Nest Healthcare Tz
'PATA USHAURI WA AFYA &TIBA YA MAGONJWA TABIA, Tumia dawa zilizo tengenezwa kwa mimea,wanyama wa bah
09/02/2019
MWANAMKE KUWA MAKINI NA MAMBO HAYA WAKATI WA HEDHI.
(Sio mbaya kwa wewe MWANAUME kusoma makala hii mpya niliyoandaa ili uweze kushea kwa wanawake walio karibu nawe)
Mwanamke katika jamii yoyote ni wamhimu saaana, na mwili wa mwanamke katika swala la kupata maradhi au matatizo ya kimwili ni vyepesi kutokana na walivyoumbwa, ila umakini wa mwanamke huyu na kujali kwake afya ndio itakuwa ponea yake.
Kwa ufupi tu, mwanamke ukiwa kwenye usitumie vitu hivi vinne.
1. Usinywe vinywaji vya baridi (hasa vile vyenye barafu)
2. Usinywe carbonate drink (Pepsi, Coca, Soda za aina yote)
3. Pamoja na n**i (hata maji yake usinywe wakati wa hedhi)
Usinywe kwa sababu mirija inakuwa wazi ambayo inaweza ikakusababishia kuumwa kwa kichwa na kujihisi vibaya. Ni hatari sana, na madhara haya unaweza ukayahisi wakati wa ujana hata uzee.
4. Usile tango, unapokuwa katika hedhi,
kwa sababu maji yaliyopo kwenye tango yanaweza yakasababisha hedhi kubaki kwenye kuta ya uzazi.
Kwakuongezea katika mzunguko huo wa hedhi, mwili usiweze kudondokewa kupigwa au kugongwa na vitu vizito kwasababu itapelekea kutapika damu na kuumia, huo ndio mwanzo wa saratani ya mfuko wa mayai.
Utafiti umethibitisha kuwa matumizi ya vinywaji vya baridi wakati wa hedhi vinaweza vikasababisha damu ya hedhi kubaki kwenye kuta ya uzazi,
Hivyo basi ukiendelea kutumia vitu hivyo, baada ya miaka 5-10 unaweza ukapata saratani ya mfuko wa uzazi.
Wanawake mna umuhimu saaana katika maisha, hivyo basi
NAKUOMBEA KWA MUNGU EWE MWANAMKE,
MUNGU AKULINDE NA AKUPE UFAHAMU JUU YA AFYA NA MATUNZO YA MWILI WAKO.
_______________________________________________
26/11/2018
JINSI YA KUPUNGUZA AU KUONDOA MAUMIVU YA KICHWA WAKATI WA UJAUZITO.
By
Nest healthcare tz
Wanawake wengi hupata tatizo la kuumwa kwa kichwa wakati wa ujauzito. Hili tatizo huweza kutokea wakati wowote wa ujauzito lakini mara nyingi hutokea wakati wa trimester ya kwanza (miezi mitatu ya kwanza) na trimester ya tatu (miezi mitatu ya mwisho) ya ujauzito.
Katika miezi mitatu ya kwanza kuumwa kwa kichwa mara nyingi husabababishwa na kuongezeka kwa hormone na damu inayosukumwa mwilini.
Kuumwa kwa kichwa kunaweza kuongezeka zaidi pale mwanamke mjamzito akiwa na stress, kukosekana kwa usingizi, uchovu, mafua, kuwa na low blood sugar(sukari isiyotosha kwenye damu), ukosekanaji wa maji ya kutosha mwilini(dehydration), kwa wale waliozoea kunywa kahawa kuacha kunywa kahawa kunaweza kusababisha kuumwa kwa kichwa.
Kuumwa kwa kichwa wakati wa trimester ya mwisho husababishwa na kuongezeka kwa uzito unaoweka stress kwenye mwili, mwili kutokuwa balanced, pamoja na wanawake wengine kuwa na high blood pressure wakati wa ujauzito(preeclampsia).
Mara nyingi mama mjamzito hashauriwi kunywa dawa zozote zile kwa kipindi hiki kwasababu kuna uwezekano wa dawa kupokelewa na mtoto na kumdhuru kwa namna moja au nyingine. Hii ni sababu maalaamu kujaribu kutumia njia natural kupunguza maumivu yoyote yale mama anayopatwa nayo kwa kipindi hiki.
Jinsi ya kupunguza au kuondoa maumivu ya kichwa wakati wa ujauzito.
-Jaribu kutuliza misuli ya uso na kupumzika.
-Uwe makini na madawa ya aspirin na jamii za dawa hii, kwa vile dawa yoyote uinywao inaweza kumuaffect mtoto.
-Ukisikia maumivu jaribu kunywa maji glass 2 - 3, kwasababu wakati mwingine maumivu husababishwa na kukosa maji ya kutosha mwilini.
-Fanya zoezi la kutembea halafu kunywa maji mengi ya kutosha.
-Chunguza vyakula unavyokula unaweza ukawa unapata reaction.
-Pumzika vya kutosha na kupata mazoezi ya relaxation.
-Fanya mazoezi mara kwa mara k**a unavyotakiwa kwa mama mjamzito.
-Kula chakula chenye afya kwa mama mjamzito.
-Unaweza kuweka kitambaa cha moto kwenye eneo la macho, pua na kichwa k**a kuuma kwa kichwa kunasababishwa na mafua au weka kitambaa cha baridi kwenye sehemu inayouma k**a ni maumivu ya kichwa ya kawaida.
-Hakikisha unabalance kiasi cha sukari kwenye damu(blood sugar)yako kwa kula kiasi kidogo cha chakula kila baada ya muda mfupi badala ya kusubiri kwa muda mrefu halafu kula mlo mkubwa.
-Ukipata massage ya shingo, mabega na uti wa mgongo itapunguza stress na kupunguza maumivu ya kichwa.
-Pumzika kwenye chumba chenye giza halafu jaribu kuvuta pumzi na kuachia ili kuondoa stress mwilini.
-Oga maji ya moto au baridi.
