AFYA YA UZAZI
TUNAWASAIDIA WANAWAKE KUTATUA CHANGAMOTO YA KUTOKUSHIKA UJAUZITO.
Nina imani kwamba hata wewe umetumia njia nyingi sana na k**a ndio umehitimisha na umekata tamaa basi napenda nikushauri kwamba ili uweze kunielewa vizuri katika haya machache hakikisha unaachilia mbali yote ambayo ulishauriwa kuyafanya na hayajakupa matokeo.
Kumbuka hukuzaliwa na maumivu makali ya hedhi au ya tumbo au ya mgongo na hukuzaliwa kuwa mtu mwenye mateso kuhusu afya yako ya uzazi.
*UGONJWA WA POLYCYSTIC OVARIAN SYNDROME*
Mwanamke huwa ana o***y mbili za kuzalisha mayai kila mwezi yaani,
🌹 O***y Ya Kushoto.
🌹 O***y Ya Kulia.
Ndani ya kila o***y ya mwanamke kuna kuna mayai ambayo hayajakomaa(Follicle cells).
Hizi "follicle cells" ndizo hukomazwa kila mwezi na kuwa yai ambalo hurutubishwa endapo litakutana na mbegu ya kiume(Sperm cell)
Sasa inapotokea izo Follicle cells zimekomaa vizuri kwenye o***y na zinatakiwa zipasuke zitoe mayai bahati mbaya kitendo hicho kinashindikana hivyo izo Follicle cells ambazo zimeshindwa kupasuka na kutoa yai zinabaki na umbo k**a njegere na muonekano huu kitaalamu tunauita *'Cyst'* na kwa kuwa ziko nyingi tunaita *Polycystic*
Hali hii huambatana na dalili nyingi ambazo zinavuruga mwili wako kwa sababu ya o***y zako kutengeneza cyst nyingi *Polycystic* na kwa pamoja dalili hizi tunaziita *Syndrome* maana yake *mkusanyiko wa dalili nyingi*
*Nini Kinapelekea Unapata Ugonjwa Huu Wa Polycystic Ovarian Syndrome(PCOS)*
âš« Kuongezeka kwa homoni za kiume k**a Androgens ambazo ni Testosterone.
Kwa kawaida mwanamke huwa ana kiwango kidogo sana cha homoni hii ya kiume Testosterone.
Kuongezeka kwa homoni hii kwa mwanamke huashiriwa na dalili zifuatazo:-
🌹 Kuota ndevu kidevuni.
🌹Chunusi sugu.
🌹Kuongezeka Uzito kupita kiasi.
🌹Kuwa na kitambi.
*Wagonjwa wengi wa Tatizo hili hupewa dawa k**a Metformin, lakini hii dawa kimsingi haitibu tatizo, katika somo lijalo nitaeleza kwa nini wanapewa dawa hii*
*Zifuatazo ni baadhi ya homoni ambazo zikivurugika mwilini mwako husababisha tatizo la Polycystic Ovarian Syndrome(PCOS )*
âš« Kiwango cha Estrogen kuongezeka kupita kiasi. Hii hupelekea ukuta wa kizazi kujengeka na kuwa mnene kupita kiasi(Endometrial Hyperplasia) na hatimaye unaweza kuwa katika hatari ya kupata uvimbe kwenye kizazi au kansa ya kizazi.
⚫Follicle Stimulating Homoni(FSH) Inashuka kiwango. Kazi ya homoni hii ni kukomaza mayai kwenye o***y. Ikishuka husababisha ugumba.
⚫Lutenizing Homoni(LH) kuwa katika kiwango kidogo. Kazi yake ni kushinikiza o***y itoe mayai kila mwezi yale yaliyokomaa. K**a homoni hii ni ndogo haitafanya kazi ya kuamuru mayai yaliyokomaa kuja kwenye mirija ya uzazi kurutubisha.
*Makundi Ya Watu Wenye Tatizo Hili La Polycystic Ovarian Syndrome*
⚫Kundi la kwanza ni la mwanamke amepima amekutwa na o***y zake zina Polycysts hapati hedhi mara kwa mara na ana dalili za homoni za kiume.
âš« Mwanamke mwenye o***y zenye Polycysts ana dalili za homoniza kiume lakini mzunguko wake upo vizuri( hawa wapo wengi)
âš« Kundi jingine ni mwanamke mwenye O***y yenye Polycysts hana dalili za homoni za kiume lakini mzunguko wake wa hedhi ni mbovu sana.
*Vyakula unavyotakuwa kula mara kwa mara k**a una tatizo hili*
💎 Samaki wabichi.
💎 Karanga.
💎 Ufuta mbichi.
💎Alizeti.
💎Korosho.
💎Almonds.
💎 Nyama nyeupe.
💎Mayai ya kienyeji.
Hope umeongeza ufahamu wako. K**a una swali lolote kuhusu haya uliza hapa hapa.
Tupigie kwa 0745674037 au bofya link kwa huduma zaidi
https://wa.me/message/J556DIEUA2EAI1
Asanteni.
Click here to claim your Sponsored Listing.
Category
Contact the business
Website
Address
Ilemela
Mwanza
