Afya Bora
Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Afya Bora, Health/Beauty, Nyegezi, Mwanza.
SHINIKIZO LA DAMU/PRESHA YA KUPANDA/KUSHUKA(PRESSURE).
SHAMBULIO LA MOYO, KUTANUKA KWA MOYO/KUTANUKA KWA MISULI YA MOYO.
DAWA YA ASILI YA MATIBABU YA PRESHA, MOYO KUTANUKA, SHAMBULIO LA MOYO.
PRESHA/SHINIKIZO LA DAMU.
Ni msukumo wa damu kwenye kuta za mishipa inayo safirisha damu.
Unapo pima shinikizo la damu (presha) majibu yake hutoka na namba mbili:-
1. Namba iliyo juu (systolic)
Hii humaanisha nguvu ambayo moyo wako unasukuma damu kwenda sehemu mbalimbali za mwili.
2. Namba iliyo chini (Diastolic)
Hii humaanisha nguvu ya damu yako inayotembea kwenye mishipa ya damu wakati moyo umepumzika baada ya kusuma damu katika kila pigo.
⏹️ VIWANGO VYA UPIMAJI PRESHA.
√ Chini ya 110/65mmHg Hypotension (Presha ya kushuka au shinikizo la damu la chini)
√ Chini ya 120/80mmHg Normal (Kawaida)
√ Kati ya 120-129/80mmHg Pre- hypertension (Hatari ya kupata presha ya juu
√ Kati ya 130-139/80-89mmHg 1st stage hypertension ( presha ya juu steji ya kwanza)
Ifikapo 130 na kuendelea basi presha yako iko juu ni vyema kuwa makini zaidi kwa Afya yako.
√ 140/90mmHg au zaidi 2nd stage hypertension (presha ya juu steji ya pili)
Kuanzia 180/120 na kuendelea , Hypertensive crisis ( shinikizo la damu la juu zaidi).
Huku visababishi vya presha vikibakiwa kuwa ulaji usiofaa, magonjwa ya moyo, uzito mkubwa/unene/kitambi, matumizi yasiyo sahihi ya dawa za presha, kurithi, uvutaji wa sigara na unywaji wa pombe kali.
⏹️ ISHARA NA DALILI ZA SHINIKIZO LA DAMU (PRESHA).
Mara nyingi watu wenye shinikizo la damu hawana ishara yeyote na huwa inagunduliwa baada ya kufanya uchunguzi wa kiafya au presha kubwa kwa muda mrefu inapokuwa imefanya uharibifu mkubwa ndani ya mwili ni pamoja na dalili zifuatazo:-
➡️ Maumivu ya kichwa hasa nyakati za asubuhi.
➡️ Kuhisi kizunguzungu
➡️ Mapigo ya moyo kwenda kwa kasi
➡️ Maumivu ya kifua
➡️ Kupoteza fahamu
➡️ Kupumua kwa shida
➡️ Kujisikia uchovu usiokwisha
➡️ kutoona vizuri
➡️ Kukohoa
➡️ Kuhisi ukelele sikioni n.k
⏹️ SABABU/CHANZO CHA SHINIKIZO LA DAMU (PRESHA).
➡️ Umri
➡️ Msongo wa mawazo (strees)
➡️ Kuwa na mazoea ya kutumia chumvi nyingi kenye chakula
➡️Ulaji usiofaaa
➡️ Ukosefu wa shughuli za kimwili
➡️ Ulevi uliokithiri
➡️ Kuwa na unene uliopitiliza
➡️ Ujauzito
⏹️MADHARA YA KUENDELEA KUISHI NA SHINIKIZO LA DAMU (PRESHA).
➡️ Moyo kushindwa kufanya kazi (Heart Failure)
➡️ Moyo kutanuka (Cardiomegaly)
➡️ Shambulio la moyo ( Heart attack)
➡️ Kiharusi/Kupooza (stroke)
➡️ Kuharibu figo na figo kushindwa kufanya kazi
➡️Kusababisha upungufu wa nguvu za kiume.
⏹️ ZINGATIO.
Licha ya uwepo wa dawa mbali mbali za kukabiliana na tatizo hili bado huendelea kuwatesa na kuwaua wengi kila mwaka.
Pamoja na jitihada mbali mbali bado utasikia kila mwaka milioni 8 hufa kutokana na changamoto hii.
Huku watu bilioni moja duniani kote wanaathiriwa na shinikizo la juu la damu likiwapelekea kupata shambulio la moyo, kupooza na moyo kutanuka.
Na ni kwa mujibu wa WHO.
Muhimu, iko tiba ya asili inayoweza kutibu kabisa tatizo hili wapo wengi walioitumia na kupata matokeo mazuri.