Baadhi ya vyakula vinaweza kuchangia kuumwa kwa kichwa. Unaweza kujaribu kuvitoa kwenye diet yako kuona k**a vitasababisha kupunguza maumivu ya kichwa.
Hivi vyakula ni pamoja na:
-Chocolate
-Vinywaji vikali
-Mtindi, jibini, sour cream
-Karanga
-Mikate yenye yeast
-Nyama zilizowekwa kemikali ili kuzisaidia kukaa kwa muda mrefu bila kuharibika.(processed milk)
-Ongea na daktari k**a umejaribu vitu hivi na bado maumivu yapo au yan**idi au kuumwa kwa kichwa kunaambatana na kizungu zungu, kuvimba kwa mwili, maumivu kwenye maeneo ya juu ya tumbo au kuongezeka kwa uzito ghafla.
29/12/2017
MATUMIZI SAHIHI YA PEDI | makosa yanayofanywa katika uchaguzi na matumizi ya pedi kwa wanawake
By Nest Healthcare Tz
Kumekuwa na ongezeko kubwa la magonjwa ya mfumo wa mkojo (UTI) na uzazi kwa wanawake, hii inasababishwa na sababu nyingi ikiwemo ya kukosa uelewa sahihi wa kanuni za afya na usafi wa mwili pamoja na mazingira yanayomzunguka mwanamke.
Mada za usafi wa mwanamke ni pana sana siwezi kumaliza kusema kila kitu, hivyo leo nitajikita zaidi katika matumizi sahihi ya pedi na mambo ya kuzingatia kabla ya kununua pedi.
Wadada wengi wamekuwa wakitumia pedi na kuziacha zikizagaa mitaani hali inayofanya nijiulize k**a tu ameshindwa kujua sehemu sahihi ya kuhifadhi au kutupa pedi aliyotumia yeye mwenyewe, Je anauelewa upi katika matumizi sahihi ya pedi hizo kabla hajazitumia?
Somo la leo nitajikita katika njia sahihi ya kuchagua na kutumia pedi, makosa yanayofanywa katika matumizi ya pedi na ushauri juu ya matumizi sahihi ya pedi na vitambaa kwa wale wanaovitumia.
Yafuatayo ni makosa yanayofanywa katika uchaguzi na matumizi ya pedi kwa wanawake:
1. Kutonawa mikono kabla na baada ya kutumia pedi. Mikono hushika sehemu mbalimbali hivyo kuna uwezekano ikawa na vimelea vinavyosababisha magonjwa kwa hiyo kushika pedi bila kunawa mikono kwa sabuni kunaweza kuhamisha vimelea hivyo kutoka mikononi na kwenda kwenye pedi inayotegemewa kuvaliwa.
2. Kutunza pedi bafuni au chuoni. Wadada wengi hupendelea kutunza pedi zao chooni/bafuni. Vyumba vingi vya choo/bafu havina mwanga wa kutosha na kuwa na unyevunyevu hali inayoweka mazingira mazuri ya ukuaji wa vimelea vya magonjwa k**a bacteria na kitendo cha kutunza pedi katika sehemu hizo kunaweza kusababisha kuhama kwa vimelea hao kutoka bafuni/chuoni kwenda kwenye pedi isiyovaliwa na kupelekea pedi hizo kuwa na vimelea vya magonjwa na mwanamke anakuwa katika hatari za kupata maambukizi.
3. Kutoangalia muda wa matumizi wa pedi kabla ya kutumia au baada ya kuzihifadhi kwa muda mrefu hali inayopunguza kiwango cha ufanisi cha pedi sababu ya kuisha kwa muda wake wa matumizi.
4. Kununua pedi zinazouzwa kiholela kwa njia ya utangazaji na za bei rahisi (promotion) ambazo baadhi zimeonekana kutengenezwa kwa malighafi zilizo chini ya kiwango au kukaa kwa muda mrefu hivyo kuuzwa kwa bei rahisi ili zitoke na kutumika haraka kabla ya kuisha muda wake.
5. Kutumia pedi ambazo zipo katika majaribio maalum. K**a tunavyojua kuna kila aina za pedi mpya katika soko kwa kadri siku zinavyozidi kwenda na baadhi ya pedi huingizwa sokoni kinyemela pasipo tafiti za kutosha na bila hata kuthibishwa na mamlaka husika.
6. Kutumia pedi kwa muda mrefu. Wanawake wengi hususani katika nchi zinazoendelea huwa hawamudu kutumia pedi moja kwa muda wa masaa mawili k**a inavyoshauriwa na wataalamu hivyo kujikuta katika hatari ya kupata magonjwa ya mfumo wa mkujo na njia za uzazi .
7. Kupendelea pedi zenye uwezo mkubwa wa kufyonza unyevunyevu ili ivaliwe muda mrefu pia ni tatizo sababu kwa kadri muda wa kuvaa pedi moja unapozidi kuongezeka na hatari za maambukizi ya magonjwa pia in**idi kuongozeka.
Wanawake wanashauriwa kufanya yafuatayo ili kuhakikisha usalama wa afya zao :
1. Kunawa mikono vizuri kwa sabuni kabla ya kugusa pedi ambayo unatarajia kuivaa na baada ya kuvaa kunawa tena mikono vizuri.
2. Kutohifadhi pedi bafuni au chuoni au sehemu yote yenye unyevunyevu na isiyo na mwanga wa kutosha ili kutotengeneza mazingira ya kukua kwa vimelea vya magonjwa ndani ya pedi.
3. Kuangalia kwa makini muda wa matumizi ya pedi kabla ya kununua au baada ya kutunza pedi kwa muda muda mrefu ili kuepuka kutumia pedi zilizopita muda wake wa matumizi.
4. Kuepuka kununua pedi zinazouzwa kiholela na zisizothibitishwa na TBS na mamlaka nyingine zenye dhamana ya kuangalia ubora wa pedi hizo. Mwanamke anatakiwa kuangalia nembo ya uthibitisho wa mamlaka hizo na kujiridhisha kuhusiana na usalama wa pedi hizo kabla hajanunua.
