
5. Choo KIGUMU k**a Cha mbuzi
6. Kutopata choo Kwa mda mrefu
7. Kutoka damu wakati wa haja kubwa
ATHARI ZAKE
1. KUPATA upungufu wa damu
2. KUPATA tatizo la kutohimili choo
3. Hupunguza za kiume na kuondoa hamu ya tendo la ndoa
4. Kuathiri kisaikolojia
5. Kukosa molali ya kufanya kazi kutokana na maumivu makali.
Ukitaka kuelewa zaidi na maelezo juu ya kutibu tatizo hili endelea kunifollow katika page yangu hii au wasiliana na me Kwa Whatsapp number+255 753 107 557

26/04/2023

FANGASI ZA UKENI
0753107557

SABABU ZA UKE KUTOA HARUFU MBAYA, MAJI MAJI YA NJANO au MEUPE

Ni matumaini nyote mnaendelea vyema,
Leo naona ni bora tukazungumzia tatizo la kutokwa na harufu mbaya ukeni maana watu wengi hudhani kuwa na harufu mbaya itokayo ukeni ni matokeo ya uchafu tu na ndio maana wanaume huwachamba wake zao kuwa hawajuhi kujisafisha na kufanya wanawake kuongeza jitihada katika kujisafisha ukeni,leo napenda kuzungumzia tatizo hili linalowasumbua wanawake wengi na kuwaumiza kichwa kutokana na kwamba lina athari kubwa sana kwani hufanya ndoa zao kudumaa NK,
~kitaalamu Hali ya mwanamke kutokwa na maji yenye rangi nyeupe au njano ni Hali ya kawaida na sio tatizo Lakini endapo maji yanatoka yapo katika Hali ya ute mzito wenye rangi nyeupe au kahawia na yanatoa harufu kali au kuwasha hapo una tatizo
~majimaji au ute unaoteleza kutoka sehemu za siri ni njia inayowezesha viungo vya uzazi vya mwanamke kujisafisha au kutoa uchafu wa seli zilizokufa na mabaki ya damu ya hedhi nnje ya mwili pia huvikinga viungo vya uzazi dhidi ya maaambukizi ya bacteria
~Kwa kawaida huwa hayatoi harufu na huwa hayawashi na huwa na rangi nyeupe au njano pia huwa na asidi ya LACTIN ambayo huzuia bacteria kuzaliana
~mwanamke hutoa kiasi cha grams 2 za seli zilizokufa kutoka kwenye mji wa kizazi na grams 3 za ute mwepesi kila siku, kiwango hicho kinaweza kuongezeka au kupungua kutegemeana na mzunguko wa hedhi pia Kuna wakati ute huwa mwepesi na unaovutika na Kuna wakati pia huwa mzito wa rangi ya njano hautoi harufu
VISABABISHI VYA TATIZO HILI
~sababu za kutokwa na uchafu ukeni una vyanzo vingi sana vifuatavyo ni vyanzo vya tatizo hili
(1)BACTERIA VAGINOSIS
~Chanzo halisi cha ugonjwa huu hakijafanikiwa kuwa wazi,kinachotokea ni kuongezeka kwa ghafla kwa idadi ya ya bacteria hawa na kubadilisha uwiano wa kawaida katika mazingira ya uke, wanawake wenye wapenzi wengi na wanaofanya mapenzi kwa njia ya mdomo Wana hatari ya kupata tatizo hili
(2)TRICHOMONAS
~maambukizi haya hutokana na Aina ya protozoa wa seli moja, trichomonas mara nyingi huambukizwa kwa njia ya ngono, protozoa huyo huweza kukaa kwenye unyevu unyevu kwa Muda wa saa 24 Bila kufa hivyo kufanya taulo na chupi zisizokauka kuwa chanzo kingine cha tatizo hili
(3)YEAST INFECTION
~kwa kawaida Kuna kiwango kidogo cha yeast (candida albicans) katika uke, huwa tunasema Kuna maambukizi pale kiwango kinapozidi Hali ambayo inatokana na kubadilika kwa Hali ya hewa ukeni (Change in the PH balance of va**na)
~maambukizi ya yeast hayatokani na tendo la ndoa na tendo la ndoa, mambo ambayo huchangia tatizo hili ni MATUMIZI YA DAWA ZA KUZUIA MIMBA, MAWAZO, UJAUZITO, KISUKARI NA MATUMIZI YA ANTIBIOTICS
(4)VAGINAL OR CERVICAL CANCER,
~mtu anapokua na kansa ya uke, hutokwa na maji ya harufu mbaya, hivyo ni heri uwe unafanya check up ili kujua Afya yako na kwakuwa cancer ya kizazi inapona hivyo ni vema ukatambua mapema uanze tiba