Kwa mawasiliano piga
+255620106461
Presha ni msukumo wa damu kwenye vishipa vya damu, msukumo huo huzalishwa baada ya moyo kusukuma damu kwenye sehemu mbalimbali za mwili.
Aina za presha.
Zipo aina kuu mbili za presha, yaani;
(I) PRESHA YA KUPANDA
(II) PRESHA YA KUSHUKA.
PRESHA YA KUPANDA.
Presha ya kupanda ni msukumo wa damu unaosukumwa na moyo kwenda kwenye vishipa vya damu (artery) kuwa mkubwa kuliko njia ya mishipa hiyo.
Presha itaitwa kuwa presha ya kupanda ikiwa iko juu zaidi ya presha ya kawaida ambayo ni 120/80mmHg.Presha yaweza kupanda mpaka kufikia 240/120mmHg.
Sababu kuu za kupanda kwa presha.
(i) Utumiaji wa chumvi nyingi kwenye chakula.
(ii) Unywaji wa pombe/sigara uliokithiri.
(iii) Msongo wa mawazo na kutokufanya mazoezi
(iv) Familia zenye matatizo ya moyo pamoja na kurithi.
(v) uzito mkubwa,unene na kitambi.
Dalili za presha kupanda.
(I) Kushikwa na kizunguzungu
(II) Kichefuchefu, tumbo kujaa na kutapika kusiko kwa kawaida
(iii) Kuvimba/kujaa maji kwa miguu,uso na mikono.
(iv)Kutokuona vizuri (kuona ukungu).
Madhara yatokanayo na presha ya kupanda.
1️⃣ Uvimbe kwenye kuta za vishipa vya damu/kuziba kwa mishipa ya damu(artery) inayopelekea shambulio la moyo (Heart attack).
2️⃣Moyo kushindwa kusukuma damu (Heart failure)
3️⃣Kiharusi(stroke)
4️⃣ Kuharibika kwa ubongo.
Kwa upande mwingine;
PRESHA YA KUSHUKA.
Presha ya kushuka ni ile hali msukumo wa damu unakuwa mdogo kuliko upana (unene) wa vishipa vya damu hali inayopelekea damu chache kufika kwenye ubongo na viungo vingine vya mwili.
Presha ikishuka mpaka kufikia 90/60mmHg kutokea 120/80mmHg inatafsiriwa k**a presha iliyoshuka.
Presha ya kushuka huchangiwa hasaa na moja ya sababu zifuatazo;
_Matatizo ya homoni.
_Maradhi ya moyo pamoja na maambukizo ya vishipa vya damu.
_Kisukari.
_Kubeba Ujauzito.
_Ukosefu wa virutubisho mwilini k**a vile protini,madini ya chuma,Vitamin B-12 n.k
_Kushikwa na hasira pamoja na msongo wa mawazo.
Na moja ya dalili za presha hii ni k**a vile;
_Mchoko(udhaifu), mwili kukosa nguvu na kuhisi kizunguzungu.
_Maumivu ya kifua pamoja na homa kali
_Kupumua kwa shida na moyo kwenda mbio (mapigo ya moyo yasiyo ya kawaida).
_Maumivu kwenye kifua, bega la kushoto pamoja na kiwiko cha mkono.
Moja ya madhara yanayotajwa yatokanayo na presha hii ni mshtuko/kifo cha ghafla kunakotokana na viungo vya mwili kutokupata oxygen ya kutosha.
Epuka,dhibiti moja ya mambo yafuatayo ikiwa unasumbuliwa na tatizo la presha (aina zote) pamoja na athari zitokanazo na magonjwa ya moyo.
1.Kupata wasaa wa kufanya mazoezi ya viungo, kukimbilia au kuendesha baiskeli (wastani wa dk 45 kwa siku)
2.Epuka matumizi ya sigara, pombe na matumizi mengine ya madawa k**a Heroine
3.Tumia kiasi sahihi cha chumvi, sukari au mafuta kwenye chakula chako(Sikiliza miongozo ya wataalamu).
4.Pata wasaa wa kupumzika (Zaidi ya saa 8 kwa siku)
5.Punguza unene au uzito uriokithiri.
Muhimu zaidi;
_Ipo mimea tiba yenye uwezo wa kutibu matatizo ya presha na kuondoa athari zitokanazo na magonjwa ya moyo.
Nakukaribisha tena kupata suluhisho la tatizo lako.
Kwa mawasiliano piga
+255620106461
TIBA YA MIFUPA NA MAUNGIO KWA WASUMBULIWAO NA
MAUMIVU YA NYONGA, KIUNO, MGONGO NA MAUNGIO (JOINTS)?