5. Kubadilisha pedi kila baada ya masaa mawili, k**a tunavyojua damu ni moja wapo ya chakula kizuri sana kwa vimelea vya magonjwa k**a bacteria, unyevunyevu unaosababishwa na kuvaa pedi kwa muda mrefu pia unapelekea ustawi wa bacteria hao na joto ambalo lipo katika maumbile ya ndani ya mwanamke vikiungana kwa pamoja vinatengeneza mazingira mazuri ya ukuaji wa bacteria , hivyo wanawake wanashauriwa kutovaa pedi hizo kwa muda usiozidi masaa mawili ili kuepuka mazingira hayo.
6. Kuchagua aina sahihi inayokutosha ina kuepuka pedi zinazobana sana kupita kiwango sababu zinaweza pia kukufanya usiwe huru na kutengeneza joto la ziada na michubuko katika maumbile ya mwanamke,hivyo mwanadada unashauriwa kutumia pedi itakayokukaa vizuri(isilegee sana wala kuachia sana)
7. Kwa wadada wanaotumia vitambaa badala ya pedi ni muhimu pia kuzingatia kanuni za kiafya na usafi kabla na baada ya kutumia vitambaa hivyo k**a vile kuchagua kitambaa angavu ,kukiloweka na kukifua vizuri, kuanika kwenye sehemu yenye mwanga wa jua wa kutosha na upepo wa kutosha pasipo na unyevunyevu ,kupiga pasi kabla ujakihifadhi na kabla ya kutumia ili kuuwa vimelea vya magonjwa na kuvitunza sehemu nzuri ambayo haina unyevunyevu, penye hewa na mwanga wa kutosha na mwisho ni kubadilisha kitambaa hicho kila baada ya masaa mawili pamoja na kunawa mikono vizuri kabla na baada ya matumizi ya vitambaa hivyo.
15/11/2017
TATIZO LA KUKOJOA KITANDANI (Enuresis)
By Nest healthcare tz
Tatizo la kukojoa kitandani kwa jina la kisayansi inaitwa ENURESIS ambapo mtoto aliye katika umri ambao uwezo wa kuzuiya mkojo unatarajiwa, anakua bado anaendelea kukojoa kitandani au kwenye nguo ni tatizo la kushindwa kuzuia mkojo wakati wa mchana au usiku katika umri wa miaka mitano au zaidi. Watoto wengi wanaacha kukojoa kitandani usiku katika umri wa miaka mitatu. Asilimia 5 hadi 15 ya watoto wa miaka mitano wanaoendelea kujikojolea kitandani wengi wao ni wavulana ambayo ni asilimia 7 kuliko wasichana ambayo ni asilimia 3. Katika miaka 15 wanaoendelea kujikojolea kitandani ni asilimia 2 hadi 3 tu, na asilimia moja tu katika miaka 18. Kwahiyo kujikojolea siyo ugonjwa. Ni utofauti katika ukuaji wa fiziologia ya kuzuiya mkojo kwa mtoto.
Mkojo unapo hifadhiwa katika kibofu cha mkojo, kibofu kinatanuka k**a pulizo. Katika sehemu fulani neva za kutanua kuta za kibofu cha mkojo zinapeleka ishara ya kuzuia mkojo katika akili. Hii hutokea katika sehemu ya ubongo inayohusika na matendo yasiyo ya hiari. K**a ubongo wa mtoto haujapata ishara hii, au ukishindwa kujua maana ya hiyo ishara, hatua ya makusudi ya kuzuia mkojo haitafanyika. Hii mara nyingi husababishwa na kuchelewa kwa ukuaji wa kibiologia wa utendaji kazi wa kuzuia mkojo. Ukuaji wa kijinsia inaweza kusababishwa na;
1} Kushindwa kwa akili kutambua ishara kutoka kwenye kibofu cha mkojo,
2} Ujazo mdogo wa kibofu cha mkojo; au 3} Usingizi nzito.
Kwa sasa tafiti zinaonyesha kwamba watoto wanaokojoa kitandani ni wagumu kuamka kutoka usingizini kuliko ambao hawana tatizo hilo. Ni muhimu kutambua kwamba watoto hawajikojolei kwa makusudi na kawaida huona aibu kwa sababu hiyo. Wazazi wasiwadhalilishe kwa kuwaaibisha au kuwaadhibu.
Mara nyingi tatizo la kujikojolea imegawanyika katika sehemu mbili.
Ya kwanza ni pale mtoto anaposhindwa kukuza uwezo wa kuzuiya mkojo tangia utoto wake,
Ya pili ni pale mtoto anaweza kujizuiya kujikojolea kwa miezi sita au zaidi, halafu anaanza kujikojolea tena. Ya kwanza ni tatizo la kurithi na huwapata watu wa familia moja. Tafiti kutoka somo la vinasaba inaonyesha kwamba ikiwa wazazi wote walikuwa wanakojoa kitandani, asilimia 77 ya watoto watajikojolea zaidi ya miaka mitano na ikiwa mzazi mmoja alikuwa na tatizo hili, asilimia 44 ya watoto watajikojolea zaidi ya miaka mitano. Na ikiwa wazazi wote hawakuwa na tatizo hili la kukojoa kitandani, asilimia 15 ya watoto watajikojolea zaidi ya miaka mitano.
CHANZO CHA TATIZO
Kuchelewa kukomaa kwa uwezo wa kibofu kuzuia mkojo ndio chanzo kikuu cha tatizo hili. Watoto hawa huwa hawana tatizo la hisia/kisaikolojia na k**a wanalo ni matokeo tu ya maangalizi mabaya au matatizo wanayoyapata kutokana na tatizo walilonalo la kushindwa kuzuia mkojo kwa kukojoa kitandani au kujikojolea na sio k**a chanzo kikuu.
