MTU WA WATU
Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from MTU WA WATU, Health/Beauty, Mwanza.
08/05/2024
... โ๏ธ ๐๐๐ง๐ ๐๐๐๐ก๐ฌ๐ ๐๐๐๐๐ฅ๐๐ฆ๐๐.
Hakuna timu ambayo haijanufaika au kuumizwa na makosa ya waamuzi msimu huu na misimu iliyopita โ๏ธ
Tunachopaswa ni kuyazungumza mapungufu ya waamuzi k**a ni tatizo kiujumla sio kuaminisha watu kuwa timu moja au mbili au tatu zinapendelewa.
Mfano :
โ Mwamuzi kukataa goli halali la Elvis Rupia dhidi ya Simba SC (LITI) na kusababisha Singida FG kupoteza Mchezo (1-2).
โ Mwamuzi kuruhusu mabao (2) ya Off-side round ya kwanza na ya pili ya Azam FC dhidi ya Young Africans SC.
โ Mwamuzi kumpa kadi nyekundu Lameck Lawi badala ya yellow card, Young Africans dhidi ya Coastal Union.
โ Mwamuzi kukataa bao la Tabora United dhidi ya klabu ya Simba SC.
โ Mwamuzi kukataa bao la Azam FC alilofunga Kipre Jr dhidi ya Mtibwa sugar.
Ni matukio mengi sana nikiandika yote wino wa kalamu yangu utaisha.
Nataka kusema nini ?!
Nimesikia baadhi ya wachambuzi leo wakizungumzia tukio la waamuzi kukataa bao la Tabora United dhidi ya Simba, baadhi wanasema ni goli lakini waamuzi wote walikuwa mbali hivyo wasilaumiwe.
Wanasahau jinsi walivyoshikia Bango tukio la Lameck Lawi kuoneshwa kadi nyekundu bila kuzungumzia scenario ya tukio hilo kwamba mwamuzi pia alikuwa mbali ambapo alishindwa kutoa tafsiri vizuri kutokana na Mulumba na Lawi kuwa kwenye mstari 1 akiamini Lawi alikuwa beki wa mwisho hivyo kumvuta jezi Aziz Ki alistahili red card ambayo aliitoa na kufutwa na bodi ya ligi.
Leo kwa Tabora United wanazungumzia umbali waliokuwepo waamuzi, kuhusu Lawi walisema Yanga kabebwa wakati scenario ya matukio yanafanana !!!
Hiyo ndiyo Tanzania mahali ambapo bata akinya kaharisha, kuku akinya kanya.
08/05/2024
... ๐จ ๐๐๐๐ ๐ ๐๐ก๐ ๐ช๐๐๐ 4
Kiungo wa klabu ya Simba SC, Clatous Chama amebakiza mkataba wa wiki (4+) katika klabu ya Simba SC.
Mpaka sasa bado hajasaini mkataba mpya kuendelea kuitumikia klabu ya Simba SC.
Mchezaji huyo anataka Tsh 900 Million kwa mkataba wa miaka miwili ndipo asaini.
โ 25 Million - Mshahara kwa mwezi.
โ 300 Million - Signing fee.
25m ร 24 = 600m Salaries.
600m ร 300m = 900m.
Klabu ya Simba imetuma ofa mara kadhaa kumshawishi bila mafanikio, wanashindwana kwenye kipengele cha muda wa mkataba na malipo ya mshahara kwa mwezi.
Chama anataka mkataba wa miaka (2), Simba SC wanataka kumpa mkataba wa Mwaka (1). Chama anataka Tsh 25 Million kwa mwezi, Simba wanataka kumpa mshahara wa Tsh 20 Million kwa mwezi.
Bado haijafahamika k**a Chama atalegeza msimamo na kusaini kuendelea kuitumikia klabu ya Simba au ataondoka.
08/05/2024
... โ๏ธ ๐ ๐๐๐๐ญ๐ข ๐ช๐ ๐ ๐ช๐๐ฆ๐๐ข
Mchezo wa mwisho Yanga akiwa nyumbani dhidi ya Kagera sugar | 2023.
Full โ Yanga 5 - 0 Kagera sugar
โฝโฝโฝ Aziz Ki โ 42', 45', 90'
โฝ Fiston Mayele โ 49'
โฝ Morrison โ 84'
๐ฑ๏ธ Msimu uliopita Yanga alishinda mabao (5) kwenye mechi moja katika mchezo 1 pekee dhidi ya Kagera sugar.. Msimu huu kashinda tano tano katika michezo (8).