MSHAURI: +255620106461
➡▪Hasa maumivu ya kusambaa kutoka kwenye nyonga mpaka kwenye goti
Tatizo hili huweza humpata mtu yeyote. Maumivu ya kiuno huanza chini ya mgongo na kuk**ata katika vifupa vilivyo kwa chini
karibu na makalio. Maumivu haya husambaa kulia na kushoto na wakati mwingine huteremka hadi mapajani. Pamoja na kuwepo katika vifupa hivyo pia ndani zaidi huweza kusababisha maumivu haya yatoke kwa ndani na kusambaa nje yaani katika eneo la kiuno.
Maumivu ya nyonga huweza kutokea sambamba na maumivu ya kiuno au nyonga yakawa peke yake. Nyonga huunganisha miguu na mifupa ya mapaja inayotengeneza kiuno. Nyonga ndiyo inayofanya utembee, inakuwezesha kutoka sehemu moja hadi nyingine, kukaa na kuruka.
SABABU ZINAZOPELEKEA MAUMIVU YA KIUNO NA NYONGA (mifupa kwa ujumla)
1.Kujichua muda mrefu hupelekea maumivu hayo. Zipo dawa za kuacha kujichua na kurudisha nguvu zilizopotea.
2.Namna ya kulala (style) /godoro linaweza kukusababishia maumivu hayo
3.Kubeba mizigo kwa kuinama na mzigo.
4.mawazo (stress).
5.kulala kwa muda mrefu na matumizi mabaya ya mto.
MADHARA YA MAUMIVU HAYO NI K**A YAFUATAYO;
1.Hupelekea kushindwa kufanya tendo LA ndoa.
2.hupelekea kupooza kwa baadhi ya viungo vya mwili na kushindwa kutembea (kupata kilema cha kudumu)
3.hupelekea kuwahi kufika kileleni mapema wakati wa tendo na kushindwa kurudia.
4.Unaweza kushindwa kutembea kabisa /kunyanyuka, utakaa ukiwa umelala.
Habari njema ni kwamba baada yakufanya utafiti wa kina kwa mda mrefu sasa tiba imepatikana,tiba ya uhakika na ya haraka
Kwa matibabu ya haraka na sahihi wasiliana nasi,
Au fika ktk ofisini zetu zilizopo karibu Kila mkoa
*TIBA YA KUDUMU YA BAWASIRI {NDANI NA NJE}/MGOLO
MAWASILIANO: +255620106461
*BAWASIRI {HEMORRHOIDS/PILE*
➖ Ni ugonjwa unaotokana na kuvimba kwa mishipa ya damu katika mfereji wa njia ya haja kubwa na kuoelekea kuota kinyama sehemu ya haja kubwa.
*CHANZO CHA BAWASIRI*
➖ Tabia ya kuketi sehemu moja kwa muda mrefu mfano; madereva
➖ Tatizo sugu la kuharisha
➖ Ujauzito
➖ Uzito wa mwili kupita kiasi
➖ Kufanya ngono kupitia tundu la haja kubwa (kulawitiwa)
➖ Kupata haja kubwa ngumu
➖ Kua na mgandamizo mkubwa tumboni
➖ Kunywa pombe
➖ Kula sana nyama nyekundu
➖ Vidonda vya tumbo
➖ Ngiri(Chango/Hernia
➖ Kula sana pilipili
➖ Kunyanyua vitu vizito
*DALILI ZA BAWASIRI*
➖ Kupata muwasho mkali katika eneo la juu la haja kubwa
➖ Kujitokeza kwa kinyama eneo la haja kubwa
➖ Kutokewa na kiuvimbe katika tundu ya haja kubwa
➖ Kupata kinyesi chenye damu
➖ Kupata maumivu makali wakati wa
kujisaidia haja kubwa
➖ kutokwa na uteute sehemu ya haja kubwa
➖ Kupata maumivu makali wakati wa kujisaidia haja kubwa na kusababisha mishipa ya sehemu ya haja kubwa kukwanguliwa
➖ Kuna uwezekano mkubwa wa kupata saratani ya utumbo (Cancer) kwasababu kile kinyama kinakaa k**a kidonda
➖ Uume kusinya (unapoteza urefu na ukak**avu)
*MADHARA YA BAWASIRI*
➖ Upungufu wa damu mwilini
➖Kutokwa na kinyesi bila kujitambua
➖ Kukosa hamu ya kufanya tendo la ndoa
➖ Kupungukia nguvu za kiume (kwa wanaume)
➖ Kupungukiwa na uwezo wa kufanya kazi kutokana na maumivu
➖ Kupata tatizo la kisaikolojia
➖ Kutopata ujauzito
➖ Mimba kuharibika
Call➖text&sms➖whatsapp👇
+255620106461
16/02/2022
Click here to claim your Sponsored Listing.
Category
Telephone
Website
Address
Nyegezi
Mwanza