Kwa upande mwingine tatizo la kukojoa linalokuja baadae huweza kuwa limesababiswa na matatizo ya hisia au ya kisaikolojia na msongo wa mawazo(stress). Mara nyingi hii hutokea pale anapozaliwa mdogo wake, ugomvi wa wazazi, msongo anaoupata mtoto anapoanza shule au kutengana na wazazi. Matatizo k**a haya na mengine yanayofanana yanaweza kumsababishia mtoto matatizo ya kihisia na kusababisha tatizo la kukojoa kitandani kuanza au kuzidi. Asilimia ndogo sana ya watoto wenye tatizo hili husababishwa na magonjwa au maambukizi katika sehemu ya kibofu au uwezo wa figo na hivyo kusababisha.
Tatizo hili limegawanyika katika sehemu mbili.
1. Tatizo la kukojoa kitandani wakati wa usiku (nocturnal enuresis) na lile la mtoto kujikojolea wakati wa mchana (diurnal enuresis). Tatizo la kukojoa kitandani wakati wa usiku huonekana zaidi kwa watoto wa kiume na lile la kujikojolea mchana mara nyingi huwa kwa wasichana.
MATIBABU NA JINSI YA KUMSAIDIA MTOTO
Ni muhimu kukumbuka kuwa watoto wenye tatizo hili wataacha kadiri wanavyokua na ikiwa utamsaidia inavyotakiwa, utamsaidia kuacha mapema zaidi.
Adhabu kali, kumpiga, au kumchapa mtoto mwenye tatizo hili humuongezea tatizo na kufanya tatizo lizidi au kuchelewa kuisha. Ni muhimu sana kutomuadhibu,kumtisha au kumsema vibaya mtoto mwenye tatizo hili. Kufanya hivyo sio tu k**a kutazidisha tatizo bali pia humfanya mtoto kuwa katika hatari ya kupata matatizo mengine ya kisaikolojia kwa wakati huo na hata baadae katika makuzi yake.
Ili kumsaidia mtoto mwenye tatizo hili ni muhimu na inashauriwa kumhakikishia na kumfariji mtoto kwa kumuonesha kua anapitia hatua ya kawaida ya makuzi na kuwa kadiri siku zinapita tatizo hilo linaisha. Hii itamsaidia mtoto kutopata msongo(stress) na kuusaidia mwili kufanya kazi yake vizuri ambayo hatimaye humsaidia kuondokana na tatizo hili mapema zaidi. Pia humzuia mtoto kuja kupata tatizo hili baada ya kuacha.
Pamoja na hayo; Yafuatayo husaidia kumpa mtoto mafunzo na kuufundisha ubongo kutatua tatizo hili.
1). Kupunguza unywaji wa maji na ulaji wa vyakula vya majimaji k**a vile uji masaa matatu kabla ya kulala.
2). Kumuamsha mtoto masaa mawili hadi matatu baada ya kulala ili akakojoe.
3). Kumpongeza siku ambazo hajajikojolea au kukojoa kitandani.
4). Wazazi na ndugu(eg dada) kushirikiana na mtoto kujua mida ambayo tatizo la kukojoa linatokea na kisha kutumia nyenzo za kumuamsha nusu saa au lisaa kabla(mfano alarm) kufanya hivi kwa muda Fulani kutaufanya ubongo uweze kujifunza na mtoto atakua anaamka mwenyewe hata kabla ya kuamshwa au kabla ya alarm.
-------------------------------------------------------------------------
Ahsante kwa kuwa nasi kupata elimu hii rafiki☑
PLEASE LIKE NA SHARE ILI WALEZI/WAZAZI WAJIFUNZE HILI WAWEZE KUSAIDIA WATOTO.
17/08/2017
12/08/2017
Tujiepushe Kunywa Maji Baridi Yana Madhara Kwa Afya Ya Binadamu
MADHARA YA KUNYWA MAJI BARIDI
UNYWAJI wa maji baridi, hasa katika joto kali k**a la Dar es Salaam, ni kiburudisho kikubwa cha koo na huleta faraja kubwa mwilini. Ni jambo la kawaida pia kwa mtu kuhitaji kunywa maji hayo mara baada ya kula mlo, iwe mchana au usiku.
Pamoja na ukweli kwamba maji baridi ni;matamu', lakini siyo mazuri kwa afya yako na katika makala ya leo tutaangalia ukweli kwa nini maji haya siyo mazuri.
Kwa mujibu wa utafiti uliokwisha fanywa na wataalamu wetu wa masuala ya lishe, mtu anapokunywa maji baridi mara baada ya kula chakula, maji yale yanapopita kwenye utumbo huchangia kugandisha mafuta yaliyomo kwenye chakula.
Kitendo hicho, husababisha usagaji wa chakula kuwa wa taratibu sana na hivyo kuchangia ukosefu wa choo. Mbali na ukosefu wa choo, ambao ni madhara yanayojionesha kwa muda mfupi, lakini pia kuna madhara ya muda mrefu yanayoweza kujitokeza baadaye sana.
Inaelezwa zaidi kuwa, wakati chakula kinapochelewa kusagwa kwa sababu ya kuganda kulikosababishwa na maji baridi, chakula hicho hukutana na ;acid' iliyoko tumboni ambayo huanza kuyayusha mafuta hayo haraka na kufyonzwa na utumbo kabla ya chakula chenyewe.
Hali hii inapoendelea kwa muda mrefu, tabaka la mafuta (fats) hujijenga kwenye utumbo na baadaye huweza kusababisha saratani ya utumbo.
Halikadhalika, huweza kuwa chanzo kingine cha ugonjwa wa moyo ambao madhara yake ni pamoja na kupatwa na Kiharusi na hatimaye kifo.
Ili kuepuka hatari hii, unachotakiwa kufanya ni kuacha tabia ya kunywa maji baridi na badala yake pendelea kunywa maji ya uvugu-vugu mara baada ya kula chakula. Vile vile zingatia ushauri wa kukaa kwa muda usiopungua nusu saa ndiyo unywe maji.
MAJI MOTO NA ASALI K**A DAWA
Kujiweka katika mazingira mazuri ya kuhakikisha unasafisha tumbo lako kila siku kabla ya kulala, weka utatartibu wa kunywa maji moto kiasi, yaliyochanganywa na asali.