๐ฑ๏ธ Mpaka sasa msimu huu ni Kagera sugar pekee ndio klabu ambayo haijapoteza Mchezo Dhidi ya Yanga. Kaitaba Mchezo ulimalizika kwa suluhu.
Leo nini kitatokea ?! Majibu ni saa 2 usiku baada ya Mchezo kutamatika.
05/05/2024
... ๐ ๐ฅ ๐ ๐ฉ๐ฃ ๐ ๐ง๐๐ฅ๐๐๐๐ช๐
Aziz Ki ameweka rekodi ya kutwaa tuzo nyingi za mchezaji bora wa mwezi ligi kuu Tanzania bara ndani ya msimu mmoja tangu tuzo hizo zianzishwe 2021.
Aziz Ki amechaguliwa kuwa mchezaji Bora wa mwezi April 2024 ligi kuu Tanzania bara akiwashinda, Kipre Junior wa Azam FC na Joseph Guede wa Yanga.
๐ฆ๐ฒ๐ฎ๐๐ผ๐ป : 23 | 24
โ Mchezaji bora October โ Aziz Ki
โ Mchezaji bora March โ Aziz Ki
โ Mchezaji bora April โ Aziz Ki
Aziz Ki anaisaka tuzo ya mchezaji bora wa msimu (MVP) kutokana na overall performance ya msimu ambayo imepigiwa mstari na idadi ya tuzo za mwezi.
Pia kocha wa Yanga Miguel Gamondi amechaguliwa kuwa kocha bora wa mwezi ligi kuu Tanzania bara akiwashinda, Bruno Ferry wa Azam FC na . Hii ni tuzo yake ya (2) msimu huu.
05/05/2024
... ๐ ๐๐๐ก๐
Cristiano Ronaldo amefikisha hat-trick (66) kwenye career yake, amehusika kwenye magoli (66) msimu huu ๐ฎ๐ฅ
๐ฆ๐ฒ๐ฎ๐๐ผ๐ป : 23 | 24
โ 52 - Games.
โ 52 - Goals scored.
โ 14 - Assists.
CR7 ana rekodi nyingi sana nikiandika zote ukurasa utajaa, hizi ni chache anazoshikilia.
โ Magoli mengi zaidi Duniani - (890)
โ Hat-tricks nyingi zaidi Duniani - (66)
โ Magoli mengi zaidi UEFA-CL - (140)
โ Magoli mengi zaidi (17) katika msimu mmoja UEFA champions League (2013/14).
โ Magoli mengi hatua ya mtoano UEFA (67).
โ Most seasonโs as UEFA-CL top scorer: 2008, 2013, 2014, 2015, 2016, 2017, 2018.
โ Mchezaji pekee aliyefunga goli kwenye fainali tatu tofauti UEFA champions league.
โ Mchezaji pekee aliyefunga goli kwenye mechi (11) mfululizo UEFA-CL.
โ Mchezaji pekee aliyefunga hat-trick (3) katika msimu 1 UEFA-CL (2015/16).
โ Mchezaji pekee mwenye hat-tricks (8) UEFA champions league.
โ Mchezaji pekee mwenye magoli mengi zaidi kwenye timu za Taifa Duniani (128).
โ Mfungaji bora wa muda wote wa klabu ya Real Madrid akiwa na magoli (450).
โ Mchezaji pekee ambaye amefunga magoli 50+ katika calendar ya mwaka katika misimu (7) tofauti kwenye soka la ushindani Duniani.
โ Cristiano Ronaldo ndiye mchezaji mwenye magoli mengi zaidi ya kichwa Duniani (146).
โ Mfungaji bora wa muda wote kwenye michuani ya EURO akiwa na mabao (14).
โ ๐๐ฎ๐ป๐ฎ amefunga Hat-trick ya (3) katika mechi (7) za mwisho alizocheza. Hat-tricks nyingi zaidi katika mechi chache (7) kwenye historia ya Saudi Arabia ๐ธ๐ฆ
Ana umri wa miaka (39) !! ๐ฎ
Full โ Al Nasrr 6 - 0 Al-Wehda
โฝ๏ธโฝ๏ธโฝ๏ธ Ronaldo โ 5', 12', 52'
โฝ๏ธ Otavio โ 18'
โฝ๏ธ Mane โ 45'
โฝ๏ธ Fatil โ 88'
05/05/2024
... ๐ถ ๐ข๐ง๐๐
Engineer kaenda kukamilisha dili la ?
โ (๐)๐๐ฒ๐ฎ๐ป Othos Baleke.