(5)SEXUAL TRANSMITTED DESEAS (STDs)~Kuna baadhi ya magonjwa k**a vile KASWENDE NA KISONONO yanasababishwa na ngono na kuwa chanzo cha tatizo hili
(6)POOR HYGIENE ~tatizo la kutokwa na maji wakati mwingine husababishwa na muhusika kua mchafu yan mtu unaoga kwa siku mara moja, chupi moja ndio hiyo hiyo mwaka mzima, pads unakaa nayo saa 24, ukienda kukojoa ujitawadhi na maji masafi hivyo unategemea utakua salama kweli??? Zingatia usafi mrembo
DALILI ZA TATIZO HILI
~kutokwa na uchafu ukeni unaoambatana na kuwashwa au kutokewa na vipele, hii hutokana na kuharibika kwa uwiano wa bacteria hivyo kuwa na madhara na uchafu hutoka wa aina tofauti hapa chini nitaelezea kila Aina ya uchafu na dalili zake
WENYE RANGI YA KAHAWIA AU DAMU
~huu uchafu huonyesha dalili ya kuwa mzunguko wako wa hedhi umevulugika na wakati mwingine ni dalili ya kansa ya kizazi, mwanamke anayepata tatizo hili hutoa damu nyingi kuumwa sana nyonga
WENYE RANGI YA NJANO /KIJANI WENYE HARUFU MBAYA
~Endapo uchafu huo utatoka k**a povu na wenye rangi ya kijani au njano na ukiambatana na harufu mbaya huwa ni dalili ya ugonjwa wa trichomonas, maambukizi ya parasite yanatokana na ngono zembe, dalili Yake nyingine ni maumivu na kuwashwa wakati wa kutoa haja ndogo
MWEUPE MZITO K**A JIBINI
~mara nyingi hii huwa ni dalili ya maambukizi ya fangasi(YEAST INFECTION) na dalili nyingine huwa ni kuvimba sehemu ya nje ya siri, kuwashwa na kupata maumivu makali wakati wa tendo la ndoa
MWEUPE/KIJIVU WENYE HARUFU YA SAMAKI
~uchafu wa Aina hii ni dalili ya maambukizi ya bacteria vaginosis, mara nyingi mwenye tatizo hili husikia muwasho na maumivu sehem ya nnje ya uke
~MAMBO MUHIMU YA KUZINGATIA KUEPUKA TATIZO HILI NA TIBA YAKE
~Matibabu ya tatizo hili hufanyika baada ya kugundua chanzo cha tatizo na mara nyingi tiba Yake ni tiba ya dawa za antibiotics kitu ambacho si tiba nzuri zaidi kwasababu tatizo huweza kujirudia kila wakati na kusababisha matatizo zaidi hivyo tiba nzuri ni kuepuka hili tatizo kwa kufanya yafuatayo
👉EPUKA KUJIINGIZA VIDOLE MARA KWA MARA UKENI
👉EPUKA MATUMIZI YA DAWA ZA ANTIBIOTICS MARA KWA MARA
👉PUNGUZA KULA VYAKULA VYENYE SUKARI NYINGI
👉TUMIA PADS ZENYE ANIONS NI SALAMA KWA AFYA YAKO
👉SAFISHA VIZURI NGUO ZAKO ZA NDANI NA UZIANIKE JUANI NA HATA KUZIPIGA PASI
👉KUNYWA JUICE YA APPLE,STRAWBERRY, NANASI KWA WINGI
👉EPUKA KUFANYA NGONO ZEMBE
👉HAKIKISHA UNAJISAFISHA KILA UNAPOMALIZA KUJISAIDIA
👉EPUKA KUTUMIA DAWA ZA KUZUIA MIMBA
👉EPUKA KUTUMIA SABUNI AU VITU VYA MANUKATO UKENI,
NOTE:wanawake wengi mnapenda kutumia baadhi ya dawa kwa lengo la kuongeza vionjo kwenye mapenzi pia kufanya uke kunukia vizuri, au kukaza uke rafiki uke una harufu nzuri sana ambayo haipatkan kokote hivyo haihitaji kuwekwa pafyumu Wala kusafishwa kwa sabuni za kemikali kwani huwa panajisafisha hivyo ni heri ukaacha kutumia kwani madhara Yake hayaonekani sasa ila baada ya Muda huonekana
Mpendwa msomaji nashukuru Kwa kuchukua muda wako kufatilia makala zangu za afya
Ahsante
Kwa mahitaji ya Tiba na ushauri.
PIGA 0753107557
Whatsapp 0753107557

SHARE KWA WATU NA GROUPS MBALI MBALI ILI KUSAIDIA WENGINE,wahanga wa janga hili ni wengi.

Want your business to be the top-listed Beauty Salon in Mwanza?
Click here to claim your Sponsored Listing.

Category

Website

Address


Mwanza