Chemsha maji moto au chukua maji moto yaliyopo kwenye chupa ya chai, acha yapoe kidogo na kuwa ya uvuguvugu, kisha weka kijiko kimoja cha asali mbichi kunywa kisha lala. Kunywa maji hayo nusu saa au zaidi baada ya kula chakula cha mwisho.
Kitendo hicho kitakuwezesha kuyeyusha mafuta, kusadia usagaji wa chakula tumboni na hivyo kukuwezesha kutoa uchafu na sumu mwilini kwa njia ya haja kubwa. Kwa utaratibu huu, hutakaa na uchafu tumboni wala mrundikano wa mafuta mabaya mwilini.
Ni jambo lisilo shaka kuwa iwapo kila mmoja wetu atazingatia kanuni za ulaji na unywaji sahihi, bila shaka matatizo ya moyo na shinikizo la damu yanaweza kupungua kwa kiwango kikubwa, k**a siyo kutoweka kabisa.
"Ahsante kwa kuwa nasi kupata elimu hii rafiki k**a una Swali,Maoni/Pendekezo lolote tuandikie ujumbe mfupi kwa kubofya hapa, m.me/nestpage47 utajibiwa haraka ndani ya muda.
PLEASE LIKE NA SHARE NA WENZAKO WAJIFUNZE NA KUFAHAMU.
10/05/2017
SABABU 6 ZINAZOWEZA KUCHANGIA HEDHI YAKO KUCHELEWA KUIONA.
Wasichana/ Wanawake wengi huanza kutawaliwa na hofu kila wanapoona wakati wa kuona siku zao (hedhi) umefika halafu hawaoni hali ikijitokeza.
Wengi wanapoona hali hiyo mawazo yao yote hueleka kuwa wameshashika ujauzito, lakini kumbe hali hiyo huweza kutokea kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo hizi hapa;-
1. Huweza kuwa ni mabadiliko ya homoni mwilini.
2. Huweza kuwa ni matumizi ya pedi zisizo na ANIONS kayika pedi.
3. Mabadiliko ya uzito wa mwili.
4. Msongo wa mawazo.
5. Mpangilio au mabadiliko ya mlo.
6. Maambukizi kwenye via vya uzazi.
*Kwa matumizi na mahitaji yote ya pedi bora(Neplily pads) zenye Anions na rafiki kwa afya ya mwanamke (uke) kwaujumla na zenye uwezo mkubwa wa kumkinga mwanamke na magojwa nyemelezi wasiliana na NEST HEALTHCARE Tz utapatiwa huduma popote ulipo.
Ahsante kwa kuwa nasi kupata elimu hii rafiki k**a una Swali,Maoni/Pendekezo lolote tuandikie ujumbe mfupi kwa kubofya hapa, m.me/nestpage47 utajibiwa haraka ndani ya muda.
PEDI RAFIKI, HEDHI SALAMA, JIAMINI
PLEASE LIKE NA SHARE NA WENZAKO WAJIFUNZE NA KUFAHAMU.
04/05/2017
HIZI NDIZO SABABU ZINAZOPELEKEA UKE KUTOA HARUFU MBAYA.
Ni matumaini nyote mnaendelea vyema, nami nashukuru ni bukheri wa afya njema.
Leo tutazungumzia matatizo yanayopelekea kutokwa na harufu mbaya ukeni, maana watu wengi hudhani kuwa na harufu mbaya itokayo ukeni ni matokeo ya uchafu tu na ndio maana wanaume huwachamba wake zao kuwa hawajui kujisafisha na kufanya wanawake kuongeza jitihada katika kujisafisha ukeni, leo napenda kuzungumzia tatizo hili linalowasumbua wanawake wengi na kuwaumiza kichwa kutokana na kwamba lina athari kubwa sana kwani hufanya ndoa zao kudumaa NK,
~>Kitaalamu Hali ya mwanamke kutokwa na maji yenye rangi nyeupe au njano ni Hali ya kawaida na sio tatizo Lakini endapo maji yanatoka yapo katika Hali ya ute mzito wenye rangi nyeupe au kahawia na yanatoa harufu kali au kuwasha hapo una tatizo.
~>Majimaji au ute unaoteleza kutoka sehemu za siri ni njia inayowezesha viungo vya uzazi vya mwanamke kujisafisha au kutoa uchafu wa seli zilizokufa na mabaki ya damu ya hedhi nje ya mwili, pia huvikinga viungo vya uzazi dhidi ya maaambukizi ya bacteria.
~>Kwa kawaida huwa hayatoi harufu na huwa hayawashi na huwa na rangi nyeupe au njano pia huwa na asidi ya LACTIN ambayo huzuia bacteria kuzaliana.
~>Mwanamke hutoa kiasi cha grams 2 za seli zilizokufa kutoka kwenye mji wa kizazi na grams 3 za ute mwepesi kila siku, kiwango hicho kinaweza kuongezeka au kupungua kutegemeana na mzunguko wa hedhi pia Kuna wakati ute huwa mwepesi na unaovutika na Kuna wakati pia huwa mzito wa rangi ya njano hautoi harufu.
VISABABISHI VYA TATIZO HILI
Sababu za kutokwa na uchafu ukeni una vyanzo vingi sana vifuatavyo ni vyanzo vya tatizo hili
1. BACTERIA VAGINOSIS
Chanzo halisi cha ugonjwa huu hakijafanikiwa kuwa wazi,kinachotokea ni kuongezeka kwa ghafla kwa idadi ya bacteria hawa na kubadilisha uwiano wa kawaida katika mazingira ya uke, wanawake wenye wapenzi wengi na wanaofanya mapenzi kwa njia ya mdomo Wana hatari ya kupata tatizo hili.
2. TRICHOMONAS
Maambukizi haya hutokana na Aina ya protozoa wa seli moja, trichomonas mara nyingi huambukizwa kwa njia ya ngono, protozoa huyo huweza kukaa kwenye unyevu unyevu kwa Muda wa saa 24 Bila kufa hivyo kufanya taulo na chupi zisizokauka kuwa chanzo kingine cha tatizo hili.