โ (B) ๐ฃ๐ต๐ถ๐น๐น๐ถ๐ฝ๐ฒ Kinzumbi
05/05/2024
Mbavu ya kulia ya KMC... Said Abdallah 'Lanso'โ
Aliingia KMC kwenye dirisha dogo baada ya kuiongoza Mlandege kutwaa ubingwa wa michuano ya Mapinduzi mara mbili mtawalia...!
Tangu amefika KMC kajitwalia nafasi ya kuanza kikosini na uchezaji wake unakumbusha vitu vingi hasa anapotekeleza jukumu lake mama la kuzuia!
Lanso ana:
- Uwezo mkubwa wa kupiga tacklingโ
๐ TOP LEVELS
- Uwezo mzuri wa kukaba 1v1
- Uwezo mkubwa wa kushambulia akitokea pembeni
- Akili na timing sahihi ya kusoma mwenendo wa mshambuliaji wa timu pinzani.
- Usahihi sana kwenye pasi ndefu
- Uwezo wa kuongoza wengine na kuwapa motivation ๐ฅ๐
Kuna wakati nilishawahi kuwashugulisha mkipata muda mumfuatilieโ
โ๏ธ
Ni mgumu... Kule upande wake kunahitaji uwe fit haswaa Ili umtambuke...! KMC watafanya Biashara yake siku sio nyingi!
One of the best fullbacks we haveโ๏ธ Kumbukeni hili jina๐ฆ
05/05/2024
Issookkeey...!
Mechiiliyoanza kwa ushindani mzuri ila yenye upotevu mkubwa wa muda kwa matendo yasiyo na tija kwenye utafutaji wa alama za mchezoโ๏ธ Kipindi cha pili ndio kilikuwa cha matukio mengi ya kuchosha...! Iliharibu ladha nzima ya mechi na angalau mwamuzi alifidia dakika 8.
Mashujaa wamecheza vyema ila hawakushambulia kwa usahihi... Ilionekana mpango wao upo upande tu wa Kwasi kushambulia, wakamkaba Aziz KI โ๏ธ Namba yao kushambulia haikuwa mbaya ila maarifa ya kuwavuka walinzi wa Yanga yalikuwa haba. Wamecheza vizuri sana.
Yanga SC walikutana na ugumu kuwavuka Mashujaa... Waliamua kukabia chini kwanza na hapo ndio Mudathir huibuka shujaa. Walipokumbana na uamsho wa Mashujaa kipindi cha pili walibaki kulinda na kutupa mipira mirefu. Walikuwa na kipindi cha pili kigumu.
Attohoula Yao ndiye alikuwa bora zaidi kuzuia kwa Yanga... Ameua mashambulizi manne ambayo walinzi wa kati walishavukwa tena akitokea pembeni kuingia ndani. Ni kielelezo cha mtu anayejituma. Ndiye Man of the Match โ๏ธโ
Zuberi Kassim 'Dabi' amecheza vyema mno. Ndiye alikuwa kisababu cha Yanga kupoteza mawasiliano kipindi cha pili... Alizoeleka kuwa na Msala katikati ila leo peke yake amefanya kila kitu. Kaba haraka, pasia haraka kisha achia mpira.
Kacheza vizuri sana leo Maxi Mpia. Yupo flexible sana na mpira mguuni, akiamua kucheza kuanzia chini ana uwezo huo. Work rate yake imekuwa kubwa sana! Na kuna umbali mkubwa baina yake na goli.
Omary Kindamba amezuia vizuri upande wa kulia... Hakuwa vyema kupandisha mashambulizi ila suala lake mama alilitimiza sana. Hakuruhusu kutengenezwa 1v1 ocassiojs nyingi kwa kufika haraka kwenye mali.
Djigui ni KIBURI kikubwa cha mabeki wa Yanga. Wana uhakika wa usalama wa mpira na amefuta makosa mawili ya Bacca leo.
Well Mpoki Mwakinyuke... Very professional Perfomance โ๏ธ Guede na moja moja k**a vocha...!
Ule msako wa dakika za Magharibi ya roho ni hatari sana kwa afya ya baadhi ya viungo mwilini ๐ Ilikuwa ni watu kupasua 'Hamza Kanoon'
FT' Mashujaa FC 0 vs 1 Yanga SC.
02/12/2022
Hata k**a una akili nyingi kiasi gani usiishi kwa LOGIC kwenye MAHUSIANO, yatakushinda tu......
Click here to claim your Sponsored Listing.
Category
Website
Address
Mwanza
