Jamii
Care and believe oneself
13/06/2022
Leo ni siku ya kimataifa ya Watu wenye Albinism Duniani,,na mm k**a Mtu mwenye Ualbino ,,naungana na Jumuiya ya Kimataifa kuwatakia kheri nyingi wenzangu wote kote ulimwenguni 🙏🏻
Najua sio rahisi kutoboa Kwa baadhi ya watu ,,hususan wenye mila potofu na imani haba hasa huku Afrika,,lakini INAWEZEKANA.
Unaweza kufanya lolote lile pengine kuliko linalowezwa kufanywa na Binadamu wengine ,ikiwa una malengo sahihi,,binafsi napitia changamoto nyingi za kubezwa kwa rangi yangu lakini sijawahi Kurudi nyuma.
Unaweza kuwa Msomi ,unaweza kuwa Tajiri ,unaweza kuwa Mwanasiasa ,unaweza kuwa Mwanamuziki ,unaweza kuwa Daktari ,,na hata kuwa Maarufu na Mashuhuri kweli kweli k**a nilivyo mm hii leo,,licha ya Ualbino wangu,,
Usijisikie vbaya hata kidogo na jivunie ulivyo na mshukuru Muumba wako,ww ni sehemu ya matakwa ya Mungu aliyeahidi katika Vitabu vyake kwamba,,atawaumba Wanadaamu vile atakavyo yeye.
Endelea kutumia karama zozote alizokujaalia Mungu wako ,kuionyesha Jamii kwamba YOU CAN.
Ona kaka yako Bugati,,naishi katika kundi la Wafuasi wa Mpira wenye ushindani mwingi na baadhi yao ambao si Wastaarabu,,huja na dhihaka na matusi ya kila namna Kwa sababu mm ni Albino,,nn kinatokea? Nasonga mbele na namuangalia anaekutukana najiona nimemzidi kila kitu,,kuanzia Pesa,Jina kubwa,Umashuhuri,,,Wake Wazuri na hata kuishi tu maisha ya nyumbani,,,anakukejeli ukimwangalia vema,,unaweza kumuajiri kwako kupeleka Watoto shule au kusafisha Mabanda ya kuku uani,,
Yes,,,Msikubali kuwa Wanyonge hata siku moja Kwa jinsi ulivyo,,na Inshaallah Mungu atawalinda na kuwasaidia sababu yy ndio kataka iwe hvyo,,,na Mjivunie kwake vile alivyowaumba.
Mbarikiwe sana ndugu zangu 🙏🏻🙏🏻🙏🏻🙏🏻
👏
11/06/2022
Nini maana halisi ya ualbino?
Watu wamekuwa na mitazamo tofauti tofauti kuhusu nini maana ya ualbino ?
Kumekuwa na watu wakidhani ya kwamba ualbino ni ugonjwa, wengine wakaenda mbali kwa kusema ni liana kuzaliwa katika hali hiyo la hasha sivyo tunakosea. Kuzaliwa albino siyo dhambi si kutokana na imani ziwapotoshazo jamii.
Hivyo k**a Bilblia isemavyo kuwa Mungu aliumba Binadamu kwa Sura na Mfano Wake Hivyo hivyo mungu anaimba watu kwa rangi tofauti tofauti kwa sababu yeye anafahamu au anaumba kwa makusudi yake yeye.
Ualbino ni nini ? Ni hali ya kukosa rangi kwenye ngozi na macho hivyo kufanya ngozi kuwa nyeupe na macho kuwa na uoni hafifu.
10/06/2022
Jamii ijifunze kuhusu ualbino
Nawpenda kutoa shukrani zangu kwa watanzania wenzangu. Katika page hii ni kwa ajili ya lengo la kuifahamiaha hamiii na kutoa uelewa kuhusu watu waishio na ualbino.
Nakamura uwepo wa tovuti mbalimbali ambazo zimekuwa zikielezea watu lakini zimekuwa k**a zinakawia au zimekuwa zikiwafikia wachache wao na kuwaacha wengine njia panda, hivyo kwa moyo wangu wa dhati nimejitolea kuwaeleza na kuwafundisha ikiwezekana uelewa juu ya ualbino
Katie's page hii nitawaeleza kuhusu ualbino, changamoto wapatazo watu wenye ualbino, hivyo hivyo nitaemda kuelezea jamii nini wafanye ili kuondoa imani zilizopo pia nitaenda mbali kidogo kuelezea makurdi mengine ambayo ni fofauti na hii
10/06/2022
Page hii ni kwa ajili ya kuelimisha watu kuhusu albinism kwa sababu zipo jamii za watu ambao bado wanawaona k**a siyo watu hivyo hushindwa kuwapa ushirikiano
Click here to claim your Sponsored Listing.
Category
Contact the business
Telephone
Website
Address
Nyamagana
Mwanza