3. YEAST INFECTION
Kwa kawaida Kuna kiwango kidogo cha yeast (candida albicans) katika uke, huwa tunasema Kuna maambukizi pale kiwango kinapozidi hali ambayo inatokana na kubadilika kwa hali ya hewa ukeni (Change in the PH balance of va**na)
Maambukizi ya yeast hayatokani na tendo la ndoa.
Mambo ambayo huchangia tatizo hili ni:
MATUMIZI YA DAWA ZA KUZUIA MIMBA, MAWAZO, UJAUZITO, KISUKARI MATUMIZI YA ANTIBIOTICS
4. VAGINAL OR CERVICAL CANCER
Mtu anapokua na kansa ya uke, hutokwa na maji ya harufu mbaya, hivyo ni heri uwe unafanya check up ili kujua Afya yako na kwakuwa cancer ya kizazi inapona hivyo ni vema ukatambua mapema uanze tiba.
5. SEXUAL TRANSMITTED DESEAS (STDs)
Kuna baadhi ya magonjwa k**a vile KASWENDE NA KISONONO yanasababishwa na ngono na kuwa chanzo cha tatizo hili.
6. POOR HYGIENE
Tatizo la kutokwa na maji wakati mwingine husababishwa na muhusika kua mchafu yaani mtu unaoga kwa siku mara moja, chupi moja ndio hiyo hiyo mwaka mzima, pads unakaa nayo saa 24, ukienda kukojoa ujitawadhi na maji masafi hivyo unategemea utakua salama kweli??? Zingatia usafi Mrembo
DALILI ZA TATIZO HILI
Kutokwa na uchafu ukeni unaoambatana na kuwashwa au kutokewa na vipele, hii hutokana na kuharibika kwa uwiano wa bacteria, hivyo kuwa na madhara nauchafu hutoka wa aina tofauti hapa chini nitaelezea kila Aina ya uchafu na dalili zake.
1. UCHAFU WENYE RANGI YA KAHAWIA AU DAMU
Huu uchafu huonyesha dalili ya kuwa mzunguko wako wa hedhi umevulugika na wakati mwingine ni dalili ya kansa ya kizazi, mwanamke anayepata tatizo hili hutoa damu nyingi kuumwa sana nyonga
2. UCHAFU WENYE RANGI YA NJANO /KIJANI WENYE HARUFU MBAYA
Endapo uchafu huo utatoka k**a povu na wenye rangi ya kijani au njano na ukiambatana na harufu mbaya huwa ni dalili ya ugonjwa wa trichomonas, maambukizi ya parasite yanatokana na ngono zembe, dalili Yake nyingine ni maumivu na kuwashwa wakati wa kutoa haja ndogo.
3. UCHAFU MWEUPE MZITO K**A JIBINI
Mara nyingi hii huwa ni dalili ya maambukizi ya fangasi(YEAST INFECTION) na dalili nyingine huwa ni kuvimba sehemu ya nje ya siri, kuwashwa na kupata maumivu makali wakati wa tendo la ndoa.
4. UCHAFU MWEUPE/KIJIVU WENYE HARUFU YA SAMAKI
Uchafu wa Aina hii ni dalili ya maambukizi ya bacteria vaginosis, mara nyingi mwenye tatizo hili husikia muwasho na maumivu sehem ya nje ya uke.
5. MAMBO MUHIMU YA KUZINGATIA KUEPUKA TATIZO HILI NA TIBA YAKE
Matibabu ya tatizo hili hufanyika baada ya kugundua chanzo cha tatizo na mara nyingi tiba yake ni tiba ya dawa za antibiotics, kitu ambacho si tiba nzuri zaidi kwasababu tatizo huweza kujirudia kila wakati na kusababisha matatizo zaidi hivyo tiba nzuri ni kuepuka hili tatizo kwa kufanya yafuatayo
*EPUKA KUJIINGIZA VIDOLE MARA KWA MARA UKENI.
*EPUKA MATUMIZI YA DAWA ZA ANTIBIOTICS MARA KWA MARA.
*PUNGUZA KULA VYAKULA VYENYE SUKARI NYINGI.
*TUMIA PEDI ZENYE ANIONS NI SALAMA KWA AFYA YAKO.
*SAFISHA VIZURI NGUO ZAKO ZA NDANI NA UZIANIKE JUANI NA HATA KUZIPIGA PASI.
*KULA/KUNYWA JUICE YA APPLE,STRAWBERRY, NANASI KWA WINGI.
*EPUKA KUFANYA NGONO ZEMBE.
*HAKIKISHA UNAJISAFISHA KILA UNAPOMALIZA KUJISAIDIA.
*EPUKA KUTUMIA DAWA ZA KUZUIA MIMBA.
*EPUKA KUTUMIA SABUNI AU VITU VYA MANUKATO UKENI,
NOTED :
Wanawake wengi mnapenda kutumia baadhi ya dawa kwa lengo la kuongeza vionjo kwenye mapenzi pia kufanya uke kunukia vizuri, au kukaza uke, Rafiki uke una harufu nzuri sana ambayo haipatkani kokote hivyo haihitaji kuwekwa pafyumu Wala kusafishwa kwa sabuni za kemikali kwani huwa panajisafisha hivyo ni heri ukaacha kutumia kwani madhara Yake hayaonekani sasa ila baada ya Muda huonekana.
Imetolewa na ndug:
£rnest kuye
(Nest Healthcare Tz)
*Kwa mahitaji yote ya pedi bora(Neplily pads) zenye Anions na rafiki kwa afya ya mwanamke/uke kwaujumla na zenye uwezo mkubwa wa kumkinga mwanamke na magojwa nyemelezi.
HEDHI SALAMA, PEDI SALAMA, JIAMINI
Ahsante kwa kuwa nasi kupata elimu hii rafiki k**a una Swali,Maoni/Pendekezo lolote tuandikie ujumbe mfupi kwa kubofya hapa, m.me/nestpage47 utajibiwa haraka ndani ya muda.
PLEASE LIKE NA SHARE NA WENZAKO WAJIFUNZE NA KUFAHAMU.
14/02/2017
DALILI HIZI ZITAKUONYESHA UNA TATIZO LA KIAFYA.
Kawaida mwili ukiwa umepungukiwa aina yoyote ya kirutubisho (ingredients), huonesha dalili kabla ya kujitokeza kwa ugonjwa. Bahati mbaya sana, watu wengi hawana uelewa wa dalili hizo. Katika makala haya, nakutajia dalili chache miongoni mwa dalili hizo.
•Midomo Kukauka,
Midomo huakisi afya ya mwili na hali ya maji katika mwili mzima. K**a una maji ya kutosha mwilini, basi hata midomo yako itakuwa laini na yenye unyevu. Unapokuwa na upungufu wa maji, ngozi huwa kavu. Kwa wale akina dada ambao hulazimika kulainisha midomo yao kila wakati kwa kutumia ‘lip sticks’, wajue kwamba wana upungufu wa maji mwilini.
Dalili nyingine…
Kuumwa kichwa, kukosa haja ndogo kwa muda mrefu, kukojoa mkojo wa njano-nyeusi au mkojo wenye harufu kali, ngozi kavu na unapoiminya ngozi ya nyuma ya kiganja inachelewa kunyooka, nazo ni dalili kwamba mwili una upungufu wa maji.
Suluhisho
Kunywa maji ya kutosha kulingana na uzito wa kazi unazozifanya. Kiwango cha chini ni angalau lita moja ya maji safi na salama, hakikisha umekunywa maji hata k**a husikii kiu. Vile vile ulaji wa matunda na unywaji wa juisi zitokanazo na matunda au mboga mboga, huweza kuondoa upungufu wa maji mwilini.
•Kukosa Haja Kubwa,
Kitendo cha kukaa zaidi ya siku moja bila kupata haja kubwa ni dalili ya wazi ya ukosefu wa kamba lishe (fibre) mwilini. Kwa kawaida binadamu anatakiwa kupata choo kikubwa kila siku kilicho laini na kingi. Iwapo hupati choo kila siku na ukipata unapata kigumu, tena kidogo, jua una matatizo!
Haja kubwa ni muhimu kwa sababu ndiyo inayosafisha tumbo, uchafu unapokaa tumboni kwa muda mrefu, sumu zilizomo kwenye haja kubwa hurejea mwilini na husababisha matatizo mengi ya kiafya, kuanzia magonjwa ya uvimbe, moyo na hata ubongo. Sumu huvuruga pia mtiririko wa homoni mwilini na hudhoofisha kinga ya mwili.
Suluhisho
Kula kwa wingi matunda mbalimbali, mboga za majani na vyakula vitokanavyo na nafaka zisizokobolewa, k**a vile ugali wa dona, mtama, ulezi, n.k. Ulaji wa vyakula hivyo bora, siyo tu kutaondoa tatizo la ukosefu wa haja kubwa, bali vitakulinda pia dhidi ya magonjwa ya kisukari, presha, ugonjwa wa moyo na mengine mengi.
•Vidonda Pembeni ya Mdomo,
Utafiti umeonesha kwamba kupasuka kwa midomo na kutokea kwa vidonda pembeni ya midomo, huwa ni dalili moja wapo ya upungufu wa vitamini B mwilini na mara nyingi huwatokea watu wanaopenda kunywa kilevi kupita kiasi, kula vyakula vya kwenye makopo (processed foods) na kula sukari kwa wingi.
Suluhisho
Suluhisho ni kula vyakula vyenye kuongeza vitamin B kwa wingi. Miongoni mwa vyakula vyenye kiwango kingi cha vitamin B ni pamoja na kiini cha mayai ya kienyeji, viazi vitamu, nyama ya ng’ombe na ya kuku, maini na vyakula vitokanavyo na nafaka isiyokobolewa.
Ingawa unaweza pia kula vidonge lishe vya vitamin B ili kuondoa upungufu huo, lakini tahadhari lazima ichukuliwe na ina shauriwa kula vyakula vya kuongeza vitamini hiyo zaidi kuliko vidonge.
Imetolewa na ndug:
£rnest Kuye
(Nest Healthcare Tz)
Ahsante kwa kuwa nasi kupata elimu hii rafiki k**a una Swali,Maoni/Pendekezo lolote tuandikie ujumbe mfupi kwa kubofya hapa, m.me/nestpage47 utajibiwa haraka ndani ya muda.
PLEASE LIKE NA SHARE NA WENZAKO WAJIFUNZE
28/01/2017
UCHAFU UKENI -MAMBO 10 YA KUZINGATIA
Kwanza napenda kutoa shukrani nyingi sana kwa wateja wetu wote wa pedi za Neplily katika mikoa ya Mwanza, Shinyanga, Kahama, Dsm, Tanga, Arusha, Dodoma, Mbeya, Morogoro, Arusha, Songea, Babati, Iringa, Tanga, Dodoma, Bukoba, Ngara, Zanzibar na mikoa mingine yote🙏 ahsanten sana.....
K**a wewe ni mwanamke mwenye uke unaotoa harufu mbaya basi yamkini Mungu amekusikia kilio chako, leo utapata angalau machache yanayoweza kukusaidia katika kupambana na jambo hili lenye kutia aibu na wasiwasi. Pole sana, Harufu hii huwa kero sana hasa kwa wanamahusiano na wanandoa mpaka wengine inapelekea kuwa na ndoa isiyokuwa na tendo la ndoa. Harufu hii inayotokea ukeni hasa wakati na baada ya kufanya tendo la ndoa na wengine wakati wa siku za hedhi na baada ya siku za hedhi. Kawaida kila mwanamke hujua harufu ya uke wake katika siku za kawaida, na harufu mbaya mfano k**a shombo ya samaki ni dalili ya kwamba uke si shwari – Ushauri wa haraka ni kumuona dakatari.
VITU VIWILI UNAWEZA KUVIONA KWA WAZI KABISA.
1• Kwanza ni uchafu mweupe au wa njano unatokea mara kwa mara wakati wa tendo la ndoa au wakati wowote bila tendo la ndoa, unaweza kuwa na harufu au ukawa hauna harufu.
2• Pili ni harufu mbaya k**a “shombo ya samaki” ambayo huweza kutokea wakati wa tendo la ndoa au wakati wowote ule.
KWA NINI UNAKUWA NA UCHAFU NA HARUFU MBAYA UKENI?
ZAMA NDANI HAPA. Uke ni kiungo muhumu sana katika mwili wa mwanamke, uke unahitaji kupumua na pia kuingiza hewa safi, Uke unahitaji kuwa na usawa mzuri wa uchachu na uchungu (alkaline and acidity)
1• Sababu kubwa ya uchafu na harufu mbaye ukeni ni uharibifu wa uchachu/uchungu ukeni (PH) ambao hupelekea kuotea kwa bakteria na fangasi wabaya.
2• Kukosekana kwa hewa safi ya oxgeni ukeni, uchafu na uzembe. Bacteria na wadudu wengine wabaya huzaliana vizuri ikiwa uke hautapata oxgeni ya kutosha.
3• Magonjwa, hasa ya zinaa na yale yatokanayo na jamii ya bacteria na fangasi au utando pia ni chanzo cha harufu mbaya ukeni.
4• Upungufu wa kinga ya mwili na uharibufu wa homoni pia ni tatizo.
BAADHI YA MBINU UNAWEZA TUMIA ILI KUEPEUKANA NA HARUFU MBAYA NA UCHAFU UKENI NI PAMOJA NA;
1: VAA NGUO ZA NDANI ZA PAMBA NA ZISIZOBANA –Nguo za ndani ni vizuri ukavaa za pamba na zenye kuwa safi kabisa, kuvaa chupi angalau 2 katika masaa24 ni muhimu sana. Nguo za pamba huruhusi hewa kutoka na kuingia kirahisi.
2: CHAGUA PEDI ZILIZOTENGENEZWA KWA PAMBA NA ZENYE KUUNDA OXGENI –Hili tumeliongelea sana ndugu zangu, pedi nyingi zimetengenezwa kwa malighafi ambazo ni masalia ya takataka na maboksi , hazina uwezo wa kuunda oxgeni ambayo ni muhimu kwa ajili ya kuuwa wadudu waharibifu ukeni na wanaosababisha harufi mbaya. Zingine zina madini mabaya yanayo haribu mfumo wa uzazi na pia kuharibu PH ya uke. Pedi
bora mpaka sasa ni NEPLILY
3: ACHA KULA WANGA NA VYAKULA VYA SUKARI -Tumeshaongea sana kuhusu hili, vyakula vya wanga na sukari, chips soda pia pombe ni hatari kabisa kwa uke wako, lazima unuke. Achana/Punguza vyakula hivi k**a tayari umeanza kuhisi mambo si shwari maeneo yako.
4: MWANAUME ASIYETAHIRIWA NI SHIDA -Mara nyingi mwanaume asiyetahiriwa huwa na uchafu katika ule mfuko wa kichwa cha uume, uchafu huu unaweza bakia ukeni na kuwa sehemu ya kutengeneza bacteria na fangasi na hatimaye kuanza kutoa harufu mbaya.
5: BAADA YA HAJA KUBWA JISAFISHE KWA KUFUTA KUANZIA MBELE KURUDI NYUMA -Hii ni kwa sababu k**a utajifasisha kwa kuja mbele kuna uwezekano wa uchafu(mavi) kuingia ukeni na kuanza kutengeneza wadudu waharibifu ambao watazaliana haraka sana na kuanza kuharibu PH ya uke na kutoa harufu mbaya.
6: KUNYOA NI USAFI LAKINI USINYOE UPARA -Unajua nini? Unyoaji wa upara ukeni unasababisha vimelea kutengeneza vipele na kushindwa kupumua na hivyo kuanzisha makazi ya wadudu wabaya.
7: MTINDI -Kunywa mtindi karibu kila siku, unaweza pia kujisafisha kwa kutumia mtindi ukeni. Mtindi unabakteria wazuri ambao wanaweza kurudisha PH ya uke vizuri.
8: MAJI SAFI -Maji ni dawa kubwa sana katika kusafisha mwili na sumu zilizojaa mwilini,kunywa maji zaidi ya lita 3 kwa siku au glasi 8. Safisha uke na maji ya kawaida kabisa. Oga mara kwa mara, hakikisa uke umekauka vizuri ndio uvae nguo za ndani.
9: HEWA SAFI -Achia uke upate hewa, hasa mida ya usiku ukilala.
10: ONANA NA DAKTARI -Mara nyingi uchafu na harufu mbaya ni dalili ya ugonjwa flani wa bacteria na fangasi, inaweza pia kuwa ni ugonjwa wa zinaa, kutoka kwa mwanaume au wewe mwenyewe. Haya yote huwezi yajua k**a hutaonana na daktari. Vunja ukimya usikae na aibu yako na kuogopa kumwona dakatari. Unaweza pia baada ya kupima kuonana na washauri wa afya (tiba mbadala).
PEDI ZA NEPLILY ZINAPATIKANA Mwanza, Kahama, Iringa, Ngara, Njombe, Shinyanga, Singida, Mbeya, Arusha, Morogoro, Tanga, Zanzibar, Babati, Bukoba, Dodoma, Dar es salaam na mikoa mingine yote
Kwa ushauri zaidi wa matumizi ya sabuni, upatikanaji wa Pedi wasiliana nasi.
Ahsante kwa kuwa nasi kupata elimu hii rafiki k**a una Swali,Maoni/Pendekezo lolote tuandikie ujumbe mfupi kwa kubofya hapa, m.me/nestpage47 utajibiwa haraka ndani ya muda.
LIKE PAGE HII NA SHARE Post NA WENGINE WAJIFUNZE.
Click here to claim your Sponsored Listing.
Category
Website
Address
Mwanza
